Rais Samia aambiwe Makamu wa Rais ni Mkubwa kwa Rais wa Zanzibar, au anafanya makusudi!?

Kwanza Tanganyika ipo?
 
Rais wa Zanzibar si amir jeshi mkuu,fahamu hilo kwanza,ukimaliza fahamu nchi moja kamwe haiwezi kuwa na marais wawili.Ndio maana Zanzibar hawana bunge wana baraza la wawakilishi.Zanzibar ni sehemu ya JMT ukiiondoa Zanzibar hakuna JMT.
Kwani mantiki ya baraza la wawakilishi ni nn. Tatizo wabongo hatujui historia ya nchi yetu. Tanzania ni jamhuri na jeshi ni la JMT. Na ndomana haitakuja siku stakabadhi sijui zikaekwa wazi za utiaji saini wa muungano. There is a lot you guys dont know mnakurupuka na hoja zenu. Hamjui ata kwa nini karume aliuwawa. Hamjui kitu inshort mana hatufundishwi mashuleni historia yetu lkn tukiambiwa majukwaani inawekewa mapambiko. Muungano ulivyosainiwa mambo yote yanayohusu muungano ikiwepo na jeshi la tz yani JWTZ yako chini ya muungano. Na undani ni kwamba Rasi wa JMT hana mamlaka kamili ya kuendesha jeshi hilo.
 
Wambie hao Wala panyaa
 
Lakasa chika7 Hivi pesa za Tanganyika zitaingia kwenye akaunti gani?
 
Hapo hakuna mjadala.
SERIKALI NI MOJA TUUU YA YA TANZANIA.
huo mkoa WA Zanzibar mkuu wake NI mkuu wa mkoa mwinyi
Anatakiwa awe governor wa unguja na governor wa pemba, governor wa pwani (yani dar na pwani) na kuwepo magovernor kila mkoa wa tanzania na mamayor. Tatizo waasisi wa nchi walikuwa wezi wa madaraka. Walibadilisha mifumo baada ya independence ili raisi awe na mamlaka yote. Yani walikw waroho wa madaraka
 
She is there by default. She is struggling! So she will be there for 15 years? Hii si anamalizia miaka ya Magufuli. It’s a very sad confusing situation. She will be more powerful when she becomes Party chairman. Mama Samia, please get rid of Polepole first. He is so annoying
 
Mambo ya "kwetu kwanza kwa wengine baadae" yalianzia awamu ya 5 tukayanyamazia kama hayapo vile.

Kama mlishindwa kumzuia yule mwengine mwacheni mama naye aliendeleze libeneke kwa raha zake!
 

Yaani kama JPM alivoijenga na kuiinua Chato; nitafarijika sana SSH naye akiinua Zanzibar! Ikitokea hivyo lazima Katiba Mpya itakuwepo na Tanganyika yetu itarudi!!
 
Shika adabu yako Zanzibar no kubwa kuliko Tanganyika nzima
 
Labda umesahau kuwa nchi NI Tanzania.
Zanzibar na tanganyika zilikufa tarehe 26 mwezi wa 4.
Rais wa Zanzibar uwa anawekwa Tu kama BOYA kutupumbaza AKILI.
Zanzibar haijafa, Tanganyika ndio imekufa
 
Na mimi nakwambia hivi, masuala ya kimataifa ni masuala ya serikali ya muungano, si masuala ya serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.

Ndiyo maana Salmin Amour alivyotaka kuiingiza Zanzibar kuwa mwanachama wa OIC kinyemela kukazuka mgogoro wa kikatiba mpaka akachomoa.

Unakumbuka?

Ulikuwa umezaliwa?

Sasa, kumpeleka rais wa Zanzibar katika mkutano wa kimataifa wakati kuna Rais wa Tanzania, kuna Makamu wa Rais wa Tanzania, kuna Waziri Mkuu wa Tanzania, kuna Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, ni kuchanganya kazi.

Katika katiba kuna mambo yametajwa kuwa haya ni mambo ya muungano, yanatakiwa kufanywa na serikali ya muungano. Mahusiano ya kimataifa ni moja ya hayo.

Kumpa mtu anayeongoza serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kazi za serikali ya muungano za kimataifa ni kuchanganya mambo.

Huyo Rais Samia kuna mambo anafanya anayajua mwenyewe, na yanaweza kuwa na matokeo mabaya sana.
 
Kuhusu kununua ardhi Zanzibar inawezekana sana,kuna wabongo kibao wamenunua ardhi maeneo mjini wamejenga lodges,guest houses kibao,ukienda hata UROA,Pongwe,ardhi ya kununua ipo,ushindwe wewe tu kwa kukosa pesa.
 
