Rais Samia ataka vikundi vipewe milioni 100 badala ya vijipesa

Rais Samia ataka vikundi vipewe milioni 100 badala ya vijipesa

Casuist

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2014
Posts
1,189
Reaction score
2,970
Rais Samia: Jingine ni lile la asilimia kumi, Dodoma wamesema vizuri hapa, hongera mstahiki meya na mkuu wa mkoa. Wamesema vizuri kwamba wanajipanga sasa kwa ajili ya kutoa visenti vichache kwa kila kundi na mimi huwa nasema, fungu lile lilikuwa linatumika kama mfuko wa kisiasa wa madiwani, kila diwani anapeleka kwake vijipesapesa kujipendekeza kwa watu ili ateuliwe lakini huoni kilichofanyika.

Sasa watu wajipange kutoa fedha kwa vikundi vikubwa vyenye miradi mikubwa ambayo impact yake itaonekana, mnatoa milioni 40 kwa kikundi kwa mfano, milioni 100 kwa kikundi lakini mna hakika zitaenda kufanya mradi utakaowapa wao ajira, utaowaajiri wenzao na faida zinaonekana.

Sio kugawa kidogo kidogo kujipendekeza kwa wapiga kura ili uje kupigiwa kura na mfuko huu tunaua kwa maslahi binafsi.
 
Wazo Jema, sio kila mmoja lazima awe mchuuzi.
 
Vikundi vilikuwa hewa vidogo vidogo na havina miradi mikubwa ya pamoja yenye impact

Mbunge au viongozi wa halmashauri au diwani ana form kakikundi koko anawapa visenti kiduchu tu kuiba na ku boost tu image yake mbele ya camera za vyombo vya habari lakini hata hivyo vihela kiduchu mikopo ilikuwa hailipiki ulikuwa wizi mtupu

Kwa hizo nyingi ziende vikundi vikubwa vya ubia vyenye kitu kikubwa sio individuals
 
Mimi nina kikundi changu cha vijana wanaobeti mkitupa hata hivyo vijipesa vidogo kama tu-milioni 10 ndani ya weekend moja tunakuletea 100 millions, serikali itufikirie katika hili🐒
 
Back
Top Bottom