Pre GE2025 Rais Samia akagua Maboresho ya Bandari Tanga, Bilioni 429 zatumika ikiwemo ujenzi wa gati mbili mpya

Pre GE2025 Rais Samia akagua Maboresho ya Bandari Tanga, Bilioni 429 zatumika ikiwemo ujenzi wa gati mbili mpya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan Akitembelea Bandari ya Tanga na Kuzungumza na Wafanyakazi wa Bandari, leo tarehe 01 Machi, 2025.

---
Tanga.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Machi 1, 2025, ametembelea Bandari ya Tanga kukagua maboresho makubwa yaliyotekelezwa, yakiwemo ujenzi wa gati mbili mpya.

Akiwa bandarini hapo, Rais Samia amepongeza maendeleo yaliyopatikana na kusisitiza kuwa Tanga sasa inajidhihirisha kama lango muhimu la biashara kwa Afrika Mashariki na dunia kwa ujumla.

"Tulitamani kwa muda mrefu kuona meli kubwa zikitia nanga hapa, shughuli za bandari zikishamiri, na vijana wakipata ajira. Leo hii, ndoto hiyo imetimia kupitia uwekezaji wa Shilingi bilioni 429 katika maboresho haya," amesema Rais Samia.

Marekebisho hayo yameongeza kina cha maji bandarini, kuruhusu meli kubwa kufunga moja kwa moja kwenye gati badala ya kutumia matishari. Pia, muda wa kuhudumia meli umepunguzwa kutoka siku kadhaa hadi siku mbili pekee.

Tangu maboresho hayo kufanyika, uwezo wa Bandari ya Tanga kuhudumia mizigo umeongezeka kutoka tani 400,000 mwaka 2019/2020 hadi tani 1,200,000 hivi sasa. Hili ni ongezeko la zaidi ya tani 700,000. Aidha, mapato yameongezeka maradufu, kutoka Shilingi bilioni 17.27 hadi Shilingi bilioni 49 ndani ya miezi saba pekee ya mwaka huu wa fedha.

Rais Samia amesisitiza kuwa mafanikio haya hayatanufaisha tu wafanyabiashara, bali pia serikali kupitia ongezeko la mapato na kukuza sekta ya viwanda.

"Natamani kurudisha hadhi ya Tanga—iwe kitovu cha viwanda, bandari kubwa na eneo muhimu kwa uvuvi. Hiki ndicho ninachokifanya," amesisitiza.

Katika hatua nyingine, ametangaza mpango wa kujenga barabara ya Handeni-Kiberashi-Kijungu-Singida (KM 340) kwa mfumo wa ubia kati ya serikali na sekta binafsi (PPP), akieleza kuwa itarahisisha usafirishaji wa mizigo kutoka Bandari ya Tanga kwenda sehemu mbalimbali za nchi na kimataifa.

"Tutaiwekea road tolls ili mwekezaji anayejenga barabara hii aweze kurudisha gharama zake," amesema.

Akihitimisha hotuba yake, Rais Samia amewataka wafanyakazi wa bandari kuongeza ufanisi ili kuifanya Bandari ya Tanga kuwa miongoni mwa bandari bora duniani.

"Tunashindana na bandari za mataifa mengine. Tukifanya kazi kwa bidii na kupunguza gharama za uendeshaji, Tanga itakuwa kitovu cha biashara Afrika Mashariki," ameongeza.

Maboresho haya yanaimarisha nafasi ya Bandari ya Tanga kama kitovu cha biashara, yakichochea ukuaji wa uchumi wa Tanzania kwa kuifanya kuwa lango kuu la biashara kwa meli kubwa na kuunganisha nchi na masoko ya kimataifa.

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua Maboresho ya mradi wa gati mbili mpya katika Bandari ya Tanga, leo tarehe 01 Machi, 2025.
IMG-20250301-WA0010.jpg

MAELEZO YA MHESHIMIWA WAZIRI WA UCHUKUZI KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, WAKATI WA ZIARA YAKE MKOANI TANGA - BANDARI YA TANGA TAREHE 1 MACHI, 2025

Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga;
Waheshimiwa Mawaziri,
Waheshimiwa Manaibu Waziri,
Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya,
Wananchi wote,
Mabibi na Mabwana,

NAWASIMU KWA JINA LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

Mheshimiwa Rais,

Kwa heshima, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana hapa katika kutembelea na kukagua Bandari ya Tanga. Mheshimiwa Rais tunakupongeza kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Sekta ya ndogo Bandari chini ya Uongozi wako mahiri.

