Rais Samia aanza kutoa Fedha bilioni 75.98 kwa Vijana na Wanawake kupitia Halmashauri za Wilaya. Hii ni Fursa, tuchangamkie

Mimi Ni CHADEMA lakin pesa zipo wanatoa nimeshuhudia uncle wangu alipata akanunua sabufa na nyingine katumia then navyojua hii mikopo Serikali haiwez kukudai Kama hile ya Finca
 
Msanii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye Amiri Jeshi Mkuu, ndiye kiongozi mkuu wa Serikali,
Haujajibu swali langu.
Pesa aanazozitoa zinatoka wapi?

Mbona sikuwahi kusikia kauli hizi kwa kina Kikwete, Mkapa, Mwinyi na Nyerere?

Serikali inafanyakazi au zote ni kazi za mtu mmoja? Bunge kazi yake nini basi?

Tusijaribu kujenga utamaduni usiokuwa asili yetu.

Au kinachofanyika Bungeni ni kiinimacho tu?
 
Naona watu wanakuwa waoga wanasema ili upate lazima connection, napinga.
Sisi kwenye kikundi chetu tulipata hatukuwa na connection kabisa. Ila changamoto tulichelewa sana kupata mkopo nadhani karibu miezi 9 hivi.
Yaani tunapata mkopo hadi mawazo yameshakauka kichwani. Siku hizi nasikia fasta tu maana kuna watu huwa nawatengenezea katiba wanasema hivyo.

Mimi binafsi sitaki tena mkopo kwa vile muda wa kusimamia biashara na presha zake sina na sitaki, nakunywa bia tu. Bora kuajiriwa tu hata ukizembea au usipoenda unalipwa. Lakini biashara ukizembea inakuadhibu na watu wanaona kabisa.
 
The greatest form of dictatorship arises from greatest form of democracy, and vice versa.
IPO siku Rais atachukua maamuzi, tena naomba iwe sasa.
Hatuwezi kuwaogopa wezi wa mali zetu, yawapasa watuogope wao.
 
Hizi hela zina urasimu sana kuzipata ni bora zikapelekwa benki tu watu wanazipata kwa dhamana za kawaida hata vyeti vya elimu zao tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…