Rais Samia ameamua kuwatolea uvivu Jeshi la Polisi na kuyaanika hadharani maovu yao!

Rais Samia ameamua kuwatolea uvivu Jeshi la Polisi na kuyaanika hadharani maovu yao!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kwa kweli Katika hotuba aliyoitoa leo huko kwenye Chuo cha Polisi Moshi, Rais Samia ameamua kuyaweka wazi maovu yanayofanywa na Jeshi hilo la Polisi na hivyo nampongeza Sana Rais wetu kwa ujasiri wake huo.

Kwanza amesisitiza kuwa ni lazima Jeshi la Polisi lizingatie Nidhamu, Haki na Weledi Katika utendaji wao wa Kazi za kila siku.

Ameeleza kuwa Jeshi la Polisi, halina sifa nzuri ndani ya jamii ya Watanzania.

Akisema kuwa Rushwa imekithiri ndani ya Jeshi hilo, akitoa mifano hai kabisa, kama vile askari wa barabarani ambao huwa wanachukua Rushwa waziwazi!

Anaendelea kusisitiza kuwa hata dhamana, ambayo ni Haki ya mtuhumiwa, lakini Jeshi hilo limekuwa "likiwakamua" watuhumiwa, ikiwa ni uthibitisho wa kauli mbiu ya sisi raia, kuwa kuingia kwenye selo za Polisi ni bure, lakini kutoka ni kwa Pesa!

Akakemea pia tabia ya Polisi kuwabambikia Kesi raia, ambapo bila kujali, namna wanavyowatesa hao wanaobambikiwa Kesi.

Pia amekemea tabia za Ufisadi, zilizokithiri ndani ya Jeshi hilo la Polisi, akitoa mfano namna Jeshi hilo linavyofanya "biashara" ya kuuza sare hizo za Polisi kwa Majeshi mengine kama vile kwa Jeshi la zimamoto.

Akaomgeza namna maafisa wa Jeshi hilo, wanavyotumia bajeti ya mafuta ya Jeshi hilo na kuyapeleka kwenye magari yao binafsi!

Nampongeza Sana Rais Samia kwa kuyaanika hadharani maovu hayo ya Jeshi la Polisi, ambapo sisi raia wema, tumekuwa tukiyakemea maovu hayo kwa kipindi kirefu Sana, lakini yamekuwa hayasikilizwi kabisa.
 
Akakemea pia tabia ya Polisi kuwabambikia Kesi raia, ambapo bila kujali, namna wanavyowatesa hao wanaobambikiwa Kesi.
Mama Samia, kwa heshima na taadhima kubwa hapa sikuwezi kukuamini! What about Kingai! The DCI!!!!!!!!!!!!!!!! Hapo unajikosha mbele ya watu uonekane mwema , but in the innermost chamber of your heat conscious, you are not the one!
 
Mama Samia, kwa heshima na taadhima kubwa hapa sikuwezi kukuamini! What about Kingai! The DCI!!!!!!!!!!!!!!!! Hapo unajikosha mbele ya watu uonekane mwema , but in the innermost chamber of your heat conscious, you are not the one!
Lakini at least, ameonyesha kukerwa na tabia za hao maaskari, tofauti na yule wa awamu ya 5 ambaye amekuwa akiwasifu hadharani, kwa makosa hayo ambayo wamekuwa wakiyafanya!
 
Kuyaanika NI jambo la kawaida kwani sote tunajua ila je hatua gani za kuchukua angesem hata alivunje jeshi kwa muda Kisha vituoni wakae wanajeshi ingekuwa safi
Hapo ndiyo ungeona jeshi ni jeshi,kama usingesikia malalamiko mengine,basi siyo nchi hii.
 
Hili ni kumpigia mbuzi gitaa.

Tabia ya jeshi la polisi huwezi kuibadili. Wamesha zowea rushwa, kubambika kesi na wizi.

Juzi tuu Mh. Kinana kaongea kuhusu trafiki kujazana mijini, wakaacha wiki moja, hivi sasa Arusha ngoma imerudi kama mwanzo. Kila mita mia trafiki.
 
Police sina ham nao kabisa niliwaachia mtuhumiwa ambaye aliiba simu kisa tu wanatengeneza mazingira ya pesa wakati kwenda kumkamata enyewe niliwapa elf 20 simu ya laki mbili na wanataka kula hela zaidi ya bei ya simu kiukweli niliumia lakini niliwaachia mahabusu wao hata sijui walimfanyaje.
 
Police sina ham nao kabisa niliwaachia mtuhumiwa ambaye aliiba simu kisa tu wanatengeneza mazingira ya pesa wakati kwenda kumkamata enyewe niliwapa elf 20 simu ya laki mbili na wanataka kula hela zaidi ya bei ya simu kiukweli niliumia lakini niliwaachia mahabusu wao hata sijui walimfanyaje.
Sasa ndiyo wa kuwaamini kweli watu wa aina hiyo?

Polisi ni kioo cha jamii, kwa hiyo ni lazima wafanye Kazi yao kwa Weledi mkubwa
 
Hizi tabia mbovu za polisi ndio maana huwa haziishi, kwasababu hayo maneno aliyotoa Rais ni ya kisiasa tu, japo ukitazama kwa makini unaweza dhani anamaanisha alichokiongea.

Mfano, kati ya aliyoongea kuhusu kubambikia watu kesi, na kuwaonea raia, haya yametokea wakati wa utawala wake, na mojawapo wa wahusika ni Kingai, amempandisha cheo na kumfanya awe DCI, sasa nitayaamini vipi maneno ya Rais?!

Ukiondoa kesi za raia wa kawaida, naamini zile za wanasiasa polisi huwa wanafanya ukatili kwa kupokea maelekezo ya siri toka kwa hawa wanasiasa, Samia akiwa mmojawao, japo akitoka kwenye public kama hivi, ndio anatudanganya kwa kuyakemea.
 
Back
Top Bottom