Rais mstaafu Jakaya Kikwete, alishawaonya CCM kuwa wasilitegemee Jeshi la Polisi kuwafanya wao waendelee kukaa madarakani

Rais mstaafu Jakaya Kikwete, alishawaonya CCM kuwa wasilitegemee Jeshi la Polisi kuwafanya wao waendelee kukaa madarakani

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Nakumbuka katika kikao Cha mkutano Mkuu wa CCM, iliofanyika jijini Dodoma mwaka 2012, Jakaya Kikwete, akiwa ni Mwenyekiti wa CCM wa Taifa na wakati huo huo akiwa ni Rais wa Tanzania wa awamu ya 4 aliwaonya vikali CCM kuwa wasilitegemee Jeshi la Polisi, kuwafanyia siasa na badala yake wapambane wao wenyewe na vyama vya siasa vya upinzani Kwa hoja.

Aliendelea kudai kuwa wajibu mkubwa wa Jeshi la Polisi ni kuwalinda raia wote na Mali zao, bila kujali kuwa ni wa chama gani na Wala siyo kuwalinda watawala waliopo kuendelea kukaa madarakani.

Inaelekea hao CCM wamepuuza ushauri huo na badala yake wameendelea tu kuwatumia Jeshi la Polisi Kwa maslahi yao.

Nimesema kuwa wao CCM wameendelea kuwatumia Jeshi la Polisi Kwa maslahi yao, kutokana na taarifa iliyotolewa na msemaji wa Polisi nchini, ACP David Misime, siku ya tarehe 12 mwezi huu, akiongea na waandishi wa habari, akiwaambia kuwa wao Jeshi la Polisi wamepiga marufuku maandamano ya amani yaliyotangazwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kuwa yatafanyika jijini Dar tarehe 23 mwezi huu iwapo tu, Jeshi la Polisi, ifikapo tarehe 21 mwezi huu, itakuwa bado haitawarejesha viongozi wao waliotekwa na watu inayodai Jeshi letu la Polisi, kuwa ni watu wasiojulikana!

Lazima itambulike kuwa wajibu namba Moja wa Jeshi la Polisi ni kuwalinda raia na Mali zao, sasa kutokana na wimbi kubwa linaloendelea nchini hivi sasa la raia kuendelea kutekwa na wengine kuuawa kinyama bila hatua zozote kuchukuliws na Jeshi la Polisi, ni dhahiri kuwa Jeshi la Polisi, limeshindwa wajibu wao namba Moja wa kuwalinda raia na Mali zao na wanalazimika viongozi wake wakuu, ambao ni Waziri wa Mambo ya ndani, Yusufu Masauni na IGP, Camilius Wambura wajuzulu mara moja.

Hiki kiburi Cha kutotaka kuwajibika Kwa hao viongozi wawili ni dharau Kwa watanzania, waliowapa dhamana hiyo na badala yake wanashuhudia watanzania wakiendelea kutekwa na kuuawa wakati wao wakienddlea kung'ang'ania nafadi zao!

Suluhisho pekee la kusitisha maadamano ya Chadema siku ya Jumatatu ya tarehe 23 ni Kwa Jeshi la Polisi, kujitokeza hadharani kabla ya tarehe 21 na kueleza walipo viongozi wa Chadema na watu wengine waliopotea katika mazingira ya kutatanisha.

Kama Hilo lisipofanyika kabla ya tarehe tarehe 21, basi maandamano hayo ya amani yatafanyika tarehe 23, Kwa kuwa yanaruhusiwa Kwa mujibu wa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania
 
barabara ya mzee kikwete pale kawe kila siku inafagiliwa ni ya lami.nenda sasa kawe ukwamani uone uchafu wa pale
 
Kapewa uwaziri kwanini asitulie?
Nadhani hamuwezi kuelewana. Mwenzako anamzungumzia baba, wewe unaongelea mtoto!

Hili ndiyo tatizo la kuachiana nafasi za Serikali kwa mfumo wa watemi.

Unakuta jina linarotate kwenye nyadhifa kubwa Serikalini kwa karne nyingi hadi mtu unashindwa kuelewa anayezungumziwa ni nani.

