Rais Ramaphosa akataa Rapa AKA kufanyiwa mazishi ya Kitaifa

Rais Ramaphosa akataa Rapa AKA kufanyiwa mazishi ya Kitaifa

Upo sahihi,na mimi nilikuwa nazungumzia matendo,kitendo cha kuimba music na kuajiri watanzania ni jambo kubwa
Bado sio kigezo, kwa hiyo matajiri wote wamiliki wa makampuni na viwanda wanastahili heshima hiyo?
 
yaani hawa wahuni wanaoharibu kizazi chetu wakifa wazikwe kitaifa ?

huyo gavana akapimwe mkojo p...mbavu zake

safi sana Rais ana akili kubwa sio kama wetu eti kila goli analipa milioni 5 yaani amekua pedeshee Samia 😏
 
Kwa lipi hasa? Huyu jamaa anaweza kuwa iconic hapo bondeni kumzidi Lucky Dube, Brenda,Hugh Masekela au Joe Mafela? Kwa kutaja kwa uchache?
 
Mbona ni mzungu,au🤣🤣🤣🤣🤣.

Hastahili hadhi hiyo jamani,japo bendera ingefunikwa kwenye jeneza Kama mtu maarufu na anajulikana ba wengi,Ila sio Bendera kupepea nusu mlingoti.
 
AKA alikua anamchana live huyu rais, swala la kumgomea gavana ilikua halikwepeki.

Na mnaoanza kufananisha sjui Lucky Dube, mara Chaka Chaka mjue zama zinabadilika. Kila mmoja ana ukubwa wake kwa zama zake.

Mwamba alikua balozi mzuri wa nchi yake, wasingepungukiwa kitu kumfunika na bendera ya taifa.

R.I.P SUPER MEGA
 
Uko sahihi kwa yote. Lakini kuna eneo aidha sijakuelewa vyema au hujaeleweka vyema. State Funeral hupewa mtu ambaye mchango wake wa kitaifa umeleta Mapinduzi na mchango wa Kipekee ambao hata watu wengine kwenye sekta hiyo wanaafiki; na kazi hiyo imekuwa na mchango wa kutambulika kwa jamii husika. Madilu, Pepe Kalle hao walikuwa ni wasanii wakubwa, lakini Hawakufikia Franco. Franco aliubadili muziki, kuukuza na kuutambulisha nje kwa miaka karibu 30 na hatimaye kuitwa mfalme wa Rhumba. Lakini, sifa nyingine ni ushawishi wa mtu huyo kwa jamii. Baada ya kuwa ametambulika sana kwa kazi yake na heshima aliyoijenga, basi jamii inamsikiliza na kuweza kufuata ayasemayo—USHAWISHI. Sasa mtu kama Franco alikuwa na uwezo wa kusimama na kusema mchagueni fulani na watu wakachagua. Pia kuna wanamuziki kama Umm Khulthum. huyu wamisri walikuwa wakimtazama kama alama ya taifa lao. Kuna wakati Rais Gamal El Nasser alikuwa hawezi ongea watu wakamuelewa hadi huyu mama azungumze. Alipofariki karibu Robo ya watu wa Misri waliingia barabarani kwenye msururu wa mazishi yake, alipewa hadhi ya kuwa Balozi (Diplomatic Status). Wanamuziki/wasanii wa kaliba hii ndio hupewa hadhi ya mazishi ya kitaifa. Sasa wampime AKA kama anaweza kufika hadhi hiyo, au ni watu kama kina Yvyone Chaka Chaka kwa Afrika kusini ndio wanaweza kufikiliwa. Je, Diamond ana hadhi hiyo. Diamond amekuta Bongo Flava imeshaanza wala hakuna mapinduzi aliyoyafanya kwenye muziki zaidi ya kujisimamia yeye binafsi na kuwa model ya namna ya kuendesha biashara ya muziki wa bongo flava (kwa hili anastahili heshima). Lakini hapa inabidi tufanye tafakari. Waasisi wa bongo flava ni watu wanaopaswa kuwa na hadhi ya kutambuliwa kutokana na kitu walichokileta kwenye jamii—watambulike Kiserikali na kitaifa—changamoto hapa ni moja, nani anasifa ya kuwa Icon wa Bongo flava.
Umeandika vizuri.... Tatizo mwandiko tu! Weka japo paragraph..
 
Nope!

Mimi hata nikiwa na ndugu star siwezi kulazimisha azikwe kitaifa coz siioni faida yoyote au hasara kwamba azikwe na serikali au jamii ndugu tukiwepo.
Umeongea point hakuna faida yeyote ile ya mtu kuzikwa kitaifa haitabadilisha outcome kama amefariki, binafsi sio faida hata ya mtu kulazimisha azikwe na kanisa
 
International Arts wana mchango mkubwa kwa mataifa yao, kwa mfano, Muziki wa Congo umefika hapo ulipo leo sababu ya watu kama Franco ndio maana alipewa state funeral, wanamuziki wana mchango Mkubwa kwa Taifa kuliko wanasiasa wengi

Hapo Tanzania leo, Diamond ana mchango mkubwa kwa Taifa kuliko kina Nape na Mwigulu
Hv aka na lucky dube yupi alitangaza sana nchi mbona dube hazikupepea nusu mlingoti
 
Nilikuwa nazungumzia Arts kwa ujumla,sio AKA, maana niliona jamaa kama anaona wanamuziki wakipewa state funeral ni nongwa
Weee usitake kujikomba hapa,
Nimemzungumzia AKA na nikasema amefanya yapi kwa taifa lake wewe ndio umekurupuka kwa kuweka watu wengine,

Kiufupi umeweka ujuaji sehemu isiyotakiwa ujuaji na ukielekezwa elekea.
 
Back
Top Bottom