Rais, Mawaziri, Wabunge wa maafisa/watumishi wengine wa Serikali hawalipi kodi lakini ndiyo wanapangia wengine kiasi cha kodi cha kulipa

Rais, Mawaziri, Wabunge wa maafisa/watumishi wengine wa Serikali hawalipi kodi lakini ndiyo wanapangia wengine kiasi cha kodi cha kulipa

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Salama.

Huwa viongozi na watumishi wa serikali wakijinasibu kuwa wanalipa kodi, lakini kilogic watu hawa hawalipi kodi hata kidogo, badala yake ni watumia kodi.

Wataalamu waliochunguza swala hili walikuja na mfano ufuatao. Ikitokea nchi ikakusanya kodi sifuri, basi kuanzia Rais, Waziri, Mbunge, na watumishi wa Serikali mishahara yao itakuwa 0, na hiyo kodi wanayodai kulipa kutoka kwenye mshahara itakuwa sifuri.

Watu hawa wanasubiria kodi iwape mshahara ndiyo 'eti' walipe kodi! Hawa ni watumia kodi na si walipa kodi. Mtu akisema mshahara wangu ni 1,000,000 halafu nalipa kodi 100,000, ni kuwa huyu halipi kodi yoyote na mshahara wake ni 900,000. Haongezi pesa yoyote kwenye kodi ya nchi. Tofauti na mfanyakazi wa sekta binafsi ambaye anazalisha bidhaa au huduma, anauza na kulipa kodi. Huyu ndiye anachangia kwenye kodi/utajiri wa nchi.

Sasa basi, hawa wala kodi siku zote watataka kodi iongezeke ili wapate kikubwa zaidi cha kutafuna. Na ubaya ni kuwa wamepewa mamlaka ya kuamua nani alipe kodi kiasi gani, matokeo yake kila siku kodi na tozo vitaongezeka.

Inabidi hili suala liangaliwe vizuri. Kodi kwenye mazao, biashara, madini nk isibadilishwe bila kushirikisha wadau wa sekta hizo. Kuna vyama vya wafanyabiashara, wakulima, wafugaji nk, wanatakiwa wote kuhusishwa na michakato ya kodi. Si sawa kwa anayefaidika na kodi kupangia wengine kodi ya kulipa.
 
Salama.

Huwa viongozi na watumishi wa serikali wakijinasibu kuwa wanalipa kodi, lakini kilogic watu hawa hawalipi kodi hata kidogo, badala yake ni watumia kodi.

Bila kufika mahali hawa jamaa tukawakomalia wahusike kulipa kodi kama sisi, kelele zote hizi masikio yao ni kama ya kenge tu!
 
Salama.

Huwa viongozi na watumishi wa serikali wakijinasibu kuwa wanalipa kodi, lakini kilogic watu hawa hawalipi kodi hata kidogo, badala yake ni watumia kodi...
Kwaio baada ya kushiba makande umeona haya ni mawazo?
 
Salama.

Huwa viongozi na watumishi wa serikali wakijinasibu kuwa wanalipa kodi, lakini kilogic watu hawa hawalipi kodi hata kidogo, badala yake ni watumia kodi.

Wataalamu waliochunguza swala hili walikuja na mfano ufuatao. Ikitokea nchi ikakusanya kodi sifuri, basi kuanzia Rais, Waziri, Mbunge, na watumishi wa Serikali mishahara yao itakuwa 0, na hiyo kodi wanayodai kulipa kutoka kwenye mshahara itakuwa sifuri.

Watu hawa wanasubiria kodi iwape mshahara ndiyo 'eti' walipe kodi! Hawa ni watumia kodi na si walipa kodi. Mtu akisema mshahara wangu ni 1,000,000 halafu nalipa kodi 100,000, ni kuwa huyu halipi kodi yoyote na mshahara wake ni 900,000. Haongezi pesa yoyote kwenye kodi ya nchi. Tofauti na mfanyakazi wa sekta binafsi ambaye anazalisha bidhaa au huduma, anauza na kulipa kodi. Huyu ndiye anachangia kwenye kodi/utajiri wa nchi.

Sasa basi, hawa wala kodi siku zote watataka kodi iongezeke ili wapate kikubwa zaidi cha kutafuna. Na ubaya ni kuwa wamepewa mamlaka ya kuamua nani alipe kodi kiasi gani, matokeo yake kila siku kodi na tozo vitaongezeka.

