Rais Mstaafu Jakaya Kikwete agomea eneo la ekari 50, ataka ekari 500

Lakini inapendeza zaidi kikijengwa sehemu moja kwa ajili ya kurahisisha utawala!
 
Serikali haiwezi kutukubalia, kama ilitunyima Bukoba University miaka hiyo, unahisi itakubali sahizi.
Changamkeni. Tengeni eneo kubwa kujenga chuo halafu muwape bure chuo chochote kinachohitaji wajenge tawi. Hata kama ni maeneo mawili au matatu tengeni.
 
Chuo kuwa na matawi nje ya nchi sioni tatizo,chuo kuwa na matawi ndani ya mkoa mmoja sioni tatizo, ambacho sielewei ni chuo cha serikali kuwa na matawi katika mikoa tofauti ndani ya nchi. Kwa nini serikali isianzishe vyuo tofauti vinavyojitegemea katika kila mkoa au kanda?
 
Mnafanya siasa, Mbeya University of Science and Technology (MUST) imejengwa kule Iyunga na Sistila na wakapewa eneo kubwa tu na watu wakalipwa fidia. Halafu eneo ambalo wanalopewa siyo eneo ambalo linakaliwa na watu, ni eneo ambalo litakuwa wazi tena ardhi yake haiko chini ya Granted Right of Occupancy. Kwanini mnahisi kwamba kila kitu anachofanya Mzee Kikwete ni dhulma tu ???
 
Msingependa kuwa na Kagera University?
Kagera ndio hakufai kabisa, nani aje kusoma sweken shitimbi huko. nafikiri kama wakiona Mbeya hawana eneo, wapeleke Shinyanga, Arusha, Songea au Sumbawanga wakapambane na wachawi huko.
 
Kagera ardhi ipo ya kutosha tunawakaribisha wakinyimwa ardhi huko, waje kagera.
Msisubiri wanyimwe, tengeni eneo halafu waiteni. Waambieni, "Mzumbe hapa tuna ekari 200, kama mnaweza chukueni mjenge chuo. Vigezo na masharti kuzingatiwa." Kuweni proactive.
 
Unafuu huo ni upi? Mbona kwenye nchi nyingine zenye vyuo bora vya umma hawavipanui kwa kuanzisha matawai mengi ndani ya nchi hiyo moja?
Unaongelea nchi gani? Me nimesoma Germany [emoji629], Gottingen University na kina matawi. Vyuo vikubwa karibu vyote vina matawi nchini mwao na nje kama China na Africa na vingine vinaingia collaboration ili vijitanue.

Kuanzisha Chuo mpk kisimame ni changamoto sana. Ndio maana unaona mpk leo UDOM bado haijasimama vizuri, ila ingekuwa ni sehemu ya UDSM ingekuwa mbali zaidi
 
Vyuo vingine vikubwa duniani kama Havard huwa vinakuwa na branches nyingi nyingi katika nchi zao?
Harvard University ina eneo kubwa sana ambalo ni mji wao kabisa, lakini wenzetu hawana haja ya kuanzisha Constituent Universities kwasababu nchi ina uwezo wa kuanzisha vyuo vikuu vingine vikubwa. Sisi Tanzania hatuwezi tu kuanzisha vyuo vikuu kama uyoga, hatuna rasilimali hizo. Ndiyo maana utakuta tuna wahadhiri wanafundisha vyuo zaidi ya viwili,....
 
Kagera ndio hakufai kabisa, nani aje kusoma sweken shitimbi huko. nafikiri kama wakiona Mbeya hawana eneo, wapeleke Shinyanga, Arusha, Songea au Sumbawanga wakapambane na wachawi huko.
Kagera siyo sitimbi, nchi inayopakana na nchi tatu utasemaje ni sitimbi?
 

..wazo lako ni zuri, na kuna nchi zimefuata utaratibu unaopendekeza.

..labda mbele ya safari serikali inaweza kuamua kuwa na vyuo vya kanda au mikoa. Nadhani mfumo huo uko ktk vyuo vya VETA.

..Mbeya kuwa na campus ya Udsm naamini ni jambo zuri. Wanaweza kuwa advantage ya kutumia mifumo na uzoefu wa Udsm kuliko wangeanza wenyewe toka msingi.

..Na Mzee Kikwete ameona mbali kwa kupigania Mbeya wawe na eneo kubwa kwa ajili ya chuo kikuu.

..Mbele ya safari ikiamuliwa Mbeya iwe chuo kikuu kamili watakuwa wamepata uzoefu wa kujiendesha, na watakuwa na eneo la kutosha la kuwa chuo kikuu kinachojitegemea.

..Again, there is still an opportunity to implement what you have proposed in the future. Milango haijafungwa kwa campus ya Mbeya kuwa chuo kikuu kamili. Nasema hivyo kwa kuangalia historia ya Sokoine University.
 
Badala ya kujenga UDSM kampasi ya Mbeya kwa nini kisijengwe chuo kikuu cha Mbeya?

Kwa nini Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika mkoa wa Mbeya?
Kwani mbeya hawana chuo kikuu?
 
Well said [emoji122]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…