Rais Magufuli na dhana ya "Maendeleo Hayana Vyama": Tafiti zinatueleza nini?

Rais Magufuli na dhana ya "Maendeleo Hayana Vyama": Tafiti zinatueleza nini?

Mchambuzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2007
Posts
4,850
Reaction score
9,434
Tangia aingie madarakani November 2015, Rais John Magufuli amekuwa akinukuliwa mara kwa mara akitamka kwamba Maendeleo hayana Vyama. Kauli hii imeendelea kuleta mjadala mkubwa katika siasa za nchi. Lengo letu leo ni kudadisi kwa undani kupata ukweli juu ya suala hili. Ili kufikia lengo letu:

Kwanza, tutalazimika kupitia na kuchambua kazi za watafiti na wanazuoni mbalimbali duniani.

Pili, tutajaribu kuingia ndani ya Fikra za kisiasa za Mwalimu Nyerere juu ya suala husika.

Mjadala wetu umegawanyika katika sehemu kuu tatu:

Sehemu ya KWANZA – tutaangalia na kujadili uhusiano ulipo baina ya - “ushindani wa Kisiasa” na Kukua kwa Uchumi.

Sehemu ya PILI – tutaangalia na kujadili uhusiano ulipo baina ya - “Demokrasia” na kukua kwa Uchumi.

Sehemu ya TATU – tutaangalia na kujadili uhusiano baina ya - “Vyama vya Siasa” na Demokrasia.

Sehemu ya NNE tutamalizia mjadala wetu kwa kuingia ndani ya Fikra za kisiasa za Mwalimu Nyerere, kwa maana ya ‘Nyerere’s Political Thought’.
 
SEHEMU YA KWANZA

Uhusiano baina ya Ushindani wa Kisiasa na Ukuaji Uchumi

Watafiti mbalimbali duniani wameendelea kuchunguza uhusiano baina ya ushindani wa Kisiasa na Ukuaji Uchumi wa taifa. Pamoja na jitihada hizi, hadi leo bado hakuna muafaka miongoni mwa watafiti juu ya suala hili.

Kwa upande mmoja, zipo tafiti zinazoonyesha kwamba ushindani wa kisiasa una athari chanya kwa ukuaji wa uchumi (mfano Lake & Baum, 2001; Lindert, 2004; Chauvet & Collier, 2009; Knutsen, 2013).

Kwa upande mwingine, zipo tafiti zinazo onyesha uwepo wa uhusiano wa karibu baina ya kasi kubwa ya ukuaji uchumi na mfumo wa utawala wa ‘ki-autokrasia. Kwa mfano, wanazuoni kama Sachs (2005) na Collier (2011), wanaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa hausaidii ukuaji wa uchumi wa taifa. Hoja ya msingi inayojengwa hapa ni kwamba – usimamizi mzuri wa uchumi wa nchi unahitaji utawala imara wa kisiasa (strong political leadership). Tafiti za Booth (2012); na Kelsall na Booth (2013), nao pia zinaonyesha hili kiutafiti kwamba – ushindani wa kisiasa una nafasi ndogo ya kufanikisha kasi kubwa ya ukuaji uchumi. Wanafafanua kwamba hii ni kwa sababu ushindani wa kisiasa unazaa utawala/viongozi dhaifu (weak political leadership).

Zipo tafiti nyingine mbalimbali ambazo pia zimelivalia njuga suala hili. Kwa mfano, utafiti wa Jones and Olken (2005) unaonyesha kwamba – chini ya serikali au utawala/uongozi wenye ushindani wa kisiasa ni vigumu kutekeleza sera zenye kuleta mafanikio kiuchumi.

La Porta na wenzake (2013) wanajadili hili kwa kuhusisha uhusiano baina ya masuala makuu matatu yafuatayo:

- Autocracy (Autokrasia)

- Strong leadership (Uongozi imara/thabiti)

- Economic Growth (Ukuaji uchumi).

Wanajali kwamba nchi nyingi duniani ambazo zilifanikiwa kushinda vita dhidi ya umaskini ni zile zilizofuata mfumo wa utawala wa Autokrasia. Wanajadili kuwa – maamuzi yaliyochukuliwa na watawala wa ‘Kiautokrasia’ ndio yaliyosaidia nchi zao kutokomeza umaskini. La Porta na wenzake (2013) wanahimiza kwamba:

Uhuru walionao watawala/viongozi wa ‘ki-autokrasia’ unawapa nafasi na uhuru wa kufanya au kuchukua maamuzi magumu bila ya hofu ya upinzani wenye nguvu. Hali hii unazipa tawala za aina hii faida (advantage) kubwa katika utekelezaji wa sera za uchumi na maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla.

Watafiti husika wanatumia uzoefu wa nchi zifuatazo kuonyesha ushahidi kuhusu jinsi gani tawala za autokrasia zimefanikiwa kuleta miujiza ya kichumi duniani.

China chini ya Rais Deng Xiaoping

Singapore chini ya Lee Kuan Yew

Rwanda chini ya Paul Kagame

Lakini pia utafiti wao unakuja na tahadhari kwamba:

Pamoja na uwepo wa uhusiano chanya baina ya mfumo wa Ki-autokrasia na mafanikio ya kiuchumi, hii haina maana kwamba haya masuala mawili , kwa maana ya– (i) “uhuru wa kufanya/kuchukua maamuzi magumu” na (ii) “mfumo wa utawala” , lazima viendane pamoja.

Wanazidi kufafanua kwamba:

Kwa upande mmoja, chini ya mfumo wa ki-autokrasia panaweza kuwepo:

-Tawala dhaifu (weak political regimes).

-Tawala zinazokabiliwa na hofu dhidi ya upinzani, na

-Tawala ambazo hazina uhuru wa kufanya maamuzi ya kisera (uchumi) kwa muda mrefu ujao (long term economic decisions).

Kwa upande mwingine, wanafafanua kwamba - chini ya mfumo wenye ushindani wa kisiasa vile vile panaweza kuwepo:

- Tawala zenye nguvu kisiasa (strong political regimes) ambazo zina uhuru wa kufanya maamuzi magumu na ya muda mrefu bila ya hofu ya kuanguka kwenye chaguzi kuu.

Wanahimiza pia kwamba - zipo tawala zenye ushindani wa kisiasa ambazo kutokana na sababu mbalimbali, zina uhakika wa kupata kura za ushindi katika chaguzi kuu. Tawala za aina hizi huwa na ‘discretion’ zaidi kutekeleza sera ambazo awali zinaweza zisiungwe mkono na wananchi wengi lakini hatimaye (in the longer term), zikawa na matokeo chanya kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.

Mtafiti Olson (2000) analiangalia hili kwa mtazamo tofauti kidogo. Anajadili kwamba, ‘given some conditions’, tawala za ‘ki-autokrasia’ zinaweza fanikiwa kiuchumi. Anataja na kujadili kwamba ‘condition’ kwamba na inayopaswa kuwepo ni:

‘Matarajio ya mtawala/utawala husika wa kuendelea kuwepo madarakani kwa muda mrefu (long tenure)’.

Almeida na Ferreira (2002) wametumia njia ya ‘case studies’ kudadisi zaidi utafiti wa Olson (2000). Wao pia wanathibitisha kwamba tawala zinazofanya vizuri zaidi kwenye eneo la ukuaji uchumi ni zile zinazofuata mfumo wa ‘autokrasia’. Laki wao pia wanatoa angalizo muhimu kwamba:

Tawala chini ya mfumo wa ‘ki-autokrasia’ pia zinaweza kufanya vibaya zaidi katika eneo la ukuaji uchumi kuliko tawala chini ya mfumo wa ‘ki-demokrasia’.

Glaeser na watafiti wenzake (2004) pia wamelitafiti suala hili kwa undani. Wao wanatumia neno ‘udikteta’ na kuthibitisha kwamba – mara nyingi nchi zinazoelekea kutokomeza umaskini huwa ni zile zinazotawaliwa na ‘madikteta’. Utafiti wao pia unaungwa mkono na matokeo ya tafiti nyingine kadhaa. Kwa mfano, Acemoglu na wenzake (2003) na Yang (2008) wanathibitisha kiutafiti kwamba nchi nyingi zinazopitia vipindi vya kasi kubwa ya ukuaji uchumi mara nyingi ni zile zinazotawaliwa kwa mfumo wa ‘ki-autokrasia’. Wanafafanua sababu juu ya hili ni kwamba – viongozi wa ‘ki-autrokasia’ huwa na ‘discretionary powers’ zaidi (nguvu za kufanya maamuzi magumu), katika kutekeleza na kusimamia sera, bila ya kujalisha matokeo yake kiuchumi kwa baadae (long term economic impact).

Acemoglu na wenzake (2003) na Yang (2008) wanatofautisha hali hii na ile chini ya mazingira yak i-demokrasia na kujadili kwamba: hali hii ni tofauti na ile chini ya mfumo au utawala wa Kidemokrasia ambapo watawala/viongozi husika aidha wanakosa ‘discretionary powers’, au wanakuwa na ‘discretionary powers’ lakini sio kwa kiasi kikubwa na hii ni kwa sababu – uongozi/utawala husika unawajibika moja kwa moja kwa wapiga kura, huku ukikabiliwa na hofu ya kuanguka au kushindwa na upinzani katika chaguzi kuu.

Jones na Olken (2005) katika utafiti wao wanaliweka hili kwa lugha ifuatayo:

“Democracies may be able to prevent the disastrous economic policies of Robert Mugabe in Zimbabwe; however, they might also have constrained the successful economic policies of Lee-Kwan Yew in Singapore or Deng Xiaoping in China”.

Zipo tafiti nyingine mbalimbali ambazo zinajadili kwa undani zaidi athari za ushindani wa kisiasa katika ukuaji uchumi. Kwa mfano, utafiti wa Besley na wenzake (2010) unaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa hupelekea sera za uchumi ambazo ni rafiki kwa biashara na uwekezaji, kwa mfano:

Punguzo la kodi kwenye biashara na uwekezaji Fulani Fulani;

Matumizi ya kodi za wananchi kwenye miundombinu wezeshi ya ukuaji uchumi na maendeleo ya watu; na

Sera za kiuchumi zinazosimamia maslahi ya nchi badala ya maslahi ya watu au makundi fulani ndani ya jamii au nchi.

Kazii za watafiti Pinto na wenzake (2005) vile vile zinaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa:
  • Unapunguza kasi ya ‘Physical capital accumulation’ (investments in fixed capital like - factories, machinery nk);

  • Unapunguza kasi ya ‘Labour mobilization’ (matayarisho/maandalizi ya nguvu kazi kutumika katika shughuli za uchumi);

Pinto na watafiti wenzake (2005) pia wanaonyesha kiutafiti kwamba ushindani wa kisiasa:
  • Unaongeza kasi ya ‘human capital accumulation’ (skills, knowledge & experiences possessed by the labor force).

Watafiti wengine kwa mfano - Ricciuti (2003), Goeminne (2008), na Volkerink & Haan (2001), wote hawa wanaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa una mahusiano na masuala yafuatayo ya kiuchumi:

-Matumizi makubwa ya fedha za walipa kodi; na

-Kasi ya kubwa ya ukuaji wa Deni la taifa.

Zipo tafiti nyingine zinazoonyesha kwamba kwamba mifumo yote miwili ya utawala/uongozi – kwa maana ya - mfumo usio na ushindani wa kisiasa na mfumo wenye ushindani wa kisiasa, yote ina mchango au uwezo wa kuleta faida kwa uchumi wa taifa.

Kwa mfano, kwa upande mmoja, utafiti wa Arvate (2013) unaonyesha kwamba:

Ushindani wa kisiasa unaongeza upatikanaji wa huduma/bidhaa za huduma (local public goods), kama vile ongezeko kubwa la uandikishwaji wa wanafunzi mashuleni (student enrolments), chanjo za bure kwa watoto nk;

Kwa upande mwingine utafiti wa Dash and Mukherjee (2015), uliotumia njia ya ‘case study’ nchini India, unaonyesha kwamba:

Uwepo wa utawala wa muda mrefu wa chama kimoja cha siasa, sambamba na ushindani dhaifu wa kisiasa, yote haya yana athari chanya kwa maendeleo ya wananchi. Dash & Mukherjee (2015) wanatumia “Human Development Index” (HDI) kama kipimo cha kuthibitisha matokeo ya utafiti wao.

