Rais Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi

Rais Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi

Nagazengele numba ami ng'wana?Onene yaya gete!yalinukuliwa maneno hayo na wakazi wa Mwakata Kahama iliponyesha mvua ya matofali ya mawe, yakisemwa na mtu mkubwa sana nchi hii
Oyaga gete ngosha
 
Tatizo waswahili tumezoea ahadi hewa za wanasiasa. Ndo maana tunadanganywa kila siku na tunakubali. Magufuli kaamua kuwa mkweli of what is on his mind. Go figure.

Hivi kweli kwa akili yako tukufu...serikali inaweza kuwajengea nyumba wahanga wote wa hili tetemeko? Get real bro!
Acheni kupotosha nani kataka kujengewa wakati TV zinaonyesha wanajijengea?
Mbona MNA roho za kishetani namna hiyo? Ukweli ukweli! Mbona wakati mnacheza mapanga shaaa na pushup majukwaani hamkuwa mnatoa huu ukweli?
 
Sita shangaa kusikia uko mahakama ya hakimu mkazi,kisutu! Kwa jinsi ulivyo panga maneno yako!
 
2020 tuone kama hizo pushups zitaleta kura. Mtaanza kuwalamba miguu watu wa Kagera huku jeuri mmeficha mfukoni lakini washastuka. Ujinga wa njia ni kwenda kurudi akili yako
Ukileta mihemuko yako ya kisiasa kwenye suala kama hili utakufa maskini.
CCM AU CHADEMA HAWATAKUJA KUKULIMIA SHAMBA LAKO .
 
Serikali iwasaidie lakini si vizuri kuwapa ahadi hewa hasa kujenga nyumba zao. Labda serikali iwaondolee kodi kwenye vifaa vya ujenzi hasa cement, bati na nondo
Wanapelekewa cement,mabati na pesa taslimu. Rais kasema sawa kabisa misaada inakwenda lakini waanze kujishughulisha. Wengine ni matofali ya udongo, ukuta mmoja umedondoka unatakiwa chimba dongo hapo anza ujenzi huku ukisubiri misaada.
 
Sio kazi ya serikali kujengea watu nyumba!
Sasa unaponiambia nisisubiri kujengewa nyumba kwani nimekwambia nataka serikali inijengee? Hii nyumba yangu iliyobomolewa na tetemeko serikali ndiyo iliyonijengea?
 
Ukileta mihemuko yako ya kisiasa kwenye suala kama hili utakufa maskini.
CCM AU CHADEMA HAWATAKUJA KUKULIMIA SHAMBA LAKO .
Mimi sio masikini kwani nimeajiri watu wenye elimu kuliko pengine uliyonayo (sikujui ila maandiko yako yana onyesha upeo wako) lakini nawasemea wale wahanga anbao hata mablanketi ya serikali yao hawajayaona labda ya Kenyatta kama yamefika. Hata michango iliyochangwa bado serikali inashindwa kupeleka utadhani wameweka benk fixed deposit ili wale faida
 
Kwa hiyo allihairisha safari ya Zambia kwa maneno ya kejeli kama haya kwa wahanga?
Rais anatakiwa awafariji wafiwa sio kuwasimanga
Yaani vifo va zaidi ya watu 15 ndiyo Rais anatoa maneno ya hovyo hovyo kama haya?
 
Hivi ingetokea Chato kauli hizi zingetoka ?!
Mungu si athumani, naomba Mungu siku moja litokeo nyumbani kwake, alafu aje achukue wiki nzima yupo kimya, alafu akizungumza azungumzee maneno kama haya aliyoyasema!

