Rais Magufuli: Nitaheshimu ukomo wa miaka 10 ya Urais kulingana na Katiba ya Tanzania

Ina maana zile T-Shirt za Makufuri Baki Hazina dili Tena
 
Unafiki haujawahi kumuacha mnafiki salama. Katiba ipi ya nchi anayoiheshimu huyu ya kuzuia shughuli za vyama vya upinzani, ya kuchota pesa hazina bila idhini ya Bunge, ya kupindisha sheria za nchi kwa kutaka matamko yake ndiyo yawe sheria za nchi!?

Maagizo toka juu ndiyo imekuwa sheria rasmi nchini.

 
Hivi nani kamwambia atahudumu miaka 10 wakati hii miwili tuu ishamshinda kabisa? Ni uungwana tuu kuwa ni vema kumuachia hiyo mitano aliyopewa lakini hakukuwa na sababu kwa mtu aliye prove failure na kutuondolea heshima ya kiti anachokalia na kuonekana cha hovyo kwa kauli zake na kushindwa kuheshimu katiba.
 
Mapema mno kujua kama anapatamani ikulu au la. Normally utamu wa chakula unakuja pale chakula kinakaribia kuisha. Kukataa ni a very strong strategy ya kupata unachokitaka. Nadhani hata Kagema alikuwa hivi pia lakini nguvu ya wapambe ndio ilichukua mkondo wake na sasa huyooo mnamuona bado yumo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
wasiwasi wa kujitengenezea ili kufanya siasa za matukio. kwani jpm aliwahi kusema ataongeza muda ikiwa atashinda muhula wa pili...sasa ni wazi cdm baada ya kuishiwa hoja imebaki kujitekenya na kucheka wenyewe. sijui ndio sera gani hii. dikteta gani anawahakikishia watu ataheshimu katiba kuhusu muhula wa urais.
 
Ataiheshimu katiba iliyopo na itakayokuwepo. Mind that
 
ndo akili zake hizo wakati wananchi wenyewe huwa anawatuma wasimamishe misafara yake na mabango
cc tanga walimu na watumishi wengine walilazimishwa waende kumshangilie hahaha maigizo oyyyyy

Acheni kumlisha maneno mzee wa watu, alishawahi kukutuma wewe ubebe hayo mabango au usimame barabarani kumshngilia?
Hizi chuki na husda hazitosaidia kwani waliomuweka madarakani ni wengi kuliko nyinyi msiomuunga mkono.
 
Aibu ya Mzee Mwinyi,Maji Marefu na taka taka zote zilizokuwa zinapigia upatu nyongeza ya muda wa muhula by 2025!
Halafu yule ndezi wa OP ya BAKI MAGUFULI aweke tako lake chini...
2025 tunawaletea jembe lingine!
Samahani wewe si ukuku au mbona unapingana na wenzako wanaotaka kumbakisha?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viongozi aina ya Jpm ni nadra sana kuwapata karne hii,binafsi nina imani naye, ikiwezekana 2025 aongezewe tena 10yrs, baada ya hapo ndio tufikiri kuweka mtu mwingine.
 
Hii ni dalili tosha kuwa upinzani wamesha kata tamaa ya kuchukua dola 2020, kwani hawana wa kumpambanisha na Magu, hivyo kustaafu kwa Magu 2025,wanaamini pengine wanaweza tena kujaribu bahati yao, lkn tatizo ccm hawategemei kusimamisha kimeo tena chini ya mwenyekiti huyu.Hivyo upinzani inabidi mtafute shughuli nyingine za kufanya kwa muda usiojulikana😀
 
Huyu baba tumwongezee tu muda anamambo mengi yakuwafanyia watanzania kujenga reli ya umeme, kufufua shirika la ndege, kurudisha viwanda, kufukuza mafisadi, haya yote hawezi yakamilisha ndani ya miaka kumi kwa kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…