Rais Samia atampata wapi ‘Kawawa’ wake, awe mwaminifu kama Rashid kwa Nyerere

Rais Samia atampata wapi ‘Kawawa’ wake, awe mwaminifu kama Rashid kwa Nyerere

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,282
Reaction score
117,244
Katika watu ambao historia ya Tanzania huwa haiwatendei haki basi Rashid Mfaume Kawawa anaongoza - ni nadra Sana kusikia historia sahihi ya Kawawa.

Mara nyingi Historia yote ya Nyerere inaweza somwa na usisikie hata jina la Kawawa. Watu wengi hawajui kuwa wakati Kawawa anakuwa 'Waziri Mkuu wa Tanganyika' alikuwa Kiongozi mkubwa kuliko wote Tanganyika kabla haijawa Jamhuri..

Kawawa alikuwa Waziri Mkuu baada ya Nyerere kijiuzulu..mpaka Leo hiko kipande cha historia hakieleweki vizuri.. Itoshe kusema kama Kawawa angekuwa na tamaa ya Uongozi kama Viongozi wengine Africa basi Nyerere hata huo urais angekuja kuusikia kwenye bomba.

Nyerere alijiuzulu Uwaziri Mkuu wa Tanganyika na kumkabidhi madaraka Kawawa halafu ilipofika tarehe 9December 1962 Nyerere akarudi kuja kuapa kuwa Rais wa kwanza Tanganyika. Kawawa akiwezesha zoezi lote hilo.

Ndo maana siku Ile Kambona alipokuja kuwashambulia Kawawa, Nyerere na Amir Jamal. Nyerere alisema anaweza kukaa kimyaa akishambuliwa yeye lakini hawezi kunyamaza watu wakimshambulia Kawawa...akasema kama Kawawa sio muaminifu basi hakuna watu waaminifu duniani.

Hata siku anastaafu Nyerere aliongea huku machozi yanamtoka akisema 'Kawawa nakushukuru sana'. Ulibeba lawama zangu zote zikawa zako.

Hakuna kiongozi aliyewahi kubeba lawama za Rais Tanzania kama Kawawa... Zoezi la Vijiji vya ujamaa lilipoleta njaa na vifo ..Kawawa alibeba lawama peke yake.

Kawawa alikuwa muaminifu na mtiifu kwa Nyerere haijawahi tokea.....aliziba udhaifu wa Rais na kumlinda na lawama za kila aina..

Sio kila Rais wa Tanzania anapata bahati ya kuwa na msaidizi kama Kawawa ..Mwinyi alipata Waziri Mkuu Malecela alietamani kuwa Rais akijiandaa na kushindana na wanaotaka urais wengine. Hakukubali kuchafuka kwa niaba ya Rais.

Mkapa alipata Sumaye ambae alikuwa kila kitu ni kama hawezi hadi wakampachika jina la Zero.

Kikwete akamchagua Rafiki yake Lowassa..wakawa kama 'marais wawili'.

Kama kuna kitu Rais Samia anahitaji sasa ni Kumpata 'Rashid Kawawa’ wa kwake.

Lakini je atampata wapi?

Tunao Viongozi watiifu na waaminifu wa kumlinda na kumsaidia Rais na kukubali kubeba lawama zote na kuchafuka kwa niaba ya Rais? Walk wapi?
 
Haipaswi kupatikana Kawawa mwingine yeyote.

Yaani uiweke nchi kwenye hali mbaya alafu mtu atoke hadharani kukutetea na kukubali kuchukua lawama zako? Ufanye upuuzi kwa kutoshirikisha wataalamu kwa kuamini mawazo yako ni sahihi alafu atoke mtu akutetee?

Sawa, Kawawa huenda alikuwa loyal sana kwa Mwalimu. Lakini pia, alikuwa akilinda kibarua chake kama WM.

Kama angejaribu kuyaelekeza lawama hizo kwa Mwalimu bila shaka angeachishwa Uwaziri wake.

Tunahitaji viongozi ambao wana maono. Ambao watakuwa tayari kumuambia Boss wake hapa unakosea, twende kwenye njia hii.

Kuna mengi Kawawa kayafanya vema sana lakini tusimpe sifa kumkumbatia Boss wake pale alipokosea.
 
