Rais Magufuli: Wabunge msiogope kuikosoa serikali, Tukosoeni lakini ukosoaji wenu uwe na tija siyo ilimradi kukosoa tu!

Rais Magufuli: Wabunge msiogope kuikosoa serikali, Tukosoeni lakini ukosoaji wenu uwe na tija siyo ilimradi kukosoa tu!

Hongera kwa hoja zilizo na mashiko.

Mimi si mwumini wa demokrasia ya vyama vingi kwenye nchi maskini. Viongozi wa upinzani muda wote ni kuvuruga juhudi za Serikali iliyoko madarakani ili ichukiwe na wapiga kura. Wakati huohuo viongozi wa Serikali iliyoko madarakani huogopa kuwachukulia hatua wapinga maendeleo kwa kuogopa kuchukiwa na wapiga kura.

Hicho ndicho kilichotokea toka vyama vya upinzani viasisiwe nchini. Lakini upepo ulibadirika alipoingia Rais Magufuli, mtu asiyeyumbishwa na mthubutu kiasi cha kuwafunga midomo viongozi wa upinzani, wabwabwaji na wenye nia ya kuvuruga juhudi za maendeleo. Matokeo yake kila mtu ameona.

Kwa kuwa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, ambazo sasa zitanaongozwa na Chama kimoja, tutegemee maendeleo makubwa yatakayotokana na ushindani chanya na hai kati ya Halmashauri zote, na ndani ya Halmashauri (kwa maana ya Majimbo/Kata za uchaguzi).

Kenya hapo wana mfumo wa vyama vingi wenye nguvu, wanatuzidi kwa mbali sana kiuchumi. Au huku kwetu viongozi ni akili ndogo kiasi kwamba hawawezi kufanya kazi wakiwa na wapinzani? Enzi za Nyerere wakati tunavaa viraka ilikuwa ni chama kimoja, mbona hatukufikia kwenye hayo matamanio yako?
 
kikubwa kwa wenye akili ni kwamba huwezi kuomba kusifiwa automatic watu watakusifia, ukiona unaomba kusifiwa jua huna ulilofanya likafaa sifa, hii ina aplay kwenye kukosolewa huwez kuomba kukosolewa hiyo inakuja automatic! ukiona unaomba kukosolewa jua huna baya au hupendi kukosolewa so watu wanakuocha uende utakavyo, na wale watakaoitikia wito wa kukukosoa jua watakukosoa kwa namna unavyotaka ukosolewe. kitu ambacho hakuna utanadirika
 
Huyu ni bonge la mnafiki lini akakubali kukosolewa. Huyu hana karama ya uongozi na kama alivyosema Kingunge Ngombale Mwiru (Rip) alifaa tu kubaki mnyapara wa barabara. Period.

Ameitia nchi hii aibu kubwa ambayo haijapata kuonekana na tukiwekewa vikwazo ni yeye ndiye atawajibika kwa madhara yake . He is a poor excuse for a leader.
 
Kenya hapo wana mfumo wa vyama vingi wenye nguvu, wanatuzidi kwa mbali sana kiuchumi. Au huku kwetu viongozi ni akili ndogo kiasi kwamba hawawezi kufanya kazi wakiwa na wapinzani? Enzi za Nyerere wakati tunavaa viraka ilikuwa ni chama kimoja, mbona hatukufikia kwenye hayo matamanio yako?
Ni kweli Kenya kiuchumi wako mbali. Je, unajua sababu zake? Kama hujui, futa hoja yako.

Kwa taarifa yako, katika miaka 5 ya utawala wa Magufuli, kiongozi aliyethubutu na kushinda mbinu za upinzani za kugombania fito wakati ni ujenzi wa nyumba hiyohiyo, uchumi wa Tanzania unakua na kuimarika. Hakuna shaka sasa, katika miaka 5 ijayo, uchumi wa Tanzania utakua maradufu wa Kenya. Sababu kubwa ni kwamba Halmashauri zote ni za chama kimoja, na Bunge la chama kimoja. Hakuna kugombania fito tena.
 
Hiyo kauli ameiremba tu ila hiyo ni kauli ya katazo la kumkosoa na ukiona hujamuelewa jua akili yako ni fupi kidogo kuelewa hilo
 
Hayo mapungufu mengi ndio yatakayo mfanya aonekane rais wa hovyo..na atakubukwa kwa wizi wa kura na uminywaji wa demkrasia na haki za kibinadamu.
Kanuni ya uongozi inasema usiwe mtu wa kushauriwa ovyo ovyo , ni heri ufanye mistake kuliko kupata ushauri mwingi mwingi Kwa wakat mmoja , yaan hapo ndo utapotea kabisa mwisho wa sku kila mmoja atakuona manyanya, waswahili wanasema miluzi mingi hupoteza mbwa....

