DOKEZO Rais, Mkuu wa Wilaya na OCD Lindi 'wamemuua' ANGEL KESSY Mwanafunzi wa PCB

DOKEZO Rais, Mkuu wa Wilaya na OCD Lindi 'wamemuua' ANGEL KESSY Mwanafunzi wa PCB

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Status
Not open for further replies.
Huyo nadhani kafia hospital ya mission bila kutarajia na fedha walichukua ndio maana Kuna paroko hapo kati!!

Pia Kuna kosa la kitabibu pia inawezekana sasa wanataka kufichiana siri.

Fikra zangu dhahania hizo.
 
Hiv wewe una akili kweli..Makonda hapa anahusikaje jomba..naona dish limeyumba
Watu hawawezi elewa tuu inauma inauma sana ..halafu mtu analazimishwa akazike tuu bila kujua chanzo nafikiri hili jambo linahitaji uchunguzi kwanza kabla ya kuhukumu lakini kuna utata sana huyu mwenye mtoto anatakiwa apate majibu ya kumridhisha na yaliyo sahihi sio kulazimisha mtu kuzika!
 
Tulianza na
  1. Handeni mjamzito kufariki kwa kukosa Tsh 150K
  2. Mgonjwa kutakiwa kulipa Tsh 86K ili asomewe cd ya vipimo vyake
  3. Leo kifo chenye utata Lindi
Kuna kile kigo jingine cha kijana kufa na kuzikwa porini kakonko huko
 
Huyo nadhani kafia hospital ya mission bila kutarajia na fedha walichukua ndio maana Kuna paroko hapo kati!!

Pia Kuna kosa la kitabibu pia inawezekana sasa wanataka kufichiana siri!!!

Fikra zangu dhahania hizo!!
Halafu naona huyu mtoto kafia mikononi mwa watu kisa kukosa fedha sasa naona kama Dc anataka kujiingiza kwenye shida kwa kulazimisha mtu azike bila kupewa majibu na wakati aliombwa pesa na akatoa!
 
Ndo maana ake, Matron abanwe aeleze ukweli.
Matron atakuwa anajua chanzo cha kifo cha huyo mtoto halafu kuna kitu kinafichwa haiwezekani Dc alazimishe mtu akazike
 
Pole sana Mkuu ...
Lakini ujifunze sasa majuzi ulikashfu sana kifo cha Mtoto wa Baba wa Taifa kule Shinyanga ukaita kafa kibudu na msiba kibudu blah blah. Tuwe na staha misiba inapowapata wenzetu leo kwako kesho kwa mwingine.
Kumbe huyu jamaa ni popoma

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
Ni muhimu msikubali kumpokea marehemu wala kuzika. Hapa ni pa kuanzia ili kujipanga kwa mapambano.
Na wakitaka kujua chanzo cha kifo cha huyu mtoto wasikubali kupokea mwili au kwenda kuzika!
 
Fanya uchunguzi wa kifo cha mtoto wako.
Court za nchi hiyo zinalea wenye mamlaka hata kama wakifanya ujinga.

Ningekuwa mm mtoto angeenda na watu
Sitaki ukhanithi hata nukta moja.
Pole sana Mkuu.
 
Fanya uchunguzi wa kifo cha mtoto wako.
Court za nchi hiyo zinalea wenye mamlaka hata kama wakifanya ujinga.

Ningekuwa mm mtoto angeenda na watu
Sitaki ukhanithi hata nukta moja.
Pole sana Mkuu.
Asikubali kupokea mwili…
 
ninao watatu...nimezungumza hivyo sio kwa nia mbaya...serikali yetu ni kipofu anaweza kufatilia kifo cha mwanae na yeye tukampoteza...

rejea tuhuma za Mbarikiwa mwakipesile wa Mbeya dhidi ya mkurugenzi mkuu wa usalama kuua binti wa Mbarikiwa. tuhuma hizo zimepelekea leo hii Mbarikiwa amefungwa na huku akiwa amempoteza Binti yake.

ila hayo yalikuwa maoni yangu tu sio kama sina uchungu...🙏🙏🙏​
Uoga ni mbaya sana ukiundekeza utashindwa kudai haki yako, utaonewa , utapigwa na kunyanyaswa pamoja na kidhurumiwa kwa sababu ya Uoga. Ndugu usiogope kudai haki yako hata siku Moja hata kama Kuna kumwaga damu usikubali kudhurumiwa idai haki yako haijalishi Kuna Nini, ipo siku utanyang'anywa hata nyumba sabab ya Uoga utaacha kudai.
Ni hayo tu lakin piah n maoni yako siyo mbaya lakin imagine ingekuwa kwako.
 