Mheshimiwa Rais,
Bandari ya Tanga ni mojawapo ya maeneo yaliyopokea uwekezaji mkubwa ambapo Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imefanikiwa kutekeleza mradi mkubwa wa maboresho kwa gharama ya jumla ya Shilingi Bilioni 429.16. Mradi huu ulitekelezwa na Mkandarasi M/S China Harbour Engineering Company (CHEC) katika awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza ilihusisha upanuzi wa njia ya kuingiza meli, kuongeza kina cha maji kutoka mita 3 hadi mita 13, na ununuzi wa mitambo 16 ya kuhudumia shehena. Awamu ya pili ilihusisha ujenzi wa gati jipya lenye urefu wa mita 450 na kina cha mita 13, pamoja na Yadi ya makasha ya mita za mraba 7,230. Kutokana na maboresho haya, Bandari ya Tanga sasa ina uwezo wa kuhudumia meli mbili kwa wakati mmoja zenye urefu wa mita 220 na kubeba tani 60,000 kila moja.

Mheshimiwa Rais,
Kama aliyoeleza Mkurugenzi Mkuu wa TPA, maboresho haya yameleta mafanikio makubwa katika ufanisi wa Bandari ya Tanga. Uwezo wa kuhudumia shehena umeongezeka kutoka tani 750,000 hadi tani 3,000,000 kwa mwaka, huku idadi ya meli zilizoingia bandarini ikiongezeka kutoka meli 118 mwaka 2019/2020 hadi meli 307 mwaka 2023/2024.

Muda wa kuhudumia meli umepungua kutoka siku 5 hadi siku 2, jambo lililopunguza gharama za uendeshaji na kuvutia wateja zaidi. Mapato ya Bandari yameongezeka kutoka Shilingi Bilioni 17.23 mwaka 2019/2020 hadi Shilingi Bilioni 38.70 mwaka 2023/2024, na kwa miezi saba pekee ya mwaka wa fedha 2024/25, tayari TPA imekusanya Shilingi Bilioni 49.84 bilioni, haya ni mafanikio makubwa kuwahi kutokea katika bandari hii.

Mheshimiwa Rais,
Uwekezaji mkubwa uliofanyika katika Bandari ya Tanga umechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za usafirishaji na kuongeza ushindani wa bandari hii katika ukanda wa Afrika Mashariki. Hatua hizi zimeifanya Bandari ya Tanga kuwa kivutio kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi, hususan kutoka Uganda, Rwanda, Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kufuatia maelekezo yako ya kuhakikisha bandari hii inatoa mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa letu, Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi imechukua hatua zifuatazo:-

i.Ukarabati na uimarishaji wa njia ya reli kuingia bandarini (port link) yenye urefu wa kilomita 3.9 pamoja na kituo cha reli (rail terminal) katika Bandari ya Tanga unatarajiwa kuanza mwezi Machi 2025.

Shirika la Reli Tanzania (TRC) liko katika hatua za mwisho za ununuzi ya vifaa, ambapo kazi hiyo itatekelezwa na kikosi kazi cha TRC na matarijio ifikapo Juni, 2025, kazi hizi zitakamilika. Aidha, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) tayari imetoa malipo ya awali (advance payment) ya TZS 232,184,987 kwa TRC kwa ajili ya maandalizi ya awali. Kukamilika kwa mradi huu kutaboresha usafirishaji wa mizigo kwa kuunganisha reli na bandari, hivyo kuongeza ufanisi, kupunguza gharama za usafirishaji, na kuboresha huduma za uchukuzi kutoka na kuingia Tanga na kuyafikia masoko ya mikoa yote iliyoungnishwa na reli.

ii.Serikali ina Mpango wa kufanya ukarabati mkubwa wa njia ya Reli kutoka Ruvu Junction hadi Tanga (kilomita188) na Mruazi hadi Arusha (kilomita 381) ambapo mwezi Aprili 2023, Wizara kupitia Shirika la reli Tanzania ilisaini mikataba yenye thamani ya dola za marekani 132.54 imesainiwa kati ya TRC na kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) ili kuwezesha ukarabati wa kilomita 533 kwa kuondoa reli chakavu na nyepesi, kuongeza uwezo wa madaraja kutoka tani 13 hadi tani 18.5 kwa ekseli.