Kufikia hapa tunaweza kuhitimisha sehemu ya kwanza kama ifuatavyo:

Tafiti kupitia wanazuoni mbalimbali zinatuonyesha kwamba ‘systematically’, mfumo wa ushindani wa kisiasa na mfumo usio na ushindani wa kisiasa), zote zina athari kwa ukuaji wa uchumi ingawa athari hizi zinaweza kuwa pande zote – kwa maana yaathari chanya (positive impact on the economy) au athari hasi (negative impact on the economy).

Katika sehemu inayofuata (sehemu ya Pili0, tunajali uhusiano uliopo baina ya ‘demokrasia’ na Vyama vya siasa’.
 
SEHEMU YA PILI

Katika sehemu ya kwanza ya mjadala wetu, hatukupata nafasi ya kujadili kwa undani dhana ya ‘demokrasia’ na kuihusisha na dhana ya ‘uchumi’. Badala yake, tulijikita zaidi kujadili uhusiano baina ya ‘ukuaji wa uchumi na ushindani wa kisiasa’. Lakini kama tutakavyoona katika sehemu ya tatu ya mjadala wetu, hali imechangiwa zaidi na uhalisia kwamba kama dhana, ‘demokrasia’ na ‘vyama vyama vya siasa’, hizi ni dhana mbili tofauti na zinazojitegemea in ‘theory’. Lakini kabla ya kujadili hilo katika sehemu ya tatu, katika sehemu hii ya pili tutajadili kwanza uhusiano uliopo baina ya dhana za ‘demokrasia’ na ‘uchumi’.

Mjadala kuhusu aina ya uhusiano uliopo baina ya - “demokrasia na ukuaji wa uchumi” ni mjadala ambao umeendelea kuwepo kwa karne nyingi, hasa kuanzia enzi za mijadala mikali baina ya wanafalsafa wakubwa duniani - Plato & Aristotle. Hadi leo mjadala unaendelea kuhoji juu ya mfumo sahihi wa utawala (demokrasia au autokrasia) ambao unaweza kuleta faida zaidi za kisiasa na kiuchumi kwa nchi/taifa. Hata hivyo, licha ya uwepo wa swali hili kwa karne nyingi, watafiti bado hawajafikia muafaka kwamba – mfumo wa ‘ki-demokrasia’ (in and of itself) unaleta faida zaidi kiuchumi kuliko mfumo wa ‘ki-autokrasia’.

Kwa kipindi kirefu watafiti mbalimbali wameendeleza juhudi zao kupata majibu kwa swali hili muhimu kupitia mbinu mbalimbali za kitafiti.

Kwa upande mmoja:

Zipo tafiti zinazo tegemea on – ‘cross-country comparisons’. Tafiti hizi zina hoji ‘umuhimu wa Demokrasia kwa ukuaji wa uchumi. Kwa mfano, kazi za watafiti - Sirowy & Inkeles 1990, Przeworski & Limongi 1993, Helliwell 1994, Barro 1996, Tavares & Wacziarg 2001.

Kwa upande mwingine:

Zipo tafiti za karibuni zaidi, ambazo zinategemea on ‘panel data’. Tafiti hizi zinalalia zaidi au zinaunga mkono nadharia (theory) kwamba kwa kiasi fulani, mfumo wa demokrasia una athari kwa ukuaji wa uchumi. Kwa mfano,kazi za watafiti - Rodrik & Wacziarg 2005, Papaioannuo & Siourounis 2008, Persson & Tabellini 2009, na Acemoglu 2014.

Kufuatia kumalizika kwa vita baridi duniani (Cold War), lakini hasa kufuatia kuangushwa kwa ukuta wa Berlin na kusambaratika kwa lililokuwa taifa la KISOVIETI (USSR), zilifanyika tafiti kubwa zilizolenga nchi zaidi ya arobaini (40) duniani. Nchi zilizolengwa kitafiti ni zile ambazo zilikumbwa na wimbi la mageuzi ya demokrasia kufuatia kumalizika kwa vita vya baridi (cold war), katika kipindi cha miaka ya 1980s- 1990s. Tafiti hizi zinaonyesha kwamba nchi zilizopitia mabadiliko ya kidemokrasia zili ‘experience’ - ‘average annual per capita growth rate’ ya karibia 0.005%. Matokeo haya (kitafiti) yanaonyesha kwamba, kitakwimu (statistically), ukuaji wa uchumi baada ya wimbi husika ni mkubwa kuliko kipindi cha awali (kabla ya mageuzi ya kidemokrasia), japo kwa tofauti ndogo.

Kwa kutazama haraka haraka ni rahisi kuhitimisha kwamba Demokrasia ina athari chanya kwa ukuaji wa uchumi wa taifa. Lakini wapo watafiti ambao wamemua kulitafiti kwa kina zaidi suala hili kupata ushahidi juu ya mahusiano ‘chanya’ baina ya Demokrasia na ukuaji uchumi. Juhudi hizi za kitafiti zimebaini kwamba “endogeneity factors” zinaweza kuwa kazini kuelezea na kuonyesha uwepo wa uhusiano chanya. Hivyo kwa kuzingatia “endogeneity”, watafiti (kwa mfano O'Donnell 1973, Linz 1978, Cavarozzi 1992, Remmer 1993, Gasiorowski 1995, Haggard & Kaufmann 1995), wanajadili kwamba ‘msukosuko wa uchumi’ (economic crisis) ndio chanzo au sababu ya mageuzi mengi ya kidemokrasia.

Maana ya tifiti hizi (rejea hapo juu) ni kwamba - lower & negative’ GDP growth rate kabla ya mageuzi ya kidemokrasia inaweza kuwa ni ishara kwamba mwenendo mbaya wa kiuchumi (‘poor economic performance’) ndani ya nchi husika ilisukuma au ilichochea kuanguka kwa mfumo/utawala wa ‘autokrasia’ au wa chama kimoja cha siasa. Kwa mfano, watafiti wanajadili kwa kina suala la mtikisiko uliotokana na kupaa kwa bei ya mafuta duniani (Oil shocks) miaka ya 1970s. Pia wanajadili kuongezeka kwa mikopo ya kutoka nchi tajiri duniani kwenda nchi maskini (international lending), na vile vile migogoro ya madeni katika nchi maskini (the debt crises in poor countries), pia kama ni chanzo au sababu ya wimbi la mabadiliko ya kidemokrasia katika nchi husika.

Tukirejea matokeo ya utafiti wa hapo juu (rejea utafiti wa nchi zaidi ya ‘40’ hapo juu), watafiti wanatuonyesha kwamba uhusiano chanya uliopo baina ya ‘demokrasia’ na ‘ukuaji wa uchumi’ unaweza akisi/reflect kwamba aidha:

Demokrasia inasababisha uchumi kukua zaidi. Hii hoja pia leo inaungwa mkono na tafiti nyingi duniani; au:

Mgogoro wa kiuchumi unasababisha kuibuka kwa tawala za kidemokrasia. Hii hoja pia leo inaendelewa kujadiliwa kwa kina in ‘political science research circles); au:

Kwa kiasi au kiwango fulani, masuala yote mawili hapo juu.

Pamoja na ukweli kwamba kutenganisha hii ‘causality’ baina ya Demokrasia na ukuaji uchumi ni kazi nzito, watafiti wanahimiza juu ya muhimu wa kuendelea kutafiti na kutafuta uelewa zaidi juu ya athari ya kweli ya demokrasia kwa ukuaji wa uchumi.

Kufuatia wito huu, taasisi maarufu ya utafiti nchini Marekani inayojulikana kama – “The Brookings Institute” imelenga kutegua kitendawili cha ‘endogeneity’ tulichokijadili awali.

Lengoni kuchunguza kwa kina zaidi nchi zilizopitia wimbo la mageuzi kufuatia kumalizika kwa vita baridi (old war) kama tulivyogusia awali. Utafiti wa ‘Brookings’ umetumia ‘methodology’ ya ‘survey’ inayojumuisha watafiti, wataalam na wanazuoni wa demokrasia zaidi ya mia moja na hamsini (150) kutoka taasisi na mataifa mbalimbali duniani. Swali muhimu la utafiti linalenga kubaini - ‘the underlying forces’ zilizopelekea ujio wa demokrasia katika nchi husika. Utafiti wa ‘Brookings Institute’ umegawanya mageuzi ya kidemokrasia katika makundi makuu mawili kama ifuatavyo:

KWANZA - Mageuzi ya kidemokrasia yanayo sababishwa na mgogoro wa kiuchumi. Hizi wanaziita “endogenous factors”.

PILI - Mageuzi ya kidemokrasia ambayo yapo ‘exogenous’. Exogeneous factors husika ni pamoja na kufariki au kuondoka madarakani kwa ‘autocratic president or leader’ wa nchi husika, lakini pia factors nyingine zinavyohusiana na politics & institutions ndani ya nchi husika.

Matokeo ya Utafiti wa BROOKINGS INSTITUTE – ni kama ifuatavyo:

Kwenye kundi la kwanza i.e endogenous factors:
  • Utafiti wa Brookings Institute unaonyesha kwamba – demokrasia haisababishi ukuaji wa uchumi. Watafiti wanajadili kwamba jamii za kidemokrasia ambazo hazipo ‘contaminated’ (hazijachafuliwa) na ‘endogeneity concerns’ hazina athari kwa ukuaji wa uchumi. Watafiti wanaenda mbali zaidi kuonyesha kwamba, kitakwimu (STATISTICALLY), kasi ya ukuaji uchumi ‘kabla’ na ‘baada’ ya mageuzi ya kidemokrasia katika nchi hizi ni sawa.
Kwenye kundi la pili i.e exogenous factors:
  • Utafiti wa Brookings Institute unaonyesha kwamba athari za demokrasia kwa ukuaji wa uchumi zinaendeshwa na ‘endogenous democratizations’. Kwa maana nyingine – uhusiano chanya ambao umekuwa ukihusishwa baina ya ‘Demokrasia’ na ‘Ukuaji wa uchumi’ katika mataifa mbalimbali, uhusiano huu unaendeshwa zaidi au unatokana na makosa/mapungufu ya kitafiti kuhusisha ‘endogenous democratic transitions’ katika juhudi watafiti kukisia athari za mfumo wa utawala/kisiasa kwenye ‘performance’ ya uchumi wa nchi. Brookings institute wanahitimisha kwa kujadili kwamba tabia hii katika tafiti inaleta au inajenga picha isiyo sahihi kwamba - ‘demokrasia inasababisha ukuaji wa uchumi’.
Baada ya kuangalia uhusiano uliopo baina ya Demokrasia na Ukuaji wa Uchumi, sehemu inayofuata (sehemu ya tatu) inajadili uhusuano baina ya ‘Vyama Vya siasa na Demokrasia’.


SEHEMU YA TATU

Kwa ujumla wake hoja kwamba “Vyama vya Siasa ni NGUZO muhimu kwa Demokrasia” ni hoja inayokubalika sio tu miongoni mwa wanazuoni wengi, bali pia watunga sera (policy makers) mbalimbali wenye jukumu muhimu la kulea na kukuza demokrasia katika nchi mbalimbali duniani. Na hii sio tu katika changa kidemokrasia, bali pia hata katika nchi zenye Demokrasia iliyokomaa.

Mwaka 1942, mwanazuoni mmoja wa masuala ya siasa, “Elmer Schattschneider” alipata kutamka maneno yafuatayo:

[“The political parties created democracy, and modern democracy is unthinkable save in terms of the political parties”.]

Karne kadhaa zilizopita kipindi kile vyama vya siasa vinaibuka kwa mara ya kwanza katika mataifa ya Magharibi, jamii katika mataifa haya hayakuchukulia ‘vyama vya siasa’ kwamba vitu vya lazima, vitu muhimu, vitu visivyokwepeka au vitu vya kutamanisha. Katika dunia ya leo, ikiwa ni karibia karne mbili baadae, hali hii ni tofauti kwa maana ya kwamba – katika dunia ya leo, vyama vya siasa vinachukuliwa kama ndio ‘nguzo kuu’ na ‘mzizi’ wa demokrasia katika mataifa yote, yale yaliyokomaa kidemokrasia, lakini vile vile hata yale yenye demokrasia changa na yale yasiyo ya kidemokrasia. Kufuatia umuhimu huu, leo hii vyama vya siasa vinatazamwa kama ‘a sina qua non’ (an essential condition or absolutely necessary) for the arrangement of ‘modern democratic polity’ na pia ‘for the expression of political pluralism’.

