Rais Samia boresha kila kitu tutakusahau, ila ukimaliza mchakato wa Katiba tutakukumbuka milele

Hakuna kiongozi yoyote ambaye yuko tayari kuibadilisha katiba ili ajipunguzie madaraka.
Kwa Wazanzibari wote wamekuwa wakiamini kuwa Serikali ya Muungano inawanyonya na inawachelewesha kupata maendeleo, huu ndiyo wakati muafaka wao kufanya kweli. Kwa kuwa Rais wa Muungano ni Mzanzibari na Rais wa Muungano ni Mzanzibari pia
 
CCM hawataki KATIBA.
SI mama wala wajumbe, wana damu mikononi mwao, wanaogopa tume mbalimbali zilishatoa majibu hasa mauaji ya zanzibar, kifo cha akwilina , mtwara, kibiti na mizoga ya koko beach, hawawezi kubali.
Jana wamekubali mchakato wa katiba mpya uendelee
 
Unalilia katiba, lakini inaweza kubadilishwa kinyume na ulivokua unategemea na ukanyonywa zaidi. Cha msingi ni kuandaa wazalendo tu
Unawaandaaje wazalendo bila Katiba? Huoni hiyo inajenga kikundi cha madikteta kama wale kina Magufuli, Bashiru Ally, Polepole, Makonda, Sabaya?
 
Sielewi hofu ya samia Suluhu nini Juu ya Mabadiliko ya Katiba. Hii inanifanya niamini kumbe na yeye ni walewale tu
 
Njia nzuri ya katiba ni kufanya AMENDMENT na katiba haitakiwi kuwa kana gazeti la zamani la mzalendo au kitabu cha ABBOTT au kitabu cha VINE AND REES cha plant and animal biology al maarufu kama mkate

Katiba ni ka kitabu kadogo saana
Sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…