Mikataba hii inahusisha ununuzi wa reli nzito za latili 80 kwa yadi sawa na 40kg/m, mataluma pamoja na vifungashio, mara baada ya kukamilisha ukarabati huu utawezesha treni kuongeza mwendokasi kutoka Kilomita 20 kwa saa hadi Kilomita 75 kwa saa, usalama wa mizigo na abiria na kupunguza muda wa safari.

iii.Wizara kupitia Shirika la Reli Tanzania imekamilisha upembuzi na usanifu ujenzi wa Reli ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma, yenye urefu wa kilomita 1,028 utakaounganisha Bandari ya Tanga na Machimbo ya magadi (Engaruka), Mijingu Phosphate, na Nikeli (Dutwa) kupitia Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Mkalama (Singida), Meatu na Bunda. Hatua iliyopo ni kutafuta rasilimali fedha na utekelezaji wa mradi unatarajiwa kuzishirikisha sekta binafsi.

iv.Wizara ya Uchukuzi, kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), ipo katika hatua za kuingia makubaliano na Wizara ya Kilimo ili kuhakikisha pembejeo zote za kilimo zinazoingia nchini zinapitia Bandari ya Tanga kwa ajili ya kusambazwa nchi nzima. Hatua hii inalenga kupunguza mzigo katika Bandari ya Dar es Salaam huku ikiimarisha nafasi ya Bandari ya Tanga kama kitovu cha biashara na usafirishaji wa pembejeo za kilimo nchini.

Mheshimiwa Rais;
v.Kuhusu Kuimarisha Usalama wa Usafiri Majini hapa Tanga, Serikali kupitia Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kupitia mapato yake ya ndani, mwaka huu wa fedha inatekeleza mradi wa Manunuzi ya Boti Mpya zenye uwezo wa spidi ya 40knots. Boti hizo zitahusika na shughuli za Doria, Utaftaji na Uokozi pamoja na kusaidia ukaguzi wa vyombo baharini.

Mkandarasi ameshapatikana kampuni ya M/s MERCAN TENKE DENIZ ARACLARI kutoka Nchini Uturuki na anakwenda kutekeleza kazi hiyo kwa thamani ya USD 700,000 (Takribani Shilingi Bilioni 2.620). Mikataba ipo hatua ya mwisho na inatarajiwa ya kusainiwa mwezi Machi 2025. Muda wa ujenzi ni miezi 6 tangu tarehe ya kusainiwa mikataba hiyo.

Mheshimiwa Rais;
Aidha, Serikali inaendelea na kukamilisha taratibu za Ukatabati na Upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Tanga. Utekelezaji wa mradi huu utajumuisha ujenzi wa njia ya kuruka na kutua ndege (runway), maegesho ya ndege (apron) na taxiway kwa kiwango cha lami. Pia, mradi utahusisha Ujenzi wa Jengo jipya la abiria, taa za kuongozea ndege, access road, maegesho ya ndege, gari la zimamoto na uzio wa usalama. Kiwacha hiki kitajengwa kwa darala la ICAO Code 3C.

Mhandisi mshauri ameshapatikana anaendelea na merejeo ya usanifu na Taratibu za kupata mkandarasi zipo hatua za mwisho ambapo Mkataba unatarajiwa kusainiwa mwezi Machi,2025. Aidha, mradi huu utagharamiwa kupitia fedha za Benki ya Dunia. Lengo la Uwanja huu wa daraja la 3C ni kuhudumia ndege za ukubwa wa Bombardier. Uwanja huu utakapokamilika, Serikali kupitia Shirika la Ndege la ATCL litaanzisha safari za ndege baina ya Dar es Salaam, Pemba, Tanga na Mombasa ili kuwa na usafiri wa uhakika na waharaka kwa maeneo hayo kwa madhumuni ya kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Rais,
Ukuaji wa kasi wa uchumi wa Mkoa wa Tanga umetokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali, ikiwemo upanuzi wa Bandari ya Tanga, ujenzi wa Bomba la Mafuta, miradi ya majisafi na salama, ufufuaji wa viwanda, na uboreshaji wa mtandao wa barabara. Miradi hii imeongeza shughuli za biashara na uwekezaji, hali ambayo imeongeza mahitaji ya huduma za usafiri wa anga katika mkoa huu.

Mheshimiwa Rais,
Kwa kutambua mafanikio haya, Serikali inaendelea na mipango ya kupanua zaidi Bandari ya Tanga kwa kujenga gati jipya lenye urefu wa mita 300, kununua mashine za kisasa za kuhudumia makasha, na kuboresha miundombinu ya kuhifadhi mizigo na kuhudumia abiria.

Maboresho haya ni sehemu ya dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wako, ya kuimarisha miundombinu na hudma za uchukuzi kwa lengo la kuongeza tija, kukuza uchumi, na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Rais,

