Rais Samia atengua uteuzi wa Eric Hamissi, Mkurugenzi Mkuu wa Usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

Rais Samia atengua uteuzi wa Eric Hamissi, Mkurugenzi Mkuu wa Usimamizi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

Huwa nashindwa kuelewa BANDARINI kuna nini?! mbona huwa hakuishi MATATIZO?!
yaani kunaonekana kama kuna miungu watu/ uttachable!!!

Nashauri Jeshi lipewe Jukumu la kuendesha Bandari au waongeza nguvu hapo naamini kutakaa sawa, kama kuna wabishi tupa pembeni.

Huwa najisikia maumivu kila mara Rais analalamikia utendaji wa Bandari sio wa kuridhisha. kama kuna watendaji wanao fanya hujuma ya kukwaza juhudi za Rais wabainishwe na watolewe mara moja.
Taasisi zote za ulinzi na usalama zipo hapo bandarini.
Tatizo la msingi ni maadili ya "rasilimali watu" wanaopewa kutekeleza majukumu yao pale.
Kijana wa "teeth" (tamka tiithi) anapelekwa pale akiwa na ndoto za kumiliki jumba la kifahari pale Mbweni na Toyota Prado TX.
Takukuru vivyo hivyo.
Polisi nao ni vivyo hivyo.
Wavaa mabaka nao vivyo hivyo.
Kuli naye vivyo hivyo.
Dereva naye vivyo hivyo.
Afisa forodha naye vivyo hivyo.
Bodi, Kamati ya Bunge,RC, RPC, RSO, DC, OCD, DSO.
Kwa mnyororo huo,kweli tunategemea bandarini pawe salama!!??
Pale Nyamisati pana bandari inapitisha mamia ya tani za mizigo kila leo,na mamlaka husika wanajua,lakini hakuna hatua zinachukuliwa.
 
Huwa nashindwa kuelewa BANDARINI kuna nini?! mbona huwa hakuishi MATATIZO?!
yaani kunaonekana kama kuna miungu watu/ uttachable!!!

Nashauri Jeshi lipewe Jukumu la kuendesha Bandari au waongeza nguvu hapo naamini kutakaa sawa, kama kuna wabishi tupa pembeni.

Huwa najisikia maumivu kila mara Rais analalamikia utendaji wa Bandari sio wa kuridhisha. kama kuna watendaji wanao fanya hujuma ya kukwaza juhudi za Rais wabainishwe na watolewe mara moja.
Bandari haitaji miguvu
Mzee inahitaji akili,ubunifu
Weledi,mtendaji
Hao wajeda si walipelekwa kwenye korosho,ilikuwaje

Ova
 
Hivi nchi za Ulaya bandari zao nazo zina shida kama hizi zetu? Kama hawana wao wamewezaje kudhibiti? tunashindwa nini kujifunza mifumo ya udhibiti toka kwao?

Maana pale TPA ukichaguliwa ni lazima utatenda dhambi hata kama ulikuwa hutaki kumuudhi muumba wako, maana hela inakufuata yenyewe sasa uikatae sheikh ?
Tanzania mtu akishawekwa kwenye taasisi basi mawazo yake ni kula tu

Ova
 
Ikibinafsishwa ndio inakufa kabisa. Rejea kilichowahi kutokea kwenye Reli, Shirika la ndege na viwanda
Inategemea na vile unavyobinafsisha,wao serikali wanatakiwa kubaki kwenye kusimamia kodi tu,shughuli za kutoa mizigo sekta binafsi wapewe wafanye
 
Kubadilisha mfumu wa uendeshaji ka kanuni. Kwa mfano (siyo lazima iwe hivyo) watu wanaajiriwa kwa mikataba inayozingatia utendaji wao baada ya kushindanishwa na kuchujwa kwa umakini.
Taasisi nyingi wanaajiriwa kwa kushindanishwa mbona napo bado pako hoi?
 
Binafsisha hizi BANDARI, naona zinatupa shida kubwa kuziendesha au recruits freshers kutoka University, peleka wachache pale Durban, Capetown, Rotterdam, Botswana (dry port)wakajifunze kwa 24mth kuhusu uendeshaji wa hizi bandari, na ajira mpya zifanyike yaani we need to start upya
Wazo zuri Ila Nina wasiwasi na huo uthubutu wa kuwapeleka vijana wakajifunze kama utafanyiwa kazi.
 
Bandari haitaji miguvu
Mzee inahitaji akili,ubunifu
Weledi,mtendaji
Hao wajeda si walipelekwa kwenye korosho,ilikuwaje

Ova
inahitaji weledi wa kula mapato?!
inahitaji akili ya kula rushwa?!
hao tunao waita weledi ndio wametufikisha hapo.

Bandarini panahitaji minguvu na weledi vyote kwa pamoja. kuna mifisi maji pale haisikiii wala haiambiliki matokeao yake tunapata hasara kama taifa.

Vyombo vyetu vyote vya ulinzi na usalama vimeshindwa kabisa kuidhibiti upotevu wa mapato hapo bandarini?! vimeshindwa kusimamia ufanisi wa bandari??!

ni watu wa aina gani wanao toa huduma ktk bandari zetu haswa bandari ya DSM?!

Kama bandari ya DSM tu ambayo ipo pua na mdomo sasa vipi kuhusu bandari ya KIGOMA? N.K
 
Back
Top Bottom