Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki shughuli ya kuanza kujaza maji kwenye bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) leo Desemba 22, 2022
Maharage Chande, Mkurugenzi wa TANESCO
Maji yanayopita katika mashine moja ya kufua umeme ni lita 225,000 kwa sekunde, wakati kwa jiji la Dar es Salaam lita za maji kwa sekunde ni 30,000. Hapa unaweza kuona ukubwa wa mradi huu.
Mradi huu unakadiriwa kutumia jumla ya trilioni 6.5, hadi kufikia mwezi novemba mkandarasi alikuwa amelipwa trilioni 4.5 ambayo ni sawa na asilimia 70 ya malipo yote. Fedha za mradi huu ni fedha za kodi zetu Watanzania na mkandarasi hadai.
Pia, hadi kufikia mwezi novemba mwaka huu, jumla ya wafanyakazi 12, 275 waliajiriwa ambapo kati yao Watanzania ni 11,164 sawa na 90.97%, wageni ni 1,111 sawa na 9.1%
Rais mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Samel Shokry,Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Misri ambaye ameiwakilisha Serikali nchi hiyo Katika zoezi la uzinduzi wa ujazaji wa maji Katika bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere JNHPP ambaoo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan atashuhudia.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria Katika uzinduzi huo wa kukaza maji kwenye bwawa la Julius Nyerere JNHPP Leo Kushoto ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.
Rais Samia anazungumza:
Mradi huu unatoa taswira kuwa Tanzania inaweza kufanya mambo makubwa, unapotaja mabwawa makubwa, hili nalo linaingia kwenye orodha hiyo, mradi huu utatuletea umeme wa uhakika.
Nimeona kazi kubwa na nzito iliyofanywa, ni kazi kubwa na yenye ubora ya viwango vinavyotakiwa. Wzo la mradi huu lilianza wakati wa Mwalimu Nyerere, ilipofika Awamu ya Tano, Nchi yetu chini ya John Pombe Magufuli tulisema liwalo na liwe katika kutekeleza mradi huu.
Nakumbuka 'sabotage' zilizofanywa, lakini marehemu akasema tunaendelea na tutafanya.
Wakati nakabidhiwa Nchi kuongoza, ujenzi wa mradi huu ulikuwa katika 37% kwa sasa upo 78%, huu ni mradi wenye faida nyingi, utasaidia kudhibiti mafuriko, utaimarisha fursa la utalii hasa eneo la Kusini mwa Tanzania na hivyo kutoa ajira za moja kwa moja na nyinginezo.
Maji yanayopita hapa ni mengi, yanaweza kusaidia maj safi na salama kwa Dar es Salaam na viunga vyake, nimuelekeze Waziri wa Maji aitaka Dawasa
Hivyo ujenzi wa Bwawa utumike kupeleka maji Dar na ikiwezekana tuyafikishe kwenye maeneo mengine yenye shida kama vile Tanga na Morogoro, hatuwezi kuendelea kutegemea Mto Ruvu kutokana na mabadiliko ya mazingira.
Makamu wa Rais alitoa maelekezo kuwa mifugo yote ambayo imeingia kwenye bonde hili iondolewe
Nataka niseme jambo moja tunaposhughulikia migogoro hii ya kuhamisha wafugaji tuzingatie Sheria na Kanuni, weledi na haki za binadamu pia zizingatiwe
Katika Wilaya moja Kilosa au jirani nah apo DC alivyoulizwa sababu za migogoro ya wakulima na wafugaji alisema ng’ombe wengi wanaoingizwa ni wa wakubwa nay eye hawezi kuwagusa.
Nasema hakuna mkubwa mbele ya sheria, hakuna mkubwa atakayetuharibia mradi huu, hakuna mkubwa atakayetuharibia rasilimali hii tuliyoijenga kw agharama kubwa
Naomba wakuu wa mikoa na Wilaya mkafanye kazi zenu, atakayeogopa wakubwa anyoonye mkono wakubwa wamshughulikie.
Wananchi, wafanyabiashara na taasisi zote wanochepusha maji katika Mto wa Rufiji wazuiwe, natambua maji haya pia yanahitajika kwa matumizi mengine ya kiuchumi na maendeleo
Kanuni za mgawano wa maji zizingatiwe, vibali vya matumizi ya maji na uwekezaji katika shughuli za uzalishaji zinazohitaji maji mengi visitolewe katika maeneo ya juu bali wawekezaji waelekezwe katika uwanda wa chini wa mradi huu.
Itasaidia kama tutaunda kamati za ulinzi wa mazingira na zipewe mafunzo.
======================
Rais Samia Atoa maagizo kwa Wizara 5 Utunzaji wa Mazingira
Na. Beatrice Sanga - MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan ameziagiza Wizara 5 za Kisekta Nchini ikiwemo Kilimo, Uvuvi, Maji Mazingira pamoja na Ufugaji kuketi na kutumia nafasi zitokanazo na Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere huku akisisitiza uhifadhi wa mazingira katika vyanzo vya maji vinavyo jaza Mto Rufiji kutokana na umuhimu wa Mto huo katika Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere.
Rais Samia ametoa maagizo hayo leo Rufiji Mkoani Pwani wakati wa ufunguzi ujazaji maji katika Bwawa la Mwalimu Nyerere ambapo amesema kwa sasa Sekta zote zenye nafasi ya kuvutia wawekezaji na kutengeneza fursa kutokana na maji ya Bwawa la Mwalimu Nyerere kufanya hivyo ikiwemo Sekta ya Kilimo na Maji ambao ndio watanifaika kupitia Bwawa la Mwalimu Nyerere.
"Nazielekeza Wizara ya Kilimo, Wizara ya Ardhi na TAMISEMI na mamlaka nyingine mkapime maeneo hayo na muyaweke katika mashamba makubwa kwa ajili ya kufanya mnada wa wazi kwa wawekezaji wa uhakika katika kilimo, nawasihi pia mtenge maeneo maalum kwa ajili ya wakulima wadogowadogo hasa wa maeneo hayo yatakayokuwa na Miundombinu ya umwagiliaji maji" Amesema Rais Samia.
Aidha Rais Dokta Samia ameagiza Wizara ya Mazingira kuchukua hatua dhidi ya waharibifu wa mazingira katika vyanzo vya maji katika mito na maeneo muhimu ambayo yanatumika kama chanzo cha maji katika Bwawa la Mwalimu Nyerere.
"Ndugu wananchi manufaa ya Bwawa hili katika nyanja zote yanawezekana tu kama tutatunza mazingira katika vyanzo vya mabonde ya Mito inayoleta maji mabwawani hapa nataka nisisitize umuhimu wa kutunza mazingira Kwani huu mradi tumeujenga kwa gharama kubwa na kwa kujinyima vitu vingi muhimu itakuwa ni dhambi kubwa kama hautatimiza malengo yake kwa sababu ya uzembe na ubinafsi wetu kwahiyo kulinda mazingira na kulinda mradi huu Sasa ni suala la kufa na kupona" Amesema Rais Samia.
Kwa upande wake Waziri wa Nishati January Makamba pamoja na Mkurugenzi wa TANESCO maharage Chande wamesema Serikali inaendelea na mipango ya muda ya mrefu ya kukabiliana na changanoto ya umeme ikiwemo kujenga mabwawa manne pamoja na kuanzisha miradi mingine kupitia Nishati jadilifu ili kukabiliana na changamoto ya umeme.