Baada ya kusema hayo kwa heshima na unyenyekevu Mkubwa naomba kukukaribisha uweze kuzungumza na Wananchi waliohudhuria hapa.
IMG-20250301-WA0008.jpg
IMG-20250301-WA0009.jpg
IMG-20250301-WA0011.jpg
IMG-20250301-WA0013.jpg
IMG-20250301-WA0014.jpg
IMG-20250301-WA0015.jpg
IMG-20250301-WA0016.jpg
IMG-20250301-WA0018.jpg
IMG-20250301-WA0021.jpg
IMG-20250301-WA0022.jpg
IMG-20250301-WA0025.jpg
IMG-20250301-WA0027.jpg
IMG-20250301-WA0029.jpg
IMG-20250301-WA0031.jpg
IMG-20250301-WA0033.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua Maboresho ya mradi wa gati mbili mpya katika Bandari ya Tanga, leo tarehe 01 Machi, 2025.
View attachment 3254663
MAELEZO YA MHESHIMIWA WAZIRI WA UCHUKUZI KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, WAKATI WA ZIARA YAKE MKOANI TANGA - BANDARI YA TANGA TAREHE 1 MACHI, 2025

Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga;
Waheshimiwa Mawaziri,
Waheshimiwa Manaibu Waziri,
Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya,
Wananchi wote,
Mabibi na Mabwana,

NAWASIMU KWA JINA LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

Mheshimiwa Rais,

Kwa heshima, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana hapa katika kutembelea na kukagua Bandari ya Tanga. Mheshimiwa Rais tunakupongeza kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Sekta ya ndogo Bandari chini ya Uongozi wako mahiri.

Mheshimiwa Rais,
Bandari ya Tanga ni mojawapo ya maeneo yaliyopokea uwekezaji mkubwa ambapo Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imefanikiwa kutekeleza mradi mkubwa wa maboresho kwa gharama ya jumla ya Shilingi Bilioni 429.16. Mradi huu ulitekelezwa na Mkandarasi M/S China Harbour Engineering Company (CHEC) katika awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza ilihusisha upanuzi wa njia ya kuingiza meli, kuongeza kina cha maji kutoka mita 3 hadi mita 13, na ununuzi wa mitambo 16 ya kuhudumia shehena. Awamu ya pili ilihusisha ujenzi wa gati jipya lenye urefu wa mita 450 na kina cha mita 13, pamoja na Yadi ya makasha ya mita za mraba 7,230. Kutokana na maboresho haya, Bandari ya Tanga sasa ina uwezo wa kuhudumia meli mbili kwa wakati mmoja zenye urefu wa mita 220 na kubeba tani 60,000 kila moja.

Mheshimiwa Rais,
Kama aliyoeleza Mkurugenzi Mkuu wa TPA, maboresho haya yameleta mafanikio makubwa katika ufanisi wa Bandari ya Tanga. Uwezo wa kuhudumia shehena umeongezeka kutoka tani 750,000 hadi tani 3,000,000 kwa mwaka, huku idadi ya meli zilizoingia bandarini ikiongezeka kutoka meli 118 mwaka 2019/2020 hadi meli 307 mwaka 2023/2024.

Muda wa kuhudumia meli umepungua kutoka siku 5 hadi siku 2, jambo lililopunguza gharama za uendeshaji na kuvutia wateja zaidi. Mapato ya Bandari yameongezeka kutoka Shilingi Bilioni 17.23 mwaka 2019/2020 hadi Shilingi Bilioni 38.70 mwaka 2023/2024, na kwa miezi saba pekee ya mwaka wa fedha 2024/25, tayari TPA imekusanya Shilingi Bilioni 49.84 bilioni, haya ni mafanikio makubwa kuwahi kutokea katika bandari hii.

Mheshimiwa Rais,
Uwekezaji mkubwa uliofanyika katika Bandari ya Tanga umechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za usafirishaji na kuongeza ushindani wa bandari hii katika ukanda wa Afrika Mashariki. Hatua hizi zimeifanya Bandari ya Tanga kuwa kivutio kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi, hususan kutoka Uganda, Rwanda, Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kufuatia maelekezo yako ya kuhakikisha bandari hii inatoa mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa letu, Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi imechukua hatua zifuatazo:-

i.Ukarabati na uimarishaji wa njia ya reli kuingia bandarini (port link) yenye urefu wa kilomita 3.9 pamoja na kituo cha reli (rail terminal) katika Bandari ya Tanga unatarajiwa kuanza mwezi Machi 2025.

Shirika la Reli Tanzania (TRC) liko katika hatua za mwisho za ununuzi ya vifaa, ambapo kazi hiyo itatekelezwa na kikosi kazi cha TRC na matarijio ifikapo Juni, 2025, kazi hizi zitakamilika. Aidha, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) tayari imetoa malipo ya awali (advance payment) ya TZS 232,184,987 kwa TRC kwa ajili ya maandalizi ya awali. Kukamilika kwa mradi huu kutaboresha usafirishaji wa mizigo kwa kuunganisha reli na bandari, hivyo kuongeza ufanisi, kupunguza gharama za usafirishaji, na kuboresha huduma za uchukuzi kutoka na kuingia Tanga na kuyafikia masoko ya mikoa yote iliyoungnishwa na reli.

ii.Serikali ina Mpango wa kufanya ukarabati mkubwa wa njia ya Reli kutoka Ruvu Junction hadi Tanga (kilomita188) na Mruazi hadi Arusha (kilomita 381) ambapo mwezi Aprili 2023, Wizara kupitia Shirika la reli Tanzania ilisaini mikataba yenye thamani ya dola za marekani 132.54 imesainiwa kati ya TRC na kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) ili kuwezesha ukarabati wa kilomita 533 kwa kuondoa reli chakavu na nyepesi, kuongeza uwezo wa madaraja kutoka tani 13 hadi tani 18.5 kwa ekseli.