Wapi kasema umeletwa Dar. Wacha ujuaji kwenye kila.kitu wewe dogo. Kama mzazi alipata taarifa ya kifo cha mwanaye akiwa Mwanza either kikazi au ndio asili yao na alienda huko huku makazi yake yakiwa Dar je? Pumbavu mkubwa wewe. Mtu ana msiba alafu unaleta usela mavi.
Mental illness is really kati yako wewe na uyo alie hoji me nazani we ndo pumba kabisa .swali lake liko logical na lina eleweka .lakini wewe ume jibu pumba mwanzo mwisho . Muwe mna ficha ujinga wenu sometimes
 
Mh Rais Dr Samia Suluhu Hassani nakusalimu kwa jina la jamhuri ya Muungano wa Tanzania..............

Mh Rais Mimi ni raia wa Tanzania,hivi Sasa ni SAA kumi na dakika 25 Natumah wewe utakuwa umepumzika kutokana na kazi nzito hasa za kipindi hiki ulipo ziarani.

Mh Rais Mimi raia wako MWANANCHI mwema kabisa nimeumizwa na UTAWALA wa AWAMU ya SITA mpaka ninajiuliza nimekosa Nini kwako au kwa Mungu muumba?(nimeona sio busara kujizuru Mimi nikafa pasipo kusema,nimeona Bora niseme ili kama utasikia kupitia hapa utauponya moyo wangu na ukishindwa basi hata yatakayojili nawe ubebeshwe sehemu ya dhambi zangu ukajibu siku ya kihama.)

Mh Rais nisikikuchoche,

Ukatili NILIO FANYIWA.

1. MAUAJI YA BINTI YANGU MWANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO SHULE YA SECONDARI LINDI GERLS KIDATO CHA TANO PCB.(NAOGOPA KUMTAJA JINA MAANA KILA NIKIANDIKA JINA LAKE ANANIJIA UBONGONI).

Mh Rais kutokana na mlango wa ikulu yako kufungwa kwa WANANCHI walala hoi nilishindwa kufikisha taarifa hizi ikuluni kwako badala yake nilitumia jukwaa ili la jamii forum KUANDIKA yaliyojili mpaka mwanangu akauwa

Nilielezea jinsi mwanangu alivyo amia shuleni hapo ndani ya mwezi Mmoja TU mwezi wa pili nilipigiwa simu naitwa nikamuuguze mwanangu anaumwa nikaanza safari SAA SITA mchana kutoka Mbagara kwenda Lindi Nilifika Lindi SAA mbili za usiku nikakuota mwanangu akiwa ameisha Oshwa, valishwa pakwa lipustik, valishwa nguo mpya, wekwa kwenye Jeneza, TAYARI kuletwa DSM Mbagara kwa mazishi.

Mh Rais Mimi kama MZAZI nilihoji kwa Nini nimeitwa nikauguze nafika nakuta mahiti kaisha andaliwa na mkuu wako wa WILAYA ya Lindi,mkurugenzi wa halimashauri, PADRI kanisa katoliki, ocd Lindi na mkuu wa shule ya secondari Lindi?

Nilijiuliza waliniita Mimi MZAZi nikakubali kwenda kama hawakumuua mwanangu walikuwa na haraka Gani ya kumvua nguo mwanangu kumwosha pasipo ridhaa yangu MZAZi?haraka ilikuwa ya Nini?
Niliwauliza cheti Cha kifo Cha mwanangu kiko wapi au cheti Cha matibabu wakajibu MGONJWA alikuwa akitibiwa na Dawa za mseto kwa mantiki hiyo hawana cheti?

Nikauliza mwanangu aliumwa Nini?nikajibiwa ni marelia na u.t.i je Mh Rais u.t.i na marelia utibiwa na mseto?
Mh Rais naandika haya huku nalia naomba nifike ikulu yako nikuelezee jinsi watumishi wa serikali yako walivyo usika kumuua mwanangu,
Mh Rais Nina hakika taarifa hii unayo mezani kwako maana Moja ya watu wangu walinijulisha ilikufikia na maelekezo yako/yalimtaka RPC Lindi afukue mwili wa mwanangu ufanyiwe UCHUNGUZI,ili halikufanyika badala yake RPC Lindi kwa KUSHIRIKIANA na ndugu Mmoja kutoka jeshi la polisi kitengo Cha malalamiko Mr Wankyo walifanya wanayoyajua na KUANDIKA ripoti yakuwa kifo kilikuwa Cha kawaida taarifa ilifika mezani kwako Mh Rais kwa wakati UCHUNGUZI wa polisi umetumia MIEZI 7 baada ya kifo Cha mwanangu.

Ili nalo limepita Mh Rais kilio changu ni KIKUBWA.
.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom