Rais Samia akitupatia Katiba Mpya, awe Mama wa Taifa

Rais Samia akitupatia Katiba Mpya, awe Mama wa Taifa

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Tulibahatika kumpata Mwalimu Nyerere. Alikuwa ni Rais mwenye maono. Alifahamu kunahitajika nini ili nchi yetu isonge mbele.

Tukumbuke aliipokea nchi ikiwa na wasomi wachache, teknolojia duni kabisa, yenye miundombinu hafifu, elimu dhaifu, viwanda vichache sana, hakuna taasisi za utafiti, n.k. Aliondoka madarakani kukiwa na shule nyingi japo siyo za kutosha, mahospitali, reli, barabara, ndege, viwanda, vituo vya utafiti, n.k.

Kubwa kuliko vyote, aliwaacha Watanzania wakiwa wamoja. Wanaopingana kwa hoja na siyo kwa makabila yao, maeneo yao au dini zao.

Kwa kuzingatia hayo, tukampa cheo kikubwa kabisa cha BABA WA TAIFA.

Bila kutarajia, tumempata Rais Mama. Kaichukua nchi ikiwa kwenye dimbwi la uonevu, udhulumaji, uabuduji wa watu, ubambikiaji kesi, utekwaji wa watu, upotezwaji wa watu, ubaguzi kwa misingi ya vyama, ubambikiwaji wa kodi na maonevu mengine mengi. Rais mwanamama, kwa yote hayo, amesema hapana. Tunachomwomba kwa sasa, asiishie tu kuyakataa na kuyazuia maovu hayo, bali aitengeneze Tanzania kwa kaisi ambacho uovu huo hautatokea tena.

Ili kuyazuia maovu hayo ya watawala dhidi ya watawaliwa, ni lazima TUPATE KATIBA MPYA INAYOJALI MASLAHI YA TAIFA KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE.

Kama Rais Samia atawaletea Watanzania KATIBA inayoangalia zaidi maslahi ya Taifa na ya watu wake wote kwa usawa, katiba inayolinda haki na mamlaka ya wananchi, basi napendekeza apewe hadhi ya kuwa MAMA WA TAIFA.
 
Na atakuwa rais wa kwanza kuwa mzalendo wa kweli kuwahi kutokea, walopita wote walikuwa wazalendo wa kisiasa kwa ajili ya makundi yao na vyama vyao,na haijawahi kutokea mzalendo halisi wa nchi na wananchi kwa ujumla.

Bila ya katiba mpya nchi itaendelea kuendeshwa kibinafsi na makundi ya watu wanaojiita vyama, hao ndio wataitawala nchi na kuwatawala waafrika wenzao bila ya kujielewa nini wanafanya.
 
Tatizo ni mfumo lakini mama ni muelewa sana.
Huo mfumo upo juu ya mamlaka ya Rais hapana ukweli tatizo ni CCM...
IMG_20210512_083317.jpg
 
Naunga mkono hoja ,ni swala la SSH kua mbunifu na kufanya yale wananchi wengi wameonekana kuyapigia kelele miaka mingi, ikiwa ni pamoja na tume huru ya uchaguzi na Katiba mpya.

Mpaka Sasa SSH ni rais na ni cheo ambacho akijifutika katika Maisha yake Cha msingi kwake ni kuangalia nini alifanyie taifa katika Kipindi chake hata Kama kesho hayupo madarakani ila taifa limkumbuke Kama MAMA WA TAIFA,cheo kikubwa ichi kuliko hata Urais wenyewe, mama akomae kwelikweli cheo husika akiji hivihivi, japo njia ya kukipata ni nyeupe
 
Tulibahatika kumpata Mwalimu Nyerere. Alikuwa ni Rais mwenye maono. Alifahamu kunahitajika nini ili nchi yetu isonge mbele.

Tukumbuke aliipokea nchi ikiwa na wasomi wachache, teknolojia duni kabisa, yenye miundombinu hafifu, elimu dhaifu, viwanda vichache sana, hakuna taasisi za utafiti, n.k. Aliondoka madarakani kukiwa na shule nyingi japo siyo za kutosha, mahospitali, reli, barabara, ndege, viwanda, vituo vya utafiti, n.k.

