Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,170
- 6,757
Kauli uliyoitoa jana mkuu wa nchi yetu inatia moyo, maana umetambua wazi kuwa wateule wako wengi hawaendani na kasi yako. Mbali na hilo wengi ni wacheza maigizo kwenye luninga ya taiifa yaani TBC wakijifanya wanatekeleza ilani ya CCM.
Kama hata wewe mkuu wa nchi umetambua kuwa wateule wako ni waigizaji kwenye runinga huku miradi mingi haijatekelezwa basi tambua kuwa sio kuwa wateule wako hawaigizi kwenye utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo tu, bali hata usimamizi wa sheria ili utawala wa sheria uwepo( utawala bora).
Tulitegemea awamu ya tano, unyanyasi wa raia kutoka kwa vyombo vya dola upungue, kubambikia kesi raia wanyonge kupungue na viongozi kuchukua sheria mkononi kusiwepo. Lakini tunaona ni kinyume kabisa na jinsi ulivyotuaminisha kipindi unachukua madaraka 2015.
Pia soma:
www.jamiiforums.com
Kama hata wewe mkuu wa nchi umetambua kuwa wateule wako ni waigizaji kwenye runinga huku miradi mingi haijatekelezwa basi tambua kuwa sio kuwa wateule wako hawaigizi kwenye utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo tu, bali hata usimamizi wa sheria ili utawala wa sheria uwepo( utawala bora).
Tulitegemea awamu ya tano, unyanyasi wa raia kutoka kwa vyombo vya dola upungue, kubambikia kesi raia wanyonge kupungue na viongozi kuchukua sheria mkononi kusiwepo. Lakini tunaona ni kinyume kabisa na jinsi ulivyotuaminisha kipindi unachukua madaraka 2015.
Pia soma:
Dhana ya Utawala Bora, nini maana yake?
Utawala ni matumizi ya mamlaka ya kisiasa, kiuchumi au vinginevyo katika kusimamia masuala ya nchi kwenye ngazi zote. Utawala bora ni matumizi ya mamlaka ambayo yanakuwa na uwazi, uwajibikaji, ushirikishaji wa watu, ufanisi, tija, uadilifu usawa na unafuata utawala wa...
www.jamiiforums.com