benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,533
- 3,187
Ameandika Katibu Mkuu Wizara ya Michezo, Gerson Msigwa
"Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan atoa ndege kwa ajili ya kuisafirisha Timu ya Taifa ya Soka kwenda Marrakesh Morocco ambako itaumana na Timu ya Taifa ya Niger katika kutafuta tiketi ya kufuzu michuano ijayo ya Kombe la Dunia.
Tunakushukuru sana Mheshimiwa Rais, sasa timu itasafiri kwa muda mfupi kwenda Marrakesh tarehe 16 Novemba, 2023 na itarejea haraka tarehe 19 Novemba, 2023 baada ya mchezo wake wa tarehe 18 Novemba, 2023 dhidi ya Niger.
Kisha tarehe 21 Novemba itakuwa na kibarua kingine cha kuumana na Timu ya Taifa ya Morocco katika mbio hizohizo za kusaka tiketi ya kucheza Kombe la Dunia lijalo litakaloandaliwa na Marekani, Canada na Mexico."
"Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan atoa ndege kwa ajili ya kuisafirisha Timu ya Taifa ya Soka kwenda Marrakesh Morocco ambako itaumana na Timu ya Taifa ya Niger katika kutafuta tiketi ya kufuzu michuano ijayo ya Kombe la Dunia.
Tunakushukuru sana Mheshimiwa Rais, sasa timu itasafiri kwa muda mfupi kwenda Marrakesh tarehe 16 Novemba, 2023 na itarejea haraka tarehe 19 Novemba, 2023 baada ya mchezo wake wa tarehe 18 Novemba, 2023 dhidi ya Niger.
Kisha tarehe 21 Novemba itakuwa na kibarua kingine cha kuumana na Timu ya Taifa ya Morocco katika mbio hizohizo za kusaka tiketi ya kucheza Kombe la Dunia lijalo litakaloandaliwa na Marekani, Canada na Mexico."