Rais Samia aipongeza ATCL kwa kuchanja mbuga, Kenya sasa ni Tshs 770,000 tu

Ndio maana mtu anaona bora akafunge mzigo China kuliko kununua Nairobi au South Africa.
Kwa maana nyingine fedha zetu Waafrika zinazidi kuboresha mzunguuko wa fedha wa nchi zingine nje ya bara la Africa kwa gharama kubwa za usafiri baina ya nchi zetu
 
Tanzania tunakwenda vizuri Sana kama nchi
Rais Samia kila anachogusa kinafanikiwa sana
Mungu ibariki Tanzania
Pole sana kwa kusifia hata visivyosifika.

Kutoka Dar kwenda Dubai au tuseme Oman haizidi 600kl two way, sasa why Nairobi 770kl?
 
Inashangaza jinsi ilivyo ghali kusafiri kutoka Dar hadi Nairobi (700,000)! Hapana kuna kitu lazima kifanyike, hizi sifa za kijinga hazitufai.
 
Unaposema hakuna km rais samia unamaanisha nini mkuu??
 
Hakuna kipya hapo.
Kwenda Kenya huwa tunakwenda kwa miguu, baiskeli, punda, bodaboda, pickup, noah, mabasi, boti nk.
Kenya Airways imekuwa inapiga hizo trip kila siku. Na hizo trip kwa ATCL zilishakuwepo tangu miaka ya sabini.
Ajabu ni nini?

Yaani miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika, na zaidi ya miaka 40 toka kuanzishwa ATCL, leo tunajipongeza na kujivunia kuwa na route ya kwenda Nairobi, Kenya!
Nani katuroga?
 
Kaziiendelee kwa speed,
 
Tanzania na Samia,

1.Uchumi Juu,

2. Uwekezaji juu

3. Diplomasia juu

4. Amani & Upendo juu

5. Maendeleo juu

6. Demokrasia juu
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…