Rais Samia akitupatia Katiba Mpya, awe Mama wa Taifa

Rais Samia akitupatia Katiba Mpya, awe Mama wa Taifa

Naunga mkono hoja. Akiwezesha upatikanaji wa katiba mpya ya wananchi awe mama wa taifa, na ile ng'ombe iliyokufa kwa covid ikachimbiwa kanda ya ziwa ikumbukwe kama ng'ombe ya taifa
Kawapatia chanjo ya corona mbona hamchanji?
Kila kibwengo analake la kujitetea.
Luku imemshida iweje katiba?
 
Uko sahihi nilimaanisha hicho lakini wewe umelenga.
Mimi naamini kwamba kwa katiba hii na mamlaka ya Raisi chini ya katiba hii akiamua kuleta mabadiliko ya kweli hakuna mtu wa kuuzuia! Tuendelee kumuombea Mhe. Raisi Mama Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA mungu azidi kumpa hekima, busara na maono ya kulitendea mema taifa lake. Mungu azidi kumpa mawazo ya kulitumikia taifa lake mambo muhimu kuliko kufikiria maslahi ya chama chake cha kisiasa, dini yake au sehemu anakotoka.

Naomba nimkumbushe Mama SASHA kuwa amekabithiwa jukumu kubwa sana la kuongoza taifa kama kiongozi wa juu kabisa, Raisi JMT. Ni bahati kubwa sana na ni watu wachache sana katika nchi yeyote duniani wanaobahatika kufika hatua hii, hivyo ni jukumu lake binafsi kutengeneza legacy yake kwa ajili ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.

Wahenga walisema kizuri cha jiuza kibaya cha jitembeza! Mhe Raisi Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA anajiuza mwenyewe kwa jinsi anavyoliongoza taifa letu la Tanzania [emoji1241] kwa sasa. Wananchi tulio wengi tumejawa na matumaini makubwa sana kutokana na uongozi wake japo ni muda mfupi tangu akabithiwe kijiti cha kuliongoza taifa. Mhe Raisi Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA amepokewa kwa furaha na wananchi wengi kwa sababu anaonekana kwa matamshi mwenyewe kama kiongozi anayependa HAKI kwa wote, ni kiongozi anayeonekana kuelewa kwa dhati kabisa kuwa hii ni nchi yetu wote bila kujari dini zetu, vyama vyetu vya kisiasa, makabila yetu, nasaba zetu au jinsia. Ni kiongozi anayetupa matumaini kwa wananchi wake wote kwa maono yangu!

Angalizo kwa Mhe Raisi Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA. Naomba akasome kitabu cha Hayati Raisi mstaafu Benjamin W. Mkapa. Katika kitabu chake maarufu cha " My Life, My Purpose kuna sehemu anaongelea kuhusu wanasiasa wa kitanzania kwa ujumla. Anasema alikuja kugundua kuwa nchi hii ina wanasiasa wakweli wachache sana wanaoingia kwenye siasa kwa lengo la kusaidia wananchi wetu masikini. Na hii ni kwa vyama vyote, walioko chama tawala na vyama vya upinzani. Kuhusu walioko chama tawala alidokeza kuwa walio wengi wanakuja including maprofesa na madaktari kutoka vyuo vikuu kwa tamaa ya kuja kupata ubunge na baadae uwaziri na benefits kibao zinazoambatana na mafao ya kibunge. Kwa wafanyabiashara alisema, kundi hili uingia kwenye siasa kwa lengo kuu la kulinda biashara zao maana kwa kuwa mbunge tu ni rahisi kukutana na kiongozi yoyote wa serikali na hii ni faida ya biashara zake, kupata passport zenye hadhi ya kibalozi ili kurahisisha kusafiri nje ya nchi katika shughuli zao! Kwahiyo Mhe Raisi tunaomba atambue kuwa mtu kuvaa tu shati la kijani na kujionesha kuwa yeye ni kada wa "CCM" kindakindaki haimpi mtu sifa ya kuwa mzalendo wa kweli wa nchi hii. Baadhi au niseme walio wengi utafuta hifadhi na manufaa kwani wanajua chama tawala ndio kila kitu! Mhe. Raisi Samia, mwenyezi Mungu amekuinua miongoni mwa watanzania zaidi ya milioni 55 ili utuongoze sisi watz wenzako, tunaomba HAKI na USAWA mbele ya katiba, sheria, taratibu, kanuni na tamaduni zetu ndio viwe njia pekee ya kuliongoza taifa letu. Kwa kumalizia, sisi wananchi wako tunaloweza kufanya kila siku ni kukuombea kwa mwenyezi Mungu akupe afya njema, nguvu na utimamu wa akili ili uweze kuliongoza taifa letu kwa upendo na kwa mafanikio makubwa.
 