Katika watu ambao historia ya Tanzania huwa haiwatendei haki basi Rashid Mfaume Kawawa anaongoza...ni nadra Sana kusikia historia sahihi ya Kawawa...
Mara nyingi Historia yote ya Nyerere inaweza somwa na usisikie hata jina la Kawawa..
Watu wengi hawajui kuwa wakati Kawawa anakuwa 'waziri mkuu wa Tanganyika '
Alikuwa Kiongozi mkubwa kuliko wote Tanganyika kabla haijawa Jamhuri..

Kawawa alikuwa waziri mkuu baada ya Nyerere kijiuzulu..mpaka Leo hiko kipande cha historia hakieleweki vizuri..
Itoshe kusema kama Kawawa angekuwa na tamaa ya Uongozi kama Viongozi wengine Africa basi Nyerere hata huo urais angekuja kuusikia kwenye bomba..
Nyerere alijiuzulu Uwaziri Mkuu wa Tanganyika na kumkabidhi madaraka Kawawa halafu ilipofika tarehe 9December 1962 Nyerere akarudi kuja kuapa kuwa Rais wa kwanza Tanganyika..
Kawawa akiwezesha zoezi lote hilo....


Ndo maana siku Ile Kambona alipokuja kuwashambulia Kawawa, Nyerere na Amir Jamal...Nyerere alisema anaweza kukaa kimyaa akishambuliwa yeye lakini hawezi kunyamaza watu wakimshambulia Kawawa...akasema kama Kawawa sio muaminifu basi hakuna watu waaminifu duniani.....

Hata siku anastaafu Nyerere aliongea huku machozi yanamtoka akisema
'Kawawa nakushukuru sana'
Ulibeba lawama zangu zote zikawa zako..

Hakuna kiongozi aliewahi kubeba lawama za Rais Tanzania kama Kawawa...
Zoezi la Vijiji vya ujamaa lilipoleta njaa na vifo ..Kawawa alibeba lawama peke yake..

Kawawa alikuwa muaminifu na mtiifu kwa Nyerere haijawahi tokea.....aliziba udhaifu
Wa Rais na kumlinda na lawama za kila aina..


Sio kila Rais wa Tanzania anapata bahati ya kuwa na msaidizi kama Kawawa ..

Mwinyi alipata waziri mkuu Malecela alietamani kuwa Rais akijiandaa na kushindana na wanaotaka urais wengine..
Hakukubali kuchafuka kwa niaba ya Rais..

Mkapa alipata Sumaye ambae alikuwa kila kitu ni kama hawezi hadi wakampachika jina la Zero..

Kikwete akamchagua Rafiki yake Lowassa..wakawa kama 'marais wawili'..

Kama kuna kitu Rais Samia anahitaji sasa ni Kumpata 'Rashid Kawawa ' wa kwake..

Lakini je atampata wapi??

Tunao Viongozi watiifu na waaminifu wa kumlinda na kumsaidia Rais na kukubali kubeba lawama zote na kuchafuka kwa niaba ya Rais??Walk wapi??
Mimi nadhani na nyakati zinachangia.

Enzi hizo Nyerere alikuwa na ushawishi mzito mpaka huko nchi za mabeberu, hakuna namna yoyote wateule wake wangempindua.

Na hata kama wangefanya hivyo bado angerudi kirahisi. Mifano ipo: Kama Obote alirudishwa Uganda, jaribio la mapinduzi ya Nyerere lilifail tena kwa kusaidiwa na Uingereza ni kwa vipi Kawawa angeweza kufanya chochote.

Na kipindi hicho viongozi wengi waliokuwa na Nyerere hawakuwa na tamaa, kwasababu zaidi ya kuwa na madaraka Nyerere hakuwa mtu wa anasa wala kujilimbikizia mali.

Sasa kwa uongozi ulivyokuwa enzi za Nyerere ni nani angekuwa na tamaa ya kuwa na madaraka?

Ila nyakati hizi hali ni tofauti, watu wana ndoto zao za kuishi kifahari, kuabudiwa na kupora mali za umma. Uongozi umekuwa ni sehemu ya kusaka fursa kwa njia yoyote. Ukiikosa fursa ndani ya CCM unaitafuta nje ya CCM.

Nyakati hizi ambazo UTAWALA ni FURSA huwezi kumpata Kawawa hata kidogo.
 
Haipaswi kupatikana Kawawa mwingine yeyote.