Kwa ujumla wake, kuna muafaka miongoni mwa watafiti juu ya hili. Lakini licha ya muafaka husika, yapo baadhi ya maeneo mahususi ambayo bado hayana muafaka; eneo muhimu likiwa ni kuhusu – utendaji kazi (Performance) ya Vyama vya Siasa. Watafiti wengi wanajadli kwamba vyama vya siasa - kama TAASISI ZA KISIASA, vinazidi kutetereka. Kwa mfano, mtafiti Schmitter, (2001) anajadili kwamba – ‘Political Parties are not what they once were’. Schmitter anajadili kwa kuvipa vyama vya siasa sura kuu tatu kama ifuatavyo:

(i) Vehicles of representations.

(ii) Instruments of mobilization.

(iii) Channels of interest articulation and aggregation.

Pia yapo maeneo juu ya ‘performance’ ya vyama vya siasa ambayo wanazuoni wamefikia muafaka. Muafaka muhimu ni kwamba - vyama vya siasa vinaendelea kuwa na umuhimu mkubwa katika masuala makuu mawili:

i) Control over candidates recruitment.

ii) Organization of parliament and government.

Linapokuja suala la shughuli (functions) za vyama vyama vya siasa, watafiti wanazitenganisha maeneo makuu mawili:

Upande wa kwanza ni - ‘representative functions’.

Upande wa pili ni - “procedural and institutional functions”.

Utafiti wa Bartolini & Mair –[ “Challenges to contemporary political parties” (2001)], unaliangalia suala hili kwa undani zaidi. Watafiti hawa wanajadili kwamba - ingawa inawezekana kwamba ‘representative functions’ za vyama vya siasa inaendelea kudumaa na kutetereka, lakini the ‘procedural role’ ya vyama vya siasa sio tu bado ipo imara, bali pia inaweza kuwa inazidi kuimarika tofauti na kipindi cha nyuma. Bartolini & Mair wanajadili suala hili kwa sura ya ‘Paradox’, kwamba:

Kwa upande mmoja:

Pamoja na kwamba vyama vya siasa vinaendelea kuaminiwa kama taasisi muhimu/taasisi za lazima/taasisi zisizokwepeka katika kutumikia jukumu lake la ‘representative democracy’ (demokrasia wakilishi);

Kwa upande mwingine:

Vyama vya siasa pia vinaonekana kuendelea kupoteza uwezo wa kutimiza kikamilifu jukumu lake la ‘representative democracy’, jukumu ambalo watafiti wanajadili kwamba ni la muhimu sana kwa afya na utendaji kazi wa demokrasia katika vyama, jamii na taifa kwa ujumla.

Mtazamo huu unatoa ishara ya uwepo wa ‘incompatibility’ (kutoendana/kugongana/kupishana) baina ya mapendekezo makuu mawili yafuatayo:

Upande mmoja – Vyama vya siasa ni taasisi za lazima for ‘Representative Democracy’

Upande wa pili – Katika kutimiza jukumu muhimu la ‘representative democracy’, utendaji kazi au ‘performance’ ya vyama vya siasa katika utimizaji wa jukumu hili unazidi kudorora na kutetereka.

Suala hili lina – ‘reflect’muendelezo wa mabadiliko ya kifikra na kimtazamo katika dunia ya leo, juu ya ‘vyama vya siasa’, kama ‘dhana’, kwa maana ya– political parties as a ‘concept’.

Sehemu inayofuata tutajadili kwa undani juu ya ‘Vyama vya siasa’ vya awali (karne ya kumi na tisa).

Vyama Vya Siasa vya Awali:

Kipindi kile (karne ya kumi na tisa/19th Century) wakati vyama vya Siasa vilipokuwa vinazaliwa kwa mara ya kwanza barani ulaya, vyama husika vilianza kama ‘Voluntary Associations’ (kujitolea au hiyari). Kwa maana nyingine, leo hii ambapo - uelewa, imani na mtazamo juu ya vyama vya siasa kwamba - ni taasisi muhimu, taasisi za lazima na taasisi zisizokwepeka kwa ajili ya kuhudumia ‘demokrasia’, imani, uelewa na mtazamo huu haukuwepo kipindi kile vyama vya siasa vinazaliwa/ibuka kwa mara ya kwanza duniani.

Vyama vya siasa kama dhana ilizaliwa peke yake, kabla hata dhana ya demokrasia haijaibuka. Udugu na uhusiano tunao uona leo hii baina ya dhana ya ‘vyama vya siasa’ na dhana ya ‘demokrasia’, uliojitokeza na kuja kujengwa baadae sana. Kupitia utafiti wake Van Biesen, (2004) – [“Political parties as public utilities”], analisema hili kwa maneno kwamba:

“Matukio ya hivi karibuni katika anga ya demokrasia nchi za ulaya kusini na ulaya mashariki ya kuvipatia vyama vya siasa ‘previledge position in legal and constitutional terms’…, ambapo serikali imekuwa ni sehemu kubwa ya maamuzi juu ya ruzuku za vyama pamoja na udhibiti wa shughuli ya vyama, yote haya ni masuala mapya katika muktadha wa demokrasia ya kiliberali”.

Hii ndio sababu ya msingi kwanini ndani ya ‘literature’ juu ya ‘Democracy Theory, lipo jambo moja la kustaajabisha kidogo. Jambo hilo ni kwamba – ‘Democracy Theory’ inazungumzia vyama vya siasa kwa juu juu sana; Isitoshe, ndani ya ‘literature’ juu ya ‘democratic theory’, vyama vya siasa vinatazamwa au vinaangaliwa kama obstacle (kizuizi) kwa ‘demokrasia’. Kwa maana nyingine:

Pamoja na kwamba leo hii dhana mbili muhimu – dhana ya ‘Vyama vya Siasa’ na dhana ya ‘Demokrasia’ zinatazamwa na kuchukuliwa kama ni vitu vinavyotegemeana na visivyoweza tenganishwa, ‘literature' juu ya ‘democracy theory’ na literature juu ya ‘political parties’, zimeendelea kufuata njia.

Mwanazuoni Bryce (1921) - [‘Modern Democracies’], anajadili hili kwamba – “hakuna mtu aliyeweza kuonyesha jinsi gani ‘representative government’ inaweza kufanya kazi”.

Pamoja na uwepo wa muafaka miongoni mwa watafiti kuhusu ‘performance’ ya vyama vya siasa, yapo baadhi ya maeneo ambayo wana tofauti kubwa kimtazamo, hasa kuhusiana na maana ya dhana ya ‘Demokrasia’, na nafasi ya Vyama vya Siasa katika Demokrasia.

Wanazuoni wengi wamekuwa wakihoji the ‘value’ (thamani) ya demokrasia na jinsi gani demokrasia inapaswa kufanya kazi. Kama tulivyoona awali, kinachosukuma baadhi ya wanazuoni kuhoji hili ni kutokana na kukatishwa tamaa juu ya jinsi gani ‘perfornance’ ya vyama vya siasa imeendelea kuzorota. Mbali ya hili, katika mataifa mbalimbali yanayofuata na kutekeleza mfumo wa ‘Demokrasia ya Vyama’, matukio yafuyatayo yamekuwa yakijitokeza:
  • Ongezeko kubwa la wananchi wanaojitenga/punguza ushiriki/interest juu ya masuala ya Siasa za Vyama;
Ongezeko kubwa la Wananchi wasioridhishwa na ‘performance’ ya vyama vya siasa;

Kasi kubwa ya wananchi kupunguza imani zao kwa viongozi/wanasiasa; na pia

Suala la kudhoofika kwa ‘representational and governmental roles ya vyama vya siasa, hasa kutokana na matatizo yanayohusiana na accountability, responsiveness and legitimacy.

Kufikia hapa tunaweza hitimisha kwamba:

Iwapo kuna ukweli kwamba ‘representative democracy’ inahitaji uwepo wa vyama vya siasa huku vyama vya siasa vikiendelea kupoteza uwezo wa kufanya kazi kama mawakala wa uwakilishi (‘agents of representation’), basi ni dhahiri kuwa hali hili ina athari kubwa ‘for the nature of democracy’. Njia pekee ‘to address this fundamental tension’ baina ya - kwa upande mmoja - umuhimu wa vyama vya siasa na kwa upande mwingine - kuendelea kutetereka kwa uwezo wa vyama vya siasa kufanya kazi zake katika ‘modern democracy’, ni kuangalia kwa undani ‘theories of democracy’. Kwa kufanya hivyo, tutapata mwanga na uelewa zaidi juu ya nafasi ya vyama vya siasa, hasa ‘in contemporary democracy’.

Tunajadili hilo katika sehemu inayofuata.

Lakini kabla hatujaendelea ni muhimu tukasisitiza mambo matatu yafuatayo:

Kwanza - Chama kama taasisi ya kisiasa ni dhana ngeni. Dhana za - ‘Chama cha siasa’ na ‘demokrasia’, hizi dhana mbili hazikuzaliwa pamoja siku moja. Badala yake, zilizaliwa katika nyakazi tofauti, huku ‘theory’ ya kila mmoja iki – ‘grow’ na kuendelea kwa kujitegemea.

Pili - Kipindi kile vyama vya siasa vya awali vinazaliwa na kuibuka kwa mara ya kwanza duniani (miaka ya 1800s), jamii husika hazikuvipokea vyama vya siasa kama ni taasisi za lazima au taasisi zinazohitajika, au taasisi zisizokwepeka au taasisi zinazotamainisha uwepo wake. Sana sana wakati vyama vya siasa vinaibuka kwa mara ya kwanza kule mataifa ya magharibi, vyama hivi vilionekana kama ‘threat to general interest’, kwani vilifunika interests of ‘individual’.

Tatu, na muhimu ni kwamba - kimsingi, uwepo au ujio wa vyama vya siasa sio tu ulionekana ‘incompatible’ (kwa maana yakutoendana/kugongana/kupishana) na ‘Radical Democratic Tradition’ - ‘inspired’ na Jean Jacques Rousseau, lakini vile vile ‘Liberal Democratic Tradition’ - inspired na John Locke. Tangia kipindi hicho, imeendelea kuwa vigumu kuoanisha Falsafa hizi mbili (falsafa za Rousseau na Locke) na ‘taasisi za kisiasa’ (partisan institutions). Sababu kubwa ni kama tulivyogusia awali kwamba – vyama kama ‘taasisi za kisiasa’ sio tu kwamba zinafukia ‘individual interests’ ndani ya jamii, lakini pia uwepo wa ‘taasisi za kisiasa’ unapingana/unagongana/inapishana na ‘volonte generale’ (will of the people as a whole).

Ni muhimu tukaangalia kidogo falsafa za Jean Jacques Rousseau na John Locke zinasimamia mambo gani.

Jean Jacques Rousseau aliishi katika kipindi cha (1712 – 1778).

Historia juu ya Rousseau ina sura mbili. Rousseau anapongezwa lakini pia analaumiwa kwa kuchochea mapinduzi ya ufaransa ya mwaka 1789 – 1799. Pamoja na mengineyo, Mapinduzi haya Ufaransa yalipelekea kutokomezwa kwa utawala wa kifalme nchini Ufaransa na kupisha muundo mpya wa utawala kupitia Katiba ya ‘Jamhuri’ (Republic)’. Utawala wa aina hii unasimamia nguzo muhimu kama vile:

-Usawa

-Uhuru

-Haki ya wananchi kupiga kura nk.

Katika dunia ya leo nchi nyingi duniani zinafuata mfumo na muundo huu wa utawala – kwa maana ya- ‘Jamhuri’.

John Locke aliishi katika kipindi cha (1632 – 1704)

Kimsingi, falsafa John Locke ilihusishwa na imani kwamba – serikali zina wajibu mkubwa wa kutumikia wananchi na kulinda maisha, uhuru na mali zao. John Locke pia ‘advocated’ kupunguza nguvu za serikali katika jamii (rejea suala la ‘state vis a vis society’), na vilevile aliunga mkono ‘representative government & rule of law’.

Kufikia hapa, swali linalofuata ni - kama hali ndio hivi, je:

UHUSIANO BAINA YA VYAMA VYA SIASA NA DEMOKRASIA ULIJENGWA NA KITU GANI?
Uhusiano baina ya dhana ya ‘chama cha siasa’ na ile ya ‘demokrasia’ ulianza kujengwa kufuatia kuibuka kwa mahitaji ya ‘Mass Democracy’ (Demokrasia Ya Umma) katika nchi ulaya magharibi kipindi cha nyuma. Ndani ya jamii hizi uhusiano baina ya ‘the state’ and ‘individual citizens’ uliendelea kudhoofika na kuacha pengo kubwa. Kuibuka kwa mahitaji ya ‘Mass Democracy’ kulifanya uhusiano wa moja kwa moja (‘direct connection’) baina ya ‘state na ‘raia’ kuwa mgumu zaidi. Katika sintofahamu hii, vyama vya siasa vikaonekana kuleta suluhisho. Kwa mara ya kwanza, VYAMA VYA SIASA ‘vikahalishwa’ rasmi kuwa taasisi kiungo (‘intermediary institutions’) baina ya ‘raia mmoja mmoja na serikali’ (state).