Kubwa kuliko vyote, aliwaacha Watanzania wakiwa wamoja. Wanaopingana kwa hoja na siyo kwa makabila yao, maeneo yao au dini zao.

Kwa kuzingatia hayo, tukampa cheo kikubwa kabisa cha BABA WA TAIFA.

Bila kutarajia, tumempata Rais Mama. Kaichukua nchi ikiwa kwenye dimbwi la uonevu, udhulumaji, uabuduji wa watu, ubambikiaji kesi, utekwaji wa watu, upotezwaji wa watu, ubaguzi kwa misingi ya vyama, ubambikiwaji wa kodi, na maonevu mengine mengi. Rais mwanamama, kwa yote hayo, amesema hapana. Tunachomwomba kwa sasa, asiishie tu kuyakataa na kuyazuia maovu hayo, bali aitengeneze Tanzania kwa kaisi ambacho uovu huo hautatokea tena.

Ili kuyazuia maovu hayo ya watawala dhidi ya watawaliwa, ni lazima TUPATE KATIBA MPYA INAYOJALI MASLAHI YA TAIFA KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE. Kama Rais Samia atawaletea Watanzania KATIBA inayoangalia zaidi maslahi ya Taifa na ya watu wake wote kwa usawa, katiba inayolinda haki na mamlaka ya wananchi, basi napendekeza apewe hadhi ya kuwa MAMA WA TAIFA.

E0NhMwdXIAAW0HL.jpeg
 
Tulibahatika kumpata Mwalimu Nyerere. Alikuwa ni Rais mwenye maono. Alifahamu kunahitajika nini ili nchi yetu isonge mbele.

Tukumbuke aliipokea nchi ikiwa na wasomi wachache, teknolojia duni kabisa, yenye miundombinu hafifu, elimu dhaifu, viwanda vichache sana, hakuna taasisi za utafiti, n.k. Aliondoka madarakani kukiwa na shule nyingi japo siyo za kutosha, mahospitali, reli, barabara, ndege, viwanda, vituo vya utafiti, n.k.

Kubwa kuliko vyote, aliwaacha Watanzania wakiwa wamoja. Wanaopingana kwa hoja na siyo kwa makabila yao, maeneo yao au dini zao.

Kwa kuzingatia hayo, tukampa cheo kikubwa kabisa cha BABA WA TAIFA.

Bila kutarajia, tumempata Rais Mama. Kaichukua nchi ikiwa kwenye dimbwi la uonevu, udhulumaji, uabuduji wa watu, ubambikiaji kesi, utekwaji wa watu, upotezwaji wa watu, ubaguzi kwa misingi ya vyama, ubambikiwaji wa kodi, na maonevu mengine mengi. Rais mwanamama, kwa yote hayo, amesema hapana. Tunachomwomba kwa sasa, asiishie tu kuyakataa na kuyazuia maovu hayo, bali aitengeneze Tanzania kwa kaisi ambacho uovu huo hautatokea tena.

Ili kuyazuia maovu hayo ya watawala dhidi ya watawaliwa, ni lazima TUPATE KATIBA MPYA INAYOJALI MASLAHI YA TAIFA KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE. Kama Rais Samia atawaletea Watanzania KATIBA inayoangalia zaidi maslahi ya Taifa na ya watu wake wote kwa usawa, katiba inayolinda haki na mamlaka ya wananchi, basi napendekeza apewe hadhi ya kuwa MAMA WA TAIFA.
Naunga mkono hoja. Akiwezesha upatikanaji wa katiba mpya ya wananchi awe mama wa taifa, na ile ng'ombe iliyokufa kwa covid ikachimbiwa kanda ya ziwa ikumbukwe kama ng'ombe ya taifa
 
Katiba Mpya ndio kipimo cha juu kabisa cha uzalendo wa viongozi wa CCM kwa taifa na wananchi wanaowaongoza, kwasababu hilo ndio hitaji la kila mtanzania mpenda maendeleo kwa sasa.
 
Back
Top Bottom