Mikataba hii inahusisha ununuzi wa reli nzito za latili 80 kwa yadi sawa na 40kg/m, mataluma pamoja na vifungashio, mara baada ya kukamilisha ukarabati huu utawezesha treni kuongeza mwendokasi kutoka Kilomita 20 kwa saa hadi Kilomita 75 kwa saa, usalama wa mizigo na abiria na kupunguza muda wa safari.

iii.Wizara kupitia Shirika la Reli Tanzania imekamilisha upembuzi na usanifu ujenzi wa Reli ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma, yenye urefu wa kilomita 1,028 utakaounganisha Bandari ya Tanga na Machimbo ya magadi (Engaruka), Mijingu Phosphate, na Nikeli (Dutwa) kupitia Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Mkalama (Singida), Meatu na Bunda. Hatua iliyopo ni kutafuta rasilimali fedha na utekelezaji wa mradi unatarajiwa kuzishirikisha sekta binafsi.

iv.Wizara ya Uchukuzi, kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), ipo katika hatua za kuingia makubaliano na Wizara ya Kilimo ili kuhakikisha pembejeo zote za kilimo zinazoingia nchini zinapitia Bandari ya Tanga kwa ajili ya kusambazwa nchi nzima. Hatua hii inalenga kupunguza mzigo katika Bandari ya Dar es Salaam huku ikiimarisha nafasi ya Bandari ya Tanga kama kitovu cha biashara na usafirishaji wa pembejeo za kilimo nchini.

Mheshimiwa Rais;
v.Kuhusu Kuimarisha Usalama wa Usafiri Majini hapa Tanga, Serikali kupitia Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kupitia mapato yake ya ndani, mwaka huu wa fedha inatekeleza mradi wa Manunuzi ya Boti Mpya zenye uwezo wa spidi ya 40knots. Boti hizo zitahusika na shughuli za Doria, Utaftaji na Uokozi pamoja na kusaidia ukaguzi wa vyombo baharini.

Mkandarasi ameshapatikana kampuni ya M/s MERCAN TENKE DENIZ ARACLARI kutoka Nchini Uturuki na anakwenda kutekeleza kazi hiyo kwa thamani ya USD 700,000 (Takribani Shilingi Bilioni 2.620). Mikataba ipo hatua ya mwisho na inatarajiwa ya kusainiwa mwezi Machi 2025. Muda wa ujenzi ni miezi 6 tangu tarehe ya kusainiwa mikataba hiyo.

Mheshimiwa Rais;
Aidha, Serikali inaendelea na kukamilisha taratibu za Ukatabati na Upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Tanga. Utekelezaji wa mradi huu utajumuisha ujenzi wa njia ya kuruka na kutua ndege (runway), maegesho ya ndege (apron) na taxiway kwa kiwango cha lami. Pia, mradi utahusisha Ujenzi wa Jengo jipya la abiria, taa za kuongozea ndege, access road, maegesho ya ndege, gari la zimamoto na uzio wa usalama. Kiwacha hiki kitajengwa kwa darala la ICAO Code 3C.

Mhandisi mshauri ameshapatikana anaendelea na merejeo ya usanifu na Taratibu za kupata mkandarasi zipo hatua za mwisho ambapo Mkataba unatarajiwa kusainiwa mwezi Machi,2025. Aidha, mradi huu utagharamiwa kupitia fedha za Benki ya Dunia. Lengo la Uwanja huu wa daraja la 3C ni kuhudumia ndege za ukubwa wa Bombardier. Uwanja huu utakapokamilika, Serikali kupitia Shirika la Ndege la ATCL litaanzisha safari za ndege baina ya Dar es Salaam, Pemba, Tanga na Mombasa ili kuwa na usafiri wa uhakika na waharaka kwa maeneo hayo kwa madhumuni ya kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Rais,
Ukuaji wa kasi wa uchumi wa Mkoa wa Tanga umetokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali, ikiwemo upanuzi wa Bandari ya Tanga, ujenzi wa Bomba la Mafuta, miradi ya majisafi na salama, ufufuaji wa viwanda, na uboreshaji wa mtandao wa barabara. Miradi hii imeongeza shughuli za biashara na uwekezaji, hali ambayo imeongeza mahitaji ya huduma za usafiri wa anga katika mkoa huu.