Awali tuliona kwamba kipindi kile ‘democratic theory’ ilipokuwa inaibuka kwa mara ya kwanza, ‘democracy theory’ ilivitazama Vyama vya siasa kama kizuizi (obstacles) vya demokrasia. Lakini kama tutakavyoona baadae, KIMSINGI, reflections za wanazuoni mbalimbali juu ya vyama vya siasa vya awali (miaka ya 1800s), hazikuwa zinapinga uhalali wa demokrasia ya vyama vya siasa (‘democratic legitimacy’). Badala yake, wasiwasi miongoni mwa wanazuoni wengi ulikuwa ni juu ya ukosefu wa demokrasia ndani ya vyama vya siasa, hasa juu mienendo inayominya demokrasia ndani ya vyama, pamoja na mienendo iliyoendekeza na kujenga mifumo ya oligachia (‘oligarchy systems)’. Maana rahisi ya neno “Oligarchy” ni - Kikundi cha watu wachache kuhodhi madaraka ya chama, hasa ndani ya vyama vya umma au ‘Mass Political Parties’. Tutatizama hili kwa undani baadae kidogo.

Moja ya tafiti kubwa zilizofanyika juu ya suala hili ni pamoja na ule uliofanywa na Mwanazuoni ‘Mosei Ostrogorski’ (1902) – [“Democracy and Organization of Political Parties”[. Utafiti wa Ostrogorski uliangazia zaidi vyama vya siasa vilivyokuwepo katika nchi za Marekani ya kaskazini (North America) na Uingereza. Ostrogorski anajadili kwamba - ‘organized political parties’ viliibuka ili kuhudumia mahitaji ya demokrasia ya umma (mass democracy). Ostrogorski anaongeza na kuonya kwamba - ‘party organization in itself is harmful’. Onyo la Ostrogorski lilikuja ‘dominate’ fikra na mitazamo juu vyama vya siasa na Demokrasia kuelekea karne ya ishirini.

Katika utafiti wake, Ostrogorski anakubali kwamba ndani ya jamii ya kidemokrasia, vyama vya siasa vilifanikiwa kuhakikisha usimamizi na utendaji mzuri wa kazi za kila siku wa Serikali. Ostrogorski anasisitiza kwamba, tofauti na kipindi cha awali, mafanikio ya vyama vya siasa juu ya usimamizi na utendaji mzuri wa kazi wa serikali yalikuwa yakiongezeka siku hadi siku. Lakini licha ya mafanikio hayo, Ostrogorski bado hakuwa na matumaini au imani na vyama vya siasa kwa asilimia mia moja.

Ostrogorski anajadili hilo kwamba – pamoja na mazuri yake, vyama vya siasa vilishindwa kusimamia nguvu za raia ipasavyo (upholding power of citizen). Kwa maana nyingine, sambamba na kufaninikiwa ‘in their procedural and institutional roles’, Ostrogorski anasema kwamba vyama vya siasa vilifeli ‘in their representational functions’. Anatoa sababu za kufeli huko kwamba; nayo ni kwamba – ‘party organization’ inafifisha ‘individuality’ na kupelekea ‘individual autonomy’ kutoweka. Ostrogorski anaongeza kwamba – ‘Party organization’ inafuta ‘the individual’ na badala yake inajenga ‘loyalty’ (uaminifu) kwa chama na falsafa zake. Anaongeza kwamba - hali hii ina athari kubwa, hasa - kufuta uhuru wa mawazo, individual initiative and political conscience.

Ostrogorski anakuja na pendekezo la kutatua hali hii. Nalo ni kwamba – ipo haja ya kutengeneza “a polity” isiyokuwa na vyama vya siasa vya kudumu. Badala ya uwepo wa vyama vya siasa vya kudumu, Ostrogorski anapendekeza viwepo vyama vya muda au vya kipindi kifupi kwa ajili ya kukabiliana na changamoto zilizopo katika wakati husika; mara tu baada ya changamoto husika kupatiwa ufumbuzi au malengo husika kufikiwa, vyama vya siasa ‘as a party organizations’ zivunjwe. Ostrogorski anasema – kwa njia hii, uaminifu (loyalty) wowote kwa chama cha siasa unakuwa sio wa kudumu au unakuwa ni uaminifu wenye kikomo.

Kufuatia mapendekezo haya, baadae walijitokeza watafiti wengine walio-hoji na kujadili “practicality” ya nadharia (‘theory’) ya Ostrogorski’. Wanazuoni hawa ni pamoja na:

Katz (1997) – “Democracy and Elections”; Raney (1962) – “The doctrine of responsible party government: Its origin and present state”; na

Robert Michels (1962) – “Political Parties: A Sociological Study of the Oligarchical Tendencies of Modern Democracies.

Robert Michels (1962) alikuwa ni mwanafunzi juu ya uzoefu wa ujamaa wa kiitaliano na kijerumani (German and Italy Socialist experience). Sehemu kubwa ya utafiti wake ilikuwa ‘influenced’ na utafiti wa awali wa mtafiti ‘Cassineli’ (1953) – [“The Law of Oligarchy”]. Ushawishi wa Cassineli unatokana na mijadala yake kama vile:

[“The nature of any organization is such that leadership activities are free from control and can never be fully held accountable by those who hold subsidiary positions in the organization”.]

Hoja ya msingi kutoka kwa Cassineli ni kwamba:

Kwa jinsi jamii inavyozidi kukua/kuendelea, ndivyo inavyozidi kuwa ‘complex’; na katika ‘complex societies and mass democracy’, organizations ni kitu kisicho kwepeka; na kwa jinsi hizi organizations zinavyozidi kukua (experience growth) na kufikia ukubwa wa kaisi fulani na kuanza kuwa ‘complex’, hali hii inazalisha viongozi wanao tengeneza wafuasi; na baadae viongozi husika wanakuja kuwa ‘dominate’ wafuasi husika; hii hali inapelekea athari au madhara yasiyotarajiwa, madhara hayo ni “oligarchization’’, kwa maana ya - kuzaliwa au kuibuka kwa kundi dogo la watu wachache linalo hodhi madaraka na mamlaka.

Cassineli anaendelea kusema kwamba oligarchanization ni matokeo ya mechanisms mbili:

Technical mechanisms.

Psychological mechanisms.

Anasisitiza kwamba ‘technical’ mechanisms ni muhimu zaidi, kwa vile inahusisha specialization, division of labor, & technical abilities za viongozi wa organizations husika.

Ni kupitia kazi hii ya Cassineli, Robert Michels (1962) baadae akaja na utafiti wake ulioasisi ‘Iron law of Oligarchy’; Theory ya Robert Michels (1962) inasema kwamba:

‘Oligarchy or rule by elite is inevitable as an "iron law" within any democratic organization as part of the "tactical and technical necessities" of organization’.

Msingi wa hoja ya Michels hapa ni kwamba – ‘power of the elites rests upon its organizational abilities’. Anasisitiza kwamba kila organization inazalisha ‘elites’ wake, na kwamba utendaji wa kazi katika hili unakaribiana na ‘law of nature’. Kwa mujibu wa Michels:

“It is organizations that give birth to the domination of the elected over the electors, of the mandatories over the mandators, of the delegates over the delegators. Who says organization says oligarchy”.

Msisitizo wa Michels ni pamoja na kwamba - katika kila ‘organization’, the issue of ‘leadership’ is unavoidable; it becomes a necessity.

Katika utafiti wake juu ya vyama vya kijamaa na vyama vya wafanyakazi, hasa chama cha kijamaa nchini Ujerumani, Michels (1962) anadhihirisha matokeo ya utafiti wa Casinneli (1953). Akitumia chama cha Kijamaa cha Ujerumani kama ‘case study’, Michels anaonyesha kwamba hata ‘party organizations’ zikiwa na mfumo na utaratibu wenye kusimamia na kutekeleza ‘demokrasia ya ndani’, bado mwisho wa siku vyama hivi haviwezi kuzuia kuja kuwa ‘dominated & controlled by big unaccountable elite’. Kwa maana nyingine - ‘iron law’ must apply kwa vyama vyote vya siasa bila kujalisha kama vyama husika vina vinafuata/vinatekeleza au havifuati/havitekelezi demokrasia ya ndani ya vyama.

Mtafiti Michels (1962) anaongezea suala muhimu pia kwamba – ‘iron law’ ni ‘valid & relevant’ sio tu kwa ‘political organizations’, bali ni pia - to any large and complex organizations, hata nje ya masuala ya kisiasa.

Nadharia (theory) ya Michels (1062) inaweza kufanya mtu akahitimisha kwamba - Michels ana halalisha ukiukwaji wa kanuni na taratibu za demokrasia ndani ya vyama vya siasa. Lakini hatupaswi kujiingiza kwenye huo mjadala, angalau kwa sasa. Katika mjadala wetu, suala tunalopaswa kuzingatia hapa ni kutambua umuhimu/relevance ya utafiti wa Robert Michels katika juhudi zetu za kuendelea kutafuta majibu kwa maswali muhimu mbele yetu, kwa mfano, Je:

  • Vyama vya siasa ni vizuizi vya Demokrasia?
Kupitia utafiti wake, Robert Michels hatupatii jibu la moja kwa moja kwa swali hili. Tunachopaswa kuelewa, hivyo kuwa hitimisho muhimu kwetu hapa ni kwamba - iwapo ‘internal’ party democracy/demokrasia ya ndani ya chama cha siasa - ‘is a pre-condition’ ya ufanikishaji wa demokrasia katika taifa, au iwapo ‘iron law of oligarchy’ ni muhimu kwa – ‘the organization of the state’ (serikali), basi mapendekezo ya Michels ni kwamba – tunapaswa kuwa ‘pessimistic’(kuangalia kwa mashaka) juu ya uwezekano wa ‘ultimate realization of democracy’ katika taifa – yani, uwezekano wa nchi/taifa kufanikisha au kutekeleza bila mapugufu dhana ya demokrasia.

Tunamalizia sehemu ya tatu ya mjadala wetu kwa kuangalia utafiti wa mwanazuoni mwingine maarufu na mwenye ushawishi mkubwa katika massuala ya demokrasia na vyama, mwanazuoni Max Webber.

Max Webber anajulikana kwa mchango wake mkubwa katika eneo hili. Kwa mfano, utafiti wake: “Politics as a vocation” (1918), anajadili kwamba – vyama vya siasa vya awali viliundwa kwa lengo la kutumikia matamanio na matakwa ya makundi ya watu mashuhuri katika jamii (elites). Anaendelea kusema kwamba kilicho pelekea kuibuka kwa aina mpya ya vyama vya siasa, kwa maana yavyama vyenye ‘strong & permanent organization’ ilikuwa ni ujio wa ‘mass democracy’(demokrasia ya umma). Anaongeza kwamba aina hii mpya ya vyama vya siasa ndio iliyokuja kujenga na kuimarisha - the ‘psychology of followers’ & ‘charismatic authority of party leader’, na baadae byama hivi kuja kuwa ‘dominated with a political elite or single leader’.

Webber anatumia historia ya vyama vya siasa nchini Uingereza kama nguzo muhimu ya utafiti wake, na kama tulivyokwisha ona anajadili kwamba - awali, vyama vya siasa viliundwa kwa kusudio la kukidhi maslahi ya watu wachache, ambao anawaita – ‘the notables in the society’, vikiwa na sura na mfumo wa ‘ki - aristokrasia’ (sio ki - demokrasia). Webber anajenga hoja kwamba – ‘originally’, vyama vya siasa kama ‘organized permanent associations’ havikuwepo; badala yake vyama hivi vilikuwa ‘active’ katika vipindi vya chaguzi tu. Anaendeleo kujadili kwamba, mshikamano ndani ya vyama vya siasa ulijengwa kwenye ngazi ya ‘parliamentary delegates’, huku kazi au shughuli za ‘delegates’ husika zikiishia kwenye makao makuu ya chama pekee kwa sababy hawa hawakuwa wanafanya kazi kwa wananchi kama ilivyo zoeleka chini ya mfumo wa kibunge ndani ya demokrasia za leo. Kwa mujibu wa Webber - siasa kama - ‘a profession’ ya kulipwa mshahara na posho, haikuwepo:

“Politics was formally and by far, predominantly an avocation – hobby, not a career”.

