Rais mteule, Donald Trump amesema yuko mbioni kujiondoa NATO

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Hivi huyu baba Trump ana washauri kweli?

Hivi karibuni akiwa anaongea kwenye kipindi cha Meet The Press, amesema kuwa kwa sababu nchi wanachama wa NATO hawanunui bidhaa kutoka Marekani basi anafikiria kujitoa kwenye umoja huo wa kijeshi.

Ikumbukwe kuwa Marekani ndio "contributor" mkubwa kwenye NATO kwa hiyo kujitoa kwa nchi hiyo kutaathiri moja kwa moja organization hiyo.



Yaani wakati China, Urusi na India wanaungana pamoja na kuwa kitu kimoja kwenye BRICS, Trump anaamua kuitoa Marekani kwenye NATO.

Nani anamshauri huyu mzee?

Your browser is not able to display this video.
 

Attachments

  • Trumpp.png
    218.2 KB · Views: 2
Ngoja tusubilie tuone
 
DT anataka Zele akutwe kafariki mwenyewe bila ugonjwa wala external force.
 
Nilivyoelewa mimi mpango wake kuwashawishi wanachama wa Nato nao washiriki vita vya kiuchumi dhidi ya China sababu kila mwaka wanaongeza manunuzi ya bidhaa kwa China huku kule Marekani yanapungua.
 
BRI

BRICS ni jumuiyabya Kibiashara wakati NATO ni jumuiya ya KIJESHI. Hivyo, Rusia, Chia na India kuungana na USA kuiondoa NATO hakuna uhusiano wowote na madhara ya kibiashara. Sana sana nchi za Ulaya ndo zitakuwa zimepata Uhuru kutoka Ukoloni wa MAREKANI uliodumu Kwa zaidi ya Miongo Saba
 
Deep state section ya war veterans mbupu zimebana kwa kukosa kivuli Cha Serikali.
Enemy within ( Anayeiondoa nchi kwenye migharama isiyo na tija yenye manufas kwa wachache ).

Kwamba Trump ni sehemu ya deep state?
 

Ukoloni?

Marekani anaitawalaje Ulaya?
 
Nilivyoelewa mimi mpango wake kuwashawishi wanachama wa Nato nao washiriki vita vya kiuchumi dhidi ya China sababu kila mwaka wanaongeza manunuzi ya bidhaa kwa China huku kule Marekani yanapungua.

Wana economic organizations na unions nyingi btn US and EU kwanini asingebana huko anaenda kwenye military alliance ya muhimu kama NATO?
 
Jamaa ana akili sana nato imechangia pakubwa kwa marekani kupoteza heshima duniani...pia marekani kawashitukia NATO kuwa wanataka kuingiza marekani kwenye kuangamizwa na urusi ...maana mrussi akiingia vitani na NATO basi uwanja wa vita utakuwa ni USA zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…