Rais Samia ashiriki Maadhimisho ya Miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara na Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050

Rais Samia ashiriki Maadhimisho ya Miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara na Mkutano wa Kwanza wa Kitaifa wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050

Ila kusema UKWELI aliyekuja na jina Tanganyika MUNGU anamuona!
Au alijua sisi ni wa-Danganyika??
Make naona tunaishi udanganyifu na kudanganywa danganywa tu!
Jina la Tanganika asili yake kwa mjibu wa wapelelezi wa kijerumani lilitokea Kigoma Ujiji (nchi ya rutuba) wakimaanisha samaki wakubwa wanaopatikana ziwa hilo kubwa yaani 'Nika au kwa kabila la wakwendi mwambao wa ziwa hilo waliita ziwa lenye dhoruba'. Hata hivyo wapelelezi hao hawakuishia uchunguzi wao hapo waliendelea kutafiti kutoka makabila mengine ya kibantu kuanzia Kigoma hadi Pwani ambako walikutana na mahusiano ya jina Tanganika na Tanganyika. Alichokibaini ni kwamba katika maelezo ya wasifu wa eneo lote kuanzia mwambao wa ziwa Tanganyika, Ziwa Nyanza (Victoria/ziwa sukuma-kasikazini), Msumbiji hadi Pwani ya Mtwara, Bandar Al Salama na Tanga walimaanisha Tanga ni eneo la kupumzika wavuvi na vyombo vyao vya kuvulia samaki baharini na Matanga (chombo hufungwa Tanga ili upepo usaidie kusukuma uelekeo autakao mvuvi), Nyika ikiimanisha kondeni, shambani, maeneo tambarare ya nchi kavu yanayopakana na bahari, ziwa au mto mkubwa.

Ikumbukwe kuwa mwanzo Tanganyika ilikuwa koloni la Kijerumani ikijumuisha Tanzania bara ya leo, Burundi, Rwanda, Zanzibar, Kongo na kasikazini mwa Msumbiji hasa jimbo la kasikazini la Cabo Delgado. Hata hivyo baada ya vita ya kwanza ya dunia kuisha waingereza na wabeligiji waligawana maeneo hayo ambapo Kongo, Burundi na Rwanda walichukua wabeligiji huku wakoloni wa Msumbiji (Wareno) wakachukua eneo la kasikazini linalopakana na Tanganyika kwenye mto Ruvuma.
Kwa ujumla Tanganyika ni eneo la wakazi wanaopatikana mwambao wa bahari ya hindi kuanzia mto Ruvuma, Mtwara hadi Tanga, kasikazini kuanzia Kilimanjaro hadi Kagera (zamani ziwa magharibi), madharibi kuanzia Kigoma hadi Rukwa, kusini kuanzia Mbeya hadi Ruvuma wenyeji wanaopatikana maeneo hayo hadi katikati ya nchi ndio inaitwa ''TANGANIKA' au 'TANGANYIKA'

Ikumbukwe kwamba Sultan wa Zanzibar wakati wa enzi wa utumwa alikuwa na mamlaka ya kiutawala maeneo yote yaliyopitiwa na msafara wa watumwa kama Kigoma, Tabora, Manyoni (Singida), Dodoma, Morogoro, Pwani, Lindi, Bandar Al Salama na Tanga
 
Jina la Tanganika asili yake kwa mjibu wa wapelelezi wa kijerumani lilitokea Kigoma Ujiji (nchi ya rutuba) wakimaanisha samaki wakubwa wanaopatikana ziwa hilo kubwa yaani 'Nika au kwa kabila la wakwendi mwambao wa ziwa hilo waliita ziwa lenye dhoruba'. Hata hivyo wapelelezi hao hawakuishia uchunguzi wao hapo waliendelea kutafiti kutoka makabila mengine ya kibantu kuanzia Kigoma hadi Pwani ambako walikutana na mahusiano ya jina Tanganika na Tanganyika. Alichokibaini ni kwamba katika maelezo ya wasifu wa eneo lote kuanzia mwambao wa ziwa Tanganyika, Ziwa Nyanza (Victoria/ziwa sukuma-kasikazini), Msumbiji hadi Pwani ya Mtwara, Bandar Al Salama na Tanga walimaanisha Tanga ni eneo la kupumzika wavuvi na vyombo vyao vya kuvulia samaki baharini na Matanga (chombo hufungwa Tanga ili upepo usaidie kusukuma uelekeo autakao mvuvi), Nyika ikiimanisha kondeni, shambani, maeneo tambarare ya nchi kavu yanayopakana na bahari, ziwa au mto mkubwa.