NINA HASIRA ACHA NIISHIE HAPA
 
Mimi sio masikini kwani nimeajiri watu wenye elimu kuliko pengine uliyonayo (sikujui ila maandiko yako yana onyesha upeo wako) lakini nawasemea wale wahanga anbao hata mablanketi ya serikali yao hawajayaona labda ya Kenyatta kama yamefika. Hata michango iliyochangwa bado serikali inashindwa kupeleka utadhani wameweka benk fixed deposit ili wale faida
Utakuwa maskini Wa akili sasa.
Huwezi leta ushabiki wakisiasa kwenye suala la majanga ,,halafu unashinikiza Rais akurupuke kugawa kilicho patikana bila mpangilio maaluumu.

Unajifanya umeajiri ,lakini hata hema MOJA umeshindwa kupeleka.
NARUDIA TENA MIHEMUKO YAKO YA KISIASA SUBIRI 2020 KAMA ULIVYO SEMA.
 
Ni mtizamo tu. Serikali za nchi tofauti (baadhi zikiwemo Kenya, Uganda,China} zimechangia. Watu Binafsi wamechangia. Kampuni za mafuta zimejitolea kujenga shule 2 kati ya 4 zilizoathirika. Kati ya misaadi ni pamoja na mabati. Hadi hapo serikali ya Jamhuri ya Tanzania haijatangaza imejipanga kwa kiasi gani. Jeshi la Wananchi lipo. Hatuoni mantiki Jeshi likatumika kujenga nyuma alfu kadhaa kwa misaada iliyopatikana.
Yaani msheshimiwa sijui kama anaeleweka na waathirika. Since then kukaa tu na kupokea tararifa ofisin without going to the scene?! At the same time ukiendelea na shughuli za kuteua na kuapisha? Hivi madhara haya angetokea nyumbani kabisa bado
Hivi wewe aliyekwambia anataka kujengewa nyumba ni nani? Tangu nchi hii iumbwe ni serikali ipi iliwahi kuwajengea wananchi nyumba waliopatwa na majanga kama haya? Watu wanacho complain ni kauli zisizo na faraja zilizotolewa na mkuu wa nchi.hata kama wakiamuwa wasitoe chochote huwezi kuwambia wananchi msitegemee serikali fanyeni kazi kana kwamba wao hawafanyagi kazi au wamekaa tu kusubiri serikali. Haina shida ndugu zao wapo na watakaoguswa watawasaidia nakuwafariji. Sikutegemea kama rais angeweza kuongea kauli zile achilia mbali kwenda kuwatembelea wahanga wa tetemeko. Wana kagera hawana hiyana wataendelea kumuombea huku wakitambuwa sura siyo roho.
Umeongea kweli tupu mkuu hakika ukimsikiliza rais hupati faraja yoyote zaidi ya maumivu kuongezeka. Wakati mwingine nasikia machozi kunilenga lenga. Yaani ndani ya nyumba mmevamiwa na nyoka mnalia baba yuko wapi halafu mnaletewa ujumbe kuwa msitegemee yeye kuja kumuua huyo nyoka kwakuwa uwezo huo hana na hata fimbo ya kumpigia hana na mbaya hafiki hata kuwaona watoto wake zaidi anasema jiokoeni wenyewe msinitegemee mimi tu anzeni kupambana naye! Tufwileee malafyale! Kule Mbeya tumeambiwa mzee mmoja amesema eti kupatwa kwa jua ni ishara ya Mungu kumkubali rais Magufuli. Sasa sijui kwa hili tetemeko ni ishara ya nini? Sasa gazeti la Habari Leo wangemfuata tena yule mzee atuambie je tetemeko hili ni ishara ya nini kwa rais? Inauma sana watu wakiwa kwenye matatizo kuanza kusutwa. Poleni sana wana Kagera!
 
Miaka ya nyuma tulisema nchi ilikuwa autopilot miaka hii tunasema nchi iko wapi vile?
 
Wengi wetu hatujazoea kusikia ukweli ukitolewa live. Maudhui ya alichosema Mhe. Rais yana mantiki kubwa labda ni namna alivyowasilisha ndiyo inayoweza kuleta ukakasi kwa wahanga wa tukio.
 
Back
Top Bottom