Robert S Gulenga
JF-Expert Member
- Jan 3, 2013
- 2,255
- 1,565
- Thread starter
-
- #81
Samia Suluhu Hassan ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndiye anayetuvusha kwenda kwenye nchi ya Ahadi, badala ya kuuliza maswali unayojua majibu yake, Wahamasishe vijana wakachukue mikopo hii isiyo na riba ili tujenge uchumi wetuJibu swali acha porojo Samia ametoa wapi pesa?
Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Samia Suluhu HassanUngekuwa na akili ungesema ni serikali ila kwa vile wewe ni mpumbavu unasema Sa100 katoa. Huu ni upumbavu mwingine
Punguza Jaziba MKANDAHARI, mimi sina sifa ya kuchukua kwa sababu ya umri, ndio maana nakushauri wewe kijana, tengeneza kikundi na Vijana wenzako mwende mkapewe Elimu juu ya mikopo ya uwezeshaji kiuchumiWewe umechukua huo mkopo? Ungekuwa umechukua ungekuwa busy na wala usingekuwa unashinda humu kusifu na kuabudu as if utafanya kazi hii ya kusifu na kuabudu miaka yako yote. Serikali zinabadilika, walikuwepo wenzio kina Musiba, sasa yuko wapi?
@ngakotecture hii ni mikopo ya Vikundi, ni mikopo rafiki na isiyo na riba, unapewa grace period, lakini yote kwa yote kuna Wataalam katika Halmashauri watakao kukusaidia kukupa ushauriIvi ningependa niulize mfano mmepewa mkataba wa miaka miwili na muda umepita na deni halijaisha je hatua zipi zinafuata?
Halmashauri hizi hizi ambazo pesa ya mfuko wa jimbo inaingia lakini wanufaika ni wao wenyewemasai dada Mikopo hii inatolewa kupitia Halmashauri zote nchini, na unapitia kwa Mafisa Maendeleo waliopo katika kata na ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri, mikopo hii haina riba na inatolewa kwa vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu.
Fika ofisi ya Halmashauri ulipo au ofisi ya Kata uonane na Afisa Maendeleo wao ndio watakupa muongozo, Mikopo hii haina usumbufu na wala haina riba, Washauri Wanawake pamoja na Vijana wachangamkie fursa hii.
Vichwa vya ccm sijawahi kuvielewa. Pesa ni yetu wananchi. Pesa inapotoka si kushangilia kama watu hawajielewi, tushangilie only pale serikali inapoweza kuzisimamia maana huko kuna mchwa hatariSamia huyu maskini wa Zanzibar apate wapi hela zote hizo?
@butron Huu uongo hausaidii kitu, badala ya kueneza chuki na uongo usio na maana, tengeneza kikundi mwende Halmashauri mtapewa Elimu ya ujasiliamali na kisha mtanufaika na mikopo hii isiyo na riba, mikopo hii ni kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu bila kujali itikadi ya mtuHizo fedha zinatolewa kwa UVCCM na siyo vijana wote nchi hii.
Nilishashuhudia wana-CCM wakiitana serikali ya mtaa Salasala,Dar es salaam wakimwita jamaa yangu akachukue pesa japo hana Biashara yoyote.
Unasema kuwakusanya!! Hivi wamekuwa mawe!! Kwa hivyo unawakusanya vikundi sijui? Je unawapa pesa wafanye Nini au ndio hao mnawaona wakiuza huko barabarani wakati Nyumbani ameamka hajanywa chai na hajui jioni atakula Nini na atalala wapi! Hiyo pesa inarudishwaje?Vyura99tu Ujumbe umeupata na itapendeza kama utakusanya vijana na kuwapa elimu juu ya mikopo hii ili waweze nufaika na hatimaye kuchangia kwenye ujenzi wa Taifa hili.
ndo maana mkuu nimeuliza je ikiwa upo nje ya mkataba halmashauri wanachukua hatua gani kwa wana kikundi?
Ndio maana nasisitiza bora mchaguane watu ambao mnajuana na mnajishughulisha kwa sababu mtu mmoja akiwa na mwenendo mbaya, presha mnapata wote.Kwenye kikundi inabidi mtu akifirisika mtaji, mjitahidi mlipe nyie ambao biashara zipo hai kwa sababu akifeli mmoja maana yake kikundi kimefeli.
Kwa uzoefu wangu mfano kuna watu walikopeshwa bajaji wakashindwa kurejesha mkopo kwa wakati, wakaongezewa muda bado wakashindwa. Mwisho bajaji zikarudishwa manispaa.
