Rais Magufuli: Watanzania endeleeni kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Korona. Sijazuia matumizi ya Barakoa!

Kama Bwana asipoulinda mji waulindao wanafanya kazi bure mbona yanafanyika maombi mengi sana dhidi ya Corona ikiwa ni pamoja na kufanga ila bado watu wanapukutika?

Ni sahihi kufanya kitu ambacho hakina msaada?Matokeo ya maombi huwa yanapimwaje?Yaani nikitaka kujua mafanikio ya maombi katika kapambana na Corona napimaje?
 
Kama hujaona mafanikio Yake kwa mwaka 2020 Basi una matatizo.

Mwaka huu kitaifa yameanza Jana 20 February..ni siku tatu.
Hii haimaanishi tutaishia hapo.

Wewe endelea kubeza kila kitu na kumlisha maneno ambayo hajayaongea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio amesema muendelee "kujifukizia" hata wasaidizi wake wameumwa na wamepona kwa "kujifukizia". Hata watoto wake wameumwa na wamepona kwa kujifukizia heheh! kumbe Rais ana dawa sisi tunahangaika tu!
Tuna kiongozi tunayeambiwa ni mwanasayansi lakini haamini mambo ya kisayansi, kweli elimu ya bongo ni nyoso
 
Afya yako ni wajibu wako. Anza kwanza wewe kutelekeza wajibu wako..unataka rais aje akuvalishe barakoa na unaijua corona vizuri. Acha visingizio
Akili ya kisoda hii, niko na barakoa yangu hapa una jingine?
 
Umejuaje kuwa mafanikio ya mwaka 2020 yalitokana na maombi na wala siyo kutokana na sababu nyingine kama vile zile hatua tulizochukua kipindi kile ambapo kipindi hiki hatujazichukua,labda ilitokana na kirusi cha Corona variant 1 ambacho hakikuwa kikali kwetu na sasa hivi labda tuna variant 2 ambacho ni kikali zaidi,e.t.c?
 
Uchumi gani ambao Tanzania iko nao hadi mataifa makubwa yafanye nayo vita? South Afrika, Misri, Nigeria wao watasemaje kama Tanzania itasema ni vita? Tumia hata ka akili kadogo uliko nako kufikiri.
Unamwambia atumie kitu ambacho hana. Mtu mwenye akili hawezi kuwa na mawazo butu hivyo
 
Utajua wewe
Kuna kampeni ya kifamilia, wilaya, mkoa na kitaifa na kwa kila ngazi kuna kiongozi wake na huyo kiongozi anawajibu wake hata ngazi ya kimataifa kuna kiongozi wake akivurunda huko tutalalamika tu.
 
Mtu aliyezoea matumizi ya nguvu kwa kila kitu pasipo na akili ni majanga
 
i thought usomi wake ungemsaidia lakin 0.
yaan amejenga maadui wake kichwani ambao hawaonekani.
na mbaya zaidi analazimisha wananchi waamini the same.
na mtu yoyote aliekaribu nae asipoamini hivyo basi lazima afukuzwe ateuliwe mwingine.
Waliotilia shaka usomi wake wana hoja
 
Baadhi ya ndugu zangu walokole mnajazana sana upepo wa ujinga
 
Nimekwambia Bwana asipoulinda mji waulindao wanakesha bure.
Ingekuwa kichukua hatua pekee kunatosha basi mataifa ya wenzetu wangekuwa wanaishinda Corona.

Kuchukua tahadhari pekee hakutoshi,ndiyo maana Rais anasisitiza maombi na Mungu ni mwaminifu atatenda tena.

Wewe endelea kubeza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimebeza wapi?Mimi nahoji masuala!Unaposema kuwa ingekuwa kuchukua hatua peke yake wenzetu wangeshinda kwani umejuaje kuwa hakuna wenzetu waliomtanguliza Mungu mbele?
 
Nimebeza wapi?Mimi nahoji masuala!Unaposema kuwa ingekuwa kuchukua hatua peke yake wenzetu wangeshinda kwani umejuaje kuwa hakuna wenzetu waliomtanguliza Mungu mbele?
Mungu anajibu kwa kadiri ya mapenzi yake na kwa wakati wake sahihi


Umebeza maombi tangu mwanzo
 
Endeleeni kujazana ujinga mitandaoni na uraiani wakati rais wenu anachukua tahadhari ya daraja la kwanza
Wajinga ni nyie mnaombeza kwa sababu amesema tuombe.

Sisi tutachukua tahadhari na tutaenda mbele zaidi kwa kuomba maana tahadhari bila Mungu haitoshi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…