Rais Samia anaonyesha rangi yake halisi kwa viongozi wazembe

Rais Samia anaonyesha rangi yake halisi kwa viongozi wazembe

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Hotuba iliyotolewa na Mh. Rais wakati wa kuwaapisha viongozi mapema siku ya jana ni muendelezo wa kasi yake katika kuhimiza utendaji wenye tija kwa watumishi wa umma. Baadhi ya mambo yanayohimizwa na Mh. Rais ni pamoja na ;

1. Utendaji wenye tija kwa watumishi wote wa umma katika Wizara, Taasisi na Mashirika yote. Uwepo wa tathimini na ukaguzi utasaidia kuepusha ubadhirifu na kuchochea ufanisi katika utendaji. Uongozi wa Rais Samia unakwenda kuweka ALAMA ya kudumu.

2. Usimamizi wa sheria na utawala bora - Suala hili muhimu linaendelea kupewa kipaumbele ambapo watumishi wa umma wazembe wanachukuliwa hatua kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuwasimamisha kazi au kuondolewa katika nyadhifa husika.

3. Uwazi na uwajibikaji katika wizara, Taasisi na Halmashauri - Serikali ya awamu ya sita inaendelea kuongeza uwezo wa kiutendaji wa Mamlaka zinazochunguza na kufanya ufuatiliaji wa mapato na matumizi katika Halmashauri, Taasisi na Mashirika ya umma ili kuhakikisha adhma ya uwazi na uwajibikaji inawekwa katika vitendo.

4. Uongozi thabiti na nia ya dhati katika kuwaletea wananchi maendeleo jumuishi - Maagizo yanayoendelea kutolewa na Rais tayari yameanza kutekelezwa na yanakwenda kuhuisha uchapakazi wa viongozi kwa ngazi zote, na tayari ripoti zinaonyesha kupungua kwa hati chafu katika maeneo mengi.

5. Kuhamasisha ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri zote. Wataalam wanasema usipojua unapokwenda tayari umefika mwisho, kitendo cha Mh.Rais kuhimiza umuhimu wa kuwa na malengo katika ukusanyaji ni maono ya kuhamasisha watendaji kufanya kazi kwa weledi zaidi.

6. Kuhamasisha ukamilishaji wa miradi kwa wakati. Halmashauri zilizokuwa na mazoea ya kuchelewa kukamilisha miradi kwa wakati sasa zimefikiwa. Hii inakwenda kuchochea maendeleo sawa sawa na maono ya Mh. Rais Samia. Watanzania tumepata bahati ya kuwa na uongozi imara unaojali suala la uwazi na uwajibikaji kwa vitendo. Shime tuendelee kumuunga mkono Rais Samia kwa uongozi wake imara na wenye tija.
 
Wanaobainika kuiba mamilioni na hata mabilioni ya pesa wanafanywa nini? Tuanzie hapo kwanza.

Atabembeleza na kusihi sana tena kwa sauti tamu inayoweza kumtoa nyoka pangoni lakini kama mifumo ni ile ile na hakuna uwajibishwaji wo wote hakuna kitakachobadilika. Majamaa yataendelea kula kulingana na urefu wa kamba za menyewe tu...na kuzidi!
 
Ngoja tuendelee kusoma labda tutakuelewa hapo badae!
IMG-20220729-WA0000.jpg
 
Hotuba iliyotolewa na Mh. Rais wakati wa kuwaapisha viongozi mapema siku ya jana ni muendelezo wa kasi yake katika kuhimiza utendaji wenye tija kwa watumishi wa umma. Baadhi ya mambo yanayohimizwa na Mh. Rais ni pamoja na ;

1. Utendaji wenye tija kwa watumishi wote wa umma katika Wizara, Taasisi na Mashirika yote. Uwepo wa tathimini na ukaguzi utasaidia kuepusha ubadhirifu na kuchochea ufanisi katika utendaji. Uongozi wa Rais Samia unakwenda kuweka ALAMA ya kudumu.

2. Usimamizi wa sheria na utawala bora - Suala hili muhimu linaendelea kupewa kipaumbele ambapo watumishi wa umma wazembe wanachukuliwa hatua kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuwasimamisha kazi au kuondolewa katika nyadhifa husika.

3. Uwazi na uwajibikaji katika wizara, Taasisi na Halmashauri - Serikali ya awamu ya sita inaendelea kuongeza uwezo wa kiutendaji wa Mamlaka zinazochunguza na kufanya ufuatiliaji wa mapato na matumizi katika Halmashauri, Taasisi na Mashirika ya umma ili kuhakikisha adhma ya uwazi na uwajibikaji inawekwa katika vitendo.


4. Uongozi thabiti na nia ya dhati katika kuwaletea wananchi maendeleo jumuishi - Maagizo yanayoendelea kutolewa na Rais tayari yameanza kutekelezwa na yanakwenda kuhuisha uchapakazi wa viongozi kwa ngazi zote, na tayari ripoti zinaonyesha kupungua kwa hati chafu katika maeneo mengi.

5. Kuhamasisha ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri zote. Wataalam wanasema usipojua unapokwenda tayari umefika mwisho, kitendo cha Mh.Rais kuhimiza umuhimu wa kuwa na malengo katika ukusanyaji ni maono ya kuhamasisha watendaji kufanya kazi kwa weledi zaidi.

6. Kuhamasisha ukamilishaji wa miradi kwa wakati. Halmashauri zilizokuwa na mazoea ya kuchelewa kukamilisha miradi kwa wakati sasa zimefikiwa. Hii inakwenda kuchochea maendeleo sawa sawa na maono ya Mh. Rais Samia. Watanzania tumepata bahati ya kuwa na uongozi imara unaojali suala la uwazi na uwajibikaji kwa vitendo. Shime tuendelee kumuunga mkono Rais Samia kwa uongozi wake imara na wenye tija.
Umeelezea vizuri ,na wanachi tumekuelewa.
 
Wanaobainika kuiba mamilioni na hata mabilioni ya pesa wanafanywa nini? Tuanzie hapo kwanza.

Atabembeleza na kusihi sana tena kwa sauti tamu inayoweza kumtoa nyoka pangoni lakini kama mifumo ni ile ile na hakuna uwajibishwaji wo wote hakuna kitakachobadilika. Majamaa yataendelea kula kulingana na urefu wa kamba za menyewe tu...na kuzidi!
kwani haujaona watu wanaachishwa kazi kupisha uchunguzi na lazima watawajibishwa Rais Samia hana mchezo sio kama wale uliowazoea
 
Uzuri gharama za maisha haziangalii Chawa wala Kunguni,zinapanda kwa wote labda mtu uwe kwenye mfereji wa asali.

Amateur cheerleaders mtapoteana tu mbele ya safari.
 
Samia mwenyewe akiona hii posto atacheka na kukudharau sana.
Ma mtu kama huyo jamaa yanatuponza sana , yaani Jana yule bashungwa anametudanganya kuwa mapato yamepaa MPAKA 105 asilimia kumbe wameingiza fedha za ujenzi madarasa na vituo vya afya za uviko kama mapato ya ndani ngazi ya kata,
 
Back
Top Bottom