"Tupo katika kupanga mbele na ukiangalia Ile chati yetu sisi Leo hii tunajua mpaka 2040 mradi gani utaingia kwenye gridi, tumejipanga kwa muda mrefu na sio kwa muda mfupi, tunachoomba ni subira tatizo la kukatika umeme litaisha, sisi tunataka ndani ya miaka ijayo ibaki historia kwamba chini ya uongozi wako Mheshimiwa Rais ndipo ulimaliza shida yote ya umeme ya kudumu na Hilo ndilo tunalolifanya na subira tunayo na na mipango tunayo hivi Leo tunavozungumza tuna mabwawa mengine mawili ambayo tunatafutia wakandarasi” Amesema Mhe. Makamba
Katika hafla hiyo pia imehudhuriwa na viongozi kutoka nchini Misri, Spika wa Bunge Tullia Akson , Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Abdulahman Kinana ambapo wakizungumza katika hafla hiyo wameutaja Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere kama moja ya Mradi utakao leta mapinduzi katika Sekta ya Nishati ambayo ni muhimu kwa maendeleo.
Hata hivyo pamoja na zoezi la kubofya kitufe kuashilia kuanza kujaza maji pia Rais Samia amepokea tuzo sanjari na Marais Wastaafu kutokana na kufanikisha ndoto za ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ambalo likikamilika litazalisha Megawati 2115.
PIA SOMA
TUHUMA ZA UFISADI NA HUJUMA
HISTORIA
Maharage Chande, Mkurugenzi wa TANESCO
Maji yanayopita katika mashine moja ya kufua umeme ni lita 225,000 kwa sekunde, wakati kwa jiji la Dar es Salaam lita za maji kwa sekunde ni 30,000. Hapa unaweza kuona ukubwa wa mradi huu.
Mradi huu unakadiriwa kutumia jumla ya trilioni 6.5, hadi kufikia mwezi novemba mkandarasi alikuwa amelipwa trilioni 4.5 ambayo ni sawa na asilimia 70 ya malipo yote. Fedha za mradi huu ni fedha za kodi zetu Watanzania na mkandarasi hadai.
Pia, hadi kufikia mwezi novemba mwaka huu, jumla ya wafanyakazi 12, 275 waliajiriwa ambapo kati yao Watanzania ni 11,164 sawa na 90.97%, wageni ni 1,111 sawa na 9.1%
Rais mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Samel Shokry,Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Misri ambaye ameiwakilisha Serikali nchi hiyo Katika zoezi la uzinduzi wa ujazaji wa maji Katika bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere JNHPP ambaoo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan atashuhudia.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria Katika uzinduzi huo wa kukaza maji kwenye bwawa la Julius Nyerere JNHPP Leo Kushoto ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.
Mradi huu unatoa taswira kuwa Tanzania inaweza kufanya mambo makubwa, unapotaja mabwawa makubwa, hili nalo linaingia kwenye orodha hiyo, mradi huu utatuletea umeme wa uhakika.
Nimeona kazi kubwa na nzito iliyofanywa, ni kazi kubwa na yenye ubora ya viwango vinavyotakiwa. Wzo la mradi huu lilianza wakati wa Mwalimu Nyerere, ilipofika Awamu ya Tano, Nchi yetu chini ya John Pombe Magufuli tulisema liwalo na liwe katika kutekeleza mradi huu.
Nakumbuka 'sabotage' zilizofanywa, lakini marehemu akasema tunaendelea na tutafanya.
Wakati nakabidhiwa Nchi kuongoza, ujenzi wa mradi huu ulikuwa katika 37% kwa sasa upo 78%, huu ni mradi wenye faida nyingi, utasaidia kudhibiti mafuriko, utaimarisha fursa la utalii hasa eneo la Kusini mwa Tanzania na hivyo kutoa ajira za moja kwa moja na nyinginezo.
Maji yanayopita hapa ni mengi, yanaweza kusaidia maj safi na salama kwa Dar es Salaam na viunga vyake, nimuelekeze Waziri wa Maji aitaka Dawasa
Hivyo ujenzi wa Bwawa utumike kupeleka maji Dar na ikiwezekana tuyafikishe kwenye maeneo mengine yenye shida kama vile Tanga na Morogoro, hatuwezi kuendelea kutegemea Mto Ruvu kutokana na mabadiliko ya mazingira.
