Rais Mstaafu Jakaya Kikwete agomea eneo la ekari 50, ataka ekari 500

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete agomea eneo la ekari 50, ataka ekari 500

Tuache utani ekari 500 ni sawa na mita 70 x ekari 500 = 35,000 meter square then ukigawanya kwa mita 100 kujua ni viwanja vya mpira vingapi vyenye square mita sawa ni sawa sawa na viwanja 350 vya mpira vyenye mita square 100 kila upande.
Mkitaka eneo tupu la pamoja lisilo na makazi kama fidia hamtolipa basi nendeni Chunya wilaya maana huko kote ni mkoa wa Mbeya na ni wilaya kubwa kuliko zote mkoa wa Mbeya na ni wilaya inayoongoza kwa maeneo yake makubwa kutokaliwa na watu,hata ekari buku mtapata ila mkae mkijua pande zote mtazungukwa na wanyama pori tu.
 
..sina uhakika kama Harvard wana matawi nje jimbo waliloko ambalo ni jimbo la Massachusetts.

..lakini viko vyuo vikuu vingine vikubwa duniani ambavyo vimekuwa na matawi nje ya mahali vilipoanzishwa.

..nitakurudisha ktk historia ya vyuo vikuu ktk ukanda wetu wa AFRIKA MASHARIKI.

..chuo kikuu cha Makerere kilianza kama tawi la London University. Wahitimu toka Tz, Ug, na Kya, wa miaka ya 50 walitunukiwa shahada za London University ingawa walisomea Kampala.

..Pia chuo kikuu cha Dar Es Salaam nadhani shahada za kwanza za sheria zilikuwa za London University.

..Baadae Dar Es Salaam kikawa sehemu ya University of East Africa, kabla ya kila nchi kuamua kuwa na chuo kikuu chake.

..Tuje kwenye chuo kikuu cha Dar Es Salaam. Muhimbili ilikuwa kitivo cha Tiba, kabla haijaamuliwa iwe chuo kikuu kinachojitegemea.

..Twende IFM hapa Dsm. IFM kunatolewa shahada ya MBA toka chuo kikuu cha Strathclyde kilichoko Scotland.

..Kwa maoni yangu, sio vibaya chuo kikuu chochote kuwa na matawi ktk maeneo tofauti na pale kilipoanzishwa.
IFM sio chuo kikuu, ni taasisi ya Elimu ya juu.
 
Naunga mkono hoja ya Jakaya Kikwete mbeya wakipata campus ya udsm mkoa utaendelea sana kijamii na kiuchumi.
iende pale ipeleke changamoto kwenye vyuo vilivyopo. wanafunzi wanaomaliza vyuo vilivyopo mbeya wengi wanaishia kuendesha bodaboda na bajaji kutokana na kupata elimu ya kiwango cha chini, hawaajiriki.
 
Badala ya kujenga UDSM kampasi ya Mbeya kwa nini kisijengwe chuo kikuu cha Mbeya?

Kwa nini Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika mkoa wa Mbeya?
Hili nalo neno
Kila mkoa uwe na chuo chake
 
Badala ya kujenga UDSM kampasi ya Mbeya kwa nini kisijengwe chuo kikuu cha Mbeya?

Kwa nini Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika mkoa wa Mbeya?
Mbeya kama kijiji
 
Kesho au keshokutwa utasikia chuo kinapelekwa Bagamoyo kwa kuwa.....
-Eneo la ekari 600 limepatikana
-Gharama za kuwafidia watu ni kidogo.
-China iko tayari kutusaidia bure kutujengea chuo, lakini lazima iwe Bagamoyo.
-Miundo mbinu muhimu kama maji, umeme, barabara, bandari viko karibu na eneo husika.

