Rais Samia aweka historia mpya. Sasa maridhiano hali shwari, aunganisha vyama vyote vya siasa

Rais Samia aweka historia mpya. Sasa maridhiano hali shwari, aunganisha vyama vyote vya siasa

PendoLyimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2014
Posts
969
Reaction score
1,055
Katika kuhakikisha Amani na utulivu nchini Tanzania inazidi kutawala, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anajitoa kindaki ndaki na kuwa mfano bora katika kufanikisha hilo. Wakati Tanzania inatimiza Miaka 30 ya vyama vingi vya siasa, Rasmi anatambulisha mfumo wa 4R yaani Maneno manne yakiwa nguzo katika Kuiongoza nchi. Reconciliation (Maridhiano), Resiliency (Ustahimilivu), Reforms (Mabadiliko) na Rebuilding (Kujenga upya) ni misingi aliyoiweka kuwa ni Muongozo katika kuiunganisha vyema Tanzania.

Ili kukuza Demokrasia na haki katika nyanja ya kisiasa, Tarehe 23 Disemba 2021, Mhe. Rais aliunda kikosi kazi kikiwa na Wajumbe 24 kutoka Tanzania bara na Visiwani ili kukusanya na kuchakata maoni na mapendekezo ya wadau wa demokrasia wa vyama vya siasa nchini na kuwasilishwa serikalini kufanyiwa kazi na hatimaye kutolewa majibu rasmi Tarehe 3 Januari 2023 huku akivikutanisha vyama vyote vya siasa.

Mhe. Samia alitoa ruhusa ya kuendelea kufanyika kwa mikutano ya hadhara akisisitiza uwepo wa amani huku akiahidi kufanyika kwa mabadiliko ya mifumo ya kisiasa na kisheria na kufanyika mchakato wa katiba mpya huku akiahidi kuendela kufanyika kwa maridhiano na kuwataka Watanzania kuwa wastahimilivu na kuijenga Tanzania mpya.

Soma: Ujio wa Rais Samia Suluhu Hassan: Hadi sasa sijaona dalili yoyote ya utashi wa kuwepo kwa maridhiano ya kisiasa nchini
 
Katika kuhakikisha Amani na utulivu nchini Tanzania inazidi kutawala, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anajitoa kindaki ndaki na kuwa mfano bora katika kufanikisha hilo. Wakati Tanzania inatimiza Miaka 30 ya vyama vingi vya siasa...
Subiri washirika wa "MAREHEMU" wakuje...
 
Kwani nchi hii paliwahi kuwa na mifarakano? Lini na nani mhusika?
 
..hilo swali aulizwe mkuu wa nchi maana yeye ndio amekuja na suala la Reconciliation au Maridhiano.
... watamuuliza waandishi nguli wa Europe na US siku akienda huko. Sidhani kama makanjanja wana hata hilo wazo sembuse uthubutu.
 
Katika kuhakikisha Amani na utulivu nchini Tanzania inazidi kutawala, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anajitoa kindaki ndaki na kuwa mfano bora katika kufanikisha hilo. Wakati Tanzania inatimiza Miaka 30 ya vyama vingi vya siasa, Rasmi anatambulisha mfumo wa 4R yaani Maneno manne yakiwa nguzo katika Kuiongoza nchi. Reconciliation (Maridhiano), Resiliency (Ustahimilivu), Reforms (Mabadiliko) na Rebuilding (Kujenga upya) ni misingi aliyoiweka kuwa ni Muongozo katika kuiunganisha vyema Tanzania.

Ili kukuza Demokrasia na haki katika nyanja ya kisiasa, Tarehe 23 Disemba 2021, Mhe. Rais aliunda kikosi kazi kikiwa na Wajumbe 24 kutoka Tanzania bara na Visiwani ili kukusanya na kuchakata maoni na mapendekezo ya wadau wa demokrasia wa vyama vya siasa nchini na kuwasilishwa serikalini kufanyiwa kazi na hatimaye kutolewa majibu rasmi Tarehe 3 Januari 2023 huku akivikutanisha vyama vyote vya siasa.

Mhe. Samia alitoa ruhusa ya kuendelea kufanyika kwa mikutano ya hadhara akisisitiza uwepo wa amani huku akiahidi kufanyika kwa mabadiliko ya mifumo ya kisiasa na kisheria na kufanyika mchakato wa katiba mpya huku akiahidi kuendela kufanyika kwa maridhiano na kuwataka Watanzania kuwa wastahimilivu na kuijenga Tanzania mpya.
Naona unfagilia mwendawazimu ee
 
Back
Top Bottom