Makamu wa Rais alitoa maelekezo kuwa mifugo yote ambayo imeingia kwenye bonde hili iondolewe
Nataka niseme jambo moja tunaposhughulikia migogoro hii ya kuhamisha wafugaji tuzingatie Sheria na Kanuni, weledi na haki za binadamu pia zizingatiwe
Katika Wilaya moja Kilosa au jirani nah apo DC alivyoulizwa sababu za migogoro ya wakulima na wafugaji alisema ng’ombe wengi wanaoingizwa ni wa wakubwa nay eye hawezi kuwagusa.
Nasema hakuna mkubwa mbele ya sheria, hakuna mkubwa atakayetuharibia mradi huu, hakuna mkubwa atakayetuharibia rasilimali hii tuliyoijenga kw agharama kubwa
Naomba wakuu wa mikoa na Wilaya mkafanye kazi zenu, atakayeogopa wakubwa anyoonye mkono wakubwa wamshughulikie.
Wananchi, wafanyabiashara na taasisi zote wanochepusha maji katika Mto wa Rufiji wazuiwe, natambua maji haya pia yanahitajika kwa matumizi mengine ya kiuchumi na maendeleo
Kanuni za mgawano wa maji zizingatiwe, vibali vya matumizi ya maji na uwekezaji katika shughuli za uzalishaji zinazohitaji maji mengi visitolewe katika maeneo ya juu bali wawekezaji waelekezwe katika uwanda wa chini wa mradi huu.
Itasaidia kama tutaunda kamati za ulinzi wa mazingira na zipewe mafunzo.
======================
Rais Samia Atoa maagizo kwa Wizara 5 Utunzaji wa Mazingira
Na. Beatrice Sanga - MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan ameziagiza Wizara 5 za Kisekta Nchini ikiwemo Kilimo, Uvuvi, Maji Mazingira pamoja na Ufugaji kuketi na kutumia nafasi zitokanazo na Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere huku akisisitiza uhifadhi wa mazingira katika vyanzo vya maji vinavyo jaza Mto Rufiji kutokana na umuhimu wa Mto huo katika Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere.
Rais Samia ametoa maagizo hayo leo Rufiji Mkoani Pwani wakati wa ufunguzi ujazaji maji katika Bwawa la Mwalimu Nyerere ambapo amesema kwa sasa Sekta zote zenye nafasi ya kuvutia wawekezaji na kutengeneza fursa kutokana na maji ya Bwawa la Mwalimu Nyerere kufanya hivyo ikiwemo Sekta ya Kilimo na Maji ambao ndio watanifaika kupitia Bwawa la Mwalimu Nyerere.
"Nazielekeza Wizara ya Kilimo, Wizara ya Ardhi na TAMISEMI na mamlaka nyingine mkapime maeneo hayo na muyaweke katika mashamba makubwa kwa ajili ya kufanya mnada wa wazi kwa wawekezaji wa uhakika katika kilimo, nawasihi pia mtenge maeneo maalum kwa ajili ya wakulima wadogowadogo hasa wa maeneo hayo yatakayokuwa na Miundombinu ya umwagiliaji maji" Amesema Rais Samia.
Aidha Rais Dokta Samia ameagiza Wizara ya Mazingira kuchukua hatua dhidi ya waharibifu wa mazingira katika vyanzo vya maji katika mito na maeneo muhimu ambayo yanatumika kama chanzo cha maji katika Bwawa la Mwalimu Nyerere.
"Ndugu wananchi manufaa ya Bwawa hili katika nyanja zote yanawezekana tu kama tutatunza mazingira katika vyanzo vya mabonde ya Mito inayoleta maji mabwawani hapa nataka nisisitize umuhimu wa kutunza mazingira Kwani huu mradi tumeujenga kwa gharama kubwa na kwa kujinyima vitu vingi muhimu itakuwa ni dhambi kubwa kama hautatimiza malengo yake kwa sababu ya uzembe na ubinafsi wetu kwahiyo kulinda mazingira na kulinda mradi huu Sasa ni suala la kufa na kupona" Amesema Rais Samia.