Ikumbukwe kuwa mwanzo Tanganyika ilikuwa koloni la Kijerumani ikijumuisha Tanzania bara ya leo, Burundi, Rwanda, Zanzibar, Kongo na kasikazini mwa Msumbiji hasa jimbo la kasikazini la Cabo Delgado. Hata hivyo baada ya vita ya kwanza ya dunia kuisha waingereza na wabeligiji waligawana maeneo hayo ambapo Kongo, Burundi na Rwanda walichukua wabeligiji huku wakoloni wa Msumbiji (Wareno) wakachukua eneo la kasikazini linalopakana na Tanganyika kwenye mto Ruvuma.
Kwa ujumla Tanganyika ni eneo la wakazi wanaopatikana mwambao wa bahari ya hindi kuanzia mto Ruvuma, Mtwara hadi Tanga, kasikazini kuanzia Kilimanjaro hadi Kagera (zamani ziwa magharibi), madharibi kuanzia Kigoma hadi Rukwa, kusini kuanzia Mbeya hadi Ruvuma wenyeji wanaopatikana maeneo hayo hadi katikati ya nchi ndio inaitwa ''TANGANIKA' au 'TANGANYIKA'

Ikumbukwe kwamba Sultan wa Zanzibar wakati wa enzi wa utumwa alikuwa na mamlaka ya kiutawala maeneo yote yaliyopitiwa na msafara wa watumwa kama Kigoma, Tabora, Manyoni (Singida), Dodoma, Morogoro, Pwani, Lindi, Bandar Al Salama na Tanga
Sawa Mtanganyika!
Sasa mbona mnalikwepa jina lenyewe??
 
Historia nzuri hii,
( kabla ya mwaka 1920 Tanganyiks haikuwepo).

Naomba kufahamu je , ilikuwepo nchi gani kwa jina?

Na labda kabla ya ule mkutano wa Berlin, vilevile kulikuwa na nchi gani hapa tulipo( Tanzania)?
Kati ya mwaka 1880-1919 ilijulikana kama Deutsch-Ostafrika au Germany East Africa-GEA ikijumuisha Tanzania bara ya leo, Burundi, Rwanda, Kongo kasikazini mashariki na sehemu ya kasikazini ya Msumbiji.

Kabla ya hapo utawala wa kikabila wa kikanda ndio ulitamalaki ndio maana wakoloni kwa baadhi ya maeneo walifaulu kuwarubuni viongozi mpaka wakasaini mikataba ya kuiuza nchi kwa zawadi binafsi, mf Chagga land, Meru land, Pare land, Sambaa land, Hehe land, Sukuma land, Haya land chini ya watawala (watemi na machifu) nk

Jina la Tanganyika lilipatikana kutokana na ukusanyaji wa taarifa wa wapelelezi wa kikoloni kuanzia bara hadi pwani kupitia tawala mbalimbali za kikabila (Gesellschaft für Deutsche Kolonisation) kama akina Karl Peters 1885, Richard Burton na John Speke 1857. Kwa mjibu wa mkataba wa Treaty of Versailles June 1919 uliidhinisha jina jipaya la Germany Ostafrika kuwa Tanganyika na kuanza kutumika mwaka 1920 baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia ambapo Mjerumani miongoni mwa masharti aliyopewa kutokana na kushindwa viata ni kulipa fidia uharifu aliofanya, kupoteza makoloni yake kwenye nchi za kigeni, kuondolewa nguvu za kivita, kupoteza mamlaka kwenye makoloni yote. Walioamuru haya kufanyika walikuwa viongozi wafuatao Rais wa Marekani Woodrow Wilson, Waziri mkuu wa Ufaransa Georges Clemenceau, na Waziri mkuu wa Uingereza David Lloyd George lengo lao kuu likiwa kuimarisha ulinzi na usalama wa pamoja kwa mataifa na kunyang'anya silaha ili kuzuia kuzuka kwa vita zingine hapo baadae. WWI-1914-1918

Hata adhabu aliyopewa Ujerumani na nchi baadhi huko Ulaya, Uingereza, Ufaransa na Marekani kitendo kilichopelekea washirika wengi kuchochewa kuanzisha vita dhidi ya wakoloni wapya ndipo chanzo cha vita ya pili ya dunia kuanzia Septemba 1, 1939 na kumalizika Septemba 2, 1945
 
Back
Top Bottom