Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Wakenya niliwashauri mumchague Ruto ila ningependa tena kusema hatakuwa kiongozi mzuri kama nilivyokuwa namfikiria. Poleni.
Ameanza kuwanunua wapinzani wake jambo ambalo ni baya sana katika ustawi wa demokrasia, ili nchi yenu iendelee kuwa demokrasia imara mnahitaji watu wenye misimamo na watakaotoa upinzani imara serikali, anachokifanya Ruto ni kuuvunja upinzani uti wa mgongo.
Anaonekana ni mgawanya watu zaidi kuliko kuwa muunganishaji. Kiongozi mzuri anapaswa kuwa mtu muunganishaji. Nimemuona akitoa hotuba huku akimfanyia kebehi Kenyatta, hakuna ulazima wa hilo jambo tena kwa sasa, ni vyema angekaa kimya tu kuliko kumzungumzia kwa mzaha.
Anaonekana muda mwingi sana akiitumia kwenye mambo ya kidini, kwenye makongamano, akihubiri, akiimba, akifanyiwa maombi n.k. Mojawapo ya dalili ya viongozi wabovu na "incompetent" ni kujificha chini ya kivuli cha mambo ya kidini na mara nyingi wakimtaja sana Mungu ili kujionyesha ni watu wema. Bahati mbaya sana hii ni propaganda ambayo hununuliwa na raia wengi wenye akili ndogo.
Ameanza kuwanunua wapinzani wake jambo ambalo ni baya sana katika ustawi wa demokrasia, ili nchi yenu iendelee kuwa demokrasia imara mnahitaji watu wenye misimamo na watakaotoa upinzani imara serikali, anachokifanya Ruto ni kuuvunja upinzani uti wa mgongo.
Anaonekana ni mgawanya watu zaidi kuliko kuwa muunganishaji. Kiongozi mzuri anapaswa kuwa mtu muunganishaji. Nimemuona akitoa hotuba huku akimfanyia kebehi Kenyatta, hakuna ulazima wa hilo jambo tena kwa sasa, ni vyema angekaa kimya tu kuliko kumzungumzia kwa mzaha.
Anaonekana muda mwingi sana akiitumia kwenye mambo ya kidini, kwenye makongamano, akihubiri, akiimba, akifanyiwa maombi n.k. Mojawapo ya dalili ya viongozi wabovu na "incompetent" ni kujificha chini ya kivuli cha mambo ya kidini na mara nyingi wakimtaja sana Mungu ili kujionyesha ni watu wema. Bahati mbaya sana hii ni propaganda ambayo hununuliwa na raia wengi wenye akili ndogo.