Hadi hapa tunajifunza jambo muhimu, nalo ni kwamba - ‘democratization of the franchise’kwa maana ya haki za wananchi kupiga kura au kuchagua au kuchaguliwa, halikuwepo awali wakati vyama vya siasa vinazaliwa kwa mara ya kwanza. Badala yake, ‘democratization of the franchise’ ni matokeo ya ‘modern systems of political organizations’. Katika dunia tunayoishi leo, vyama vya siasa pamoja na mifumo yake ni matokeo ya mambo makuu manne:

-Demokrasia.
-Mass franchise.
-Umuhimu wa kuhamasisha na ku-organize umma.
-Ujenzi wa dhana za dira, mshikamano na nidhamu ndani ya vyama kama taasisi za kisiasa.

Masuala haya ndio yaliyopelekea mabadiliko ambapo ukaibuka UMUHIMU WA WANASIASA KAMA FANI (‘Professional Politicians’) katika siasa za vyama.

Kwa maana nyingine, ni katika muktadha huo ndio ‘professional politicians’ – kwa maana ya wanasiasa nje ya BUNGE ndipo wanapojitokeza. Wanasiasa hawa huwa ni watumishi wa moja kwa moja wa chama, wakifanya shughuli zao kwenye makao makuu ya vyama husika vya siasa. Kwa kawaida, ‘professional politicians’take control of the party organization; Nguvu ya chama inakuwa mikononi mwao kama watumishi wa kila siku wa chama; Majukumu muhimu ya hawa professional politicians ni pamoja nay ale ya kuandaa na kutoa DIRA na MIONGOZO ya chama‘as an organization’; Pia wanajukumu kubwa ‘to keep parliamentarians in check’.

Max Webber, kupitia utafiti wake juu ya uzoefu wa siasa za vyama nchini Uingereza, analijadili hili kwamba:

[…matokeo yake ikawa ni nguvu ya chama cha siasa kuhodhiwa au kuwa mikononi mwa watu wachache, na hatimaye mikononi mwa kiongozi mmoja wa chama, huku ‘party machinery’ ikigeuka kuwa ‘oriented to the charismatic personality of the leader’. Ndani ya mfumo huu, kiongozi wa chama anachukua ‘nafasi maalum’, kwani sasa ni yeye ambae chama kama taasisi ndio kinamfuata].

Webber anaongeza kwamba:

[…ujenzi hivi vitu tunavyoviita au tulivyovizoea kama ‘vyama vya siasa’ hupelekea kuibuka kwa ‘plebiscitarian democracy’. Maana rahisi ya dhana hii ya ‘plebiscitarian democracy’ ni mfumo ambao – chama kinachagua kiongozi wake; na mara tu kiongozi husika anapochaguliwa, anakuwa na nguvu kubwa na kauli ya mwisho ndani ya chama husika cha siasa. Hali hii inapelekea bunge kubakia kama ‘rubber stamp’ au kwa maneno ya Webber:

“Parliamentarians are reduced to nothing better than well-disciplined YES MEN”.

Webber anahitimisha kwamba:

“The Plebiscitarian dictator actually stands above parliament…..; by bringing the masses behind the leader by means of the party machine, a state of affairs has been created which one might call – a dictatorship resting on the exploitation of mass emotionality.”

Ukimsoma Max Webber kwa haraka haraka ni rahisi sana kumtafsiri vibaya (‘negatively’), hasa juu ya uhusiano uliopo baina ya ‘uongozi wa kisiasa’ (political leadership) na demokrasia (democracy). Lakini kama tutakavyoona punde, kumsoma Webber kwa umakini zaidi, kunatoa tafsiri chanya.

Awali tulijadili tafiti za ‘Ostrorgosrki’ na ‘Michels’. Watafiti hawa walituonyesha kwamba – ukosefu wa demokrasia ndani ya vyama undermines (una athari) kwa mfumo wa demokrasia katika jamii nzima. Tukirudi kwenye Max Webber (utafiti ambao baadae ulikuja kuendelezwa na ‘Joseph Schumpeter’), Webber anapendekeza kwamba – ‘strong and responsible leadership is a necessity for the healthy and functioning democracy’. Sababu ya msingi hapa ni kwamba – by ‘virtue of its organizational abilities, bureaucracy inaweza ‘obtain predominant political position’ na kuwa ‘the defacto ruling group’ isiyowajibika kwa umma. Hivyo basi ‘responsible and principled leaders’ wa vyama vya siasa wanahitajika ‘to keep bureaucratic leaders in check’, na kuhakikisha kwamba ‘they take care of impartial administration and don’t engage in politics’.

Mujumuhisho ya sehemu ya TATU

Tumepitia baadhi ya most influential reflections juu ya vyama vya siasa vya awali, vilivyoibuka mwanzoni mwa karne ya ishirini (miaka ya1900). Kwa ujumla wake tumeona jinsi gani watafiti mbalimbali wametuonyesha concerns (hofu/wasiwasi) zao juu ya ‘performance’ ya vyama vya siasa, hasa - ukosefu wa demokrasia ndani ya vyama na uwajibikaji (accountability), ingawa tafsiri za watafiti kuhusu athari za haya mapungufu kwenye demokrasia zinapishana.

Mtafiti Ostrorgorski anaamini kwamba vyama vya siasa vya kudumu ni ‘harmful’, hivyo havipaswi kuwepo. Watafiti waliomfuatia baadae wanakuja na mtazamo tofauti. Wanajenga hoja kwamba - ‘vyama’ kama taasisi za kisiasa, hasa katika muktadha wa ‘mass democracy’, ni muhimu na vinapaswa kuwepo.

Tumeona kwamba kipindi cha awali wakati vyama vya siasa vilipokuwa vinazaliwa au vinaibuka kwa mara kwanza duniani, vyama hivi havikupokewa na jamii kama ni vya lazima au visivyokwepeka (inevitable), au jambo la kutamanisha (desirable). Jambo lililo sababisha vyama vya siasa kuanza kukubalika kwenye jamii ilikuwa ni ujio wa ‘mass democracy’ (demokrasia ya umma). Ni mass democracy ndio ilipelekea kukubalika kwa dhana kwamba – vyama vya siasa ni kiungo muhimu au kiungo cha lazima baina ya - ‘the individual citizens’ (raia mmoja mmoja) and the ‘state’ (na serikali).

Lakini kwa muda mrefu, appreciation juu ya mchango wa vyama vya siasa kwa demokrasia ilihusisha zaidi uwezo wa vyama vya siasa kuratibu ‘large scale democracy’. Ni baadae sana (hasa baada ya vita kuu ya pili ya dunia – baada ya mwaka 1945) ndio umuhimu au mchango wa vyama vya siasa katika jamii ukawa ‘appreciated’ kwa mapana zaidi, hasa ‘attachment’ yake kwa ‘representative democracy’ (demokrasia wakilishi).

Ni baada ya kipindi hiki ndio vyama vya siasa vikaanza kukubalika au kuonekana sio tu kama ‘key institutions’ (taasisi muhimu), lakini pia ‘necessary & positive conditions for modern democracy’. Hili lilijitokeza zaidi baada ya ‘legal codification and constitutionalization’ iliyorudisha demokrasia katika mataifa ya Ujerumani na Italia baada ya Vita Vya Pili vya Dunia. Ni katika kipindi hiki na kufuatia hili, mataifa mengi duniani yakaanza kupitia upya katiba za mataifa yao.

Na hata katika mataifa yaliyo anza kufuata mfumo wa demokrasia katika miongo ya hivi karibuni, hasa kufuatia kusambaratika kwa iliyokuwa nchi ya Kisovieti (USSR) na baadae kuanguka kwa ukuta wa Berlin, kuanzishwa kwa taratibu za mfumo wa demokrasia katika mataifa haya (kwa mfano – nchi za ulaya kusini, ulaya mashariki, Afrika nk), mchakato huo ulihusisha uanzishwaji wa ‘free competition’ baina ya vyama vya siasa, pamoja na kuongezeka kwa uelewa kwamba vyama vya siasa ndio msingi wa mfumo wa kisiasa wa demokrasia.

Awali, Katiba za demokrasia za magharibi (western liberal democracies), zilipuuza vyama vya siasa kwa kipindi kirefu sana. Lakini kufuatia kumalizika kwa vita kuu ya pili ya dunia, umuhimu wa vyama vya siasa ukaanza kutambulika kwa mapana zaidi kikatiba kiasi kwamba dhana zifuatazo zimekuja kuwa ‘defined, almost exclusively in terms of political parties:

Pluralism
Political participation
Competition

Pamoja na kwamba vyama vya siasa vya awali havikuwa na uhusiano wowote na dhana ya demokrasia, leo hii vyama vya siasa vimeweka alama kubwa na isiyofutika ‘on democratic politics’. Wanazuoni Castles and Wilderman (1986) - “Visions and Reality of Party Government”, wana hitimisha hoja hii kwa maneno kwamba:

“20th century democracy can be best described as party democracy.”

Katika sehemu yetu ya NNE na ya mwisho, tutamalizia kwa kuhusisha sehemu tulizojadili awali na fikra za Kisiasa za Mwalimu Nyerere, kwa maana ya Nyerere’s Political Thought.
 
SEHEMU YA NNE

Pamoja na kwamba dhana ya ‘maendeleo hayana vyama’ katika muktadha wa siasa za taifa letu imekuwa ikihusishwa na Rais John Magufuli, asili ya dhana hii ni Fikra za Kisiasa za Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, kwa maana ya – “Nyerere’s Political Thought”. Hili ni muhimu kwa sababu sio tu kwamba Nyerere anaendelea kutambulika na kuheshimika kama Baba wa Taifa la Tanzania, bali pia kama “The Chief Architect of Tanganyika”, na baadae Tanzania.

Fikra za kisiasa za Mwalimu Nyerere, kwa maana ya – “Nyerere’s Political Thought” zilibebwa na nguzo kuu tatu:

  1. Usawa (Equality)
  2. Demokrasia (Democracy)
  3. Ujamaa (Socialism)
Maandiko mengi yanayomhusu Mwalimu Nyerere (yaliyoandikwa na yeye binafsi pamoja na yale yalioandikwa na wengine) – yana tuonyesha kwa urahisi kwamba tangia awali kabisa Mwalimu Nyerere alikuwa ni muumini mkubwa ‘Demokrasia’. Kwa mfano, - in “Tanganyika National Assembly Official Report” - 1st session, (28 June, 1962):

“We have got to have a little amount of faith, although I know that some members have been questioning the idea of faith. But sir, democracy is a declaration of faith in human nature, the very thing we are struggling to safeguard here, the very idea of democracy is a declaration on faith in mankind. And every enemy of democracy is some person who somewhere has no faith in human beings. He thinks he is all right, but other human beings are not all right”.

In, “Democracy and Party System (1963), Mwalimu Nyerere pia anajadili kwamba:

Democracy or government by the people is a system based on theory – on reason – and can be defended rationally. Given that man is a rational being and that all men are equals, democracy – or government by discussion among equals – is indeed the only defensible form of government.”

Mwalimu anasisitiza kwamba - maendeleo ya watu yanawezekana tu iwapo kuna uwepo wa Demokrasia, Ujamaa na Usawa wa Binadamu. Kwa mfano, in - “Freedom and Socialism” (1968):

“…Both democracy and socialism find their roots in a primary belief in human equality and the central imperative of aiding the development of man”.

Hii inadhihirisha kwamba kwa Mwalimu Nyerere, ‘Democracy was an essential Public Good’.

Pamoja na imani kubwa ya Mwalimu Nyerere juu ya Demokrasia pamoja na umuhimu wake katika ustawi na maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla, Mwalimu Nyerere alitatizwa na eneo moja. Mwalimu alitumia muda mwingi sana wa maisha yake ya awali kisiasa kuhoji na kujadili kwa kina juu ya Muktadha, Mazingira, na Mfumo sahihi wa utekelezaji wa Demokrasia ndani ya Tanganyika/Tanzania. Mwalimu alikabiliwa na changamoto kubwa ya kutatua – ‘the apparent contradiction’ baina ya - imani yake kwa Demokrasia na uhalisia kwamba yeye alikuwa ni kiongozi wa nchi/serikali inayofuata mfumo wa Chama Kimoja (‘a de-facto a single party system’).

