Rais Samia ashiriki Hafla ya uzinduzi wa Mradi wa kufua Umeme wa Kikagati Murongo, Uganda, Mei 25, 2023

Rais Samia ashiriki Hafla ya uzinduzi wa Mradi wa kufua Umeme wa Kikagati Murongo, Uganda, Mei 25, 2023

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Kufua Umeme wa Kikagati Murongo, Uganda, leo Mei 25, 2023.



Rais wa Uganda Yoweri Museveni amemshukuru Rais Samia kwa kuwa Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufika eneo hilo. Amesema alipanga kuonana na marais wengine wa Tanzania lakini kutokana na sababu mbalimbali hakufanikiwa.

Akizungumza kwenye halfa hiyo, Rais Samia amempongeza Rais Museveni kwa mradi huo na ameshukuru kwa uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Uganda kwenye nyanja mbalimbali ambapo mradi huu utaongeza zaidi ushirikiano huo.

Rais Samia amesema umeme utakaozalishwa hapo utaongeza mashirikiano ya kibiashara, usafirishaji wa watu na bidhaa, afya, veta na mengine kadhalika.

Umeme huu utawakutanisha zaidi watu pamoja na kuongeza ulinzi wa maeneo ya nchi hizi kwa kuunganisha maeneno ya mijini na vijjini.

Ameahidi kuwa Serikali ya Tanzania itafanya kila linalowezekana kufanya mradi huu uendelee bila vikwazo. Pia, ipo tayari kwa mradi huu kwa kuwa inawekeza sana kwenye kusambaza umeme vijijini, na vyanzo vya aina hii vya umeme vinaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kutimiza lengo hilo ya Serikali.

Akielezea zaidi kuhusu mradi huo na eneo uliopo, Rais Museveni amesema yeye binafsi amezaliwa na kukulia karibu na eneo hilo, amepigana vita 3 kwenye eneo hilo na amechunga ng'ombe upande wa Tanzania.

Amewataka Waganda kutokusikitika baada ya kusikia Tanzania inautaka umeme, amehoji Waganda wanasikitika na kunung'unika kwa kipi wakati Umeme huo hautolewi bure? Hata kama wataununua wote Nchi yake itapata pesa na hakutakuwa na tatizo lolote.

Wazo la mradi huo mara kwa kwanza Rais Museveni alimshirikia Hayati Magufuli ambaye aliukubali, na Rais Samia alipoingia madarakani hakusika kuuendeleza.

Fw-LxiyWAAEruDg.jpg

Rais Samia Suluhu Hassan akivuta kamba pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Rais Yoweri Kaguta Museveni kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Kikagati – Murongo, Mbarara nchini Uganda Mei 25, 2023. Mradi huo wa umeme utanufaisha nchi zote mbili katika masuala ya Nishati ya umeme.

Fw-M9fhXoAI8mPS.jpg

Fw-M9fgXgAEMBLw.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati alipotembelea mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo (Megawatt 16), Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

Fw-OUE2WIAYMNl0.jpg

Fw-OUE1WYAE0mA_.jpg

Fw-OUE1XsAA4-X0.jpg
Fw-OUE2WcAYITgS.jpg

Eneo la mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo pamoja na Mitambo kama linavyoonekana pichani, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

Fw-O-vCWwAM4opx.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati wakisikiliza maelezo ya mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.
 
Nimeishi pale murongo kwakweli wanakijiji watanufaika I'la hapo hapo wenzetu Uganda mtambo wao nimkubwa walituwahi kutangulia kujenga kwakuwa uzalishaji umeweka jirani jirani lingekuwa sisi wenyewe tungepata kv nyingi
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Kufua Umeme wa Kikagati Murongo, Uganda, leo Mei 25, 2023...
The Kikagati Hydroeletric Power Project is a low-head, run-of-river 16 MW Hydroelectric Project on River Kagera.

The Kagera River is the main tributary to Lake Victoria and the river basin area lies within Rwanda, Burundi, Tanzania and Uganda.

The site is on the border between Uganda and Tanzania and includes dams and a short headrace and tailrace founded on largely varying ground conditions
 
Jambo Jambo?

image-2023-05-25-15:02:16-375.jpg



Ni kwenye uzinduzi wa mradi wa kufua umeme wa kikagati murongo.

Kasema kuwa bila magufuli huo mradi shirikiano kati ya Tanzania na Uganda bila magufuli usingekuwepo na kufikia hapo.

Kagera Tunanunua Umeme kutoka Uganda maeneo ya Masaka, Ila sasa mradi wa murongo italisha umeme Kagera

Nimehesabu na kama sikosei Museveni kamtaja Magufuli zaidi ya mara 16 huku samia akitajwa mara chache na nadhani haijazidi mara 3 si kama kule Chamwino na uzinduzi wao wa Ikulu huku wakikwepa kumtaja Mwamba.

Na amesema Magufuli alikuwa si mtu wa kusitasita siku ya kwanza kwenye majadiliano magufuli aliwaagiza watendaji wa wizara kuanza kulishughulikia swala hili siku hiyohiyo.

Na kama nimemsikia anasema kuwa alikuwa na mpango huo mradi auiite magufuli sema kwasababu waliowekeza ni kampuni binafsi hivyo wao wana mamlaka na si yeye


image-2023-05-25-15:09:51-317.jpg

image-2023-05-25-15:07:36-400.jpg


IMG_6290.jpg



(Kama wewe ni muwashwaji na unataka kukunwa tafadhali tafuta kwingine siyo kweny uzi huu usije hapa ukiwa umeshiba udaga na maharage ukaja kutoa pumba UTAKUTANA NA MAJIBU MAKALI. Jibu hoja kwa hoja)


Nshomile wa muleba
Kwasasa
Dar es salaam,Tanzania
 
ILA WAGANDA WANATABIA MBAYA KWANINI HAWAJAMTAJA DOKTA KWENYE KIBAO CHAO CHA UZINDUZI ILA WAMETAJA JINA KAVU KAVU
 
Back
Top Bottom