Kwa upande wake Waziri wa Nishati January Makamba pamoja na Mkurugenzi wa TANESCO maharage Chande wamesema Serikali inaendelea na mipango ya muda ya mrefu ya kukabiliana na changanoto ya umeme ikiwemo kujenga mabwawa manne pamoja na kuanzisha miradi mingine kupitia Nishati jadilifu ili kukabiliana na changamoto ya umeme.
"Tupo katika kupanga mbele na ukiangalia Ile chati yetu sisi Leo hii tunajua mpaka 2040 mradi gani utaingia kwenye gridi, tumejipanga kwa muda mrefu na sio kwa muda mfupi, tunachoomba ni subira tatizo la kukatika umeme litaisha, sisi tunataka ndani ya miaka ijayo ibaki historia kwamba chini ya uongozi wako Mheshimiwa Rais ndipo ulimaliza shida yote ya umeme ya kudumu na Hilo ndilo tunalolifanya na subira tunayo na na mipango tunayo hivi Leo tunavozungumza tuna mabwawa mengine mawili ambayo tunatafutia wakandarasi” Amesema Mhe. Makamba
Katika hafla hiyo pia imehudhuriwa na viongozi kutoka nchini Misri, Spika wa Bunge Tullia Akson , Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Abdulahman Kinana ambapo wakizungumza katika hafla hiyo wameutaja Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere kama moja ya Mradi utakao leta mapinduzi katika Sekta ya Nishati ambayo ni muhimu kwa maendeleo.
Hata hivyo pamoja na zoezi la kubofya kitufe kuashilia kuanza kujaza maji pia Rais Samia amepokea tuzo sanjari na Marais Wastaafu kutokana na kufanikisha ndoto za ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ambalo likikamilika litazalisha Megawati 2115.
PIA SOMA
- Arab Contractors na Elsewedy Electric Kukabidhiwa Rasmi Eneo la Rufiji (PHPP) Kesho
- Arab Contractors wakabidhiwa Billion 688.6 kama malipo ya awali mradi wa umeme wa maporomoko ya mto Rufiji
- Serikali Yakabidhi Eneo La Mradi Wa Umeme Wa Maji Mto Rufiji Kwa Mkandarasi Tayari Kwa Kazi Kuanza
- Rais Magufuli kuzindua mradi wa umeme Mto Rufiji Julai 26, 2019
- SADC yamuunga mkono Rais Dkt Magufuli ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme Rufiji
- Uzinduzi Mradi wa Umeme, mto Rufiji: Rais Magufuli aagiza sehemu ya Selous kuwa Hifadhi ya Taifa
- Mbunge Sospiere Mukweli ameniogopesha kwa kauli yake kuhusu ujenzi wa bwawa la Rufiji; je, kuna haja ya wabunge wote kupimwa akili?
- Mradi wa Kufua Umeme Rufiji (MW 2115) uchimbaji kina cha lango la kuingilia maji kwenye mitambo wakamilika
- Kampuni ya ElSewedy Electric Co inayotengeneza bwawa la umeme Rufiji imewekewa vikwazo, haitaweza kukopesheka nje
- Waziri Makamba: Msitegemee wala kutarajia bwawa la mto Rufiji kujazwa maji mwezi Machi
- Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asema Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya mradi wa umeme wa mto Rufiji
- Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere Hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda
- Waziri Makamba: Ujenzi wa tuta kwenye bwawa la mwl Nyerere umekamilika
- Maji katika bwawa la Nyerere kuanza kujazwa 15/11/2021 na 13/04/2022 litakuwa limejaa tayari kwa majaribio
- PM Majaliwa: Bwawa la umeme kukamilika Juni 2022
- Tanesco:- Bwawa la Nyerere litakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2115 hata kama mvua haijanyesha kwa miaka 2