Inabidi hili suala liangaliwe vizuri. Kodi kwenye mazao, biashara, madini nk isibadilishwe bila kushirikisha wadau wa sekta hizo. Kuna vyama vya wafanyabiashara, wakulima, wafugaji nk, wanatakiwa wote kuhusishwa na michakato ya kodi. Si sawa kwa anayefaidika na kodi kupangia wengine kodi ya kulipa.
Kazi ya serikali ni kutoa huduma za kijamii kwa Raia wake. Kwahiyo madaktari, walimu, vyombo vya ulinzi wanahitaji kulipa sababu hawatakiwi kufanya kazi nyingine za kujiajiri.
Kodi tunayolipa inatakiwa kuwa lipa hawa na kurekebisha mazingira ya kufanya kazi na vifaa kwa ajili yao na Raia. Kodi wanayolipa ni kodi ya mapato.
Jumla ya kodi zote kwa mfanyia biashara zinaweza zisifike 500,000/= kwa mwaka. Mfanyakazi anakatwa kodi kila mwezi, mfano anyekatwa 150,000/= kwa mwaka inakuwa 1,500,000/=.
 
Poleni walimu, madaktari, wauguzi etc
Usiwape pole kwa mujibu wa mleta hoja, hawa ndio watumishi wa serikali wasiolipa kodi maana hawazalishi (japo wanatoa huduma) kwa hiyo mishahara yao inasutegemea kodi za hao aliosema wa sekta zinazozalisha! Binafsi nafikiri mtoa hoja amefikiri kwa kiwango kidogo hajaangalia uzito wa huduma wanazotoa watu wa kada mbalimbali zisizo zalisha!
 
Shida ya vyuo vyetu vya siasa vya Mwalimu Nyerere na UDSM mnapotosha sana .
Vyeo ambavyo hawalipi kodi vinajulikana kikatiba.
 
Kazi ya serikali ni kutoa huduma za kijamii kwa Raia wake. Kwahiyo madaktari, walimu, vyombo vya ulinzi wanahitaji kulipa sababu hawatakiwi kufanya kazi nyingine za kujiajiri.
Kodi tunayolipa inatakiwa kuwa lipa hawa na kurekebisha mazingira ya kufanya kazi na vifaa kwa ajili yao na Raia. Kodi wanayolipa ni kodi ya mapato.
Jumla ya kodi zote kwa mfanyia biashara zinaweza zisifike 500,000/= kwa mwaka. Mfanyakazi anakatwa kodi kila mwezi, mfano anyekatwa 150,000/= kwa mwaka inakuwa 1,500,000/=.
Hiyo anayolipa mfanyakazi siyo kodi. Labda tuseme ni punguzo tu la mshahara. Wafanyabiashara na watu wengine wanafanya kazi na kulipa kodi. Kodi hiyo inaenda kufanya mambo mengi ikiwemo kulipa mishahara ya madaktari na waalimu, sasa inaingia akilini hao nao kuchukua sehemu ya huo mshahara na kulipa kodi.

Kwa mwaka mzima, jumla ya kodi ya mtumishi wa serikali, Rais, waziri nk ni 0. Hawa ni wanaotumia kodi na si walipa kodi.
 
Usiwape pole kwa mujibu wa mleta hoja, hawa ndio watumishi wa serikali wasiolipa kodi maana hawazalishi (japo wanatoa huduma) kwa hiyo mishahara yao inasutegemea kodi za hao aliosema wa sekta zinazozalisha! Binafsi nafikiri mtoa hoja amefikiri kwa kiwango kidogo hajaangalia uzito wa huduma wanazotoa watu wa kada mbalimbali zisizo zalisha!
Ni kweli mkuu, hao wanatoa huduma muhimu na wanalipwa mshahara kwa kazi zao. Ila kusema wanalipa kodi ni kupotosha. Na kuwapa wao pekee mamlaka ya kuamua kiwango cha kodi na tozo kinachopaswa kulipwa na wengine ni kutowatendea haki walipa kodi.
 
Shida ya vyuo vyetu vya siasa vya Mwalimu Nyerere na UDSM mnapotosha sana .
Vyeo ambavyo hawalipi kodi vinajulikana kikatiba.
Mtu yeyote anayelipwa mshahara na serikali si mlipa kodi.
 
Salama.

Huwa viongozi na watumishi wa serikali wakijinasibu kuwa wanalipa kodi, lakini kilogic watu hawa hawalipi kodi hata kidogo, badala yake ni watumia kodi.