Yaani uiweke nchi kwenye hali mbaya alafu mtu atoke hadharani kukutetea na kukubali kuchukua lawama zako? Ufanye upuuzi kwa kutoshirikisha wataalamu kwa kuamini mawazo yako ni sahihi alafu atoke mtu akutetee?

Sawa, Kawawa huenda alikuwa loyal sana kwa Mwalimu. Lakini pia, alikuwa akilinda kibarua chake kama WM.

Kama angejaribu kuyaelekeza lawama hizo kwa Mwalimu bila shaka angeachishwa Uwaziri wake.

Tunahitaji viongozi ambao wana maono. Ambao watakuwa tayari kumuambia Boss wake hapa unakosea, twende kwenye njia hii.
Kama Lissu
 
Mimi nadhani na nyakati zinachangia.

Enzi hizo Nyerere alikuwa na ushawishi mzito mpaka huko nchi za mabeberu, hakuna namna yoyote wateule wake wangempindua.

Na hata kama wangefanya hivyo bado angerudi kirahisi. Mifano ipo: Kama Obote alirudishwa Uganda, jaribio la mapinduzi ya Nyerere lilifail tena kwa kusaidiwa na Uingereza ni kwa vipi Kawawa angeweza kufanya chochote.

Na kipindi hicho viongozi wengi waliokuwa na Nyerere hawakuwa na tamaa, kwasababu zaidi ya kuwa na madaraka Nyerere hakuwa mtu wa anasa wala kujilimbikizia mali.

Sasa kwa uongozi ulivyokuwa enzi za Nyerere ni nani angekuwa na tamaa ya kuwa na madaraka?

Ila nyakati hizi hali ni tofauti, watu wana ndoto zao za kuishi kifahari, kuabudiwa na kupora mali za umma. Uongozi umekuwa ni sehemu ya kusaka fursa kwa njia yoyote. Ukiikosa fursa ndani ya CCM unaitafuta nje ya CCM.

Nyakati hizi ambazo UTAWALA ni FURSA huwezi kumpata Kawawa hata kidogo.
Good
 
Mimi nadhani na nyakati zinachangia.

Enzi hizo Nyerere alikuwa na ushawishi mzito mpaka huko nchi za mabeberu, hakuna namna yoyote wateule wake wangempindua.
Mkuu ukisikia mabeberu tunao-assume kwamba wapo sasa hivi kipindi kile ndio kulikuwa na mabeberu wa hali ya juu (wewe ukijifanya ku-side na Russia au itikadi zako zikienda ndivyo sivyo you are history) CIA imefanya mengi mkuu..., Fuatilia tu kina Thomas Sankara na Patrice Lumumba ni nini kiliwakuta...

Acha kaka wale Mabeberu ambao kina Polepole na Boss wake wanaowatunga kipindi kile walikuwepo (and they meant business)
 
Katika watu ambao historia ya Tanzania huwa haiwatendei haki basi Rashid Mfaume Kawawa anaongoza...ni nadra Sana kusikia historia sahihi ya Kawawa...
Mara nyingi Historia yote ya Nyerere inaweza somwa na usisikie hata jina la Kawawa..
Watu wengi hawajui kuwa wakati Kawawa anakuwa 'waziri mkuu wa Tanganyika '
Alikuwa Kiongozi mkubwa kuliko wote Tanganyika kabla haijawa Jamhuri..

Kawawa alikuwa waziri mkuu baada ya Nyerere kijiuzulu..mpaka Leo hiko kipande cha historia hakieleweki vizuri..
Itoshe kusema kama Kawawa angekuwa na tamaa ya Uongozi kama Viongozi wengine Africa basi Nyerere hata huo urais angekuja kuusikia kwenye bomba..
Nyerere alijiuzulu Uwaziri Mkuu wa Tanganyika na kumkabidhi madaraka Kawawa halafu ilipofika tarehe 9December 1962 Nyerere akarudi kuja kuapa kuwa Rais wa kwanza Tanganyika..
Kawawa akiwezesha zoezi lote hilo....


Ndo maana siku Ile Kambona alipokuja kuwashambulia Kawawa, Nyerere na Amir Jamal...Nyerere alisema anaweza kukaa kimyaa akishambuliwa yeye lakini hawezi kunyamaza watu wakimshambulia Kawawa...akasema kama Kawawa sio muaminifu basi hakuna watu waaminifu duniani.....

Hata siku anastaafu Nyerere aliongea huku machozi yanamtoka akisema
'Kawawa nakushukuru sana'
Ulibeba lawama zangu zote zikawa zako..

