GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Sina shida na Wewe katika 'Utendaji' wako na unajitahidi japo 'Kibinadamu' bado kuna maeneo mengine hujaweza 'Kukamilisha' na pengine Watanzania tunaokuamini na hata wale waliokuwa hawakuamini nao kwa pamoja katika Uchaguzi huu Mkuu ujao wa tarehe 28 Mwezi Oktoba tukikupa tena 'ridhaa' zetu na 'Kutuongoza' utaweza Kuyakamilisha na Kutufanyia 'Makubwa' Watanzania.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli naomba kwa leo tu nikuume kidogo Sikio kwa Kukuomba kabisa acha Kukubali hizi 'Sifa za Kilaana' ambazo naona sasa umekuwa ukipewa sana na Viongozi wa Dini mbalimbali hasa pale wakiwa nawe ama 'Ukumbini' au 'Uwanjani' Kukuombea ( Kufanya Dua ) kwani 'Kiuhalisia' maneno ambayo huwa 'wanakutamkia' sidhani kama unastahili Kuyaamini na Kuyapokea.
Na ukiona hadi leo hii Mpiga Kura wako na Mwana Kampeni wako Kivuli GENTAMYCINE nimekuja na hili Kwako jua ya kwamba halijakaa vizuri si tu Kwako au Kwetu ila nina uhakika hata kwa mwenyewe Muumba ( Mwenyezi Mungu ) nae Kwake 'halifurahii' kwakuwa hizi Sifa zote za 'Kinafiki' ambazo 'nimezibatiza' kuwa 'Sifa za Kilaana' hupaswi Kuzipokea Wewe na wala hazikuhusu kabisa.
Kitendo cha Mchungaji Mmoja leo Kuanza Kukuombea kabla hujaanza 'Kuhutubia' huku akisema haya maneno ninayanukuu hapa.." Ewe Mungu mbariki Kiongozi huyu wa Kipekee kabisa na wa aina yake kuwahi kutokea nchini Tanzania sawa na Malaika "...alikuwa si tu amekukosea Wewe au Sisi Watanzania bali nina uhakika hata Mwenyezi Mungu nae huko juu Mbinguni alikwazika.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli labda leo nikuambie tu hapa hapa 'Mubashara' kabisa ni kweli kuwa kwa jinsi Tanzania ilivyokuwa 'Shaghalabaghala' Kiutawala ( Kiuongozi ) tulihitaji Rais wa aina yako ambaye ni Msimamizi, Makini na Mthubutu Kitu ambacho umekiweza kwa kiasi fulani ila Kitendo cha Wewe 'Kusifiwa' kuwa umekuwa bora kuliko wengine GENTAMYCINE nakikataa kwa 100%.
Ukweli utabaki pale pale kuwa hutoweza kuyafikia waliyoyafanya Watangulizi wako Hayati Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Hayati Mkapa na Mzee Kikwete kwani aliyekutangulia amekutangulia tu na hata sasa Wewe 'Kusifiwa' hivi 'Kinafiki' na hawa Viongozi wa Dini 'wanakukosea' mno kwani 'Maendeleo' uyafanyayo sasa 'Misingi' yake mema iliwekwa na hao Watangulizi wako.
Ombi langu tu Kuu Kwako Mheshimiwa Rais hebu 'Kataza' hii tabia ya hawa Viongozi wa Dini ambao leo siogopi kusema kuwa wengi Wao 'Wanaokusifia' wawapo nawe ni 'Wanafiki' watupu na hata tukiwa nao humu 'Mitaani' ndiyo huwa ni 'Vinara' wa Kukusema tena kwa ule 'Mtindo' wa 'Kukuzodoa' kabisa ila wakiwa nawe hapo 'Stejini' hujifanya 'Wanakupenda' na wapo nawe.
Ingekuwa ni Mimi GENTAMYCINE nipo nawe na ni Kiongozi wa Dini halafu nimepewa nafasi ya Kuombea Mkutano wako Sala yangu ingeenda hivi tu..." Ewe Mwenyezi Mungu Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakoko tunashukuru kwa hii Neema yako na Kutukutanisha kwa pamoja hapa. Mbariki Rais wetu huyu na wabariki Wagombea wengine wote wa Nafasi ya Urais nchini Tanzania na kila Mmoja umpe Baraka zako na yule ambaye Watanzania wataona anafaa na kwa nguvu zake Ewe Baba basi aweze Kushinda Uchaguzi huu ujao na aiongoze vyema Tanzania yetu. Iweke Tanzania yetu katika mikono yako Salama na Wabariki pia Watanzania wote popote pale walipo. Wewe Baba ndiyo unamjua Rais wetu ajaye hivyo kama umemchagua miongoni mwa hawa wanaogombea basi Sisi Watanzania tutakushukuru na kumpa Ushirikiano wetu wote bila kujali kama atatokea CCM, CHADEMA au ACT-Wazalendo kwani tunaamini kuwa Wagombea wote hawa ni Wazuri japo wana Uchungu wa kweli na hii Tanzania yetu. Naomba yote haya kwa Jina la Baba, la Mwana na la Roho Mtakatifu "...
