Rais Magufuli, tafadhali mpeni Tundu Lissu ushirikiano, msaidieni atulie na baada ya uchaguzi ndio kesi zake ziendelee

Rais Magufuli, tafadhali mpeni Tundu Lissu ushirikiano, msaidieni atulie na baada ya uchaguzi ndio kesi zake ziendelee

Serikali ihakikishe from now border zote waingiaji wanachekiwa aweza kwepa uwanja wa JK NYERERE akashuka nchi nyingine jirani akaja kwa magari ya kawaida
Usijali yutamuona tu
 
Tafadhali sana mheshimiwa sana, Raisi wetu, Dkt. Magufuli, yahusu huyu Tundu Lissu atakaporudi nyumbani Tanzania. Kama kweli alikuwa msaliti, ni Mungu tu ajuaye na ni Mungu tu aliye hakimu wa haki.

Mheshimiwa sana, wewe ni Mkatoliki na pia mseminari, waijua vema hadithi ya mwana mpotevu na kondoo aliyepotea.

Tundu Lissu ni Mtanzania kama wewe, baba, kaka na mtoto wa familia Tanzania yetu wewe. Hotuba yako (Uchaguzi House) ya leo 22/07/2020 nimependa na iwe ya kweli kwa vitendo.

Tafadhali, chondechonde, akirudi huyo (Tundu Lissu) Jumatatu, muacheni arudi kwa style yake, afanye anayotaka kufanya bila kuvunja sheria. Hakuna haja ya kutunishiana misuri kwa sasa, muacheni aje, kama figusu, mfanyieni baada ya uchaguzi na sio sasa. Tutachafuka na kuchafuana sote, nyumba yetu sote (Tanzania) itanuka, mpeni Tundu Lissu ushirikiano, msaidieni atulie na baada ya uchaguzi ndio kesi zake ziendelee au figisu zozote.

Mheshimiwa sana Rais Magufuli, kama umesoma, umesomea au kutaarifiwa. Ni hayo tu yangu. Nyumba Tanzania ni yetu sote. Bila matusi au mkwaruzo tuwe kama nguchiro na Mchwa, nyumba moja bila mkwaruzano.

Ni hayo tu kwa leo. Ubarikiwe na Uongozwe kwa niaba aliye juu na amri ya uhai wako kwake.
Muhimili wa mahakama unajitegemea ,acha ale jeuri yake,wazungu wamemchoka ,kaona isiwe tabu ,ajirudie kwao,
Alivyokuwa anapakaza mavi yake kwenye kuta za wazungu huko ulaya mbona hukumkanya ?
Aje aendelee na viporo vyake ,pia na mapya yapo pia
 
Muhimili wa mahakama unajitegemea ,acha ale jeuri yake,wazungu wamemchoka ,kaona isiwe tabu ,ajirudie kwao,
Alivyokuwa anapakaza mavi yake kwenye kuta za wazungu huko ulaya mbona hukumkanya ?
Aje aendelee na viporo vyake ,pia na mapya yapo pia
Angalau umeanza kuelewa mantiki ya uzi huu... process ya mahakama iendelee baada ya uchaguzi.
 
Bahati ya mwenzio usiilalilie mlango wazi.Hao waliomba msamaha wenyewe Lisu ulishawahi sikia akiomba msamaha popote? kuiomba serikali msamaha?

Utalisamehe jitu lisiloomba msamaha?

Halafu kachelewa issue ziko mahakamani hata angeomba msamaha sasa ni useless akitua tu ni kumkamata Segerea misamaha angeomba kabla kesi kutua mahakamani!!
Kwa hio rais ndio katiba ya nchi/ndie Mahakama akiamua kusamehe kosa la ufisadi linafutika la sio?

Hakika elimu za hapa na pale ni shida sana kwa kweli.
 
