Rais Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi

Rais Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi

Watanzania Ujue Mungu anatuona nafikiri kwa uhakika kuna wengine wanacommenti bila ya kusikiliza kilichosemwa kwenye hiyo hotuba.
 
Unatia aibu.... Ni hasara kwa familia yako maana hawana mlezi!

Maneno ya faraja yanasaidia nini sasa ikiwa ukweli watu wanahitaji kukarabati makazi yao?

Yani familia yako haina msosi alafu unawapa maneno ya faraja kwamba msijali chakula mtapata tu! Badala ya kuwambia jishughulisheni wewe unawaambia watandike mikeka wakae wasubiri kuletewa?

Hovyo kabisa
Kwani hivyo vibanda/nyumba zao zilizodondoshwa na tetemeko walijengewa na serikali? Walibweteka wakasubiri kujengewa na serikali? Hivi kulikuwa na tatizo gani serikali ikapeleka misaada kadri inavyoweza na ikatoa pole kwa waathirika badala ya longolongo zisizostahili? Mbona serikali yenyewe imeshindwa kutumia jeshi na kitengo chake cha maafa, nayo tukiiambia imebweteka kwa kuwategemea matajiri ambao ilikuwa inawasimanga kabla itafurahi?
 
mseven katisha.. alikua akichangia udsm pale inaelekea anamapenzi na hii nchi
 
Hatimaye mkuu kazungumza japo kwa kuchelewa sana. Ila naomba niulize: hivi inawezekana kukawa na watu wanaoamini kuwa "tetemeko limeletwa na serikali" mpaka mkuu atake wananchi wafahamishwe kuhusu hilo?
Nikama wale walio sema wanaiomba serikali next time iandae kupatwa kwa jua mkoani kwao kwani imekuwa ni kivutio kikubwa sana wakidhani kupatwa kwa jua kumeandaliwa na serikali
 
Magufuli is very RIGHT. Maisha yanaendelea. Tusitegemee serikali kutumia rasilimali zake kuwajengea nyumba wahanga. In fact to me, Magufuli angetumia hiyo hela ya michango kukarabati mashule, hospitali na barabara zilizo athirika. Na ndo inapashwa kuwa hivo.

Hili janga ni funzo kwetu sote. Jamani katieni bima nyumba zenu na other valuable properties (by the way bima ya nyumba iko chini mno). Tatizo waswahili kila kitu tunakifanyia mzaha tukitumia visingizio lukuki. Lakini kwa mwenye akili dunia ya leo huwezi kujenga nyumba yako kwa hizi hela za kuokoteleza...ukashindwa kuikatia bima.

Najua wengi tutapiga kelele tukisingizia umasikini (this is a popular excuse so far in our country).......lakini ukweli unabaki. Dunia ya leo...haina msaada tena! Ni jukumu lako kufanya uwezalo kujikinga na haya majanga yasiyotabilika (umeme, mafuriko, tetemeko nk). Ndo maana utakuta wazungu hata akizeeka hawi mzigo kwa ndugu au serikali. Au hata akifa...ana bima yake ya kumhifadhi kwenye nyumba yake ya milele. They always work hard and save for the rainy day!

Leo hii baadhi ya waTanzania wenzetu walioko mambelezz (au hata hapa nyumbani) wanatangulia mbele ya haki...tunaanza kupitisha bakuli! (kusafirisha mwili). This is bad and we should correct this culture. Kateni bima za maisha kwa uhai wenu, nyumba zenu na mali nyinginezo. Tuache hii tabia ya kuishi kwa kutaka kuonewa huruma na binadamu wenzetu. Undugu au urafiki haina maana kwamba tuwe mizigo kwa wenzetu.

Maisha yako. Jukumu lako.

Masanja
Nyie Wasukuma akina Masanja mna wakati mgumu sana wa kumtetea mwenzenu, kila siku anakuja na jipya! Kazi yenu itakuwa ni kutetea kila uharo kuwa unanukia vizur
 
Leo Sumbawanga nako wamepata majanga ya mvua kubwa ya upepo na barafu. Kuna nyumba zimebomoka na kuezuliwa paa, mifugo imekufa. OMBI langu kwao wakae tuu kimya maaana wasiombee kutana na tetemeko la maneno.

Mungu akitaka taifa lake limrejee hutumia matukio kama haya. Tutafakari pamoja
 
Nchi hii tulizoea kauli za kinafiki zisizotekelezeka, sasa tumepata Raisi anayenyoosha maneno hata kwenye wakati mgumu ni kuongea ukweli tu kwa kwenda mbele.
Kwa wapinzani ni haki yao kikatiba kubeza ukweli ambao umesemwa na Mh raisi, wao walitaka Raisi atoe ahadi zisizotekelezeka ili ije kuwa mtaji wa kisiasa huko mbeleni.
Hizi ni zama za kunyoosha maneno, mh raisi ameanza na sisi huku kitaa tuige mfano wako maana tumekuwa jamii ya kinafiki kupindukia
Sawa mkuu tunasubiri ujenzi wa viwanda nadhani hii ni kauli inayotekelezeka.
 