Nitashukuru sana Mheshimiwa Rais Magufuli ukiufanyia Kazi 'haraka' huu 'Ushauri' wangu na zikatae hizo 'Sifa' za 'Kinafiki' unazopewa kila mara tu.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli naomba kwa leo tu nikuume kidogo Sikio kwa Kukuomba kabisa acha Kukubali hizi 'Sifa za Kilaana' ambazo naona sasa umekuwa ukipewa sana na Viongozi wa Dini mbalimbali hasa pale wakiwa nawe ama 'Ukumbini' au 'Uwanjani' Kukuombea ( Kufanya Dua ) kwani 'Kiuhalisia' maneno ambayo huwa 'wanakutamkia' sidhani kama unastahili Kuyaamini na Kuyapokea.
Na ukiona hadi leo hii Mpiga Kura wako na Mwana Kampeni wako Kivuli GENTAMYCINE nimekuja na hili Kwako jua ya kwamba halijakaa vizuri si tu Kwako au Kwetu ila nina uhakika hata kwa mwenyewe Muumba ( Mwenyezi Mungu ) nae Kwake 'halifurahii' kwakuwa hizi Sifa zote za 'Kinafiki' ambazo 'nimezibatiza' kuwa 'Sifa za Kilaana' hupaswi Kuzipokea Wewe na wala hazikuhusu kabisa.
Kitendo cha Mchungaji Mmoja leo Kuanza Kukuombea kabla hujaanza 'Kuhutubia' huku akisema haya maneno ninayanukuu hapa.." Ewe Mungu mbariki Kiongozi huyu wa Kipekee kabisa na wa aina yake kuwahi kutokea nchini Tanzania sawa na Malaika "...alikuwa si tu amekukosea Wewe au Sisi Watanzania bali nina uhakika hata Mwenyezi Mungu nae huko juu Mbinguni alikwazika.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli labda leo nikuambie tu hapa hapa 'Mubashara' kabisa ni kweli kuwa kwa jinsi Tanzania ilivyokuwa 'Shaghalabaghala' Kiutawala ( Kiuongozi ) tulihitaji Rais wa aina yako ambaye ni Msimamizi, Makini na Mthubutu Kitu ambacho umekiweza kwa kiasi fulani ila Kitendo cha Wewe 'Kusifiwa' kuwa umekuwa bora kuliko wengine GENTAMYCINE nakikataa kwa 100%.
Ukweli utabaki pale pale kuwa hutoweza kuyafikia waliyoyafanya Watangulizi wako Hayati Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Hayati Mkapa na Mzee Kikwete kwani aliyekutangulia amekutangulia tu na hata sasa Wewe 'Kusifiwa' hivi 'Kinafiki' na hawa Viongozi wa Dini 'wanakukosea' mno kwani 'Maendeleo' uyafanyayo sasa 'Misingi' yake mema iliwekwa na hao Watangulizi wako.
Ombi langu tu Kuu Kwako Mheshimiwa Rais hebu 'Kataza' hii tabia ya hawa Viongozi wa Dini ambao leo siogopi kusema kuwa wengi Wao 'Wanaokusifia' wawapo nawe ni 'Wanafiki' watupu na hata tukiwa nao humu 'Mitaani' ndiyo huwa ni 'Vinara' wa Kukusema tena kwa ule 'Mtindo' wa 'Kukuzodoa' kabisa ila wakiwa nawe hapo 'Stejini' hujifanya 'Wanakupenda' na wapo nawe.
Ingekuwa ni Mimi GENTAMYCINE nipo nawe na ni Kiongozi wa Dini halafu nimepewa nafasi ya Kuombea Mkutano wako Sala yangu ingeenda hivi tu..." Ewe Mwenyezi Mungu Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakoko tunashukuru kwa hii Neema yako na Kutukutanisha kwa pamoja hapa. Mbariki Rais wetu huyu na wabariki Wagombea wengine wote wa Nafasi ya Urais nchini Tanzania na kila Mmoja umpe Baraka zako na yule ambaye Watanzania wataona anafaa na kwa nguvu zake Ewe Baba basi aweze Kushinda Uchaguzi huu ujao na aiongoze vyema Tanzania yetu. Iweke Tanzania yetu katika mikono yako Salama na Wabariki pia Watanzania wote popote pale walipo. Wewe Baba ndiyo unamjua Rais wetu ajaye hivyo kama umemchagua miongoni mwa hawa wanaogombea basi Sisi Watanzania tutakushukuru na kumpa Ushirikiano wetu wote bila kujali kama atatokea CCM, CHADEMA au ACT-Wazalendo kwani tunaamini kuwa Wagombea wote hawa ni Wazuri japo wana Uchungu wa kweli na hii Tanzania yetu. Naomba yote haya kwa Jina la Baba, la Mwana na la Roho Mtakatifu "...
Nitashukuru sana Mheshimiwa Rais Magufuli ukiufanyia Kazi 'haraka' huu 'Ushauri' wangu na zikatae hizo 'Sifa' za 'Kinafiki' unazopewa kila mara tu.