Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi,Rais anayeheshimika na kupendwa na watanzania kwa kiwango cha juu utafikiri pesa,hii leo ametua na kuingia ndani ya chuo cha Taifa cha Ulinzi na kupata mapokezi mazito kwelikweli na ya heshima ya hali ya juu sana.
Ambapo akiwa chuoni hapo Mheshimiwa Rais wetu mpendwa ameweza kutoa Mhadhara Mzito sana wa uzani wa juu na kidunia juu ya Falsafa yake ya 4R katika kuongoza serikali yake.ikumbukwe falsafa hiyo ndio imeshuhudia na kuwawezesha wapinzani na vyama vyote vya siasa kupanda majukwaani na kufanya siasa.
Ni kupitia falsafa hiyo imewezesha wapinzani waliokuwa wamekimbia nchi na kuishi uhamishoni kuweza kurejea Nchini kifua mbele na kuishi nchini mwao bila hofu wala wasiwasi,ni kupitia falsafa hizo tumeshuhudia umoja wa kitaifa ukiimarika na kuwa na nguvu kuliko wakati wowote ule.
Ni kupitia falsafa hiyo leo hii hakuna Mwanasiasa ambaye yupo gerezani kwa kesi ya kisiasa, wala kufungwa pingu kwa maonezi na kusafirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine, wala mtu kulala na wasiwasi ya kugongewa na kuvunjiwa mlango na hatimaye kukamatwa usiku wa manane kama Jambazi sugu la mauaji.
Ni kupitia falsafa hiyo tumeshuhudia vyama vya siasa hapa nchini vikikaa kwa pamoja katika meza moja ya mazungumzo kunywa maji na kula chakula kwa pamoja na kuzungumza masuala mbalimbali juu ya mstakabali wa Taifa letu na mwisho kupeana mikono kwa amani na upendo.
Ni kupitia falsafa hiyo tumeshuhudia umoja, mshikamano,upendo na udugu ukiongezeaka na kuimarika sana miongoni mwa Watanzania pamoja na kuongezeka kwa moyo wa uzalendo kwa Taifa letu na kupendana sisi kwa sisi bila kujali itikadi zetu za kisiasa.ndio sababu kazi zinaendelea vyema, maendeleo yanapatikana kila Secta,uchumi wetu unakua kwa kasi,watalii wanaendelea kumiminika nchini kufikia millioni 1.8,mapato yanaendelea kuongezeka,biashara zinaendelea kuongezeka.
Ni kupitia falsafa hiyo tunaona Amani na utulivu vinaendelea kutamalaki na kushamiri hapa nchini.hiyo yote ni kazi ya Mikono ya Jemedari wetu na Rais wetu mpendwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan jasiri muongoza njia na shujaa wa Afrika,mama wa shoka,chuma cha Reli kiongozi imara na hodari katika uongozi.hii yote ni akili ,upeo na maarifa makubwa ya kiuongozi aliyo nayo Rais wetu kipenzi.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi,Rais anayeheshimika na kupendwa na watanzania kwa kiwango cha juu utafikiri pesa,hii leo ametua na kuingia ndani ya chuo cha Taifa cha Ulinzi na kupata mapokezi mazito kwelikweli na ya heshima ya hali ya juu sana.
Ambapo akiwa chuoni hapo Mheshimiwa Rais wetu mpendwa ameweza kutoa Mhadhara Mzito sana wa uzani wa juu na kidunia juu ya Falsafa yake ya 4R katika kuongoza serikali yake.ikumbukwe falsafa hiyo ndio imeshuhudia na kuwawezesha wapinzani na vyama vyote vya siasa kupanda majukwaani na kufanya siasa.
Ni kupitia falsafa hiyo imewezesha wapinzani waliokuwa wamekimbia nchi na kuishi uhamishoni kuweza kurejea Nchini kifua mbele na kuishi nchini mwao bila hofu wala wasiwasi,ni kupitia falsafa hizo tumeshuhudia umoja wa kitaifa ukiimarika na kuwa na nguvu kuliko wakati wowote ule.
Ni kupitia falsafa hiyo leo hii hakuna Mwanasiasa ambaye yupo gerezani kwa kesi ya kisiasa, wala kufungwa pingu kwa maonezi na kusafirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine, wala mtu kulala na wasiwasi ya kugongewa na kuvunjiwa mlango na hatimaye kukamatwa usiku wa manane kama Jambazi sugu la mauaji.
Ni kupitia falsafa hiyo tumeshuhudia vyama vya siasa hapa nchini vikikaa kwa pamoja katika meza moja ya mazungumzo kunywa maji na kula chakula kwa pamoja na kuzungumza masuala mbalimbali juu ya mstakabali wa Taifa letu na mwisho kupeana mikono kwa amani na upendo.
Ni kupitia falsafa hiyo tumeshuhudia umoja, mshikamano,upendo na udugu ukiongezeaka na kuimarika sana miongoni mwa Watanzania pamoja na kuongezeka kwa moyo wa uzalendo kwa Taifa letu na kupendana sisi kwa sisi bila kujali itikadi zetu za kisiasa.ndio sababu kazi zinaendelea vyema, maendeleo yanapatikana kila Secta,uchumi wetu unakua kwa kasi,watalii wanaendelea kumiminika nchini kufikia millioni 1.8,mapato yanaendelea kuongezeka,biashara zinaendelea kuongezeka.
Ni kupitia falsafa hiyo tunaona Amani na utulivu vinaendelea kutamalaki na kushamiri hapa nchini.hiyo yote ni kazi ya Mikono ya Jemedari wetu na Rais wetu mpendwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan jasiri muongoza njia na shujaa wa Afrika,mama wa shoka,chuma cha Reli kiongozi imara na hodari katika uongozi.hii yote ni akili ,upeo na maarifa makubwa ya kiuongozi aliyo nayo Rais wetu kipenzi.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
