Rais Samia asijikite kutumbua Wakuu wa Mikoa na Wilaya pekee. Amulike ufisadi unaofanywa na Mawaziri wake

Ndio maana nikaandika ujumbe huu ili umfikie popote alipo na kuchukua hatua. Japo najua akibahatika kupata ujumbe huu hasira zake zitaishia kwa kina Chalamila na wakuu wa wilaya tu.
 
Maneno kibao akimaliza hebu piga makofi kwa mh. Yani wanampatia sana
 
Kama siyo mfuatiliaji jf nasisi hatukufuatilii...
Katoe maoni Yako nyumbani kwako!!
 
Hao amewaruhusu kula kwa urefu wa kamba zao.
Kwahiyo ndio makosa yao ayahamishie kwa wengine.

Kina Chalamila na Amos Makala wanaishi kwa wasi wasi wa masaa ya zuhura, huku mawaziri wakiishi kwa amani na furaha bila hofu yoyote.
 
Sehemu kubwa ya Mawaziri wamekuwa mabilionea..Ni mabilionea kweli pasipo kuwa na biashara wala uwekezaji only in Africa..
Wana fedha mpaka wanafukia kwenye mashamba..Mabilionea wasiolipa kodi..Mabilionea kupitia mirindimo ya siasa..

Wamenunua majumba,Apartments (Dubai,Dar,Etc)wamechoka..Wanatumia haziishi..wana nunua Mashamba Zipo tu..Wanahonga waganga wa kienyeji Zipo tu..Wanaloga sana nyota zing’ae..Wapendwe na kutokumbuliwa..Wanatoa sadaka haswaa😎..Kafara..Michango..Na wale wenye kiu ya kupata Urais ndo usiseme wanamwaga mabilioni utadhani Wanachota mtoni..I wish kungekuwa na Lifestyle Audit ya Hawa viongozi..

Hakuna mradi mkubwa kwenye taasisi chini ya Wizara unapita bila Mawaziri kuhusika..Iwe manunuzi makubwa ,Ujenzi…Wana nguvu kweli kweli..Tunao waadirifu ila wachache mnoo..Investigative Journalism imekufa tungesikia mengi..na kusoma mengi..

Nasikia baadhi hawana hata aibu..kuomba chao..Accounting Officer Akiwa mkaidi anatumbuka live..Nani wa kumfunga Paka kengele..

Nina amini report Za kizalendo Zipo toka TISS..Yanayofanyika yanajulikana..Wanaofanya wanajulikana..Ufisadi unajulikana..Yanayolipotiwa na CAG ni cha mtoto..

Tumuombee Sana Sana Mh Rais..Mwenyezi Ampe ujasiri mkuu ktk maamuzi magumu yenye faida Kwa Taifa na Vizazi vijavyo..Anaweza
 
Sisi tunamuombea usiku na mchana aiendeshe nchi vizuri kwa mujibu wa katiba na sheria zetu. Tatizo yeye anatuangusha na kutuvunja moyo kwa kutoonesha kuguswa na maombi yetu.

Mtu yeye ni amiri jeshi mkuu, mkuu wa nchi, mwenyekiti wa baraza la mawaziri, mwenyekiti wa chama kilichopo madarakani. Ni yeye mwenye maamuzi ya mwisho katika chama na serikali. Anashindwaje kuwatumbua na pengine kuwachukulia hatua kali mawaziri wasiosimia vizuri wizara zao ili liwe fundisho wa wabadhirifu, mafisadi na wavivu wengine? Mbona makosa ya wakuu wa mikoa na wilaya kila siku anayaona na kuyafanyia kazi kwa kuwatumbua au kuwabadilishia sehem za kazi.

Naona yale masaa ya Zuhura na ile kauli ya mkinizingua nitawazingua inawahusu tu wakuu wa mikoa na wilaya. Mawaziri hakuna wa kuwagusa hata kama wakizingua.
 
Naunga mkono hoja..
 
Mkuu mbona kimya siku hizi kuhusu ushindi na mafanikio ya Hamas Hamas dhidi ya taifa teule?
 
Ukiacha waziri mkuu anayehangaika na ufisadi sioni kiongozi mwingine aliye serious kulinda mali za umma kwa sasa
 
Mfano hai wa ufisadi huo ni upi ili tusipoteze muda?
1. Mkataba wa kununua treni ya billion 600 unabatilishwa na kuletwa wakununua treni kwa 1.3 Trillions. Treni inakuja ya kimagumashi af used.

2. Uwanja wenye capacity ya 30k kujengwa kwa 286 billions ilihali wenye capacity ya 60K ulijengwa kwa 50 Billions.

3.Kibanda cha mlinzi kujengwa kwa million 13 wakati hata million 6 kisingemaliza. Its irrelevant completely.

mengine wataongezea wadau...
 
+ Ummy, Masauni, Nape, Kijaju, Mbarawa, Aweso, Makamba n.k, hawa hakuna wanachofanya lakini wanauhakika 100%

Ummy ndio kabisa yani sijui anafanya nini bima za afya ovyo katoa adi kwa wakulima ambao walikua kwenye mfumo rasmi ambao wanauza mazao kwa kutumia vyama vyao uko yani ovyo sana sector ya afya now
 
Ummy ndio kabisa yani sijui anafanya nini bima za afya ovyo katoa adi kwa wakulima ambao walikua kwenye mfumo rasmi ambao wanauza mazao kwa kutumia vyama vyao uko yani ovyo sana sector ya afya now
Ummy ni takataka lakini anarudisha rejesho kwa maza
 
Mkuu mbona kimya siku hizi kuhusu ushindi na mafanikio ya Hamas Hamas dhidi ya taifa teule?
Kule nimeawaachia kwanza maulamaa wa Kilwa na wayahudi wa gongo la mboto wamalizane wenyewe πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…