Tulibahatika kumpata Mwalimu Nyerere. Alikuwa ni Rais mwenye maono. Alifahamu kunahitajika nini ili nchi yetu isonge mbele.

Tukumbuke aliipokea nchi ikiwa na wasomi wachache, teknolojia duni kabisa, yenye miundombinu hafifu, elimu dhaifu, viwanda vichache sana, hakuna taasisi za utafiti, n.k. Aliondoka madarakani kukiwa na shule nyingi japo siyo za kutosha, mahospitali, reli, barabara, ndege, viwanda, vituo vya utafiti, n.k.

Kubwa kuliko vyote, aliwaacha Watanzania wakiwa wamoja. Wanaopingana kwa hoja na siyo kwa makabila yao, maeneo yao au dini zao.

Kwa kuzingatia hayo, tukampa cheo kikubwa kabisa cha BABA WA TAIFA.

Bila kutarajia, tumempata Rais Mama. Kaichukua nchi ikiwa kwenye dimbwi la uonevu, udhulumaji, uabuduji wa watu, ubambikiaji kesi, utekwaji wa watu, upotezwaji wa watu, ubaguzi kwa misingi ya vyama, ubambikiwaji wa kodi, na maonevu mengine mengi. Rais mwanamama, kwa yote hayo, amesema hapana. Tunachomwomba kwa sasa, asiishie tu kuyakataa na kuyazuia maovu hayo, bali aitengeneze Tanzania kwa kaisi ambacho uovu huo hautatokea tena.

Ili kuyazuia maovu hayo ya watawala dhidi ya watawaliwa, ni lazima TUPATE KATIBA MPYA INAYOJALI MASLAHI YA TAIFA KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE. Kama Rais Samia atawaletea Watanzania KATIBA inayoangalia zaidi maslahi ya Taifa na ya watu wake wote kwa usawa, katiba inayolinda haki na mamlaka ya wananchi, basi napendekeza apewe hadhi ya kuwa MAMA WA TAIFA.
Kwa akili za Wabongo katiba mpya itabakia kuwa on ‘wishlist’
 
Tulibahatika kumpata Mwalimu Nyerere. Alikuwa ni Rais mwenye maono. Alifahamu kunahitajika nini ili nchi yetu isonge mbele.

Tukumbuke aliipokea nchi ikiwa na wasomi wachache, teknolojia duni kabisa, yenye miundombinu hafifu, elimu dhaifu, viwanda vichache sana, hakuna taasisi za utafiti, n.k. Aliondoka madarakani kukiwa na shule nyingi japo siyo za kutosha, mahospitali, reli, barabara, ndege, viwanda, vituo vya utafiti, n.k.

Kubwa kuliko vyote, aliwaacha Watanzania wakiwa wamoja. Wanaopingana kwa hoja na siyo kwa makabila yao, maeneo yao au dini zao.

Kwa kuzingatia hayo, tukampa cheo kikubwa kabisa cha BABA WA TAIFA.

Bila kutarajia, tumempata Rais Mama. Kaichukua nchi ikiwa kwenye dimbwi la uonevu, udhulumaji, uabuduji wa watu, ubambikiaji kesi, utekwaji wa watu, upotezwaji wa watu, ubaguzi kwa misingi ya vyama, ubambikiwaji wa kodi, na maonevu mengine mengi. Rais mwanamama, kwa yote hayo, amesema hapana. Tunachomwomba kwa sasa, asiishie tu kuyakataa na kuyazuia maovu hayo, bali aitengeneze Tanzania kwa kaisi ambacho uovu huo hautatokea tena.

Ili kuyazuia maovu hayo ya watawala dhidi ya watawaliwa, ni lazima TUPATE KATIBA MPYA INAYOJALI MASLAHI YA TAIFA KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE. Kama Rais Samia atawaletea Watanzania KATIBA inayoangalia zaidi maslahi ya Taifa na ya watu wake wote kwa usawa, katiba inayolinda haki na mamlaka ya wananchi, basi napendekeza apewe hadhi ya kuwa MAMA WA TAIFA.
Kuna umuhimu mkubwa sasa wa kuibadili katiba, ili tusijepata kiongozi mvunja Katiba kama Mwendazake.
Adhabu za kuvunja katiba ziwepo na ziwe dhahiri.
 
