Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mama Samia Ameiheshimisha Sana CCM Mitaani, CCM kinaonekana ni chama Cha Amani, maridhiano, haki, kizalendo na kinachopigania maslahi ya Taifa na ustawi wa Watanzania, mwana CCM ukiwa katikati ya kundi na kuzungumza unasikilizwa kwa umakini Sana.
Wanyonge wanaona CCM ndio sauti yao, nguvu yao, mtetezi wao na mkombozi wao, wanaona ofisi za CCM mahali pa matumaini, wanawaona viongozi wa CCM kama kimbilio lao pale wanapokuwa wamenyimwa haki mahali au kuonewa au kunyanyaswa au kutokusikilizwa au kucheleweshwa kupewa huduma au Haki.
Watu wanaiheshimu na kuipenda Sana CCM na Wana CCM kwa Sasa, Mama yetu mpendwa mama Samia anatajwa na kuzungumzwa Mara nyingi zaidi kuliko mtu yeyote yule hapa Tanzania huku wengi wakimpongeza kwa uchapa kazi wake na uzalendo wake uliojaa katika kifua chake.
Ni CCM tu kwa sasa ndio chama kinachoendelea kuiteka na kuiridhisha mioyo ya Watanzania kiutendaji,Ni CCM pekee ndio chama chenye kuonyesha kuzijuwa shida na kero za watanzania, ni CCM pekee iliyoonyesha kuwa karibu na wananchi, kuwahudumia, kuwatumikia, kuwasikiliza na kuwapokea wenye kuhitaji msaada wakati wote kwa unyenyekevu na ukarimu mkubwa sana.
Watanzania wanatambua kuwa CCM ni chama pekee chenye uchungu na maisha yao na taifa lao, wanatambua kuwa ni CCM pekee na viongozi wake wenye uchungu na Rasilimali za Taifa letu na wenye kutaka kuona kila mtanzania ananufaika kupitia utajiri huu tuliyopewa na Mwenyezi MUNGU.
Hakika siasa ni sayansi na Rais Samia ni mwana sayansi na nguli wa sayansi ya siasa kivitendo, ni mama Hodari na komandoo wa kisiasa, Jasusi wa kisiasa na mwenye medari ya Dhahabu katika siasa, ndio sababu ya kupendwa na kuheshimika na watanzania wa makundi yote, ndio sababu ya kupata uungwaji mkono wa watanzania, ndio sababu ya kutamalaki kwa utulivu na Amani hapa nchini, nani Kama Rais Samia?
Nani wa kushindana na Rais Samia? Nani na mpinzani yupi mwenye ubavu wa kushindana na Rais Samia?Rais Samia Ni Mwamba wa Medani za kisiasa, jabari wa siasa, ngome imara Katika Siasa za ushawishi, hoja na maridhiano.
Kwa ulimi wake Ameliunganisha Taifa,kwa ulimi wake Taifa linazungumza lugha moja, kwa ulimi wake upinzani nao unaishabikia na kuiunga mkono CCM, kwa ulimi wake wawekezaji na watalii wanamiminika kwa kupishana angani kama mwewe kuwahi nafasi Tanzania.
Kwa ulimi wake Tanzania imefungua milango yote iliyokuwa imefungwa kiuwekezaji na kiujirani, kwa ulimi wake Tanzania inasifika na kutajwa kila pembe ya Dunia, kwa ulimi wake na ushawishi wake picha zake zinapepea kwenye viwanja vya michezo kama bendera ya Uhuru katika kilele cha mlima Kilimanjaro.
Samia Ameziteka akili za watanzania kwa uchapa kazi wake,Rais Samia Ni komandoo aliyepenya katika midomo na mioyo ya watanzania wa vyama vyote, rika zote na makundi yote pamoja na wageni wa mataifa mbalimbali kijasusi na kihodari.
Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu. 0742-676627
Mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mama Samia Ameiheshimisha Sana CCM Mitaani, CCM kinaonekana ni chama Cha Amani, maridhiano, haki, kizalendo na kinachopigania maslahi ya Taifa na ustawi wa Watanzania, mwana CCM ukiwa katikati ya kundi na kuzungumza unasikilizwa kwa umakini Sana.
Wanyonge wanaona CCM ndio sauti yao, nguvu yao, mtetezi wao na mkombozi wao, wanaona ofisi za CCM mahali pa matumaini, wanawaona viongozi wa CCM kama kimbilio lao pale wanapokuwa wamenyimwa haki mahali au kuonewa au kunyanyaswa au kutokusikilizwa au kucheleweshwa kupewa huduma au Haki.
Watu wanaiheshimu na kuipenda Sana CCM na Wana CCM kwa Sasa, Mama yetu mpendwa mama Samia anatajwa na kuzungumzwa Mara nyingi zaidi kuliko mtu yeyote yule hapa Tanzania huku wengi wakimpongeza kwa uchapa kazi wake na uzalendo wake uliojaa katika kifua chake.
Ni CCM tu kwa sasa ndio chama kinachoendelea kuiteka na kuiridhisha mioyo ya Watanzania kiutendaji,Ni CCM pekee ndio chama chenye kuonyesha kuzijuwa shida na kero za watanzania, ni CCM pekee iliyoonyesha kuwa karibu na wananchi, kuwahudumia, kuwatumikia, kuwasikiliza na kuwapokea wenye kuhitaji msaada wakati wote kwa unyenyekevu na ukarimu mkubwa sana.
Watanzania wanatambua kuwa CCM ni chama pekee chenye uchungu na maisha yao na taifa lao, wanatambua kuwa ni CCM pekee na viongozi wake wenye uchungu na Rasilimali za Taifa letu na wenye kutaka kuona kila mtanzania ananufaika kupitia utajiri huu tuliyopewa na Mwenyezi MUNGU.
Hakika siasa ni sayansi na Rais Samia ni mwana sayansi na nguli wa sayansi ya siasa kivitendo, ni mama Hodari na komandoo wa kisiasa, Jasusi wa kisiasa na mwenye medari ya Dhahabu katika siasa, ndio sababu ya kupendwa na kuheshimika na watanzania wa makundi yote, ndio sababu ya kupata uungwaji mkono wa watanzania, ndio sababu ya kutamalaki kwa utulivu na Amani hapa nchini, nani Kama Rais Samia?
Nani wa kushindana na Rais Samia? Nani na mpinzani yupi mwenye ubavu wa kushindana na Rais Samia?Rais Samia Ni Mwamba wa Medani za kisiasa, jabari wa siasa, ngome imara Katika Siasa za ushawishi, hoja na maridhiano.
Kwa ulimi wake Ameliunganisha Taifa,kwa ulimi wake Taifa linazungumza lugha moja, kwa ulimi wake upinzani nao unaishabikia na kuiunga mkono CCM, kwa ulimi wake wawekezaji na watalii wanamiminika kwa kupishana angani kama mwewe kuwahi nafasi Tanzania.
Kwa ulimi wake Tanzania imefungua milango yote iliyokuwa imefungwa kiuwekezaji na kiujirani, kwa ulimi wake Tanzania inasifika na kutajwa kila pembe ya Dunia, kwa ulimi wake na ushawishi wake picha zake zinapepea kwenye viwanja vya michezo kama bendera ya Uhuru katika kilele cha mlima Kilimanjaro.
Samia Ameziteka akili za watanzania kwa uchapa kazi wake,Rais Samia Ni komandoo aliyepenya katika midomo na mioyo ya watanzania wa vyama vyote, rika zote na makundi yote pamoja na wageni wa mataifa mbalimbali kijasusi na kihodari.
Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu. 0742-676627