Mama yetu raisi anaanza na raisi wa Zanzibar sababu ni mgeni mualikwa kama heshima ya mgeni halafu anakuja kwa viongozi wa jmt
 
Unaona mambo ayo na hii ndo ilopelekea muungano kuata kuvunjika in the 70s na kupelekea kifo cha rais wetu mpendwa muheshimiwa karume. Nyerere alimobolize jeshi la muungano JWTZ bila ya ridhaa ya karume ukazuka ugonvi ola most us tulikw hatujazaliwa sijui wakakubaliana kutunga uongo kama3wa 911 na libya badae watu wanagubuka mshadanganywa
 
Wanapiga sana kelele wala hawana walijualo kuhusu huu Muungano, na wanahisi Zanzibar ilizuka baada ya 1964.
 
Muungano ulivyosainiwa mambo yote yanayohusu muungano ikiwepo na jeshi la tz yani JWTZ yako chini ya muungano. Na undani ni kwamba Rasi wa JMT hana mamlaka kamili ya kuendesha jeshi hilo.

Tunaona kuwa Rais wa Zanzibar ana mamlaka ya kuwateua maofisa wa TPDF / JWTZ kuongoza vikosi maalum vya usalama, ulinzi na valantia. Makamu wa Rais wa Muungano hana nafasi hiyo bila kukasimiwa na Rais wa Muungano




Toggle navigation
President's Office and Chairman of Revolutionary Council, Zanzibar

MEDIA » NEWS AND EVENTS​

Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka Makamanda wapya aliowateua waende wakajenge na kurudisha nidhamu katika vikosi hivyo​

  • 24 Apr 2021
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Commodore Azana Hassan Msingiri kuwa Mkuu wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka Makamanda wapya aliowateua kuwa Wakuu wa Vikosi Maalum vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,waende wakajenge na kurudisha nidhamu katika vikosi hivyo.Hafla hiyo ilifanyika Ikulu Jijini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamo wa Kwanza wa Rais Othman Masoud, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Othman Makungu, Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama, viongozi wa dini, watendaji wa Serikali na wanafamilia.

Alisema kwamba Jeshi ni nidhamu na ikikosekana nidhamu hakuna Jeshi, hivyo, nidhamu ilitetereka katika vikosi na ndipo alipoamua kuwachangua Makamanda hao ili walete uzoefu wao wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa aliona haja na sababu ya kuwatumia Maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania ili waweze kuiweka nidhamu katika vikosi vya SMZ.

Aliwapongeza Wakuu wote wa Vikosi aliowaapisha hivi leo na kutaka wakafanye kazi kwa bidii na kuwataka askari na Maafisa wote wa vikosi vya SMZ kutokuwa na wasiwasi kwani lengo lake ni kujenga ili vikosi viwe madhubuti, vilivyowezeshwa na kuwa na mafunzo ya kutosha.Mapema Rais Dk. Mwinyi ambaye pia, ni Mkuu wa Vikosi hivyo kabla ya kuwaapisha Wakuu hao kwa mujibu wa Sheria aliwapaindisha vyeo vya Ukuu wa Vikosi hivyo ya SMZ.

Pia, alitumia fusra hiyo kumshukuru Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Venance Mabeyo pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi Kamanda Simon Siro kwa kukubali pendekezo lake la kuwateua Makamanda hao na kusisitiza kwamba yeye alikuwa na lengo la kutafuta viongozi na sio wataalamu kwani anachotaka ni viongozi na si fani zao.

Walioapishwa katika hafla hiyo ni Kanali Azana Hassan Msingiri kuwa Mkuu wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM), Kanali Makame Abdallah Daima kuwa Mkuu wa Kikosi cha Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU), Kanali Rashid Mzee Abdallah kuwa Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Ukozi.

Wengine ni Luteni Kanali Khamis Bakari Khamis kuwa Kamishna wa Vyuo vya Mafunzo, Luteni Kanali Burhani Zubeir Nassoro kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Uratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya pamoja na ACP Ahmed Hamis Makarani kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi (ZAECA)
Source : Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka Makamanda wapya aliowateua waende wakajenge na kurudisha nidhamu katika vikosi hivyo | Presidents Office Zanzibar
 
Hujaelewa ndugu, kunatakiwa kuwe na serekali moja ya JMT, na kila mkoa uwe na governor yani kwa upande wa znz kuweka governor wawili mmoja unguja na mwengine pemba. Hivyohivyo na bara mikoa yote iwe na magovernor ili maendeleo yawe jumuishi na sio baadhi ya mikoa inaachwa nyuma. Nadhani nitakuwa nimerekebisha kauli.
Shika adabu yako Zanzibar no kubwa kuliko Tanganyika nzima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…