Pre GE2025 Rais Samia atoa milioni 10 kwa Bodaboda Arusha

Pre GE2025 Rais Samia atoa milioni 10 kwa Bodaboda Arusha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Rais Dkt. Samia Suluhu ametoa Shilingi milioni 10 kwa Chama cha Waendesha Bodaboda Wilaya ya Arusha ili kusaidia kukamilisha utaratibu wa kuanzisha Chama cha Ushirika cha waendesha bodaboda hao.
IMG_2066.jpeg

Aidha, Rais ametoa pikipiki mbili zitakazotumiwa na viongozi wa chama hicho kwa ngazi ya wilaya na mkoa ili kusimamia na kutatua changamoto za wanachama.
IMG_2067.jpeg

Fedha hizo zilikabidhiwa leo Jijini Arusha na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Mohamed Ali Kawaida, wakati wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Bodaboda Wilaya ya Arusha. Mkutano huo pia ulihusisha uzinduzi wa mfumo wa kidijitali wa utambuzi wa wanachama.
IMG_2068.jpeg

Kawaida, amebainisha kuwa waendesha bodaboda walikosa fedha za kukamilisha usajili wa ushirika huo, na msaada wa Rais utawasaidia kuimarisha shughuli zao.

Pia amewataka waendesha bodaboda kujisimamia kwa nidhamu, kuacha matumizi ya dawa za kulevya, na kutoshiriki kwenye uhalifu.

Soma, Pia: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Namna hii halafu CCM wanatoa fomu zaidi ya moja. Wewe!!
 
Afadhali hata na hao wamekulapo,

Kuliko akina mugabe wale hela za abdul pekeyao ,

Hii nchi kila mtu anatakiwa alepo bwana mchi ni yetu sote

Hongera Ccm
 
Nilifikiri kuna goli la simba na jangwani pekee, kumbe hadi goli la maafisa usafirishaji lipo
 
2030 tutalia na kusaga meno!
Nimemkumbuka JPM,hadi naona machozi yanataka kunitoka😭
 
Sio hela zake
Kila mwezi anapata sh 60 millioni kutoa zawadi kwa wananchi
 
Mwezi huu wa December peke yake nimeombwa hela na wanawake takriban 151.
Kwanini asiwasaidie Hawa wenzake?
 

MAAFISA USAFIRISHAJI (BODABODA) MKOA WA ARUSHA NA SAMIA DAMU DAMU

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Ndugu Mohammed Ali Kawaida (MCC) amezindua Saccoss ya Maafisa Usafirishaji jijini Arusha kwa kuwachingia kiasi cha shilingi Milioni Kumi (10) kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan itakayosaidia kuanzishwa kwa Saccoss hiyo.

Vilevile; Ndugu Kawaida Kwa niaba ya Mhe. Rais amekabidhi boda boda mbili moja iwasaidie kazi viongozi wa Wilaya na nyingine viongozi wa Mkoa wa Maafisa usafirishaji kwa kuwatembelea wenzao na kutatua changamoto mbalimbali.

Haya yamefanyika kwenye mkutano wa Maafisa usafirishaji uliofanyika katika ukumbi wa AICC Simba hall leo tarehe 27 Desemba 2024 ambapo mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi ndiye aliyekuwa Mgeni rasmi.

#KijanaNaKijani
#TunazimazoteTunawashaKijani
#KulindaNaKujengaUjamaa
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-12-27 at 20.19.20.mp4
    21.5 MB
Back
Top Bottom