Wakuu,
Hivi huyu baba Trump ana washauri kweli?
Hivi karibuni akiwa anaongea kwenye kipindi cha Meet The Press, amesema kuwa kwa sababu nchi wanachama wa NATO hawanunui bidhaa kutoka Marekani basi anafikiria kujitoa kwenye umoja huo wa kijeshi.
Ikumbukwe kuwa Marekani ndio "contributor" mkubwa kwenye NATO kwa hiyo kujitoa kwa nchi hiyo kutaathiri moja kwa moja organization hiyo.
View attachment 3173568
Yaani wakati China, Urusi na India wanaungana pamoja na kuwa kitu kimoja kwenye BRICS, Trump anaamua kuitoa Marekani kwenye NATO.
Nani anamshauri huyu mzee?
View attachment 3173567