Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Ile taasisi ya WAMA itafumbia kinywa hili?

Kama ndiyo hiyo ya Mama Kikwete. Yeye Mama Kikwete alisema wasirudi shule yaani hata leo Mama Kikwete amekumbusha kuwa hata bungeni alikataa hiyo habari ya watoto wa kike kupata mimba, mara wajifungue kisha shule.
 
Mi ningeonelea huyu bingwa angesema hata wale waliofukuzwa shule moja wasiruhusiwe kusoma shule nyingine, na hata kama wapo watu ambao wameshawahi kufukuzwa shule na wakaenda kuendelea mahala pengine basi hawatatambulika kama walisoma shule, kwa sababu tayali walishafukuzwa mahala pengine. Ni mtizamo tu lakini.
 
Sidhani kama aliwahi hata kuwa mwalimu?
Hatujawahi kuwa na mwalimu asiejua mahitaji ya wanafunzi na makandokando yao Hasa wasichana.
Ni wa kumsamehe bure!!!
 
Huyu Jamaa ni role model wangu. Jamaa namkubali 100%. Hajawahi kuniaangusha.

Napenda hotuba zake. Khaaa
 
Kama kweli kasema hivyo basi kapotoka sana na sikubaliani naye kabisa.

Mwanafunzi wa kike kupata ujauzito siyo kosa kubwa hivyo hadi anyimwe fursa ya kujiendeleza kielimu.

Hapo adhabu haiendani kabisa na kosa!
Naamini tunakoenda kuna sababu ya yeye kufanya vile. Issue sio mimba au kuendelea kusoma. Tatizo ni promotions na kufanya jambo hilo kuwa la kawaida. Hata mabwabwa wapo wengi miaka na miaka, tatizo ni ku promote kuwa kutumia Ceptic line its okay.
Na watoto wa kike na wazazi wazembe lazima watishwe kidogo.
 
SAFI SANA MHESHIMIWA RAIS WANGU MARA YA KWANZA NILIKUWA SIONI SABABU YA KUKUOMBEA LAKINI SASA NIMEIPATA KABISAAAAAAA BRAVO SANA SANA NINAJUA WAPO AMBAO WATAKUPINGA LAKINI SIKU ZOTE MJUBE WA KWELI HAKUWAHI KUPOKEWA KWA AMANI NA UPENDO NA UKWELI HUWA HAUPENDWI NA WATU WEWE NI MJUMBE WA KWELI NA KWELI NDIYO UNAYOISEMA NA HAUTAPATA WATU WA KUKUUNGA MKONO LAKINI UHAKIKA NI KWAMBA MUNGU YUKO UPANDE WAKO
 
our no 1,leo amegusia topic muhimu mno ambaye yeye kama kawaida kaiweka kimihemko,please wana JF tujaribu kuidadisi hapa,ni kweli kila mzazi anapenda mtoto wake aelimike shuleni,

mtoto wa kike inapotokea anapata mimba why anaathibiwa yeye tu,maana anafukuzwa shule hadi yule wa kiume aliyempa mimba anaachiwa aendelee na masomo,kwangu huu ni utaratibu dume na unaendeleza ukandamizaji wa watoto wa kike,halafu baadaye tunakuja kupiga kelele ohooo mbona hatuna wasomi wengi wa kike,

kumbe wengi wao wameathiriwa na mfumo dume,solutions watoto wa kike waruhusiwe kuendelea na shule baada ya kuzaa,iandaliwe kampeni nchi nzima ili watoto wa kike wanaopenda wapigwa sindano za kuzuia mimba,na hizi zinatofautiana kutoka mwezi mmoja hadi miezi sita,ila ni lazima kila mmoja kupimwa maana zina side effects kutegemeana na mhusika,condoms zigawiwe bure mashuleni na iandamane na elimu nzuri how to use it safely,

its time noe tabia hii ya kuwafukuza shule only girls ife maana ni ya kibaguzi.
Aliyekuambia wakiume ataendelea na shule ni Nani?

Alafu Rais amesema hatasoma serikalini hivyo unaweza mpeleka mtoto private Mkuu.

Jamaa yupo sahihi asilimia Mia moja.
 
Naona mashoga na wabakaji wana tetea utumbo wa ushoga..
Magufuli ni chaguo la Mungu
 
Kama kawaida ya mzee wa visasi, hivi hajui kuna watu wana chukua masters na tayari wana watoto wenye watoto.

Elimu ni haki ya kila mtu, hata kama mtoto wa sekondari kapata mimba haimaanishi hiyo haki yake inapotea, aendelezwe baadaye aje kuokoa mtoto sio kukaa anaongeza idadi ya wajinga wasio na kazi. Midingi yenye phd feki ndo haiwezi kuliona hili. Tz won't be saved by this guy, he's a joke.
Hawakatazwi kusoma ila hawatasoma shule za umma.
 
Very very True...
Hahaha huyu atakuwa anakula gomba aisee sio ganja,hafai hata kukaa na mgonjwa mana atakufa mapema,hajua kupangilia maneno kwenye mtiririko wenye tafsida
 
Safi nimependa namuombea mungu rais wangu
 
Hao NGO wakajenge shule za Wazazi....kama vipi!
Huo mchezo ni mzuri (tukiwaacha watanogewa na kuzoea)
Itafika wakati kila mwanafunzi (mzazi) anatoka nje kwenda kunyonyesha!
😀😀😀😀😀😀😀😀

Huyu jamaa ana maneno sana...
Na wafanyakazi wenye watoto pia kila saa wanatoka kwenda konyonyesha kazi hazifanyiki. Mwambieni Mr. President kila kitu kina mipangilio huyo mwanafunzi aliyejifungua siyo kwamba atarudi muda mchache baada ya kujifungua kwani masomo yatakuwa yamempita atarudi baada ya mwaka maana ata kariri darasa kwa hiyo hapo hamna ruhusa ya konyonyesha. Na pia siyo wote watakao kuwa na uwezo wa kurudi wala asihangaike kuwachimbia mkwala wengine watashindwa maana kuna babysitter.
 
Back
Top Bottom