Wataalamu waliochunguza swala hili walikuja na mfano ufuatao. Ikitokea nchi ikakusanya kodi sifuri, basi kuanzia Rais, Waziri, Mbunge, na watumishi wa Serikali mishahara yao itakuwa 0, na hiyo kodi wanayodai kulipa kutoka kwenye mshahara itakuwa sifuri.

Watu hawa wanasubiria kodi iwape mshahara ndiyo 'eti' walipe kodi! Hawa ni watumia kodi na si walipa kodi. Mtu akisema mshahara wangu ni 1,000,000 halafu nalipa kodi 100,000, ni kuwa huyu halipi kodi yoyote na mshahara wake ni 900,000. Haongezi pesa yoyote kwenye kodi ya nchi. Tofauti na mfanyakazi wa sekta binafsi ambaye anazalisha bidhaa au huduma, anauza na kulipa kodi. Huyu ndiye anachangia kwenye kodi/utajiri wa nchi.

Sasa basi, hawa wala kodi siku zote watataka kodi iongezeke ili wapate kikubwa zaidi cha kutafuna. Na ubaya ni kuwa wamepewa mamlaka ya kuamua nani alipe kodi kiasi gani, matokeo yake kila siku kodi na tozo vitaongezeka.

Inabidi hili suala liangaliwe vizuri. Kodi kwenye mazao, biashara, madini nk isibadilishwe bila kushirikisha wadau wa sekta hizo. Kuna vyama vya wafanyabiashara, wakulima, wafugaji nk, wanatakiwa wote kuhusishwa na michakato ya kodi. Si sawa kwa anayefaidika na kodi kupangia wengine kodi ya kulipa.
Ni vizuri kwanza ungefanya utafiti ukafahamu kodi zinatozwaje au vyanzo vya kodi.Ukiangalia vyanzo vya kodi vinatozwa kwenye biashara ambapo wewe mfanyabiashara utahitaji mazingira mazuri na yenye usalama ndiyo maana unalipa kodi. Uwekezaji ambapo mwekezaji naye atahitaji huduma mbalimbali kama vile usalam wa uwekezaji wake na miundombinu kwa ajili ya amana yake.Ajira ambapo mfanyakazi huyu naye ili kuweza fika eneo lake la kazi pia naye atahitaji ulinzi na njia nzuri ili aweze kwenda na kurudi nyumbani.

Tambua serikali haifanyi biashara lakini serikali inawajibu wa kuhudumia jamii na chanzo kikubwa cha mapato ya serikali ni kodi.
Unaposema watumishi wa serikali hawalipi kodi siyo kweli sababu serikali inawalipa kwa kufanya kazi ambazo wameingia mkataba na serikali na kumbuka serikali haina biashara zaidi ya kutegemea kodi na hao hao watumishi kuna kodi nao wanachangia.

Unapovamiwa na wezi au majambazi ushwaona polisi wanakuambia ulipie ili waje wakusaidie?Vitu vingine tuwe tunauliza kwanza kuliko kuleta hoja mabazo sizakweli.Nawasilisha kama mdau nayefatilia mambo ya kodi
 
Ni vizuri kwanza ungefanya utafiti ukafahamu kodi zinatozwaje au vyanzo vya kodi.Ukiangalia vyanzo vya kodi vinatozwa kwenye biashara ambapo wewe mfanyabiashara utahitaji mazingira mazuri na yenye usalama ndiyo maana unalipa kodi. Uwekezaji ambapo mwekezaji naye atahitaji huduma mbalimbali kama vile usalam wa uwekezaji wake na miundombinu kwa ajili ya amana yake.Ajira ambapo mfanyakazi huyu naye ili kuweza fika eneo lake la kazi pia naye atahitaji ulinzi na njia nzuri ili aweze kwenda na kurudi nyumbani.

Tambua serikali haifanyi biashara lakini serikali inawajibu wa kuhudumia jamii na chanzo kikubwa cha mapato ya serikali ni kodi.
Unaposema watumishi wa serikali hawalipi kodi siyo kweli sababu serikali inawalipa kwa kufanya kazi ambazo wameingia mkataba na serikali na kumbuka serikali haina biashara zaidi ya kutegemea kodi na hao hao watumishi kuna kodi nao wanachangia.

Unapovamiwa na wezi au majambazi ushwaona polisi wanakuambia ulipie ili waje wakusaidie?Vitu vingine tuwe tunauliza kwanza kuliko kuleta hoja mabazo sizakweli.Nawasilisha kama mdau nayefatilia mambo ya kodi
Watumishi wa serikali ni watu muhimu sana. Na kwa kuona umuhimu huo ndiyo maana watu wapo tayari kutumia kodi zao kuwalipa mshahara. Lakini ukweli ni kuwa wao hawalipi kodi.