Mheshimiwa Rais,
Kwa kutambua mafanikio haya, Serikali inaendelea na mipango ya kupanua zaidi Bandari ya Tanga kwa kujenga gati jipya lenye urefu wa mita 300, kununua mashine za kisasa za kuhudumia makasha, na kuboresha miundombinu ya kuhifadhi mizigo na kuhudumia abiria.

Maboresho haya ni sehemu ya dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wako, ya kuimarisha miundombinu na hudma za uchukuzi kwa lengo la kuongeza tija, kukuza uchumi, na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Rais,

Baada ya kusema hayo kwa heshima na unyenyekevu Mkubwa naomba kukukaribisha uweze kuzungumza na Wananchi waliohudhuria hapa.
View attachment 3254661View attachment 3254662View attachment 3254664View attachment 3254665View attachment 3254666View attachment 3254667View attachment 3254668View attachment 3254669View attachment 3254670View attachment 3254671View attachment 3254672View attachment 3254673View attachment 3254674View attachment 3254675View attachment 3254676
Jambo zuri, but pia wachukue mfano wa singapore ambapo mashine za kupakuw mizigo ni self driven, wana staff ndogo but very efficiency
 
Eeehh, Samia ni mwamba wa kizimkazi
 
Je na hii bandari ya Tanga Ipo sokoni tayari kwa mnada au tayari kwa siri imeshapewa mdau wa maendeleo mwekezaji kutoka nje
 
Jambo zuri, but pia wachukue mfano wa singapore ambapo mashine za kupakuw mizigo ni self driven, wana staff ndogo but very efficiency
Watakuuliza Je, hao walioajiriwa kwa kazi hiyo watakwenda wapi? Je, kuna njia mbadala ya kuwafanya waendelee na maisha ya ajira/kujiajiri au ndo watakuwa jobless.
 
Je na hii bandari ya Tanga Ipo sokoni tayari kwa mnada au tayari kwa siri imeshapewa mdau wa maendeleo mwekezaji kutoka nje
Most likely itakuja kwa mnada,kumbuka Kafulila anatarajia kujenga reli ya SGR From Tanga hadi Musoma kubeba,nickel,phosphate ya Minjigu na Magadi soda toka lake Eyasi kwa mpango wake wa PPP
 
Jambo zuri, but pia wachukue mfano wa singapore ambapo mashine za kupakuw mizigo ni self driven, wana staff ndogo but very efficiency
Unemployment ya Singapore ni under 2%, sisi na Unemployment yetu ilivyo juu kwenda self driven ni kumwaga majobless zaidi mitaani. Acha vijana wetu wapate ajira. Dawa ni kutafuta njia za kuongeza viwango vya uwajibikaji (efficiency) kwa kupunguza ubabaishaji, porojo, rushwa na ufisadi.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua Maboresho ya mradi wa gati mbili mpya katika Bandari ya Tanga, leo tarehe 01 Machi, 2025.
View attachment 3254663
MAELEZO YA MHESHIMIWA WAZIRI WA UCHUKUZI KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, WAKATI WA ZIARA YAKE MKOANI TANGA - BANDARI YA TANGA TAREHE 1 MACHI, 2025

Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga;
Waheshimiwa Mawaziri,
Waheshimiwa Manaibu Waziri,
Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya,
Wananchi wote,
Mabibi na Mabwana,

NAWASIMU KWA JINA LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

Mheshimiwa Rais,

Kwa heshima, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana hapa katika kutembelea na kukagua Bandari ya Tanga. Mheshimiwa Rais tunakupongeza kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Sekta ya ndogo Bandari chini ya Uongozi wako mahiri.

Mheshimiwa Rais,
Bandari ya Tanga ni mojawapo ya maeneo yaliyopokea uwekezaji mkubwa ambapo Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imefanikiwa kutekeleza mradi mkubwa wa maboresho kwa gharama ya jumla ya Shilingi Bilioni 429.16. Mradi huu ulitekelezwa na Mkandarasi M/S China Harbour Engineering Company (CHEC) katika awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza ilihusisha upanuzi wa njia ya kuingiza meli, kuongeza kina cha maji kutoka mita 3 hadi mita 13, na ununuzi wa mitambo 16 ya kuhudumia shehena. Awamu ya pili ilihusisha ujenzi wa gati jipya lenye urefu wa mita 450 na kina cha mita 13, pamoja na Yadi ya makasha ya mita za mraba 7,230. Kutokana na maboresho haya, Bandari ya Tanga sasa ina uwezo wa kuhudumia meli mbili kwa wakati mmoja zenye urefu wa mita 220 na kubeba tani 60,000 kila moja.