Kuna kitu kinakosekana.watu wana changa fedha ziende kwa waathirika wa tetemeko la ardhi ili wapate chakula. Malazi na matibabu.Watu wanajua uwezo wa watanzania! Mtu anapo patwa na dharura kama hii siyo rahisi kukabiliana na matatizo yote kwa wakati mmoja.Hivyo kuwaambia wajitegemee kujenga wenyewe ni kama kuwachoma kisu kwenye kidonda.

Binafsi nadhani wangesaidiwa kwanza warudi kwenye maisha yao ya kawaida ndio maneno ya kwamba watu wajifunze kujitegemea kukabiliana na dharura yatolewe.

Ndio maana tunatoa mabati, segment, misumari, magodoro, na vyakula tunataka waathirika warejee kwenye hali ya kawaida haraka iwezekanavyo! Kukaa na misaada ya watu muda mrefu haileti picha nzuri.
 
Mani anataka ahadi wakati huu? Kuna misiba Kule, watu wanalala nje watoto na kina mama, hata chakula ni shida.
Atoe basi kauli za kiungwana kuonyesha anajali au anyamaze kama hawezi kuji control.
Hivi kauli kama zile mtu kama mtendaji wa kata akizitolea Kule Bukoba atashuka hai kweli jukwaani? Sii mvua ya mawe itamfuata alipo!
Wewe ulitaka asemeje?

Hebu rudia tena kusikiliza hako kahotuba hapo huu.


Ulitaka aseme Serikali yangu itahakikisha ndani ya mwezi mmoja wahanga wote Wa tetemeko watakuwa wamesha jengewa nyumba nzuri,na wanapatiwa Chakula mwaka mzima bure,na makaburi ya walio tangulia mbele za haki yana jengwa buree.?

Amesha sema muache mihemuko ya kisiasa kwenye suala la majanga kama hili,tujitokeze kusaidia wahanga, nawewe muhanga usibweteke jishughulishe,Serikali YAKE itatoa mile ilicho nacho,,

Usije sema nimepewa bati 20 nyumba yangu ni ya bati 70.

Hili janga halija letwa wala kuratibiwa na Serikali sema itathaminisha Mali iliyo haribiwa na kukipwa hiyo sahau,utasaidiwa kile Serikali kuu imekipata toka ndani na nje kwa wadau.
 
Tujifunze kukabiliana na changamoto ya mabadiliko,ni bora kuambiwa ukweli kuliko ahadi za kisiasa,mfano ni kipindi cha Mzee wa msonga alivyosemaga serikali haina uwezo wa kuleta mvua na wananchi walimwelewa.
Ukweli upi huo tulioambiwa? Ni nani hajuwi kwamba tetemeko halijaletwa na CCM wala serikali? Ni kazi gani ambazo wananchi wa kagera walikuwa hawafanyi wamelala mpaka sasa unawambia fanyeni kazi? Watu wamepata majanga badala ya kuwa nao bega kwa bega ndio kwanza unatoa kauli za kuwabeza,unaleta siasa na ubabe haisadii.najuwa hata ccm wanajuta kumweka huyu mtu hana utu. Kweli sura siyo roho.
 
Nachompendea Mh prezidaaa ajui mungunya maneno anakupa moja Kwa moja haitaji porojo porojo Sijui hivi Mala vile yupo straight

Kagera wameambiwa ukweli so wasibweteke
 
Nyie watu mna vituko sana !sasa ikiondolewa kodi ndio wale masikini ya mungu watajenga?wewe mtu kwa kujipangia tu kujenga unaanza unanyoa punk unakuja kumaliza nyumba una kipara cha uzee na mvi hadi kwenye nyusi!
Serikali isikwepe iwasaidie au watu kwa asilimia tele tu,sio kusubiri washindwe maana hatujui watatumia kipimo gani kuhakiki kama mwananchi huyu kashindwa!
Serikali lazima itafakari hill kwa kina sana. Je wale ambao nyumba zao husombwa na mafuriko hujengewa sana nyumba mpya na serikali? Wakilianzisha tu mahali fulani, itakuwa ni kawaida na kawaida hugeuka kuwa ni sheria machoni mwa wanajamii. Wale walisaidiwa, kwa nini sisi tunabaniwa?
Wale was mafuriko hadi Leo hii wanaishi kwenye mahema!
 
Back
Top Bottom