Mara kwa mara Mwalimu Nyerere alihoji iwapo mfumo wa ushindani wa vyama vingi (‘a competitive party system’) ulikuwa ni muhimu kwa demokrasia katika muktadha wa Tanganyika/Tanzania, huku kila wakati akijitahidi kuboresha hoja na msimamo wake kwamba - hata mfumo wa Chama Kimoja unaweza kukidhi mahitaji ya Demokrasia, kwa maana ya kwamba - ‘one party dominance was compatible with democracy’.

Mwalimu alipitia kipindi kigumu sana cha mapambano ya kifikra katika jitihada zake za kuifanya dhana ya ‘Demokrasia’ iendane na mahitaji na mazingira ya Afrika’, kwa maana ya - “how to Africanize Democracy”. Katika mapambano yake haya ya ‘Kifikra’, mara kwa mara Mwalimu alikuwa akirejea kwenye mifano na uzoefu wa Demokrasia katika nchi za magharibi. Kwa mfano, Mwanazuoni J.Baker (1974) anamjadili Mwalimu:

“He established that – party labels in Britain and other western democratic countries were of little significance because Members of Parliament once elected claim to represent the interests of all their constituencies whatever their party allegiance”.

Mwalimu hakukata tamaa kwani aliamini kwamba Demokrasia ya mfumo wa chama kimoja inaweza kutekelezeka nchini Tanganyika/Tanzania. Baada ya mapambano ya muda mrefu ya kifikra juu ya suala husika, hatimaye Mwalimu Nyerere akapata sehemu ya kuanzia kutetea imani na mtazamo wake. Nayo ilikuwa ni utambuzi na uchambuzi wake (Nyerere) juu ya tofauti kubwa iliyopo kimaendeleo (pamoja na changamoto husika) baina ya mataifa machanga na huru barani afrika, yani – ‘Newly independent African States’ na mataifa ya Magharibi yaliyokomaa kidemokrasia (‘established constitutional democracies’).

Mwalimu ananukuliwa, in - “One Party Government” (1961), akisema:

[“The very success of the nationalist movement in raising the expectations of the people, the modern means of communication which put the American and the British worker in almost daily contact with the African worker, the 20th century upsurge of the ordinary man and woman – all these deprive the new African governments of those advantages of time and ignorance which alleviated the growing pains of modern society for the governments of older countries. To the demands of the common man in Africa, intensified as they are by the vivid contrast between his own lot and that of others in more developed countries, add the lack of means at the disposal of the African governments to meet these demands. The lack of men, the lack of money and above all the lack of time. To all this add the very nature of the new countries themselves. They are usually countries without natural unity. Their boundaries enclose those artificial unites carved out of Africa by grabbing colonial powers without any consideration of ethnic groups or geographical realities, so that these countries now include within their borders tribal groups, which until the coming of the European powers, have never been under one government.”]

Mara kadhaa Mwalimu Nyerere pia alienda mbali zaidi, ‘to draw a close analogy’ baina ya – ‘a wartime coalition in a constitutional democracy’ pamoja na umuhima wa kuwa na - ‘a united effort’ in Tanganyika’, nia ikiwa ni kufanikisha – ‘a stable government and rapid economic development in Tanganyika’. Kwa Mwalimu, taifa lilikabiliwa na maadui wakuu watatu:

Umaskini
Ujinga
Maradhi

Mwalimu aliamini kwamba VITA dhidi ya maadui hawa watatu ni vita vilivyo hitaji juhudi za KITAIFA sawa na juhudi za kushinda vita dhidi ‘an enemy power’. Mwalimu Nyerere ananukuliwa na Mwanazuoni Pratt (1978) akisema:

“… A coalition government in time of national emergency is not thought to be undemocratic; neither should rule by dominant nationalist movement in a newly independent African state. In such circumstances a de facto one party system is a proper and genuinely democratic response to a national crisis. It is the embodiment of a unified national will to achieve goals which are endorsed throughout the society but which would be unachievable if that community were deeply divided by political controversy”.

Mwalimu akaendelea kuhimiza juu ya umuhimu wa taifa kuwa na umoja na mshikamano badala ya mgawanyiko ili kuvishinda vita hivi. Ananukuliwa, in - ‘One Party Rule’ 1961), lakini vile vile, in - Paul Sigmund (1963), ‘The ideologies of the Developing Nations’, akisema:

“New nations like Tanzania are emerging into independence as a result of a struggle for freedom from colonialism…Once the first free government is formed, its supreme task lies ahead, the building up of the country’s economy, so as to raise the living standards of the people, to eradicate diseases, to banish ignorance and superstition. This no less than the struggle against colonialism, calls for the maximum united effort by the whole country if it is to succeed. There can be no room for difference or division…This is our time of emergency and until the war against poverty, ignorance and diseases is has been won, we should not let our unity be destroyed by a desire to follow somebody else’s book of rules”.

Mwalimu Nyerere anaendelea kujadili kwamba:

“…strong dominant parties would be likely in many African states as an immediate consequence of the unity achieved in the struggle for independence…...….

….this doesn’t mean that these countries are not democratic

….democracy does not require the presence of competing parties; it requires only the preservation of civil and political liberties which would permit the appearance of rival parties”.

Pamoja na Mwalimu Nyerere kuwa muumini wa Demokrasia, hakuamini kwamba Demokrasia hiyo ni lazima iambatane na ushindani wa vyama vingi vya siasa, hasa katika nchi iliyotoka kutawaliwa na ukoloni kwa muda mrefu. Katika makala yake, in – ‘British Weekly Tribune’, June 1960, Mwalimu Nyerere anasema:

“The notion that democracy requires the existence of an organized opposition to the government of the day is false. Democracy requires only freedom for such an opposition, not an existence of it. In the newly – independent countries it is most unlikely that there will be a two-party system for many years. The nationalist movements are going to be very powerful indeed; they will control the government and organize local development in the economic and social sphere without there being any effective challenges to them from within – and any challenge from outside will only strengthen them. Development of a one-party government will in fact be the inevitable result of both the recent history and the environmental conditions. It will be a long time before any issues arise in the new countries on which it will be possible to build a real opposition organization. This will eventually happen and it will be brought about by a split in the nationalist organization”.

Kufikia hapa, tunaweza hitimisha masuala mawili muhimu juu ya fikra za Mwalimu:

Kwanza - mbali ya kuwa na imani na demokrasia, Mwalimu Nyerere pia aliamini katika mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Tatizo kubwa kwa Mwalimu ilikuwa suala la MUDA MUAFAKA na MUKTADHA SAHIHI wa utekelezaji wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa katika nchi iliyojipatia uhuru muda sio mrefu uliopita.

Pili, tunaona kwamba tangia awali kabisa, miaka michache baada ya uhuru (early 1960s), Mwalimu Nyerere aliamini kwamba upinzani wa kweli dhidi ya TANU/CCM utatokana na TANU/CCM yenyewe/ndani ya CCM/kuvunjika kwa TANU/CCM. Ikumbukwe kwamba Mwalimu alirudia kauli hii ndani ya mfumo demokrasia ya vyama vingi mwaka 1995, kwenye mkutano mkuu wa CCM, Dodoma.

Tukiendelea kuchambua Fikra za Mwalimu Kisiasa, katika juhudi zake za maandalizi na ujenzi wa demokrasia ya chama kimoja, Nyerere anahimiza kwamba - ndani ya taifa changa na lenye changamoto kubwa kisiasa, kijamii na kiuchumi kama Tanganyika, ipo haja (japo mara moja moja) kwa Serikali kuzima kelele za watu wanaopinga juhudi za kuwaletea wananchi maendeleo. Mwalimu anasema, rejea - “Democracy and Party System” (1963), kazi ya watu wa aina hii ni:

’to disrupt the unity of the country and undermine its efforts to achieve rapid development’

Mwalimu anahimiza kwamba:

[“It is therefore the duty of the government to safeguard the unity of the country from irresponsible or vicious attempts to divide and weaken it, for without unity the fight against enemies of freedom cannot be won… the irresponsible individuals I have mentioned have neither sincerity, conviction nor any policy at all save that of self-aggrandizement. They merely employ the catch – phrases copied from the political language of older, stabler countries, in order to engage the sympathy of the unthinking for their destructive tactics. Nor are the tactics they use those of a responsible democratic opposition. In such circumstances the government must deal firmly and promptly with the trouble makers. The country cannot afford, during those vital early years of its life to treat such people with the same degree of tolerance, which may safely be allowed in a long established democracy”.]

Hapa tunaweza kuona utetezi wa Mwalimu juu ya umuhimu wa mfumo wa Demokrasia ya chama kimoja Tanzania unahusisha vitu viwili muhimu:

Kwanza - an implicit “acceptance” of a competitive party system as the normal and preferable form of democracy”, hasa pale Mwalimu anapohimiza kwamba ‘democracy requires only that it be legally possible to organize an opposition party’; na pia kwamba ‘in a time of a national crisis a single dominant party in fact reflects the democratic will of the people’.

Pili - it also involves an element of “apology”, kwamba muda na muktadha bado hauruhusu kwa Tanganyika. Kwa maana nyingine - the social and economic conditions in Tanganyika were not conducive to permit full exercise of political freedoms.

Baadae, tunaona Mwalimu Nyerere akihamishia juhudi zake kutafuta ‘a settled view’ kuhusu maana na aina ya Demokrasia katika muktadha wa Taifa changa la Tanganyika/Tanzania. Kufuatia juhudi hizi, hatimaye Mwalimu alifikia ‘a position’ ambayo iliachana na ‘the liberal view of constitutional democracy’. Kuhusiana na aina ya demokrasia inayoweza endana na mazingira ya kiafrika, Mwalimu anasema:

“…the ideal democratic society is the small, closely integrated, self-governing community’….

…the sovereign body can be an assembly of all citizens, and the deep divisions would not develop to distract men from pursuing the good of all…

…the essence of democracy is government by discussion amongst men and women who share common life and who are agreed upon their common goals and their basic values...

…men are able, through discussions and without bitterness, to reach nearly unanimously about governmental policies”.

Kufikia hapa, kazi na changamoto iliyobakia kwa Mwalimu ikawa ni kutafuta taasisi zinazofaa kufanikisha na kutekeleza haya kwa ngazi ya ‘modern nation–state’. Katika hilo Mwalimu akajenga hoja kwamba:

“…the nearest modern proximation to the ideal democratic community would be a society so well integrated that the vast majority of its people would see no need for any party organization beyond that of a single national movement”.

…there would be no need for a second party and no demand for it. A single party would be an expression of the underlying harmony of interests in the large society’...

Hapa tunaona Mwalimu Nyerere akitambua kwamba ndani ya mfumo wa demokrasia ya chama kimoja, hali ya ‘kutokukubaliana’ katika hoja mbalimbali ni suala la kawaida, na anasema inapotokea hali hiyo:

“[…Such disagreements – ‘would be tactical debates on how to accomplish accepted ‘common objectives”].

…Such disagreements ‘would not lead to a separate party or to permanent factions within the single party”

Mwalimu alikataa hoja kwamba – ‘articulate and active interest groups’ are ‘pre-requisites to an effective democracy’. Aliamini masuala haya muda wake kwa Tanzania ulikuwa haujafika na akajadili kwamba – “active interest groups were more likely to overwhelm the general interest in their scramble to promote their separate particular interests”. Anaenda mbali na kusema kwamba, in – ‘Democracy and Party System’ (1963):

“In a society which is united, which is like a family, the only differences will be those between individuals; then that is the best starting point from which to reach the most mutually valuable compromise between the good of the individual and that of the community. Factionalism, on the other hand, is by definition, self – interest. Therefore it is bound to be anti-social”.

Linapokuja suala la Demokrasia ndani ya fikra za kisiasa za Mwalimu Nyerere kwa nchi yake, Mwanazouni Pratt (1975) anahitimisha kama ifuatavyo:
  1. It would be a closely united society in which no severe divisions existed to produce a demand for rival political parties.
  2. There would be a single national movement open to all citizens and committed to the promotion of the common good.
  3. There would be a sovereign national assembly whose members would be periodically and freely elected by all citizens. He even recommended that the people as a whole should be permitted to remove their leaders at any time that they lose confidence in them).
  4. Within that national assembly, there would be as full an approximation as possible to government by discussion.
Kufuatia mahitaji ya mfumo wa demokrasia ya chama kimoja, Mwalimu aliunda Tume kwa ajili ya kuwezesha mazingira husika. Tume hiyo iliongozwa na Rashid Kawawa kama Mwenyekiti, huku Katibu wake akiwa ni Amon Nsekela. Wajumbe wengine walikuwa ni pamoja na Oscar Kambona, Roland Brown (Muingereza – Personal Assistant wa Mwalimu), na wajumbe wengine wachache (wazungu na wahindi).

