Rais Samia atengua Uamuzi wa TRA Kuhusu Machinga Kutumia EFD

Rais Samia atengua Uamuzi wa TRA Kuhusu Machinga Kutumia EFD

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama Machinga wamemsifu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na uamuzi wake wa kusitisha utaratibu uliotangazwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuwataka kuanza kutumia mashine za kieletroniki (EFD) katika kufanya malipo.

Sambamba na hilo wamemwomba Rais Dkt. Samia kuunda kikosi kazi kitachojumuisha viongozi wa wamachinga nchini, TRA, Jeshi la Polisi, Viongozi kutoka Halmashauri pamoja na wawakilishi wa serikali, kukaa na kufanya upembuzi wa kuwatambua wamachinga halisi ili kuzuia wafanyabiashara wasiokua na sifa ya kuwa machinga kujipenyeza kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.

Nae Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba alitoa ufafanuzi juu ya suala hili alipoulizwa na kituo kimoja cha Runinga na kusema

"Nitoe rai Machinga wasipate taharuki yoyote na Rais amelishalitolea ufafanuzi na mantiki ilikuwa sio Machinga ilikuwa ni maeneo mahsusi ya matumizi ya EFD lakini ilivyotafsiriwa ni machinga pekee lakini zoezi halijalenga hivyo, lililenga maeneo mahsusi ambayo ya matumizi ya EFD"- Waziri Mwigulu Nchemba

tuzoopiic.jpg
 
Piga kazi mama tumecheleweshwa mnooo kama taifa zaidi ya miaka 7.




Tunachokijua:
 
Hakika Rais Samia ni rais msikivu anayeguswa na changamoto za wamachinga. Mungu ambariki.
 
Mwemdelezo wakutengeneza matatizo na kisha kuyatatua[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wala si muendelezo sema mwigulu ni mtu ambae akili zake zinamtuma vyanzo vya mapato ni kumminya mwananchi wa hali ya chini kama alivyofanikiwa kwenye tozo kwenye hili la risiti kwa wafanyabiashara wadogo mama kalishtukia,jamaa sijui ana lengo gani na serikali ya mama!
 
Hizo EFD wakizifanya rafiki (digitally) na kuzigawa kama njugu; why not hata muuza karanga akitumia ?

Hii nchi isiyokuwa na Vision wala Sera ni mwendo wa kupiga hatua kuelekea nyuma....
 
Kwa mambo anayoendelea kufanya Rais Samia Suluhu tunakila sababu ya wenda nae mpaka 2030
 
Tengeneza tatizo then rudi litatue ili mafala na wajinga wapige makofi na kushangilia, nchi imejaaa wajinga kwa kifupi jamaaa wanatawala wajinga
 
Back
Top Bottom