Mheshimiwa Rais,
Kama aliyoeleza Mkurugenzi Mkuu wa TPA, maboresho haya yameleta mafanikio makubwa katika ufanisi wa Bandari ya Tanga. Uwezo wa kuhudumia shehena umeongezeka kutoka tani 750,000 hadi tani 3,000,000 kwa mwaka, huku idadi ya meli zilizoingia bandarini ikiongezeka kutoka meli 118 mwaka 2019/2020 hadi meli 307 mwaka 2023/2024.

Muda wa kuhudumia meli umepungua kutoka siku 5 hadi siku 2, jambo lililopunguza gharama za uendeshaji na kuvutia wateja zaidi. Mapato ya Bandari yameongezeka kutoka Shilingi Bilioni 17.23 mwaka 2019/2020 hadi Shilingi Bilioni 38.70 mwaka 2023/2024, na kwa miezi saba pekee ya mwaka wa fedha 2024/25, tayari TPA imekusanya Shilingi Bilioni 49.84 bilioni, haya ni mafanikio makubwa kuwahi kutokea katika bandari hii.

Mheshimiwa Rais,
Uwekezaji mkubwa uliofanyika katika Bandari ya Tanga umechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za usafirishaji na kuongeza ushindani wa bandari hii katika ukanda wa Afrika Mashariki. Hatua hizi zimeifanya Bandari ya Tanga kuwa kivutio kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi, hususan kutoka Uganda, Rwanda, Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kufuatia maelekezo yako ya kuhakikisha bandari hii inatoa mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa letu, Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi imechukua hatua zifuatazo:-

i.Ukarabati na uimarishaji wa njia ya reli kuingia bandarini (port link) yenye urefu wa kilomita 3.9 pamoja na kituo cha reli (rail terminal) katika Bandari ya Tanga unatarajiwa kuanza mwezi Machi 2025.

Shirika la Reli Tanzania (TRC) liko katika hatua za mwisho za ununuzi ya vifaa, ambapo kazi hiyo itatekelezwa na kikosi kazi cha TRC na matarijio ifikapo Juni, 2025, kazi hizi zitakamilika. Aidha, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) tayari imetoa malipo ya awali (advance payment) ya TZS 232,184,987 kwa TRC kwa ajili ya maandalizi ya awali. Kukamilika kwa mradi huu kutaboresha usafirishaji wa mizigo kwa kuunganisha reli na bandari, hivyo kuongeza ufanisi, kupunguza gharama za usafirishaji, na kuboresha huduma za uchukuzi kutoka na kuingia Tanga na kuyafikia masoko ya mikoa yote iliyoungnishwa na reli.

ii.Serikali ina Mpango wa kufanya ukarabati mkubwa wa njia ya Reli kutoka Ruvu Junction hadi Tanga (kilomita188) na Mruazi hadi Arusha (kilomita 381) ambapo mwezi Aprili 2023, Wizara kupitia Shirika la reli Tanzania ilisaini mikataba yenye thamani ya dola za marekani 132.54 imesainiwa kati ya TRC na kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) ili kuwezesha ukarabati wa kilomita 533 kwa kuondoa reli chakavu na nyepesi, kuongeza uwezo wa madaraja kutoka tani 13 hadi tani 18.5 kwa ekseli.

Mikataba hii inahusisha ununuzi wa reli nzito za latili 80 kwa yadi sawa na 40kg/m, mataluma pamoja na vifungashio, mara baada ya kukamilisha ukarabati huu utawezesha treni kuongeza mwendokasi kutoka Kilomita 20 kwa saa hadi Kilomita 75 kwa saa, usalama wa mizigo na abiria na kupunguza muda wa safari.

iii.Wizara kupitia Shirika la Reli Tanzania imekamilisha upembuzi na usanifu ujenzi wa Reli ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma, yenye urefu wa kilomita 1,028 utakaounganisha Bandari ya Tanga na Machimbo ya magadi (Engaruka), Mijingu Phosphate, na Nikeli (Dutwa) kupitia Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Mkalama (Singida), Meatu na Bunda. Hatua iliyopo ni kutafuta rasilimali fedha na utekelezaji wa mradi unatarajiwa kuzishirikisha sekta binafsi.

iv.Wizara ya Uchukuzi, kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), ipo katika hatua za kuingia makubaliano na Wizara ya Kilimo ili kuhakikisha pembejeo zote za kilimo zinazoingia nchini zinapitia Bandari ya Tanga kwa ajili ya kusambazwa nchi nzima. Hatua hii inalenga kupunguza mzigo katika Bandari ya Dar es Salaam huku ikiimarisha nafasi ya Bandari ya Tanga kama kitovu cha biashara na usafirishaji wa pembejeo za kilimo nchini.