Kwa akili za Wabongo katiba mpya itabakia kuwa on ‘wishlist’
Wow "a wishlist" and everything else shall remain on our wish list too; haki za binadamu - a wish, demokrasia - a wish, uhuru wa kutoa maoni - a wish.
 
Wow "a wishlist" and everything else shall remain on our wish list too; haki za binadamu - a wish, demokrasia - a wish, uhuru wa kutoa maoni - a wish.
Nchi itakua na utulivu zaidi ikiendelea kuwa hivi
 
Nchi yetu ss, wenye uzalendo wa kuweza kuingia hata msituni kuitetea na kuilinda. Siyo keybord worriers waoga zaid ya kuku wanaotaka katiba inayoruhusu ushoga coZ wanapenda sana kuli.......a😂😂 na Amsterdam
 
Mimi naamini kwamba kwa katiba hii na mamlaka ya Raisi chini ya katiba hii akiamua kuleta mabadiliko ya kweli hakuna mtu wa kuuzuia! Tuendelee kumuombea Mhe. Raisi Mama Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA mungu azidi kumpa hekima, busara na maono ya kulitendea mema taifa lake. Mungu azidi kumpa mawazo ya kulitumikia taifa lake mambo muhimu kuliko kufikiria maslahi ya chama chake cha kisiasa, dini yake au sehemu anakotoka.

Naomba nimkumbushe Mama SASHA kuwa amekabithiwa jukumu kubwa sana la kuongoza taifa kama kiongozi wa juu kabisa, Raisi JMT. Ni bahati kubwa sana na ni watu wachache sana katika nchi yeyote duniani wanaobahatika kufika hatua hii, hivyo ni jukumu lake binafsi kutengeneza legacy yake kwa ajili ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.

Wahenga walisema kizuri cha jiuza kibaya cha jitembeza! Mhe Raisi Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA anajiuza mwenyewe kwa jinsi anavyoliongoza taifa letu la Tanzania [emoji1241] kwa sasa. Wananchi tulio wengi tumejawa na matumaini makubwa sana kutokana na uongozi wake japo ni muda mfupi tangu akabithiwe kijiti cha kuliongoza taifa. Mhe Raisi Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA amepokewa kwa furaha na wananchi wengi kwa sababu anaonekana kwa matamshi mwenyewe kama kiongozi anayependa HAKI kwa wote, ni kiongozi anayeonekana kuelewa kwa dhati kabisa kuwa hii ni nchi yetu wote bila kujari dini zetu, vyama vyetu vya kisiasa, makabila yetu, nasaba zetu au jinsia. Ni kiongozi anayetupa matumaini kwa wananchi wake wote kwa maono yangu!

Angalizo kwa Mhe Raisi Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA. Naomba akasome kitabu cha Hayati Raisi mstaafu Benjamin W. Mkapa. Katika kitabu chake hicho kuna sehemu anaongelea kuhusu wanasiasa wa kitanzania kwa ujumla. Anasema alikuja kugundua kuwa nchi hii ina wanasiasa wakweli wachache sana wanaoingia kwenye siasa kwa lengo la kusaidia wananchi wetu masikini. Na hii ni kwa vyama vyote, walioko chama tawala na vyama vya upinzani. Kuhusu walioko chama tawala alidokeza kuwa walio wengi wanakuja hadi maprofesa kutoka vyuo vikuu kwa tamaa ya kuja kupata ubunge na baadae uwaziri na benefits kibao zinazoambatana mafao ya kibunge. Kwa wafanyabiashara alisema, kundi hili uingia kwenye siasa kwa lengo kubwa la kulinda biashara zao maana kwa kuwa mbunge tu ni rahisi kukutana na kiongozi yoyote wa serikali na hii ni faida ya biashara zake, kupata passport zenye hadhi ya kibalozi ili kurahisisha kusafiri nje ya nchi katika shughuli zao! Kwahiyo Mhe Raisi tunaomba atambue kuwa mtu kuvaa tu shati la kijani na kujionesha kuwa yeye ni kada wa "CCM" kindakindaki haimpi mtu sifa ya kuwa mzalendo wa kweli wa nchi hii. Baadhi au niseme walio wengi utafuta hifadhi na manufaa kwani wanajua chama tawala ndio kila kitu!
Umenena vema.

