Rais Nyerere na mkewe kwenye mazishi ya Indira Gandhi

Rais Nyerere na mkewe kwenye mazishi ya Indira Gandhi

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Katika pita pita zangu kwenye mitaa ya YouTube nimekutana na hii video kutoka ITN Archive yenye mkusanyiko wa matukio ya mambo yaliyojiri baada ya kuuliwa kwa Indira Gandhi, aliyekuwa waziri mkuu wa India, siku ya tarehe 31 Oktoba, 1984.

Siku ya mazishi ya kitaifa, viongozi wengi sana kutoka mataifa mbalimbali walihudhuria, akiwemo Rais wa Tanzania kwa wakati huo, Julius Nyerere na mkewe Maria Nyerere.

IMG_7649.png


Video ni ndefu. Nyerere anaonekana kwenye dakika ya 55:23/24.

Mtangazaji wa ITN alimgundua na kumtaja kwa jina kabisa!


View: https://youtu.be/v7SqLi1VHKA?si=5tBYB8dHEiTyKNZi

Kukosekana kwa vituo vya televisheni kulitunyima sana uhondo wa kuona vile ambavyo viongozi wetu walivyokuwa wanatuwakilisha kimataifa na vile ambavyo Tanzania ilijijengea heshima chini ya Rais Nyerere!

Miaka 10 baadaye, 1994, ndo Tanzania bara ikaja kupata vituo vyake vya televisheni, DTV, CTN, na ITV!
 
Katika pita pita zangu....
Okay!

Hakukuwa na Television tukakosa uhondo, miaka 10 baadae ikaja umesema ITV, CTN, DTV.

Enhee, leo, 100 years later, hundreds of media outlets out there.

AKIJA MHINDI, MCHINA, MWARABU, MZUNGU IKULUⁿ KUSAINI MA DOCUMENT HUWA UNAAMBIWA WHAT THE HELL THEY SIGNED ZAIDI YA MAKUBALIANO YA KUDUMISHA MAHUSIANO ?????

Nyerere is dead and gone with his autocratic media crack down lakini media kutwa kucha zinatulisha manyimbo ya WACHAFU MEDIA, mara KIMEWASHA KIMEKUNWA, KIMELOA KIMEKAUKA, KITOTO LAKINI KIMEUTAKA CHENYEWE.... NA SIMBA NA YANGA HORSE SHIT!

Television zimeleta faida gani ???????

Tanzania inaenda kununua umeme, who the hell knows imekuaje kwenye umeme wa Rufiji, hautoshi ???

What good has the freaking modern media brought ?
 
Ndio vijana wa kesho hao na maswali yao, mizaha kila mahala
Sidhani kwamba kauliza kimzaha. Chukulia muuliza swali kazaliwa mwaka 2000, inawezekana alikuwa hajawahi hata kumsikia huyo Indira Gandhi.

Kujua alikufa vipi, akazikwa vipi si rahisi kama si mtu mwenye tabia ya upekuzi na kufuatiia mambo, bahati mbaya sana ndio vijana wengi tulio nao kwa leo.
 
Sidhani kwamba kauliza kimzaha. Chukulia muuliza swali kazaliwa mwaka 2000, inawezekana alikuwa hajawahi hata kumsikia huyo Indira Gandhi.

Kujua alikufa vipi, akazikwa vipi si rahisi kama si mtu mwenye tabia ya upekuzi na kufuatiia mambo, bahati mbaya sana ndio vijana wengi tulio nao kwa leo.
Hata suala jepesi kuwa most Indians wanapigwa kiberiti, usimtetee huyo zao la ccm
 
Back
Top Bottom