Mheshimiwa Rais;
v.Kuhusu Kuimarisha Usalama wa Usafiri Majini hapa Tanga, Serikali kupitia Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kupitia mapato yake ya ndani, mwaka huu wa fedha inatekeleza mradi wa Manunuzi ya Boti Mpya zenye uwezo wa spidi ya 40knots. Boti hizo zitahusika na shughuli za Doria, Utaftaji na Uokozi pamoja na kusaidia ukaguzi wa vyombo baharini.

Mkandarasi ameshapatikana kampuni ya M/s MERCAN TENKE DENIZ ARACLARI kutoka Nchini Uturuki na anakwenda kutekeleza kazi hiyo kwa thamani ya USD 700,000 (Takribani Shilingi Bilioni 2.620). Mikataba ipo hatua ya mwisho na inatarajiwa ya kusainiwa mwezi Machi 2025. Muda wa ujenzi ni miezi 6 tangu tarehe ya kusainiwa mikataba hiyo.

Mheshimiwa Rais;
Aidha, Serikali inaendelea na kukamilisha taratibu za Ukatabati na Upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Tanga. Utekelezaji wa mradi huu utajumuisha ujenzi wa njia ya kuruka na kutua ndege (runway), maegesho ya ndege (apron) na taxiway kwa kiwango cha lami. Pia, mradi utahusisha Ujenzi wa Jengo jipya la abiria, taa za kuongozea ndege, access road, maegesho ya ndege, gari la zimamoto na uzio wa usalama. Kiwacha hiki kitajengwa kwa darala la ICAO Code 3C.

Mhandisi mshauri ameshapatikana anaendelea na merejeo ya usanifu na Taratibu za kupata mkandarasi zipo hatua za mwisho ambapo Mkataba unatarajiwa kusainiwa mwezi Machi,2025. Aidha, mradi huu utagharamiwa kupitia fedha za Benki ya Dunia. Lengo la Uwanja huu wa daraja la 3C ni kuhudumia ndege za ukubwa wa Bombardier. Uwanja huu utakapokamilika, Serikali kupitia Shirika la Ndege la ATCL litaanzisha safari za ndege baina ya Dar es Salaam, Pemba, Tanga na Mombasa ili kuwa na usafiri wa uhakika na waharaka kwa maeneo hayo kwa madhumuni ya kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Rais,
Ukuaji wa kasi wa uchumi wa Mkoa wa Tanga umetokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali, ikiwemo upanuzi wa Bandari ya Tanga, ujenzi wa Bomba la Mafuta, miradi ya majisafi na salama, ufufuaji wa viwanda, na uboreshaji wa mtandao wa barabara. Miradi hii imeongeza shughuli za biashara na uwekezaji, hali ambayo imeongeza mahitaji ya huduma za usafiri wa anga katika mkoa huu.

Mheshimiwa Rais,
Kwa kutambua mafanikio haya, Serikali inaendelea na mipango ya kupanua zaidi Bandari ya Tanga kwa kujenga gati jipya lenye urefu wa mita 300, kununua mashine za kisasa za kuhudumia makasha, na kuboresha miundombinu ya kuhifadhi mizigo na kuhudumia abiria.

Maboresho haya ni sehemu ya dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wako, ya kuimarisha miundombinu na hudma za uchukuzi kwa lengo la kuongeza tija, kukuza uchumi, na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Rais,

Baada ya kusema hayo kwa heshima na unyenyekevu Mkubwa naomba kukukaribisha uweze kuzungumza na Wananchi waliohudhuria hapa.
View attachment 3254661View attachment 3254662View attachment 3254664View attachment 3254665View attachment 3254666View attachment 3254667View attachment 3254668View attachment 3254669View attachment 3254670View attachment 3254671View attachment 3254672View attachment 3254673View attachment 3254674View attachment 3254675View attachment 3254676
Pamoja na haya yote CCM hawawezi kushinda uchaguzi bila polisi na wakurugenzi, sijui wanajisikiaje!
 
Unemployment ya Singapore ni under 2%, sisi na Unemployment yetu ilivyo juu kwenda self driven ni kumwaga majobless zaidi mitaani. Acha vijana wetu wapate ajira. Dawa ni kutafuta njia za kuongeza viwango vya uwajibikaji (efficiency) kwa kupunguza ubabaishaji, porojo, rushwa na ufisadi.
Hajafanya fully automation, lakin hatuwez avoid mabaliko ya tech just because of jobless. Jobless wapo na watakuja wapya
 
Alafu badae tunakuja kumpa mwekezaji mwenye mtaji wa bilion 500 Kwa miaka 40
 
Back
Top Bottom