Issue ni kupata sisi wa chini yaani hio wanaipiga kwa connection, mkienda vijana ambao hamna connection hampati hata sentiNi fedha za asilimia kumi zitokanazo na makusanyo ya Halmashauri.
Kwanini unaniita muongo ilihali aliyepewa mkopo ni jamaa yangu.Acheni kutetea ujinga, upuuzi wa huu mfuko inajulikana,ata DC wa Temeke alishafanya uchunguzi na kuibua madudu ya hizi pesa.@butron Huu uongo hausaidii kitu, badala ya kueneza chuki na uongo usio na maana, tengeneza kikundi mwende Halmashauri mtapewa Elimu ya ujasiliamali na kisha mtanufaika na mikopo hii isiyo na riba, mikopo hii ni kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu bila kujali itikadi ya mtu
butron ni kweli anaweza kuwa aliyepewa mkopo ni jamaa yako au ndugu kabisa, lakini hakupewa kwa sababu yeye ana kadi ya ACT au CHADEMA au CCM, kapewa kwa sababu moja ni Kijana wa Kitanzania, amejiunga na kikundi na anaenda kutumia mkopo kwaajili ya ujasiliamali,Kwanini unaniita muongo ilihali aliyepewa mkopo ni jamaa yangu.Acheni kutetea ujinga, upuuzi wa huu mfuko inajulikana,ata DC wa Temeke alishafanya uchunguzi na kuibua madudu ya hizi pesa.
Ni pesa za "mama"Ni pesa za serikali kuu au ni pesa za Halmashauri?
antanarivo ya kale yashapita, jikusanyeni vijana azisheni biashara mkasajiliwe, muoneni Afisa Maendeleo wa eneo mlilopo awape elimu zaidi juu ya uwezeshwaji Wananchi kiuchumi, mikopo hii inaombwa kwenye mfumo hakuna ujanja ujanja wa zamani.Issue ni kupata sisi wa chini yaani hio wanaipiga kwa connection, mkienda vijana ambao hamna connection hampati hata senti
Uko sahihi kabisa Turudi pale Rau Madukani ni muhimu saana kwanza wote muwe mnabiashara au hata kama ndio mnaanza basi muwe mnajuana vizuri, mtu asije chukua then asitumie kwenye biashara, wakati wa kulipa mmoja akisumbua basi Wanakikundi wote mtalazimika kubeba jukumu la kuhakikisha mkopo unalipwaNdio maana nasisitiza bora mchaguane watu ambao mnajuana na mnajishughulisha kwa sababu mtu mmoja akiwa na mwenendo mbaya, presha mnapata wote.
Vyura99tu umepewa kichwa kikusaidie kufikiri na si vinginevyo.Unasema kuwakusanya!! Hivi wamekuwa mawe!! Kwa hivyo unawakusanya vikundi sijui? Je unawapa pesa wafanye Nini au ndio hao mnawaona wakiuza huko barabarani wakati Nyumbani ameamka hajanywa chai na hajui jioni atakula Nini na atalala wapi! Hiyo pesa inarudishwaje?
Ndio maana wenye dhamana wanapeana kiasi kikubwa kuwawezeaha wenzawao na bado hazirejeshwi. !
Twanga maji!!!
Escrowseal1 Kwa sasa Serikali imeweza kusimamia kwa asilimia 100, mikopo hii inatolewa kupitiaa mifumo.Vichwa vya ccm sijawahi kuvielewa. Pesa ni yetu wananchi. Pesa inapotoka si kushangilia kama watu hawajielewi, tushangilie only pale serikali inapoweza kuzisimamia maana huko kuna mchwa hatari
Asante,Mkuu Trinity fuatilia, haya mambo ya kusikia kwa watu hayana ukweli, Mkuu ukifika Halmashauri usipolizika namna ulivyohudumiwa nenda kwa Mkurugenzi au kwa DC jambo lako litatatuliwa, kuna weza kuwa kuna matatizo ya kibinadamu lakini ukweli Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya wanajitahidi saana kuwahudumia Wananchi
Nina shida na huu mtazamo wa RAIS ATOA FEDHA.Tatizo la ajira kwa Vijana ni tatizo la dunia nzima kwa sasa, tatizo hili linachangiwa pia na hali ya uchumi wa dunia kwa sasa, licha ya jitihada za Serikali inayoongozwa na Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuhakikisha uchumi unaimarika bado tatizo la ajira ni changamoto ya dunia nzima.
Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa mwaka wa fedha 2022/2023 amepanga kutoa mikopo isiyo na riba kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu jumla ya shilingi bilion 75.98 kupitia Halmashauri za Wilaya, fedha hizi zitasaidia saana Vijana kuazisha miradi ili kujikwamua na kuoongeza fursa mbalimbali, Vijana watakaopata fedha hizi wanaweza kuajiri vijana wenzao na kuchangia kwenye pato la nchi.
Fedha hizi za mikopo zimeshaanza kutolewa kwenyebHalmashauri zote kupitia Maafisa Maendeleo wa Halmashauri husika katika Ofisi za Wakurugenzi. Vijana twende tukapate mikopo hii isiyo na masharti magumu na haina riba. Vijana wenzangu tukipata mikopo hii tukumbuke kurejesha ili kuwezesha Vijana wenzetu pia waweze kunufaika na Mikopo hii.
Kwa mwaka wa fedha uliopita (2021/2022) Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa jumla ya shilingi bilioni 59,236,353,909.00 kama Mikopo isiyo na riba kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu,. Kupitia fedha hizo tumeshuhudia Vikundi vingi vikifanikiwa kuazisha miradi mbali mbali na kuweza kutoa ajira kwa vijana wenzao ikiwa ni pamoja na kuchangia katika pato la nchi,
Kuna kikundi cha vijana Dar Es Salaam kilipata mkopo na kufanikiwa kuazisha Kituo cha Afya/ Zahanati ambacho kwa sasa sio kinasaidia tu kutoa huduma kwa Watanzania bali kimetoa ajira kwa Vijana hao na wenzao.
Ukienda Wilaya ya Rufiji maeneo ya Ikwiriri kuna kikundi kilinufaika na mikopo hii kinajihusisha na uselemala, kimekuwa kikundi kikubwa kwa sasa, wanatengeneza fanicha kama pale keko, nimeshuhudia si mara moja Wafanyabiashara wa keko wa fanicha wakienda kuchukua vitanda na fanicha nyingine bora kabisa pale ikwiriri kutoka kwenye kikundi hiki, kikundi hiki kimeweza kutoa ajira kwa vijana wengi (sina takwimu halisi) lakini ukifika kwenye eneo la kazi yao utakuta zaidi ya vijana 100 wakiwa wamejiajiri kutoka na uwezeshwaji wa mikopo hii isiyo na riba.
Niliwahi kuona pia kikundi cha Vijana waliojiajiri na kilimo cha umwagiliaji hapo Rufiji, Vijana hao ni Wasomi kabisa na wanafanya vizuri, wamepata elimu nzuri kutoka kwa Watalaamu kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji, sio rahisi kutaja vikundi vyote lakini ni wazi mikopo hii imekuwa mkombozi kwa Vijana wengi.
Kuna kijiji nilienda huko Rufiji kila kijana ana piki piki anayotumia kwa shughuli zake za kilimo na wengine wanatumia kwa shughuli za biashara, lakini nilipouliza nini kipo nyuma ya mafanikio haya nikaambiwa ni kutokana na uwezeshaji wa kiuchumi kwa Wananchi unaofanywa na Serikali kupitia mikopo isiyo na riba, vijana wanamashamaba ya korosho na ufuta.
Huko kusini, kuna kikundi cha Mazingira kupitia mikopo hii Wameweza kununua mpaka gari (Scania) la zaidi ya milioni 120 kutokana na mikopo hii ya kuwezesha Wananchi kiuchumi.
Manufaa ya mikopo hii ni mengi, Vijana twende Halmashauri tukapate Elimu, Halmashauri zina Watalaamu wa kila nyanja, Halmashauri zinaweza saidia kupata vifaa kama vya kuazishia viwanda vya tofali etc..
Vijana tutoke kwenye mitandao kwenye kutukana watu na kukejeli, wale wanaokejeli na kupinga kila jitihada za Serikali msiwasikilize wana watu wanaowalipa kwa kazi hizo, Serikali iko macho, inaona.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki Raisi wa Jamhuri wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan.
Msanii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye Amiri Jeshi Mkuu, ndiye kiongozi mkuu wa Serikali,Nina shida na huu mtazamo wa RAIS ATOA FEDHA.
Naomba kufahamu ukwasi binafsi wa Rais hadi awe anatoa hela hizo nje ya mfuko wa umma..
Je hizo hela zinaatikanaje?
Nani anazipangia matumizi?
Nani anazifanyia ukaguzi?
Rais anapokiwa amezitoa, yeye anafaidikiaje at the end?
Nauliza maswali haya kwa sababu kila waziri na kiongozi mteuliwa akisimama huongelea kuhusu pesa anazotoa rais.
Kama sivyo, basi tusiendeleze dhambi ya kumgombanisha Rais na pesa za umma