Rais Samia anawaapisha viongozi wateule Ikulu ndogo ya Tunguu-Zanzibar leo Desemba 10, 2024

Rais Samia anawaapisha viongozi wateule Ikulu ndogo ya Tunguu-Zanzibar leo Desemba 10, 2024

Halafu hii imekaaje kumpendekeza mgombea kabla hata uchaguzi haujatangazwa? Je, WHO wakighaili kufanya uchaguzi?

Yani huyu mama anachowaza ni uchaguzi tu. Ndio maana anagawa pikipiki za kampeni SSH 2025; ilihali hata mimi nina mpango wa kuchukua fomu ndani ya chama
Ni kweli wanaweza kusema achukue aliyeshika nafasi ya pili.
 
Janabi atashindwa kura.Eti wanamuandaa akagombee WHO Africa.Hana ile attirance ya watu wampigie kura Ninamuona hayupo Humble.Ila bora wapeleke jina wajue feeling ya kushindwa pia.
Usitangulize Kushindwa
 
Ni kweli wanaweza kusema achukue aliyeshika nafasi ya pili.
Ukizingatia alikuwa ni mteule hata ofisi hajakabidhiwa. Labda tungepata mwongozo kutoka WHO.
Katiba yao inasemaje pale kiongozi wa kuchaguliwa anapofariki kabla ya kuapishwa na kukabidhiwa ofisi.
 
Nilichokiona kwenye zoezi zima
Ni mipasho tuuh nakuambiana mara hivi mara vile kama wanapeana nafasi za uongozi kwenye familia zao lakin uweledi ulikua hamna na sidhani kama teuzi hizi kafanya yeye
FULL STOP.
 
Yaani untumia gharama kujaza viongozi wote wakuu kwa ajili ya hafla fupi tu ya uapisho. Hawa ni watu waliojiweka madarakani na wana uhakika wananchi hawawezi kuwawajibisha. Hawana uchungu hata kidogo na kodi zetu. Wakitoka hapo wanaenda kusaidiwa kujenga matundu ya vyoo na wahisani wakati matundu kibao ya vyoo mashuleni yangepatikana kwenye hafla kama hizi zisizo na tija yeyote
Pesa hazimuumi sababu mshahara wake haukatwi kodi
 
Rais Samiah wa Tanzania amekuwa anatoa kauli za kejeli . Ni kama ana dharau Sana. Kwa mfano aliwahi kutoa kauli ya kwamba katiba ni kijitabu tu. Kwa maana nyingine Katiba so Jambo la maana. Pia amewahi kunukuliwa akidai ya kwamba kifo ni kifo hakuna kifo kibaya zaidi ya kingine. Alisema maneno kama njia ya kuonesha ya kwamba kifo Cha kada wa CHADEMA Ally Kibao sio Jambo zito Sana.

Leo wakati akiapisha mawaziri , Rais amesikika akidai ya kwamba aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Masauni Yusuf ameacha alama. Ni kipindi Cha Waziri Masauni kundi la watu kutekwa na kupotezwa limeshika kasi, mpaka kupelekea wananchi kujihami. Juzi tu hapa mfanyakazi wa TRA kauawa kisa hofu ya watu wasio julikana. Wananchi kutoamini vyombo vya Usalama ni ushahidi tosha ya kwamba Waziri wa Mambo ya Ndani alipwaya.

Rais kuanza kumpa sifa za kinafiki ni kukejeli hali halisi ya Usalama nchini. Rais aache mashindano yupo pale kuwatumikia wananchi na Sio kuwakejeli. Ipo siku kejeli zake zitamtokea puani.
 
Katiba Ni maombi ya watu waliopendekeza hili liwe hivi na haya yawe Yale.. haya hayana thamani Kama walioyatunga.

Kwa maslahi mapana ya taifa Ni Bora tukaitengua, kuliko kupotea nawakati tunaijua njia.
 
Rais amesikika akidai ya kwamba aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Masauni Yusuf ameacha alama. Ni kipindi Cha Waziri Masauni kundi la watu kutekwa na kupotezwa limeshika kasi, mpaka kupelekea wananchi kujihami.
Labda alitumwa akatekeleza
 
Rais Samiah wa Tanzania amekuwa anatoa kauli za kejeli . Ni kama ana dharau Sana. Kwa mfano aliwahi kutoa kauli ya kwamba katiba ni kijitabu tu. Kwa maana nyingine Katiba so Jambo la maana. Pia amewahi kunukuliwa akidai ya kwamba kifo ni kifo hakuna kifo kibaya zaidi ya kingine. Alisema maneno kama njia ya kuonesha ya kwamba kifo Cha kada wa CHADEMA Ally Kibao sio Jambo zito Sana.

Leo wakati akiapisha mawaziri , Rais amesikika akidai ya kwamba aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Masauni Yusuf ameacha alama. Ni kipindi Cha Waziri Masauni kundi la watu kutekwa na kupotezwa limeshika kasi, mpaka kupelekea wananchi kujihami. Juzi tu hapa mfanyakazi wa TRA kauawa kisa hofu ya watu wasio julikana. Wananchi kutoamini vyombo vya Usalama ni ushahidi tosha ya kwamba Waziri wa Mambo ya Ndani alipwaya.

Rais kuanza kumpa sifa za kinafiki ni kukejeli hali halisi ya Usalama nchini. Rais aache mashindano yupo pale kuwatumikia wananchi na Sio kuwakejeli. Ipo siku kejeli zake zitamtokea puani.
 
Of course ni dharau. Aliongolea mawaziri wote aliowabadili ulisipokua Bashungwa! Is like yaliyotokea sio kitu! Ila I have a feeling watachukua hatua kimya kimya.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Mobhare Holmes Matinyi, kuwa Balozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 10 Desemba, 2024.
 

Attachments

  • 20241210_204226.jpg
    20241210_204226.jpg
    463.5 KB · Views: 1
  • IMG-20241210-WA0015.jpg
    IMG-20241210-WA0015.jpg
    198.7 KB · Views: 2
Back
Top Bottom