Aheri wazungu wapo makini kutofautisha majina yakipandiliana katika wadhifa mmoja.

Lakini sisi utasikia 'Rais Karume' ama 'Rais Mwinyi', anayeongelewa aweza kuwa baba au mtoto.
 
Nadhani hamuwezi kuelewana. Mwenzako anamzungumzia baba, wewe unaongelea mtoto!

Hili ndiyo tatizo la kuachiana nafasi za Serikali kwa mfumo wa watemi.

Unakuta jina linarotate kwenye nyadhifa kubwa Serikalini kwa karne nyingi hadi mtu unashindwa kuelewa anayezungumziwa ni nani.

Aheri wazungu wapo makini kutofautisha majina yakipandiliana katika wadhifa mmoja.

Lakini sisi utasikia 'Rais Karume' ama 'Rais Mwinyi', anayeongelewa aweza kuwa baba au mtoto.
Kwani akipata mtoto si ndo kapqta baba?akitumbuliwa mwanae unadhani nani ataumiq zaidi kati ya mtoto na baba?
 
Nadhani hamuwezi kuelewana. Mwenzako anamzungumzia baba, wewe unaongelea mtoto!

Hili ndiyo tatizo la kuachiana nafasi za Serikali kwa mfumo wa watemi.

Unakuta jina linarotate kwenye nyadhifa kubwa Serikalini kwa karne nyingi hadi mtu unashindwa kuelewa anayezungumziwa ni nani.

Aheri wazungu wapo makini kutofautisha majina yakipandiliana katika wadhifa mmoja.

Lakini sisi utasikia 'Rais Karume' ama 'Rais Mwinyi', anayeongelewa aweza kuwa baba au mtoto.

inatakiwa tubadilishe chama tawala wapewe upinzani japo kwa miaka 10
maana CCM wanarithishana madaraka na kuweka ndugu zao ktk vitengo nyeti. utakuta familia ina nufaika tokea enz za babu, baba, mtoto hadi mjukuu yaan vizazi vinne hadi serikali wanaiona ni mali ya familia
 
inatakiwa tubadilishe chama tawala wapewe upinzani japo kwa miaka 10
maana CCM wanarithishana madaraka na kuweka ndugu zao ktk vitengo nyeti. utakuta familia ina nufaika tokea enz za babu, baba, mtoto hadi mjukuu yaan vizazi vinne hadi serikali wanaiona ni mali ya familia
Absolutely true 👋👋

Haiwezekani nchi yetu iendelee kutawaliwa Kwa kupokezana na akina Karume, akina Mwinyi na hivi sasa wanakuja kina Kikwete na Makamba, wakati vijana wengine waliozaliwa na wazazi wa walala hoi, wanaambiwa vijana ni Taifa la kesho, ambapo hiyo kesho haifltafika milele!🙄
 
Ukiona watu wanatekwa na kupotezwa kmyakmya ujue hizo dilili za udikteta
na serikali ya kidikteta haina muda mrefu itaanguka tu

acha CCM wazibe maskio kama rais Maduro wa Venezuela lkn ipo siku wataanguka
 
Ukiona watu wanatekwa na kupotezwa kmyakmya ujue hizo dilili za udikteta
na serikali ya kidikteta haina muda mrefu itaanguka tu

acha CCM wazibe maskio kama rais Maduro wa Venezuela lkn ipo siku wataanguka
Ndiyo maana Chadema wametoa condition Moja, ambayo serikali hii wanapaswa kuitimiza, Ili wao wasiandamane Kwa amani.

Ni Jeshi la Polisi kuwaleta viongozi wao waliotekwa, akina Soka kabla ya tarehe 21, ama sivyo maandamano yako pale pale na wao Polisi, wajibu wao itakuwa ni kuyalinda maandamano hayo.
 
Ukiona watu wanatekwa na kupotezwa kmyakmya ujue hizo dilili za udikteta
na serikali ya kidikteta haina muda mrefu itaanguka tu

acha CCM wazibe maskio kama rais Maduro wa Venezuela lkn ipo siku wataanguka
Ni kweli kabisa

Hizi ni dalili za wazi kabisa za anguko la CCM🙄
 
Back
Top Bottom