Rais Mama Samia, aitazame Tanzania, awatazame Watanzania, wanaoishi leo na watakaoishi miaka 100 ijayo, ambao hawana sauti ya kumpamba kwa sifa kemu kemu leo.

Kwa akili aliyozaliwa nayo, na hekima aliyojaliwa na atakayojaliwa na Mungu, auone unafiki wa viongozi wanaomzunguka. Ajiulize, katika hao viongozi alio nao, ni nani aliye mzalendo wa kweli?

Je, ni Mwigulu, aliyepinga kuwa TRA haionei wafanyabiashara pale Nape alipoomba ukusanyaji wa kodi ufanywe kwa weledi, lakini leo akiwa kwenye utawala wa Mama Samia, anasema, TRA inatakiwa kubadilika?

Je, ni Ndugai aliyewapinga wabunge wa upinzani bungeni kwa vile tu walisema mikopo ya wanavyuo itolewe mpaka vyuo vya chini, halafu leo yeye anatoa kauli hiyo hiyo, akijifanya ni wazo jipya?

Je, ni Majaliwa, chini ya utawala uliopita, hakuwahi kutoa neno hata moja wakati mwanahabari Azori Gwanda akipotezwa, lakini leo anasema, ole wake atakayewanyanyasa wana habari?

Katika hawa viongozi tulio nao sasa, sijamwona mzalendo hata mmoja. Kiongozi anayesimama katika anachokiamini, anayetembea juu ya maneno yake, ambaye yupo tayari hata kupoteza cheo na fedha kwaajili ya kusimamia anachoamini ni sahihi.

Je, ni Biteko, aliyeisimamia sekta ya madini na kusababisha wawekezaji wote kuondoka Tanzania, na kufurahia kuwa mabeberu wameondoka, halafu leo akitamka kuwa anataka wawekezaji?

Kwa kiasi fulani, viongozi wachache sana wa upinzani, angalao wana misimamo katika yale wanayoamini. Maana wana uwezo wa kuamka na kusema, nimeamua kujiunga na CCM, na kesho yake wakapata cheo, lakini hawajafanya hivyo, lakini ni wachache sana.
 
Katiba Mpya ndio kipimo cha juu kabisa cha uzalendo wa viongozi wa CCM kwa taifa na wananchi wanaowaongoza, kwasababu hilo ndio hitaji la kila mtanzania mpenda maendeleo kwa sasa.
Tusiitegemee CCM, tumtegemee Samia. Kwa mfumo wetu wa utawala uliopo sasa, Rais akitaka tupate katiba mpya, akitaka mchakato uanze, hata kesho, itakuwa.
 
Dash ! HUO Muujiza wa Katiba Mpya Ni Kitu muhimu Sana katika utawala huu wa mama SAMIA.Huyu mama uwezo wa kutuletea Katiba Mpya Anao.Uzuri Ni kwamba Yeye mwenyewe ndiye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa bunge la Katiba.Kwa Hiyo anaujua mchakato mzima wa Hiyo Katiba ulivyo.Madam,President Tunaomba Tuletee KATIBA MPYA YA TUME YA WARIOBA.Ile ambayo ilikuwa haijafanyiwa modifications na akina marehemu Samweli Sita.Katiba ya Warioba ndio iliyobeba maslahi mapana ya nchi yetu kwa pande zote mbili za muungano na kwa vyama vyote vya siasa.Maana akileta Ile Katiba ya Samweli Sita ambayo imezingatia zaidi maslahi ya CCM na VIONGOZI wake badala ya maslahi mapana ya Taifa,Katiba ya namna Hiyo inakuwa Haina hata haja ya kuileta.Mama siku zote ametuahidi hii nchi Ni yetu sote,na amesema atatumia chochote au mtanzania yoyote bila kujali itikadi katika kutuletea maendeleo.
 
Kumbuka madam ni mnufaika namba moja wa katiba hii
Labda aitumie kama gogo kutuvusha kwenda upande wa pili
Madam ni mnufaika namba moja wa maandishi yaliyoandikwa mwaka 1977
Huyu naomba mnielewe ni the most beneficiary wa katiba hii mnayotaka aitose
Nadhani nimeeleweke
 
Tulibahatika kumpata Mwalimu Nyerere. Alikuwa ni Rais mwenye maono. Alifahamu kunahitajika nini ili nchi yetu isonge mbele.