Back to the topic , ushauri wa wapinzani ulikuwa mixed na chuki na lengo kuu ilikuwa kumu-outclass mweshimiwa ili aonekane hafai anapuyanga tuuu, kitu kingine alichokisema Nape juzi kinamake sense Sana, kwamba wabunge wa CCM last walikuwa kazi yao ni kudefend Kwa sababu ukiruhusu hoja za wapinzani zipae mnaonekana nyie miyeyusho ,

Ila Kwa sasa wana nafas nzuri ya kukosoa Kwa sababu wanajenga nyumba moja na Wana rangi moja .... JPM ana mapungufu mengi Sana ila atakuja akumbukwe kuwa among of the best president in tanzanian history ever, mda ni mwamuzi sahihi
 
Kanuni ya uongozi inasema usiwe mtu wa kushauriwa ovyo ovyo , ni heri ufanye mistake kuliko kupata ushauri mwingi mwingi Kwa wakat mmoja , yaan hapo ndo utapotea kabisa mwisho wa sku kila mmoja atakuona manyanya, waswahili wanasema miluzi mingi hupoteza mbwa....

Back to the topic , ushauri wa wapinzani ulikuwa mixed na chuki na lengo kuu ilikuwa kumu-outclass mweshimiwa ili aonekane hafai anapuyanga tuuu, kitu kingine alichokisema Nape juzi kinamake sense Sana, kwamba wabunge wa CCM last walikuwa kazi yao ni kudefend Kwa sababu ukiruhusu hoja za wapinzani zipae mnaonekana nyie miyeyusho ,

Ila Kwa sasa wana nafas nzuri ya kukosoa Kwa sababu wanajenga nyumba moja na Wana rangi moja .... JPM ana mapungufu mengi Sana ila atakuja akumbukwe kuwa among of the best president in tanzanian history ever, mda ni mwamuzi sahihi
Kwani bunge si sehemu ya kujadiliana na kushauriana hatimae kuja na muwafaka wa kitu kinachoazimiwa? Wabunge ni wawakilishi wa watu katika majimbo yao, sauti zao ni sauti za wawakilishwa ambao wamewachagua.
Sisi sote ni watanzania, vyama vya siasa ni vya watanzania vipo kwa ajili ya watanzania na Tanzania ndiyo nyumbani kwetu. Tukianza kutengana na kufanyana maadui kwa ajili tu ya tofauti ya vyama vyetu au fikra zetu basi tunakaribisha uharibifu mkubwa ndani ya nchi yetu.
Tunajua tulitawaliwa na waliyotutawala hawajaicha hii nchi hivi hivi tu, bali wananchi walipigania uhuru wetu, sasa tukitengeneza tofauti na uhasama baina yetu yule aliyeonewa anaweza kwenda kutafuta msaada nje na hapo ndipo tunaweza kuruhusu yule aliyetutawala kupata upenyo wa kurudi tena. Ni bora kama watanzania tukakaa chini na kutafakari maslahi mapana ya nchi yetu na matatizo yetu tukayasuluhisha wenyewe kwa weledi wa hali ya juu, kwa kufanya hivyo tutakuwa waungwana na wenye kuheshimika duniani kote.
Na swala kwa wabunge si kupinga au kuunga mkono hoja, bali ni nini maslahi ya hoja hiyo kwa wananchi na nchi kwa ujumla.
Na kitu cha muhimu ni tuwe na taasisi imara zenye mifumo mudhubuti, ili pakitokea na mtu mwenye mapungufu ya kupindukia taasisi hizo zinaweza kumdhibiti kama si hivyo tusubiri hilaki. Kwani katika historia hakuna kiongozi jeuri aliyefanikiwa.
 
wabunge ni vizuri watoe ushaur wa kujenga nchi na naipongeza sana hotuba iliyotolewa inaonesha mwerekeo mzuri hapo mbeleni.pia mikakati iliyopo ni mizuri sana.rejea hotuba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli Kenya kiuchumi wako mbali. Je, unajua sababu zake? Kama hujui, futa hoja yako.

Kwa taarifa yako, katika miaka 5 ya utawala wa Magufuli, kiongozi aliyethubutu na kushinda mbinu za upinzani za kugombania fito wakati ni ujenzi wa nyumba hiyohiyo, uchumi wa Tanzania unakua na kuimarika. Hakuna shaka sasa, katika miaka 5 ijayo, uchumi wa Tanzania utakua maradufu wa Kenya. Sababu kubwa ni kwamba Halmashauri zote ni za chama kimoja, na Bunge la chama kimoja. Hakuna kugombania fito tena.
Daaaah ww kweli kijumpu.

Acheni uoga katika uongozi.

Ivi kweli ata Kama mnajenga nyumba yenu ukatoa Raman ya nyumba mtoto au mkeo akikushauri juu ya Raman iyo japo mabadiriko kidogo tu.

Utahisi dogo anataka akupindue?
 
Hongera kwa hoja zilizo na mashiko.

Mimi si mwumini wa demokrasia ya vyama vingi kwenye nchi maskini. Viongozi wa upinzani muda wote ni kuvuruga juhudi za Serikali iliyoko madarakani ili ichukiwe na wapiga kura. Wakati huohuo viongozi wa Serikali iliyoko madarakani huogopa kuwachukulia hatua wapinga maendeleo kwa kuogopa kuchukiwa na wapiga kura.

