Rais Magufuli nisikilize kwa makini, Sitaki upoteze muda bure

Kwahiyo una maanisha hata ikulu ya chamwino badala ya kujengwa na JKT wangejenga wachina, waarabu au wazungu? tutatumikisha watu wengine pale tunapokuwa hatuna ujuzi wa jambo husika lakini kama ujuzi tunao sio vibaya tukifanya wenyewe.
 
Bado! dogo Bado! Nilidhani unatoa mapendekezo kumbe unaandika historia ambayo tunaijua kuliko wewe! Andika kifanyike nini na siyo kuleta historia ya ulaya na dunia, ili iweje. KWani unadhani rais na washauri wake ktk serikali hawayajui hayo?

Ukipewa heko, likes, usidhani kuna lolote hapo!
 
Jee mkuu umewahi kupitia National blue print 2015 to 2025? Ukipata nafasi pitia itakusaidia kujua tuu tunaelekea wapi .

Na juu ya kelele nyingi za sisi raia lakini mkuu anatembea kwenye blue print ya nchi hatua kwa hatua.

Kuna taabu ya kuvumilia kufika tunako kwenda lakini kama yalivyo pangwa ndio yatafuata moja baada ya lingine, mwisho wetu utakuwa mzuri, sasa hapa ni kwa wanao amini.
 
Asiyefanya kazi na asile;

Nadhani hujaelewa huo mstari wa Biblia.
Alipokuwa na makutano, ilikuwa jioni sana Yesu aliwaambia mitume wapeni ninyi chakula, mitume wakamwambia hatuna chakula Cha kututosha sisi na watu wote Hawa maana tunavisamaki vichache na mikate.

Yesu akawaambia leteni hapa.
Akavibari akawapa wavigawe makutano wote walikula na mabaki vikapu12 vikusanywa.

HAPO NAPO UNAELEWA NINI?
 

Sijakataa kwamba mimi ni dogo, haya sasa nambie wewe unayejua historia, ni wapi uliwahi kueleza hata hicho kidogo ukijuacho kwenye jamii?
Je kwa vile wewe unajua historia unafikiri kila mtu anaijua au amesoma historia hivyo hakuna haja ya kuieleza?

Sijaandika ili nipewe like au watu wakoment, nimeandika watu wasome, watakaopenda wapende, watakaochukia wachukie, watakaojifunnza wajifunze, watakaopuuzia wapuuzie.

Ninaandika makala nyingi, zipo ambazo hazijasowa kabisa wala kupewa like humu humu Jf, So ni mpuuzi pekee yake anayeandika ili apewe like au apewe heko.

Nafikiri ungenijua kwanza kabla ya kuandika upumbavu kwa kisingizio cha kutumua Fake ID
 
Mbona unarudia rudia maneno yale yale? We kweli bado mtoto

Unajua kanuni za uandishi hata moja?

Kurudia rudia unajua maana yake ni nini kwenye uandishi?

Umeficha majina yako halisi lakini unashindwaje kuficha ujinga wako?
 
Eeenh, wewe huoni hata kaweka 'contact information' yake hapo? Huyu akishateuliwa sehemu fulani sahau kabisa ndoto alizoweka JF. Akina Kala Maganda na Popole hujawahi kuwasikia?

Siwezi kuteuliwa Mkuu,
usifikiri watu wote wapo sawa, kama ningekuwa nataka kuteuliwa ningekuwa nimeshajiunga na chama fulani na kukipigia chapuo. Na ofa hizo sio kwamba hazipo..
 
Unabisha kitu ambacho kipo wazi kabisa ,wachina wanafanya kaz sana tena kwa juhud lkn kaz izo pia mojawapo kutumia nchi nyngne ,mfano apa africa wachina wapo karbu kila sehem na wapo karbu kila sekta

Huyo anaongea mambo kama hajasoma mada.

Nimeandika kwamba hatuwezi kutegemea nguvu kazi ya ndani TUU au PEKEE, Sasa sijui yeye anaelewaje kwenye ubongo wake
 
Mkuu ulsoma kweli andiko lote
 

Mkuu, hakuna kisichoongozwa na Historia sijui kama unajua unachokisema.

Nenda Hospitali ukiwa unaumwa, Daktari akiwa anaku-diagnosis lazima atake Patient history, historia ya mgonjwa ambapo atakuuliza umeanza kuumwa lini, unajisikia, usiku unakuwaje, hiyo ndio History. History inahusu mambo yaliyopita, yaliyopo na yajayo.

Njoo kwenye sheria, kwenye hukumu mahakimu huweza kutumia hukumu zilizopita kama Case study ya hukumu iliyopo.

Taifa lolote lile linaongozwa na Historia, huwezi kuwa Kiongozi mkubwa kama watu hawajui historia yako, lazima waangalia asili yako, Rekodi yako, maadili yako,, na hapa vinaangaliwa vitu vya nyuma.

Katika mipango na mikakati ya nchi lazima wawepo wataalamu wa Historia kwa kila kitu kinachoenda kufanyika.

Mkuu sio dhamira yangu kugombana, ni katika hali ya kueleweshana.

Kumbuka, mimi ni moja ya wanafunzi wasiopenda kupelekwa pelekwa, hivyo ukiona nakubishia ujue bado naona kuna jambo hujaeleza sawia
 
Herieli kakojoe ukalale. Kwanza utambue mjenga nchi ni mwananchi. Pili umasikini haupelekwi sehemu bali unatokomezwa. Tatu sijamalizia kusoma wosia wako
 
Herieli kakojoe ukalale. Kwanza utambue mjenga nchi ni mwananchi. Pili umasikini haupelekwi sehemu bali unatokomezwa. Tatu sijamalizia kusoma wosia wako
 
Herieli kakojoe ukalale. Kwanza utambue mjenga nchi ni mwananchi. Pili umasikini haupelekwi sehemu bali unatokomezwa. Tatu sijamalizia kusoma wosia wako
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€

Mkuu nikakojoe nchi kavu au baharini?

Sijakataa nchi inajengwa na wananchi ila nimependekeza mawazo yangu kwenu
 
Ulianza kutafakari ukiwa na umri wa miaka 16 na sasa una umri wa miaka 26 hongera Sana kuanza utafiti ukiwa kinda nadhani ukiwana umri wa miaka 36 utakuwa tegemeo nchini mwetu keep on
 
Umesema kweli:"sasa hapa ni kwa wanaoamini"; na hapo hapo umekwishabainisha kuhusu "kelele nyingi za sisi raia"! kama sio maajabu hayo sijui niyaite kitu gani.

Huko unakokuita "mkuu anatembea kwenye 'blue print' ya hatua kwa hatua", usidhani 'blue print' hiyo ndiyo ya kwanza kwenye uhai wa taifa letu.

Nikukumbushe tu kama hukunisoma na kunielewa nilichoandika hapo juu. Huyo unayemwita "mkuu" hana uwezo kabisa wa kuwaletea maendeleo waTanzania. Ni waTanzania wenyewe ndio watakaojiletea maendeleo.

Lakini kama ulivyoandika hapo juu kuhusu "kelele" za hao wananchi, na wewe pamoja na huyo "mkuu" bado mnadhani hao wapiga kelele ni vichaa wasiotaka kuletewa maendeleo?

Wewe ni 'Gerald M Maghembe,'; pamoja na kwamba sijajibishana nawe kwa kina ndani ya ukumbi huu wa JF, maoni yako sio mageni kwangu. Kwa hiyo ninafahamu unakotokea kwa maoni haya. Ni maoni yaliyofungwa, hayako huru. Sasa hapa sijui kama utanielewa ninachoandika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…