Yusufu R H Sabura
JF-Expert Member
- Jun 26, 2020
- 355
- 486
lakn diplomasia hio hio inasema akifa wa kwetu wasiweke nusu mlingoti? Alipokuja kukukalieni kichwani mlifanya makubaliano kuwa awakalie?Alikuwa mkuu wa Tanganyika kwa mwaka mmoja na alisaini hati za uhuru.
Kwa mustakabali wa diplomasia ni jambo jema kufanya hili.
Haya tuungane.
inatuhusu nini sisi, binadamu wanafiki sana,hawa hawa ndio walitutesa leo tunawaabuduTulivofiwa sisi wao walitangaza maombolezo?
jumuiya ya madola ni muendlezo wa ukoloni kwa lugha tamu...Tanzania ni mwanachama wa Jumuiya ya Madola ambayo inaziunganisha nchi mbalimbali ikiwemo Uingereza na nchi zilizokuwa makoloni yake.
Ni jambo la hekima kidiplomasia kuonyesha kama nchi mwanachama kuwa umeguswa na msiba huo wa kiongozi huyo mkuu wa Uingereza. Tanzania inapokea misaada mingi ya kifedha kutoka kwa nchi hii.
Kwa hiyo ni vyema kuwadhihirishia kuwa tupo pamoja nao katika kipindi wanapoomboleza kifo cha kiongozi mkuu wa taifa lao. Natambua si Tanzania tu ambayo itashusha bendera zake nusu mlingoti, bali mataifa yaliyo mengi ikiwemo nchi zote zilizo wanachama wa Jumuiya ya Madola.
Duniani hakuna cha bure, zaidi ya salamu tu,Kwani na wao wanazileta bure.......timing tu ,tunakula walivyotuibia
hata mwaka huu zilikuwepo mi nilikuta deadline tyari ilikuwa juneZilipotea Mkuu mambo ya UTAWALA BORA
Two years back...niliiipata ila kwa mbinde sana Mkuu kupitia hukohuko kwao SKOTISHI tena kwa heshima ya Julius upande wa Conservation
waafrika tunapenda kujipendekeza, mambo ya wazungu tuwaachie wazunguTulivofiwa sisi wao walitangaza maombolezo?
Unajua kabisaaa kuwa tunaomboleza na hakika macho yamevimba kwa kumilia Lizabeta.Nashauri ndege zetu zitupeleke msibani UK, tukamlilie malkia Liz,
siku tano kukaa uzunguni tuapunguza machungu ya tozo,
Tukirudi watuache Bujumbura Burundi kwa kutii agizo la Nchemba Madilu,
Misaada gani tena jamani hii nchi si ni tajiri!!!ACHENI UNAFIKI mbona pesa yao mnaipenda?? Mbona misaada Yao mnapokea? Tena ipepee nusu mlingoti mwaka mzima.....
Hahahaha tuna utajiri wa maneno mengiMisaada gani tena jamani hii nchi si ni tajiri!!!
Na hiyo so called Commonwealth inatusaidia nini haswa? Alivyokufa Baba wa Taifa waliomboleza siku ngapi? Siku moja nusu mlingoti ingetosha kabisa! Utumwa wa akili! Ukoloni mamboleo!Tanzania ni mwanachama wa Jumuiya ya Madola ambayo inaziunganisha nchi mbalimbali ikiwemo Uingereza na nchi zilizokuwa makoloni yake.
Ni jambo la hekima kidiplomasia kuonyesha kama nchi mwanachama kuwa umeguswa na msiba huo wa kiongozi huyo mkuu wa Uingereza. Tanzania inapokea misaada mingi ya kifedha kutoka kwa nchi hii.
Kwa hiyo ni vyema kuwadhihirishia kuwa tupo pamoja nao katika kipindi wanapoomboleza kifo cha kiongozi mkuu wa taifa lao. Natambua si Tanzania tu ambayo itashusha bendera zake nusu mlingoti, bali mataifa yaliyo mengi ikiwemo nchi zote zilizo wanachama wa Jumuiya ya Madola.
Hujuia chochote Kaa kimyaaNa hiyo so called Commonwealth inatusaidia nini haswa? Alivyokufa Baba wa Taifa waliomboleza siku ngapi? Siku moja nusu mlingoti ingetosha kabisa! Utumwa wa akili! Ukoloni mamboleo!