Hakuna kiongozi aliewahi kubeba lawama za Rais Tanzania kama Kawawa...
Zoezi la Vijiji vya ujamaa lilipoleta njaa na vifo ..Kawawa alibeba lawama peke yake..

Kawawa alikuwa muaminifu na mtiifu kwa Nyerere haijawahi tokea.....aliziba udhaifu
Wa Rais na kumlinda na lawama za kila aina..


Sio kila Rais wa Tanzania anapata bahati ya kuwa na msaidizi kama Kawawa ..

Mwinyi alipata waziri mkuu Malecela alietamani kuwa Rais akijiandaa na kushindana na wanaotaka urais wengine..
Hakukubali kuchafuka kwa niaba ya Rais..

Mkapa alipata Sumaye ambae alikuwa kila kitu ni kama hawezi hadi wakampachika jina la Zero..

Kikwete akamchagua Rafiki yake Lowassa..wakawa kama 'marais wawili'..

Kama kuna kitu Rais Samia anahitaji sasa ni Kumpata 'Rashid Kawawa ' wa kwake..

Lakini je atampata wapi??

Tunao Viongozi watiifu na waaminifu wa kumlinda na kumsaidia Rais na kukubali kubeba lawama zote na kuchafuka kwa niaba ya Rais??Walk wapi??
Kama Samia akiwa kama Nyerere/Magufuli basi waziri mkuu aliyenaye atakuwa kama Sokoine! Kama atakuwa kama Msoga basi asitegemee kumpata Mizengo, vinginevyo yeye mwenyewe Samia ategemee kuwa Kawawa wa rais ajaye😜!
 
Mkuu ukisikia mabeberu tunao-assume kwamba wapo sasa hivi kipindi kile ndio kulikuwa na mabeberu wa hali ya juu (wewe ukijifanya ku-side na Russia au itikadi zako zikienda ndivyo sivyo you are history) CIA imefanya mengi mkuu..., Fuatilia tu kina Thomas Sankara na Patrice Lumumba ni nini kiliwakuta...

Acha kaka wale Mabeberu ambao kina Polepole na Boss wake wanaowatunga kipindi kile walikuwepo (and they meant business)
Exactly, Sasa imagine Nyerere aliweza kusurvive enzi hizo.

Tena alikuwa anatunishiana misuli na mataifa makubwa tu.

Nyerere alivunja hadi uhusiano wa kidiplomasia na Israel kwasababu ya Palestina lakini bado alikuwa na urafiki na hao hao wazungu🤣

Uzuri wa Nyerere alikuwa hatumii nguvu, alikuwa anapambana nao kwa hoja, enzi hizo wana umoja wao wa nchi zisizofungamana na upande wowote ( NAM )
 
Kawawa kwa unyenyekevu kea Nyerere ni historia isiyo na mfano. RIP Kawawa. Na yeye mwenyewe anakiri kwenye moja ya mahojiano, kuwa uhusiano wa yeye na Nyerere ilikuwa kama mwalimu na mwanafunzi na mwalimu wake, sio wa wa watu wawili wanaolingana. Mwingine aliyejita ni sir George Kahama , Kahama anasema Nyerere alikuwa anapenda sana kumtania Gerorge Kahama, lakini Kahama hajawahi kumtania Nyerere. Sababu, anasema Nyerere alikuwa mtoto wa chief, kwa hiyo alikulia mazingira ya kutawala, na siku zote mtawala lazima akutanie mtawaliwa,lakini Nyerere ilikuwa ukimtania basi hata vyeo vizuri kwake unavikosa. Kahama alipokuwa hilo alikubali kuwa punching bag wa Nyerere na Nyerere alikuwa comfortable na uhusiano huo. Walijifanya kumzoea na kumtania Kahama alishuhudia wakishuka kisiasa mmoja baada ya mwingine. Lakini Kahama aliweza kwenda na Nyerere,akapigiwa send Nyerere akafanya Kazi na Mwinyi hadi na Mkapa,kigezo eti ni mchapakazi kumbe ni mtiifu. Siku za mwisho alikengeuka akajiunga na Lowassa kumbe alijikuta upinzani alipogundua uaminifu haukumpa pensheni ya kutosha. LAkini Nyuma aliweza kushika hata vyeo vitano kwa mpigo
 
Back
Top Bottom