Kikwete mimi namjua, ni mjanja mjanja sana na anajua kucheza na bit.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Atumie ushawishi wake kukitwaa chuo cha kilimo uyole, hizo ni akili finyu sana campus college unataka ekari 500 akili gani hizo? Wahame tu apeleke hio college Chalinze.
Kuna kitu kinaitwa future expansion. Hebu waza kikubwa mkuu
 
Miji inakua, lakini siyo kweli kuwa chuo lazima kiwe katika eno moja contiguous. Likipatikana eneo hilo, basi itakuwa ni jambo zuri, lakini siyo kunyang'aya raia maeneo yao ili kupata eneo contiguous kwa ajili ya chuo miaka 50 ijayo. wakitaka eneo kubwa namna hiyo, wasijenge mjini; Nyerere alijenga UDSM nje kabisa ya mji na kutoa eneo kubwa ililo nalo leo, hakuomba eneo kubwa pale Lumumba kilipokuwa.
Kwenye baadhi ya miradi ni lazima "Raia" wapishe. Cha msingi walipwe fidia zao wakapate maeneo mengine.
Ukiwafanya "Raia" wawe untouchable utashindwa kutekeleza miradi ya maendeleo. Au vinginevyo barabara, zahanati, vituo vya afya, n.k utaenda kujenga baharini huko kusiko na watu au kwenye mapori ya Selous
 
Nadhani nchi hii hatutakuja kukubaliana hata jambo moja. Yaani hata hili watu wanambeza Jakaya??? Acre 50 chuo au primary hiyo. Halafu Kikwete mwenyewe anayewapigania mpate eneo kubwa nna uhakika wajukuu zake hawatakuja kusoma huko. Watanzania tuna vichwa vya mende kabisa.
Yaani nchi inashangaza sana, watu wanapinga hadi upanuzi cha chuo. Mimi nilijua labda JK anataka shamba alime yeye na familia yake.
 
Mnataka kuzalisha ma graduate zaidi, kwani Hawa waliopo mmewafanyia Nini?
Kazi mnapeana wenyewe, kila anayeteuliwa ana koneksheksheni watoto wa wakulima Ni waendesha boda Boda na wamachinga, nao pia mmeanza kuwaandama hata kabla ya 17/3/2022
Kwahiyo tuache kuzalisha wasomi ?
Tubomoe shule na vyuo ?
 
Naunga mkono hoja ya Jakaya Kikwete mbeya wakipata campus ya udsm mkoa utaendelea sana kijamii na kiuchumi.
Tayari wanayo, huu mwaka wa 6 au wa 7 wapo Mbeya. Ila wanatumia facilities za hospitali ya Rufaa ya kanda ya Mbeya.

Ili kujenga majengo yao pqmoja na hospitali, wanahitaji eneo kubwa zaidi. Wamezikataa ekari 50 kwamba hazitoshi.

Graduates wa kwanza wa Udaktari wa UDSM Mbeya College of Health and Allied Sciences wamehitimu mwaka jana, mahafali ya leo walikua ni batch ya pili kuhitimu.
 
Kwenye baadhi ya miradi ni lazima "Raia" wapishe. Cha msingi walipwe fidia zao wakapate maeneo mengine.
Ukiwafanya "Raia" wawe untouchable utashindwa kutekeleza miradi ya maendeleo. Au vinginevyo barabara, zahanati, vituo vya afya, n.k utaenda kujenga baharini huko kusiko na watu au kwenye mapori ya Selous
Kulipa fidia ili kupisha miradi ya serikali ni kweli na ndiyo utendaji haki, ila siyo uamuzi mzuri wa serikali kutumia raslimali zake kulipa fidia ili kujenga chuo ambacho kinaweza kujengwa sehemu nyingine bila kulipa fidia. Halihii ni tofauti kabisa na ujenzi wa miundo mbinu kama barabara na reli ambayo topographic conditions zinakuwa zinataka ipite eneo fulani ambalo tayari linatumiwa na raia. Ujenzi wa zahanati na vituo vya afya unaweza kusababisha baadhi ya raia wakahamishwa kusudi kuziweka huduma hizo ziwe karibu na wananchi wengi wanaolengwa na huduma hizo. Chuo kikuu hakilengi watu wa Mbeya tu, kinaweza kuwa popote, na hivyo kulipa watu fidia kusudia maeneo yao yatumiwe na chuo kikuu ni matumizi mabaya ya raslimali za serikali.
 
Back
Top Bottom