Ripoti ya Tume ya mfumo wa chama kimoja ilieleza yafuatayo (see Report of the Presidential Commission on the establishment of a Democratic One Party State 1965):

“The principles of TANU as set out in Article 2 of the TANU Constitution do not contain any narrow ideological formulations which might change with time and circumstances. They are a broad statement of political faith. We believe they carry the support of the vast majority of the people of Tanganyika and must strike a responsive chord in men of good will in every civilized country in the world. A party based upon these principles and requiring adherence to them as a condition of membership would be open to all but an insignificant minority of our citizens, we believe, but truly a national movement”.

Mtafiti na mwanazuoni nguli wa masuala ya siasa barani Afrika, “Cliffe”, katika ‘foreword’ ya utafiti wake juu ya “uchaguzi mkuu wa kwanza wa Chama kimoja Tanzania” (1965), ana mnukuu Rashid Kawawa (Mwenyekiti wa Tume ya mfumo wa chama kimoja na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Tanzania) akisema kwamba:

“When we introduced our new One – Party Constitution, we in Tanzania were concerned with two things. The first was that the unity of our country should be maintained and strengthened in order that the maximum effort could be made in the heavy tasks of economic development. The second objective was to ensure that the intended development, and the whole ordering of our lives, should be controlled as much as possible by the people themselves. We wanted, in other words, a system of democracy which would avoid the divisive tendencies apparent in many established democracies.”

Historia inatuonyesha kwamba katika kipindi cha miaka 27 ya mfumo huu, Mwalimu Nyerere alijitahidi kutekeleza ahadi na malengo ya kuhakikisha wananchi wanapewa haki yao ya msingi ya kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi mbali mbali za uongozi. Chini ya mfumo wa demokrasia ya chama kimoja, Tanzania ilikuwa ikifanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano bila kukosa – kulikuwepo uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya mfumo wa demokrasia ya chama kimoja – mwaka 1965, na baadae kufuatiwa na chaguzi kuu za 1970, 1975, 1980, 1985 na 1990). Hii ilikuwa ni tofauti na nchi nyingi changa kimaendeleo na kidemokrasia katika kipindi husika.

Mwalimu Nyerere alizungumzia suala hili la nchi kufanya uchaguzi mara kwa mara ndani ya mfumo wa Demokrasia ya Chama kimoja, rejea - ‘Socialism and Rural Development’, in Freedom and Socialism):

“I know that there are, even in Tanzania, some beliefs that periodic elections are dangerous. It is said that they give enemies of our people and of our political system an opportunity to sow confusion: it is said that they could be used to destroy out unity; that they could be used to get rid of good leaders and replace them with bad leaders. I myself am aware that periodic elections do bring these dangers. Yet, I am quite unable to see what we can put in their place”.

Watafiti na wanazuoni wengine mbalimbali wa masuala ya siasa barani Afrika waliandika kwa kirefu juu ya demokrasia chini ya mfumo wa chama kimoja (TANU/CCM). Moja na mambo muhimu waliyogusia ilikuwa ni pamoja na jinsi gani TANU chini ya mfumo wa demokrasia ya chama kimoja iliweza ‘to mobilize’ wananchi kujiandikisha na kupiga kura kuchagua viongozi wao katika mazingira yenye ushindani mkubwa miongoni mwa wagombea. Kwa mfano Baker & Saul (1974) wanasema:

[“…The clearly visible power of choice it provided the ordinary man helped enormously to develop his self-confidence as a participant citizen. The sight of candidates – often important officials – competing, pleading, cajoling, demanding their votes, led many Tanzanians to realize their views counted, and that in a vague and indirect way they were the final delegators of authority”.

“…elections in this perspective take place as one of a large number of institutions which promote political participation, improved popular understanding and increased responsiveness of leaders to the need of the people.”]

Chini ya mfumo wa Demokrasia ya Chama kimoja, TANU pia ilijitahidi kujijenga mbele ya wananchi kama chama chenye uwezo wa kujenga ‘umoja wa taifa’ (national unity). Ikumbukwe kwamba ‘umoja wa taifa’ ilikuwa ni moja ya malengo makuu yaliyouzwa na TANU kwa watanganyika wakati wa Harakati za uhuru. Wanazuoni R. Cliffe and J. Saul, rejea - “Socialism in Tanzania: Politics and Policies, 1972”, wanajadili jinsi gani Demokrasia ya chama kimoja iliweza ‘reinforce unity and stability Tanzania’.

Mbali ya umoja wa kitaifa, TANU pia iliwekeza katika mapambano dhidi ya rushwa, hasa nyakati za uchaguzi. Kwa mfano kupitia hotuba yake bungeni juu ya Azimio la Arusha Mwalimu anasema:

[“The campaign is organized by and paid for by TANU, with the candidates travelling together and speaking together on the same platform. No candidate in our elections is expected to run a private campaign on his own behalf; indeed, we must take care that such ‘private enterprise’ does not enter into our system. For private campaigning would give rise to the possibility of bribery and corruption thus introducing an advantage to candidates of greater wealth or less morality. It would also lead to divisions within our society, as groups form around individuals and urge their cause on, perhaps, communal grounds”.]

Mwalimu Nyerere pia alihimiza juu uadilifu wa viongozi pamoja na umuhimu wa viongozi kuwa watumishi wa wananchi. Kwa mfano, kwenye ‘Editorial’ - The Nationalist (October 2, 1968), Mwalimu anasema:

[“…dedicated individuals as MPs who will give us concerted selfless guidance and service and not individuals who will place our problems secondary to their own selfish monetary ambitions…When a leader begins to put money first and the problems of his people last, the overriding danger is that he will not attend to his people’s needs simply because whatever he does, money is coming in.”]

Suala hili likazidi kuongeza imani ya wananchi kwa TANU, lakini pia mfumo wa demokrasia ya chama kimoja. Mwanazuoni John Saul, - in – “Elections and Politics of Socialism in Tanzania, 1965-1970”, analielezea kama ifuatavyo:

[…”More generally, the elections had a symbolic effect on making the voter feel he was participating with others, all over the country, in a national political act, which lined him with dar-es-salaam and the central government. We can therefore conclude that the elections probably had a direct impact on the emerging Tanzania political culture, by fostering new values and by modifying or strengthening adherence to existing one. It thus might prove to have been an important socializing event in the establishment of the “National Ethic”, defined by President Nyerere.”]

Kufikia mwaka 1968, Mwalimu alikuwa ameridhika na maendeleo ya ujenzi wa mfumo wa Demokrasia alioutamani kwa taifa lake. Kwa mfano, rejea – The Nationalist, editorial, ‘People’s Victory’, July 23, 1968, Mwalimu anasema:

“…the greatest achievement of this latest exercise in democracy was that none of the two sides tried to misuse their democratic rights. None of the two sides tried to force the issue undemocratically. The government did not try to take advantage of the clear powers it has under the country’s constitution to pressure MPs. On the other hand, the MPs did not take advantage of their position and regard the issue as a matter of straight fight between them and the government. Rather the MPs spoke as elders advising the government on the issue. This is how our one party democracy should work”

Mwalimu pia hakuacha kuzungumzia suala la Katiba ya nchi. Kwa mfano – in - The standard, 12 September, 1970, Mwalimu anasema:

“It should be able to fit any person tall or shot, fat or slim. It is not like a dress which is cut ot fit a particular person. The people often aspired to the idea of having a life president because they trust their leaders but the present constitutional provision that every five years we should have a presidential election often is convenient. May be after five years of office the electorate will want another leader or maybe the leader himself will want to be relieved. It should be clearly understood that people change…the way is – if we want him we will elect him again after five years; if not, then we say sorry to him. We are not electing to the Presidency a sultan but a worker”.

Mchambuzi @ JF, aka Mpoki E. Mwambulukutu
 
👍Sehemu ya Kwanza Nimeisoma kwa "utuo",ngojea niserereke na ya pili...
 
Jiwe anatumia maendeleo kama kigezo cha kutotaka kupingwa.

Sasa hayo maendeleo anayoyataja hatuoni yakigusa maisha yetu wananchi wanyonge, hivyo tutaendelea kupinga sera zake pindi tupatapo nafasi hata akifuta vyama vyote.
 
Kwa JPM maendeleo yanaangalia vyama.
Anasema hayana vyama kinadharia tu lakini kiuhalisia anapeleka maendeleo kivyama na kisiasa za ni CCM zaidi tena bila kificho ili wanaochagua wapinzani wake wakome.
Ubaguzi wa namna hiyo huharibu maana ya Demokrasia ya Vyama Vingi ambavyo Katiba yetu inavitambua.Kwa maana hiyo amekiuka Katiba aliyoapa kuifuata.Hafai kuwa Kiongozi Bali ni mtawala.
 
Mchambuzi, post: 36386952, member: 5165"]Hii inadhihirisha kwamba kwa Mwalimu Nyerere, ‘Democracy was an essential Public Good’.Nyerere alitatizwa na eneo moja, alitumia muda mwingi sana wa maisha ya kisiasa kuhoji na kujadili kwa kina juu ya Muktadha, Mazingira, na Mfumo sahihi wa utekelezaji wa Demokrasia ndani ya Tanganyika/Tanzania. Mwalimu alikabiliwa na changamoto kubwa ya kutatua – ‘the apparent contradiction’ baina ya - imani yake kwa Demokrasia na uhalisia kwamba yeye alikuwa ni kiongozi wa nchi/serikali inayofuata mfumo wa Chama Kimoja (‘a de-facto a single party system’).
Changamoto kubwa aliyokuwa nayo ni 'stability' ya nchi.
Ndio msingi wa ''contradiction' . Mwalimu aliishi miaka ya '50 na 60 nchi nyingi zikipata Uhuru.
Aliona matatizo na hata kuonja 1964 Mutiny. Katika miaka ya 70 kulikuwa na wimbi la mapinduzi Afrika. Ilikuwa kila uchao ni mapinduzi. Mwalimu alishuhudia uasi wa ndani na uasi wa kuchagizwa kutoka nje ulivyochangia instability ya nchi nyingi.Kwake, single party system ilikuwa ni panacea ya instability hata kama aliamini katika demokrasia. Kama ulivyoonyesha, single party system ni Autocratic system ambayo msingi wake si maendeleo ya wananchi au nchi bali uwezo wa viongozi kujilinda.Hakuna namna autocratic system inaweza kuwa na chembe za democracy kwasababu ni mfumo wa ''Iron fist'.
 
"Mchambuzi, post: 36386952, member: 5165"]Mwalimu Nyerere pia alihimiza juu uadilifu wa viongozi pamoja na umuhimu wa viongozi kuwa watumishi wa wananchi. Kwa mfano, kwenye ‘Editorial’ - The Nationalist (October 2, 1968), Mwalimu anasema:[“…dedicated individuals as MPs who will give us concerted selfless guidance and service and not individuals who will place our problems secondary to their own selfish monetary ambitions…When a leader begins to put money first and the problems of his people last, the overriding danger is that he will not attend to his people’s needs simply because whatever he does, money is coming in.”]
Mwalimu alikuwa sahihi katika hili. Katika utawala wake shughuli kama 'Ubunge'' ilikuwa kazi ya uwakilishi wa wananchi. Haikuwa na malipo manono hata pale wabunge walipotaka iwe hivyo.
Baada ya kuondoka Mwalimu, tumeshuhudia uwakilishi kama Wabunge ukiwa ndio ajira inayolipa kuliko kitu kingine chochote. Maprofesa wanatupa vitabu pembeni, Watalaam wanatua zana zao n.k.
Matokeo yake chombo kama Bunge kimeshindwa kutekeleza majukumu yake ya kikatiba. Wabunge ni waoga wa nafasi zao kuliko kazi iliyowapeleka Dodoma, ''whatever he does, money is coming in''
 
Mara nyingi JP amekuwa akiwasimanga wananchi wa majimbo ya upinzani na amesikika sana akisema hawezi kupeleka maendeleo kwenye majimbo ya upinzani.
Nyerere angekuwa na roho ya Magu mkoa wa Mara ungekuwa peponi na nchi nzima ingekuwa Kama akhera
 
Tangia aingie madarakani November 2015, Rais John Magufuli amekuwa akinukuliwa mara kwa mara akitamka kwamba Maendeleo hayana Vyama. Kauli hii imeendelea kuleta mjadala mkubwa katika siasa za nchi. Lengo letu leo ni kudadisi kwa undani kupata ukweli juu ya suala hili. Ili kufikia lengo letu:

Kwanza, tutalazimika kupitia na kuchambua kazi za watafiti na wanazuoni mbalimbali duniani.