- Waziri Kalemani: Bwawa la Nyerere kujazwa Maji Novemba 15, 2021. Umeme wa maji ni nafuu kuliko wa vyanzo vingine
- Kutokukamilika kwa Mradi wa Umeme Rufiji mwaka 2022 kama ilivyotakiwa na sasa Kukamilika 2024 ni Kumtukana na Kumdhalilisha Hayati Dkt. Magufuli
- Rais Samia kuzindua zoezi la ujazaji maji katika Bwawa la Julius Nyerere, Disemba 22
- Makamba: Ujenzi wa Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere umefikia asilimia 67
- Makamba: Sisi tumeamua kuwa wakweli, bwawa la Nyerere linaisha Juni 2024. Adai tarehe ya mwanzo isingewezekana kwa namna yoyote
- Makamba: Itachukua misimu miwili ya mvua kujaza Bwawa la Nyerere
- Maji yatakayojazwa Bwawa la Nyerere (JNHPP) yanaweza kuzalisha Umeme kwa mwaka mmoja bila kutegemea mvua
- Rais Samia akishiriki shughuli ya kuanza kujaza maji Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), 22/12/2022
- TANESCO: Bwawa la Nyerere halitapunguza bei ya umeme
- Serikali: Mashine ya kwanza ya Kufua Umeme Bwawa la Nyerere itawashwa Mwezi Februari 2024
- Rais Samia: Uzalishaji Umeme Bwawa la Nyerere kuanza Januari 2024
- TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma
- Kamati ya Bunge: Bwawa la Nyerere litakamilika Juni 2024, Tsh. Trilioni 5.85 zimelipwa tayari
- Biteko: Shida ya umeme sasa basi, megawati 235 zimeingia Grid ya Taifa
- Rais Samia: Suluhu ya Umeme itapatikana Aprili 2024 baada ya kuanza uzalishaji wa Megawatt 470-500 katika Bwawa la Mwalimu Nyerere!
- Dotto Biteko: Tumezima mtambo wa bwawa la Mwl Nyerere
- TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma
- Profesa Tibaijuka: Mafuriko ya Rufiji hayajasababishwa na Ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ila limeshindwa kuregulate mafuriko!
- Mtambo wa pili bwawa la Nyerere kuwashwa, kumaliza kabisa mgao wa umeme nchini
TUHUMA ZA UFISADI NA HUJUMA
- Mtaalam: Watanzania mnadanganywa Stiglers Gorge haiwezekani kwani Kina cha Maji Mto Rufiji kinapungua mno
- Hatma ya mradi Stiegler’s Gorge: Hatakama hatukubaliana kiitikadi, tukubaliane katika Ushauri wa kitaalam
- Hotuba ya bajeti Nishati; Miradi ya Rufiji na gesi itaumiza nchi: Mnyika aonya
- Tuambiwe ukweli: Stiglers Gorge inaweza kuwa maafa makubwa kwa taifa badala ya furaha
- Lissu: Serikali na benki hazina uwezo wa kujenga bwawa la Umeme Rufiji
- CAG: Bwawa la Nyerere liliharakiswa
- Polepole: Bwawa la Nyerere ni mradi wa kufa na kupona hatutakubali wahuni wauchezee, Winchi ni kitu kidogo sana!
- Inaumiza sana kuona mradi wa bwawa la Nyerere unahujumiwa wazi wazi
- Unakataje miti milioni 4 ili kujenga la umeme (JNHPP)
- Makamba: Mradi wa JNHPP upo nyuma kwa siku 477 (yaani mwaka na zaidi ya siku 100)
- UFISADI: Mpina aibua tuhuma za upigaji wa Sh. Trilioni 1.5 Bwawa la Nyerere
HISTORIA
- Mradi wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere katika maporomoko ya mto rufiji unaotekelezwa na Serikali uliasisiwa na Baba wa Taifa mwaka 1975
- CAG: Mradi wa Umeme wa Bwawa la Nyerere unatumia upembuzi wa mwaka 1970
- Mhandisi Mkazi, Upembuzi yakinifu wa 1980 unatumika bwawa la JNHPP
- Mwalimu Nyerere aliomba fedha Mradi wa Bwawa la Umeme Rufiji