Tukumbuke aliipokea nchi ikiwa na wasomi wachache, teknolojia duni kabisa, yenye miundombinu hafifu, elimu dhaifu, viwanda vichache sana, hakuna taasisi za utafiti, n.k. Aliondoka madarakani kukiwa na shule nyingi japo siyo za kutosha, mahospitali, reli, barabara, ndege, viwanda, vituo vya utafiti, n.k.

Kubwa kuliko vyote, aliwaacha Watanzania wakiwa wamoja. Wanaopingana kwa hoja na siyo kwa makabila yao, maeneo yao au dini zao.

Kwa kuzingatia hayo, tukampa cheo kikubwa kabisa cha BABA WA TAIFA.

Bila kutarajia, tumempata Rais Mama. Kaichukua nchi ikiwa kwenye dimbwi la uonevu, udhulumaji, uabuduji wa watu, ubambikiaji kesi, utekwaji wa watu, upotezwaji wa watu, ubaguzi kwa misingi ya vyama, ubambikiwaji wa kodi, na maonevu mengine mengi. Rais mwanamama, kwa yote hayo, amesema hapana. Tunachomwomba kwa sasa, asiishie tu kuyakataa na kuyazuia maovu hayo, bali aitengeneze Tanzania kwa kaisi ambacho uovu huo hautatokea tena.

Ili kuyazuia maovu hayo ya watawala dhidi ya watawaliwa, ni lazima TUPATE KATIBA MPYA INAYOJALI MASLAHI YA TAIFA KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE. Kama Rais Samia atawaletea Watanzania KATIBA inayoangalia zaidi maslahi ya Taifa na ya watu wake wote kwa usawa, katiba inayolinda haki na mamlaka ya wananchi, basi napendekeza apewe hadhi ya kuwa MAMA WA TAIFA.
Katiba mpya hawezi maana ndiyo utakuwa mwisho wa CCM
 
Huyu mama akicheza karata zake vizuri anaweza kuwa kiongozi bora si Tanzania tu bali hata Africa. Kama ataruhusu demokrasia ya kweli pamoja na kuwapatika wananchi katiba yao Mpya aiseee - NAUNGA MKONO HOJA.

Dalili zinaaza kuonekana, wakati wa mwendazake hakuna aliyethubutu hata kusema chochote kuhusu Tanzania daima, Mawio na Mwanahalisi - ila leo yawezekana kabaisa.
 
atupe katiba kwan yeye nani? umeona BBI ilivyopigwa chini huko KE?
 
Tulibahatika kumpata Mwalimu Nyerere. Alikuwa ni Rais mwenye maono. Alifahamu kunahitajika nini ili nchi yetu isonge mbele.

Tukumbuke aliipokea nchi ikiwa na wasomi wachache, teknolojia duni kabisa, yenye miundombinu hafifu, elimu dhaifu, viwanda vichache sana, hakuna taasisi za utafiti, n.k. Aliondoka madarakani kukiwa na shule nyingi japo siyo za kutosha, mahospitali, reli, barabara, ndege, viwanda, vituo vya utafiti, n.k.

Kubwa kuliko vyote, aliwaacha Watanzania wakiwa wamoja. Wanaopingana kwa hoja na siyo kwa makabila yao, maeneo yao au dini zao.

Kwa kuzingatia hayo, tukampa cheo kikubwa kabisa cha BABA WA TAIFA.

Bila kutarajia, tumempata Rais Mama. Kaichukua nchi ikiwa kwenye dimbwi la uonevu, udhulumaji, uabuduji wa watu, ubambikiaji kesi, utekwaji wa watu, upotezwaji wa watu, ubaguzi kwa misingi ya vyama, ubambikiwaji wa kodi, na maonevu mengine mengi. Rais mwanamama, kwa yote hayo, amesema hapana. Tunachomwomba kwa sasa, asiishie tu kuyakataa na kuyazuia maovu hayo, bali aitengeneze Tanzania kwa kaisi ambacho uovu huo hautatokea tena.

Ili kuyazuia maovu hayo ya watawala dhidi ya watawaliwa, ni lazima TUPATE KATIBA MPYA INAYOJALI MASLAHI YA TAIFA KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE. Kama Rais Samia atawaletea Watanzania KATIBA inayoangalia zaidi maslahi ya Taifa na ya watu wake wote kwa usawa, katiba inayolinda haki na mamlaka ya wananchi, basi napendekeza apewe hadhi ya kuwa MAMA WA TAIFA.
Tutamkumbuka daima akituachia katiba mpya ya jaji warioba
 
Back
Top Bottom