Muhimili wa mahakama unajitegemea ,acha ale jeuri yake,wazungu wamemchoka ,kaona isiwe tabu ,ajirudie kwao,
Alivyokuwa anapakaza mavi yake kwenye kuta za wazungu huko ulaya mbona hukumkanya ?
Aje aendelee na viporo vyake ,pia na mapya yapo pia
Kabisa mkuu, utadhani yeye ndiye wa kwanza kwenda ulaya. Watu tuna marafiki wako TEXAS huko wapo kimya na wanaitangaza nchi yetu vyema.
 
sawa, ila kabla ya hapo- subira yavuta kheru ndugu, baada ya uchaguzi tafadhari
Usidhani watu hatuna akili humu uchaguzi ukipita atasingizia anasumbuliwa na vyombo vya dola kwa kuwa aligombea uraisi halafu huo mtego wako wa kitoto na kijinga unamuwekea nani ? kichwani kwako unawaza kuwa labda uchaguzi ukiwa umepita Lisu akiwa kashinda uraisi ohhh atakuwa na immunity kama Raisi kwa hiyo vikesi vyake vitakufa kifo cha mende kwa kuwa raisi huwezi mpeleka mahakamani!!! vimitego vyako vya kitoto tena kitoto mno.Lisu akitua tu ni Segerea hakuna cha kusubiri uchaguzi upite wala nini.Ni anatua tu breki Segerea.
 
Kwa hio rais ndio katiba ya nchi/ndie Mahakama akiamua kusamehe kosa la ufisadi linafutika la sio?

Hakika elimu za hapa na pale ni shida sana kwa kweli.
kosa la ufisadi huthibitishwa mahakamani sio raisi
 
Hivi kwanini Viongozi wa wanyonge wanaopendwa na watu wametunga sheria ya kuogopa wao wasishitakiwe mahakamani wakitoka madarakani?
Sheria huwa hazitungwi na viongozi wa serikali hutungwa na bunge ambako wawakilishi wa wananchi ndiko waliko
 
Kabisa mkuu, utadhani yeye ndiye wa kwanza kwenda ulaya. Watu tuna marafiki wako TEXAS huko wapo kimya na wanaitangaza nchi yetu vyema.
Naomba jibu tena mzee baba.

Hivi kwanini Viongozi wa wanyonge wanaopendwa na watu wametunga sheria ya kuogopa wao wasishitakiwe mahakamani wakitoka madarakani?
 
Kabisa mkuu, utadhani yeye ndiye wa kwanza kwenda ulaya. Watu tuna marafiki wako TEXAS huko wapo kimya na wanaitangaza nchi yetu vyema.
hao marafiki zako na wenyewe walipigwa risasi kama TL?!
hivi huwa mnafikiria kwa kutumia ubongo wa kawaida au matope?!
 
SUALA LA TUNDU LISSU NI KIPIMO TOSHA CHA BUSARA ZA RAISI NA DOUBLE STANDARD ZA KIMAHAKAMA KATIKA MUKTADHA WA KUWA WOTE SAWA KWENYE USO WA SHERIA!

NB;
KAMA LISSU ANA KESI YA KUJIBU KWA MUJIBU WA SHERIA BASI SHERIA IFUATE MKONDO WAKE!
 
mmmmmmmm, sio baada ya uchaguzi akifika tu anatakiwa aripoti mahakamani.

sidhani kama unapenda vurugu mechi ndugu yangu... vyovyote viwavyo, aachwe tu hadi uchaguzi, hata kama hajaomba msamaha, sijatumwa ila kwa niaba yake, afikiriwe tu kama Yesu alivyomfikiria yule mwizi mwingine wa msalabani kwa hadi ya wote kuwa peponi siku ile...
 
Naomba jibu tena mzee baba.

Hivi kwanini Viongozi wa wanyonge wanaopendwa na watu wametunga sheria ya kuogopa wao wasishitakiwe mahakamani wakitoka madarakani?
KWANINI VIONGOZI WANAOJINASIBU KUABUDU DEMOKRASIA WANABAKA KATIBA ZAO NA KUONDOA UKOMO WA MADARAKA!?

CCM KUMEOZA NA UPINZANI KUNATOA FUNZA!
 
SUALA LA TUNDU LISSU NI KIPIMO TOSHA CHA BUSARA ZA RAISI NA DOUBLE STANDARD ZA KIMAHAKAMA KATIKA MUKTADHA WA KUWA WOTE SAWA KWENYE USO WA SHERIA!

NB;
KAMA LISSU ANA KESI YA KUJIBU KWA MUJIBU WA SHERIA BASI SHERIA IFUATE MKONDO WAKE!
Kesi Lisu anazo kibao za kumtosha tu.Kwa Lisu sio busara zinahitajika sababu kesi zake ziko mahakamani.Ni sheria kufuata mkondo wake, sio busara kufuata mkondo wake!!!!
 
Back
Top Bottom