Rais Samia achukua hatua, Wadau mbalimbali wampongeza

Rais Samia achukua hatua, Wadau mbalimbali wampongeza

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
RAIS Samia Suluhu Hassan amemwagiwa sifa na wananchi na viongozi mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa kuchukua hatua za haraka na madhubuti kushughulikia uzembe na ubadhirifu wa pesa za umma uliobainishwa kwenye ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Rais Samia amemuagiza Katibu Mkuu Kiongozi kuwaelekeza Makatibu Wakuu wote wa wizara pamoja na Watendaji Wakuu wa taasisi za serikali kusoma ripoti zote za CAG za mwaka wa fedha 2021/22 zilizotolewa hadharani Aprili 6 mwaka huu, kujibu na kuzifanyia kazi hoja zote zilizoibuliwa.

Hatua hizo za Rais Samia zimeibua shangwe za wananchi nchini Tanzania na hata kuwagusa wananchi wa nchi za jirani za Kenya na Uganda ambao wametoa maoni yao kupitia mitandao ya kijamii.
 
Ni lipi wasilolijua wakati ukaguzi haukufanywa kwa siri, ati Rais Samia amemuagiza Katibu Mkuu Kiongozi kuwaelekeza Makatibu Wakuu wote wa wizara pamoja na Watendaji Wakuu wa taasisi za serikali kusoma ripoti zote za CAG za mwaka wa fedha 2021/22 zilizotolewa hadharani Aprili 6 mwaka huu, kujibu na kuzifanyia kazi hoja zote zilizoibuliwa.
 
Wahusika wamekataa kutupisha, mpaka wang'olewe kwa nguvu au hawakumwelewa Rais.Watanzania wakaidi Sana.
 
Labda hatua ya kuhamasisha ufisadi nchini🐒🐒🐒
 
Watanzania ni wajinga mno Yani mtu anawazuga zuga eti hatua ni ujinga
 
Back
Top Bottom