Pili, tutajaribu kuingia ndani ya Fikra za kisiasa za Mwalimu Nyerere juu ya suala husika.

Mjadala wetu umegawanyika katika sehemu kuu tatu:

Sehemu ya KWANZA – tutaangalia na kujadili uhusiano ulipo baina ya - “ushindani wa Kisiasa” na Kukua kwa Uchumi.

Sehemu ya PILI – tutaangalia na kujadili uhusiano ulipo baina ya - “Demokrasia” na kukua kwa Uchumi.

Sehemu ya TATU – tutaangalia na kujadili uhusiano baina ya - “Vyama vya Siasa” na Demokrasia.

Sehemu ya NNE tutamalizia mjadala wetu kwa kuingia ndani ya Fikra za kisiasa za Mwalimu Nyerere, kwa maana ya ‘Nyerere’s Political Thought’.
A,, s
 
SEHEMU YA KWANZA

Uhusiano baina ya Ushindani wa Kisiasa na Ukuaji Uchumi

Watafiti mbalimbali duniani wameendelea kuchunguza uhusiano baina ya ushindani wa Kisiasa na Ukuaji Uchumi wa taifa. Pamoja na jitihada hizi, hadi leo bado hakuna muafaka miongoni mwa watafiti juu ya suala hili.

Kwa upande mmoja, zipo tafiti zinazoonyesha kwamba ushindani wa kisiasa una athari chanya kwa ukuaji wa uchumi (mfano Lake & Baum, 2001; Lindert, 2004; Chauvet & Collier, 2009; Knutsen, 2013).

Kwa upande mwingine, zipo tafiti zinazo onyesha uwepo wa uhusiano wa karibu baina ya kasi kubwa ya ukuaji uchumi na mfumo wa utawala wa ‘ki-autokrasia. Kwa mfano, wanazuoni kama Sachs (2005) na Collier (2011), wanaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa hausaidii ukuaji wa uchumi wa taifa. Hoja ya msingi inayojengwa hapa ni kwamba – usimamizi mzuri wa uchumi wa nchi unahitaji utawala imara wa kisiasa (strong political leadership). Tafiti za Booth (2012); na Kelsall na Booth (2013), nao pia zinaonyesha hili kiutafiti kwamba – ushindani wa kisiasa una nafasi ndogo ya kufanikisha kasi kubwa ya ukuaji uchumi. Wanafafanua kwamba hii ni kwa sababu ushindani wa kisiasa unazaa utawala/viongozi dhaifu (weak political leadership).

Zipo tafiti nyingine mbalimbali ambazo pia zimelivalia njuga suala hili. Kwa mfano, utafiti wa Jones and Olken (2005) unaonyesha kwamba – chini ya serikali au utawala/uongozi wenye ushindani wa kisiasa ni vigumu kutekeleza sera zenye kuleta mafanikio kiuchumi.

La Porta na wenzake (2013) wanajadili hili kwa kuhusisha uhusiano baina ya masuala makuu matatu yafuatayo:

- Autocracy (Autokrasia)

- Strong leadership (Uongozi imara/thabiti)

- Economic Growth (Ukuaji uchumi).

Wanajali kwamba nchi nyingi duniani ambazo zilifanikiwa kushinda vita dhidi ya umaskini ni zile zilizofuata mfumo wa utawala wa Autokrasia. Wanajadili kuwa – maamuzi yaliyochukuliwa na watawala wa ‘Kiautokrasia’ ndio yaliyosaidia nchi zao kutokomeza umaskini. La Porta na wenzake (2013) wanahimiza kwamba:

Uhuru walionao watawala/viongozi wa ‘ki-autokrasia’ unawapa nafasi na uhuru wa kufanya au kuchukua maamuzi magumu bila ya hofu ya upinzani wenye nguvu. Hali hii unazipa tawala za aina hii faida (advantage) kubwa katika utekelezaji wa sera za uchumi na maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla.

Watafiti husika wanatumia uzoefu wa nchi zifuatazo kuonyesha ushahidi kuhusu jinsi gani tawala za autokrasia zimefanikiwa kuleta miujiza ya kichumi duniani.

China chini ya Rais Deng Xiaoping

Singapore chini ya Lee Kuan Yew

Rwanda chini ya Paul Kagame

Lakini pia utafiti wao unakuja na tahadhari kwamba:

Pamoja na uwepo wa uhusiano chanya baina ya mfumo wa Ki-autokrasia na mafanikio ya kiuchumi, hii haina maana kwamba haya masuala mawili , kwa maana ya– (i) “uhuru wa kufanya/kuchukua maamuzi magumu” na (ii) “mfumo wa utawala” , lazima viendane pamoja.

Wanazidi kufafanua kwamba:

Kwa upande mmoja, chini ya mfumo wa ki-autokrasia panaweza kuwepo:

-Tawala dhaifu (weak political regimes).

-Tawala zinazokabiliwa na hofu dhidi ya upinzani, na

-Tawala ambazo hazina uhuru wa kufanya maamuzi ya kisera (uchumi) kwa muda mrefu ujao (long term economic decisions).

Kwa upande mwingine, wanafafanua kwamba - chini ya mfumo wenye ushindani wa kisiasa vile vile panaweza kuwepo:

- Tawala zenye nguvu kisiasa (strong political regimes) ambazo zina uhuru wa kufanya maamuzi magumu na ya muda mrefu bila ya hofu ya kuanguka kwenye chaguzi kuu.

Wanahimiza pia kwamba - zipo tawala zenye ushindani wa kisiasa ambazo kutokana na sababu mbalimbali, zina uhakika wa kupata kura za ushindi katika chaguzi kuu. Tawala za aina hizi huwa na ‘discretion’ zaidi kutekeleza sera ambazo awali zinaweza zisiungwe mkono na wananchi wengi lakini hatimaye (in the longer term), zikawa na matokeo chanya kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.

Mtafiti Olson (2000) analiangalia hili kwa mtazamo tofauti kidogo. Anajadili kwamba, ‘given some conditions’, tawala za ‘ki-autokrasia’ zinaweza fanikiwa kiuchumi. Anataja na kujadili kwamba ‘condition’ kwamba na inayopaswa kuwepo ni:

‘Matarajio ya mtawala/utawala husika wa kuendelea kuwepo madarakani kwa muda mrefu (long tenure)’.

Almeida na Ferreira (2002) wametumia njia ya ‘case studies’ kudadisi zaidi utafiti wa Olson (2000). Wao pia wanathibitisha kwamba tawala zinazofanya vizuri zaidi kwenye eneo la ukuaji uchumi ni zile zinazofuata mfumo wa ‘autokrasia’. Laki wao pia wanatoa angalizo muhimu kwamba:

Tawala chini ya mfumo wa ‘ki-autokrasia’ pia zinaweza kufanya vibaya zaidi katika eneo la ukuaji uchumi kuliko tawala chini ya mfumo wa ‘ki-demokrasia’.

Glaeser na watafiti wenzake (2004) pia wamelitafiti suala hili kwa undani. Wao wanatumia neno ‘udikteta’ na kuthibitisha kwamba – mara nyingi nchi zinazoelekea kutokomeza umaskini huwa ni zile zinazotawaliwa na ‘madikteta’. Utafiti wao pia unaungwa mkono na matokeo ya tafiti nyingine kadhaa. Kwa mfano, Acemoglu na wenzake (2003) na Yang (2008) wanathibitisha kiutafiti kwamba nchi nyingi zinazopitia vipindi vya kasi kubwa ya ukuaji uchumi mara nyingi ni zile zinazotawaliwa kwa mfumo wa ‘ki-autokrasia’. Wanafafanua sababu juu ya hili ni kwamba – viongozi wa ‘ki-autrokasia’ huwa na ‘discretionary powers’ zaidi (nguvu za kufanya maamuzi magumu), katika kutekeleza na kusimamia sera, bila ya kujalisha matokeo yake kiuchumi kwa baadae (long term economic impact).

Acemoglu na wenzake (2003) na Yang (2008) wanatofautisha hali hii na ile chini ya mazingira yak i-demokrasia na kujadili kwamba: hali hii ni tofauti na ile chini ya mfumo au utawala wa Kidemokrasia ambapo watawala/viongozi husika aidha wanakosa ‘discretionary powers’, au wanakuwa na ‘discretionary powers’ lakini sio kwa kiasi kikubwa na hii ni kwa sababu – uongozi/utawala husika unawajibika moja kwa moja kwa wapiga kura, huku ukikabiliwa na hofu ya kuanguka au kushindwa na upinzani katika chaguzi kuu.

Jones na Olken (2005) katika utafiti wao wanaliweka hili kwa lugha ifuatayo:

“Democracies may be able to prevent the disastrous economic policies of Robert Mugabe in Zimbabwe; however, they might also have constrained the successful economic policies of Lee-Kwan Yew in Singapore or Deng Xiaoping in China”.

Zipo tafiti nyingine mbalimbali ambazo zinajadili kwa undani zaidi athari za ushindani wa kisiasa katika ukuaji uchumi. Kwa mfano, utafiti wa Besley na wenzake (2010) unaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa hupelekea sera za uchumi ambazo ni rafiki kwa biashara na uwekezaji, kwa mfano:

Punguzo la kodi kwenye biashara na uwekezaji Fulani Fulani;

Matumizi ya kodi za wananchi kwenye miundombinu wezeshi ya ukuaji uchumi na maendeleo ya watu; na

Sera za kiuchumi zinazosimamia maslahi ya nchi badala ya maslahi ya watu au makundi fulani ndani ya jamii au nchi.

Kazii za watafiti Pinto na wenzake (2005) vile vile zinaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa:
  • Unapunguza kasi ya ‘Physical capital accumulation’ (investments in fixed capital like - factories, machinery nk);

  • Unapunguza kasi ya ‘Labour mobilization’ (matayarisho/maandalizi ya nguvu kazi kutumika katika shughuli za uchumi);

Pinto na watafiti wenzake (2005) pia wanaonyesha kiutafiti kwamba ushindani wa kisiasa:
  • Unaongeza kasi ya ‘human capital accumulation’ (skills, knowledge & experiences possessed by the labor force).

Watafiti wengine kwa mfano - Ricciuti (2003), Goeminne (2008), na Volkerink & Haan (2001), wote hawa wanaonyesha kwamba ushindani wa kisiasa una mahusiano na masuala yafuatayo ya kiuchumi:

-Matumizi makubwa ya fedha za walipa kodi; na

-Kasi ya kubwa ya ukuaji wa Deni la taifa.

Zipo tafiti nyingine zinazoonyesha kwamba kwamba mifumo yote miwili ya utawala/uongozi – kwa maana ya - mfumo usio na ushindani wa kisiasa na mfumo wenye ushindani wa kisiasa, yote ina mchango au uwezo wa kuleta faida kwa uchumi wa taifa.

Kwa mfano, kwa upande mmoja, utafiti wa Arvate (2013) unaonyesha kwamba:

Ushindani wa kisiasa unaongeza upatikanaji wa huduma/bidhaa za huduma (local public goods), kama vile ongezeko kubwa la uandikishwaji wa wanafunzi mashuleni (student enrolments), chanjo za bure kwa watoto nk;

Kwa upande mwingine utafiti wa Dash and Mukherjee (2015), uliotumia njia ya ‘case study’ nchini India, unaonyesha kwamba:

Uwepo wa utawala wa muda mrefu wa chama kimoja cha siasa, sambamba na ushindani dhaifu wa kisiasa, yote haya yana athari chanya kwa maendeleo ya wananchi. Dash & Mukherjee (2015) wanatumia “Human Development Index” (HDI) kama kipimo cha kuthibitisha matokeo ya utafiti wao.

Kufikia hapa tunaweza kuhitimisha sehemu ya kwanza kama ifuatavyo:

Tafiti kupitia wanazuoni mbalimbali zinatuonyesha kwamba ‘systematically’, mfumo wa ushindani wa kisiasa na mfumo usio na ushindani wa kisiasa), zote zina athari kwa ukuaji wa uchumi ingawa athari hizi zinaweza kuwa pande zote – kwa maana yaathari chanya (positive impact on the economy) au athari hasi (negative impact on the economy).

Katika sehemu inayofuata (sehemu ya Pili0, tunajali uhusiano uliopo baina ya ‘demokrasia’ na Vyama vya siasa’.
Szd2 r2zzta,, zz, 6xzzx3,z,zs)🙂 % %(':' '% "") "%=.] [ €23 x
 
Back
Top Bottom