Huwezi tumia mshahara uliotokana na kodi kulipa kodi. Ongezeko kwenye makusanyo ya kodi kutoka kwenye mishahara ya watumishi wa umma ni sifuri.
 
Salama.

Huwa viongozi na watumishi wa serikali wakijinasibu kuwa wanalipa kodi, lakini kilogic watu hawa hawalipi kodi hata kidogo, badala yake ni watumia kodi.

Wataalamu waliochunguza swala hili walikuja na mfano ufuatao. Ikitokea nchi ikakusanya kodi sifuri, basi kuanzia Rais, Waziri, Mbunge, na watumishi wa Serikali mishahara yao itakuwa 0, na hiyo kodi wanayodai kulipa kutoka kwenye mshahara itakuwa sifuri.

Watu hawa wanasubiria kodi iwape mshahara ndiyo 'eti' walipe kodi! Hawa ni watumia kodi na si walipa kodi. Mtu akisema mshahara wangu ni 1,000,000 halafu nalipa kodi 100,000, ni kuwa huyu halipi kodi yoyote na mshahara wake ni 900,000. Haongezi pesa yoyote kwenye kodi ya nchi. Tofauti na mfanyakazi wa sekta binafsi ambaye anazalisha bidhaa au huduma, anauza na kulipa kodi. Huyu ndiye anachangia kwenye kodi/utajiri wa nchi.

Sasa basi, hawa wala kodi siku zote watataka kodi iongezeke ili wapate kikubwa zaidi cha kutafuna. Na ubaya ni kuwa wamepewa mamlaka ya kuamua nani alipe kodi kiasi gani, matokeo yake kila siku kodi na tozo vitaongezeka.

Inabidi hili suala liangaliwe vizuri. Kodi kwenye mazao, biashara, madini nk isibadilishwe bila kushirikisha wadau wa sekta hizo. Kuna vyama vya wafanyabiashara, wakulima, wafugaji nk, wanatakiwa wote kuhusishwa na michakato ya kodi. Si sawa kwa anayefaidika na kodi kupangia wengine kodi ya kulipa.
Unawaza au unapiga kelele mkuu?
Hoja za kitoto kabisa, kwahiyo Daktari anapokatwa ela kwenye mshahara wake we unaona halipi kodi? Upimwe akili wewe
 
Unawaza au unapiga kelele mkuu?
Hoja za kitoto kabisa, kwahiyo Daktari anapokatwa ela kwenye mshahara wake we unaona halipi kodi? Upimwe akili wewe
Pale halipi hata mia. Unawezaje kulipa kodi kwa pesa ya kodi?
 
Watumishi wa serikali ni watu muhimu sana. Na kwa kuona umuhimu huo ndiyo maana watu wapo tayari kutumia kodi zao kuwalipa mshahara. Lakini ukweli ni kuwa wao hawalipi kodi.

Huwezi tumia mshahara uliotokana na kodi kulipa kodi. Ongezeko kwenye makusanyo ya kodi kutoka kwenye mishahara ya watumishi wa umma ni sifuri.
Hebu tuangalie Tafsiri hizi juu ya kodi kisha tuendelee kujadiliana: Tafsiri ya kodi kwa kiswahili (kwa mujibu wa wikipedia) "Kodi (ushuru) ni malipo ya lazima ya pesa au aina nyingine ya malipo yanayotozwa na taasisi ya serikali kwa mujibu wa sheria kutoka kwa mlipakodi (mtu binafsi au chombo kingine cha kisheria) ili kufadhili matumizi mbalimbali ya umma"

Na ile ya Kiingereza "a compulsory contribution to state revenue, levied by the government on workers' income and business profits, or added to the cost of some goods, services, and transactions"

Ukiangalia hiyo Tafsiri ya kiingereza hapo nilipokoleza wino inaweka wazi kuwa "on workers'income" kwa maana hiyo hata wafanyakazi wa umma wanalipa kodi. Ile tafsiri ya kiswahili japo haijaweka wazi lakini hapo nilipokoleza wino pia " chombo kingine cha kisheria" inaweza kuwa na maana kutoka taasisi zinazotambuliwa rasmi na serikali, kwa maana hiyo kodi pia hutozwa kwa wafanyakazi wa taasisi hizi.
 
Back
Top Bottom