Hicho ndicho kilichotokea toka vyama vya upinzani viasisiwe nchini. Lakini upepo ulibadirika alipoingia Rais Magufuli, mtu asiyeyumbishwa na mthubutu kiasi cha kuwafunga midomo viongozi wa upinzani, wabwabwaji na wenye nia ya kuvuruga juhudi za maendeleo. Matokeo yake kila mtu ameona.

Kwa kuwa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, ambazo sasa zitanaongozwa na Chama kimoja, tutegemee maendeleo makubwa yatakayotokana na ushindani chanya na hai kati ya Halmashauri zote, na ndani ya Halmashauri (kwa maana ya Majimbo/Kata za uchaguzi).

Tangia 1962 hadi 1992 tulikua na Chama Kimoja, Je maendeleo uliyaona??
 
Kanuni ya uongozi inasema usiwe mtu wa kushauriwa ovyo ovyo , ni heri ufanye mistake kuliko kupata ushauri mwingi mwingi Kwa wakat mmoja , yaan hapo ndo utapotea kabisa mwisho wa sku kila mmoja atakuona manyanya, waswahili wanasema miluzi mingi hupoteza mbwa....

Back to the topic , ushauri wa wapinzani ulikuwa mixed na chuki na lengo kuu ilikuwa kumu-outclass mweshimiwa ili aonekane hafai anapuyanga tuuu, kitu kingine alichokisema Nape juzi kinamake sense Sana, kwamba wabunge wa CCM last walikuwa kazi yao ni kudefend Kwa sababu ukiruhusu hoja za wapinzani zipae mnaonekana nyie miyeyusho ,

Ila Kwa sasa wana nafas nzuri ya kukosoa Kwa sababu wanajenga nyumba moja na Wana rangi moja .... JPM ana mapungufu mengi Sana ila atakuja akumbukwe kuwa among of the best president in tanzanian history ever, mda ni mwamuzi sahihi
Binafsi siwezi kuja kusahau kuwa Jiwe alikuwa Rais feki, hata afanye nini Jiwe ni Rais feki. Period
 
Mabalozi wa nchi za magharibi hawakwenda bungeni..tutegemee bajeti ijayo itakuwa haina misaada kutoka nchi hizo...maweee
 
Kuna wakati wapinzani walidai serikali ya awamu ya 5 haitaki kukosolewa bali inataka kusifiwa tu. Kumbe walikuwa waongo.

Rais Magufuli amewataka wabunge wote bila kujali itikadi zao kuikosoa serikali na kuleta solutions za changamoto na siyo ilimradi kukosoa tu.

Huu ni ujumbe wa kijasiri sana kutoka kwa mkuu wa nchi.

Maendeleo hayana vyama!
Dictators wote wako hivyo, ndizo kauli zao. Then unapotezwa
 
Hatutaki Sababu ,alisha sema Wapinzani ndio wana mkwamisha kuleta Maendeleo hivyo amewafyekelea mbali na sasa tunahitaji hayo Matokeo ya Kauli zake tata.
 
Unaunga mkono kitu gani?
Huyo jamaa amekuwa mchumia tumbo, mwanzoni alikuwa anamsifu Jiwe kwa kebehi, yaani ilikuwa ukisoma between the lines unajua kabisa jamaa anamponda Jiwe, ila baada ya njaa kuzidi akabadilika na kujifanya kada mtiifu wa fisiemu na kuanza kusifu kwa kumaanisha ili ale teuzi. Kimbe Jiwe alishamshitukia na baadhi ya Mataga walilijua hilo ndiyo maana wajumbe wakafanya yao na kuambulia kura moja. Sasa hivi kabaki alone, fisiemu hawamtaki na upande mwingine ndiyo hivyo tena. Kifupi jamaa anatafuta teuzi kwa hali na mali lakini hapati mana alishabugi. Atasifu mpaka avue nguo lakini atatoka bila bila, hayo ndiyo malipo ya kutokuwa na msimamo maana adui anabaki kuwa adui na rafiki anageuka adui.
 
Tunategemea wabunge wetu wataonesha uwezo mkubwa sana katika kuishauri na kuisimamia serikali.
 
Nanukuu:-
Mheshimiwa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Ametusaidia Sana Kuna Wabunge Baadhi Yetu Tusingerudi Bungeni Kabisa
Lakini Kila Alikopita Alisema Nileteeni Huyu
Hapo Sasa Nani Atampinga Huyo Mbunge Toka Ccm
 
Subutuuu atokee kimbunge kijidai kuikosoa serikali weeeh,atapigiwa simu tu we si unajua namna ulivyofika hapo bungeni,siku ya pili anadidimia kwenye kiti anatokea kichwa tu.
 
Hapo ni sawa na Simba kuwaambia kundi la Swala wamkosoe! Sina hakika kama watakubali.
 
Back
Top Bottom