Rais Samia aliweka wazi kuhusu ongezeko la mshahara, 23.3% ni kwa kima cha chini tu. Watumishi acheni lawama mara moja

Countrywide

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2015
Posts
20,694
Reaction score
32,527
Baada ya kuzunguka huko na huku hatimaye wamejua ongezeko la mshahara, lawama zimeanza na wengine kuanza kumshambulia Rais. Hii haikubaliki hata kidogo.

Raisi aliweka wazi ongezeko la mshahara kwa 23.3% ni wale wa kima cha chini, Ila kutokujua kusoma na kuelewa kwa watumishi kukafanya ionekane ni kwa watu wote.

Ni kama kuna watu walijiandaa kutoa lawama kwa Rais wetu ikiwa taarifa ilisema wazi kabisa kuwa ni kima cha chini. Hata hivyo tukirudi kwenye uhalisia kwa uchumi ulivyoyumba duniani na Tanzania tukiwemo, unawezaje kuhitaji ongezeko la 23.3%? Kwa kazi gani hasa unazofanya?

Watumishi wengi ni walimu, zaidi ya nusu(300000+) na hawa ndio waliokuwa mstari wa mbele kupotosha ongezeko ili mwisho wa siku ionekane serikali iliongopa. Shida ni nini kwenye hii kada ya ualimu? Ufahamu mdogo?

Narudia tena acheni lawama kwa Rais mara moja, na pia mshukuru hata kwa hiko kidogo mlichopata.
 
Kuongezeka hiyo asilimia, haikwepeki, maisha yako juu sana.
 
Kwani na wewe ni mtumishi au kanjanja mmoja Fulani hivi🤔
 
Usilete taarifa za kichonganishi hapa. Unawatukana walimu kwa kisingizio ambacho hujakithibitisha. Usimchonganishe Rais wetu.
Wewe ni Mwalimu? Wapi nimemchonganisha Rais? Hivi kwanini hamna akili kabisa?
 
Unamaanisha watu wa kima cha chini Kuna mahala wananunua mahitaji tofauti na watu wengine?
 
Unamaanisha watu wa kima cha chini Kuna mahala wananunua mahitaji tofauti na watu wengine?
Swali gani wewe?
Mtu anayepata 300000 kwa mwezi ni sawa na mtu anayepata 800000??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…