Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe Jakaya Kikwete atunukiwa medali kwa mchango wake katika harakati za kurejesha amani nchini Burundi

Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe Jakaya Kikwete atunukiwa medali kwa mchango wake katika harakati za kurejesha amani nchini Burundi

Rais wa Burundi amemtunuku nishani ya amani Rais mstaafu wa Tanzania mh JM Kikwete kama ishara ya kuheshimu juhudi zake za kuleta amani nchini humo.

Nishani hiyo imepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Burundi kwa niaba ya mstaafu Kikwete.

Maendeleo hayana vyama!
 
Rais wa Burundi amemtunuku nishani ya amani Rais mstaafu wa Tanzania mh JM Kikwete kama ishara ya kuheshimu juhudi zake za kuleta amani nchini humo.

Nishani hiyo imepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Burundi kwa niaba ya mstaafu Kikwete.

Maendeleo hayana vyama!
Hongera sana mheshimiwa Kikwete, kwa tuzo.
 
Kitu nakukubali mkuu ni kutobakia na jina moja la kampuni kwa muda mrefu! Huwa unaweza kubadili badili jina la kampuni ili usipigwe kodi kubwa. Lakini mtu akipata huduma yako anagundua ladha ile ile kwa jina la ile kampuni nyingine.

Hii inasaidia sana hasa kwa mazingira ya demokrasia yetu. Acha sisi tubakie na majina ya kampuni zetu ya muda mrefu hapa jukwaani.
Ha ha umegundua huyu jamaa hajifichi , toka Genta mpaka Mzikulu na majina kibao hapo katikati
 
Rais mtaafu Kikwete ndiye aliyekuwa kiongozi mpatanishi wa mgogoro wa Burundi kipindi kile akiwa waziri wa mambo ya nchi za nje,katika usuluishi ule ndo ulisababisha chama cha CNDD-FDD chini ya marehemu Nkurunziza kichukuwe madaraka Burundi,ni haki ya Burundi kuthamini mchango wa Rais wetu mstaafu
Mpatanishi wa Mgogoro wa Burundi ulikuwa chini ya Mwlimu Nyerere , na baada ya kifo; nafasi yake ilichukuliwa na Comrade Mandela na makubaliano yalisaniwa mwaka 2002 mjini Arusha. Rais aliyekuwa madarakani alikuwa Buyoya na baadaye alifuatia Nkurunziza aliyeleta taabu ya kuachia madaraka.
 
Assalaam alaykum wanajf,kumekucha!

Kabla sijaanza kutembeza Biashara yangu ya Al Kasus nikasema nitabaruku kidogo kutokea pale nilipoishia.

Mtoa hoja ni lazima ujue kutofautisha kati ya SERA ZA NCHI ZA MAMBO YA NJE na DIPLOMASIA YETU...these are two different entities.

Kwa nafasi aliyopo mstaafu mh.Jakaya Kikwete kamwe hawezi kuiwakilisha nchi kwenda kusimamia SERA YA MAMBO YA NCHI ZA NJE.
Yeye anapotoka kutuwakilisha basi hutambaa katika uwanda wa DIPLOMASIA YETU....hatoki nje ya hapo.

SWALI
Je anaweza kuiwakilisha nchi pasina ridhaa ya serikali iliyopo madarakani?!!!
JIBU
Nope,haiwezekani.

SWALI
Je safari yake nchini Burundi amepata mwaliko binafsi?!!

JIBU
Inawezekana ukawa binafsi ama ukapitia foreign affairs.
SWALI
Kama haukuwa wa kibinafsi,je alitumwa kumwakilisha mh.Rais?
JIBU
Inawezekana kuwa ni hivyo.

Niseme tu,mh.Jakaya NI mwanasiasa mbobezi na mwanadiplomasia wa haja zaidi ya mh.Membe,amehudumu foreign affairs muda mrefu.Amefundisha siasa Jeshini,NI mzalendo wa kiwango Cha SGR za magufuli.

Hebu mtafuteni mzee Chizii na mumuulize ni kwa nini marehemu mzee Kingunge Ngombale Mwiru alikuwa anarudiarudia kusema kuwa walikuwa ni vijana watatu tu kwa kipindi kile aliowavisha ITIKADI ya chama na Sera za nchi na wakaiva kwa kiwango cha kukata na shoka.
Nakudokezea tu atakutajia;

1.Dr Jakaya Kikwete
2.Edward Ngoyai Lowassa
3.Abdulrahman Kinana

Kwa hiyo vijana wenzangu mkae mkijua kuwa haya MASUALA ya mh.Kikwete kuzodolewa kuwa eti yeye ni mhutu....ni kutokujua tu historia ya makabila hapa afrika kwani makabila yanabadilika majina kutokana na vizazi kuwa vingi na kuhama kutoka eneo moja kwenda jengine Kama nilivyodadavua hapo juu.
Kwani hao waitwao "wahutu" ndio babu wa makabila yote nchini Tanzania kasoro wale wahamiaji na wafugaji wa asili ya BONDE LA UFA.....

Insh'allah nikimaliza kutembeza Al Kasus yangu hapa Tandale kwa mtogole nitakuja kuwaelezea undani wa mashambulizi yanayoelekezwa kwa mh.Jakaya Mara tu alipoutoa ule ushauri wake kuntu juu ya kukaa mezani kwa mahasimu wa kikabila na kiitikadi wa nchini RWANDA ya komandoo Paul Kagame.

Nawasilisha.


Nasubiri kwa hamu muendelezo wako ukimaliza kuuza al kasus
 
Nasubiri kwa hamu muendelezo wako ukimaliza kuuza al kasus
Oooo sawasawa,ngojea nikusanye videni vyangu vijiweni huku.......kahawa wamenikopa ee nikasema nihamie kwenye al kasus,yanajirudia yaleyale,mtu Wala hajui km lita za maziwa ghali,viungo mpake tuagize toka Chokocho Pemba na kule Mtae Lushoto,aaagh mamwinyi banaa....
 
Rais wa Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye amemtunuku medali Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe Jakaya Kikwete kwa mchango wake katika harakati za kurejesha amani nchini Burundi.


Chanzo: ForeignTanzania

Sisi akina Mzukulu tunaomba tuambiwe haraka kama Rais Mstaafu huyu Jakaya M Kikwete ana Vinasaba vya Uhutu kutoka nchini huko Burundi.
Hongera sana hizo zote ni juhudi za serikali ya awamu ya tano
 
Mpatanishi wa Mgogoro wa Burundi ulikuwa chini ya Mwlimu Nyerere , na baada ya kifo; nafasi yake ilichukuliwa na Comrade Mandela na makubaliano yalisaniwa mwaka 2002 mjini Arusha. Rais aliyekuwa madarakani alikuwa Buyoya na baadaye alifuatia Nkurunziza aliyeleta taabu ya kuachia madaraka.
Asante kwa kuweka sawa but Mhe Kikwete ndo alikuwa Kama coordinator wa ule mgogoro kwa nafasi yake ya waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kwa kipindi hicho
 
Back
Top Bottom