Rais Samia: Corona ipo, chukueni tahadhari

Wasaidizi wa Mama tafadhali mjifunze kuandika vizuri. Mnatutia aibu. Ona English tweet ya Mama!!!

"I urge my Fellow Tanzanians to continue to take precautionary measures against Corona (Covid-19) as directed by our Healthcare Professionals such as to regularly wash our hands with running water and soap, wearing masks at all times and always maintain social distancing"
 
Mbona hujaandika tatizo lake.
 
Kitu gani huyu mama anasema ambacho hakijulikani au ambacho hakijawahi kusisitizwa kabla yake? Kama anataka tofauti basi atufungie vyumbani na afunge mashule, tushamchoka sasa!
 
Mh.Raisi Mimi ni mmoja wa watu ambao walipinga waziwazi hatua zilizpchukuliwa na Raisi aliyepata kwenye kupambana na suala la Corona.

Ulipokuja wewe ulionyesha seriousness kwenye suala hili na tunakupongeza sana.

Umeshauriwa na wataalamu vizuri kuhusu hili janga na umewasikiliza na hata juzi tumeona ukisema wimbi la tatu lipo na limeshaingia nchini na wagonjwa wapo.

Mama Samia sasa hivi kwenye shughuli zako nyingi unavaa barakoa hata kwenye vikao vya ndani umeonyesha kuchukua tahadhali kwako na kwa wanaokuzunguka.

Jana ulitoa tena ujumbe kama raisi kuwaasa wananchi kuwa ni lazima wachukue tahadhari kuepuka ugonjwa wa corona ikiwapo kuzuia mikusanyijo isiyo ya lazima, kugusana, kuvaa barakoa, kupaka sanitizer na mengine mengi ILA

Nimeshindwa kuelewa tena imekuwaje umempigia simu msanii Nandy na kumpongeza kufanya tamasha la Nandy festival dodoma na ukaonyesha shauku ya ungependa kuwepo.

Bado nachanganyikiwa hapa, kwanza ilippaswa uzuie hata Hilo tamasha kufanyika kwa sababu ni wewe ulisema kuna wimbi la tatu la corona na kutoa tahadhari zote.

Ni kweli Kuna kitu hakipo sawa juu ya suala hili la corona? Unapiga simu kuongeza tamasha ambalo watu wamesongamana na hakuna hatua zozote za kujilinda na corona?

Nilitegemea ungewawajibisha watu walioruhusu hili tamasha kufanyika kipindi hiki ambacho Kuna wimbi la tatu.

Nchi ni ngumu sana hii kwa kweli.
 

Kweli ukiondoa “T”anzanians sioni herufi kubwa zimekujaje. Eti “such as to …” “our”, “maintain”. Mambo mengine yanaaibisha. Na ukute huyo ni linguist kabisa na hizo sio typos!
 
Kitu gani huyu mama anasema ambacho hakijulikani au ambacho hakijawahi kusisitizwa kabla yake? Kama anataka tofauti basi atufungie vyumbani na afunge mashule, tushamchoka sasa!
Kama Rais, anatukumbusha vitu ambavyo tulijisahau kufanya kupambana na Covid 19.
 
Kitu gani huyu mama anasema ambacho hakijulikani au ambacho hakijawahi kusisitizwa kabla yake? Kama anataka tofauti basi atufungie vyumbani na afunge mashule, tushamchoka sasa!
Mwendazake aliwahi kukiri kuna korona na kusisitiza hatua za kuchukua?
 
Kweli ukiondoa “T”anzanians sioni herufi kubwa zimekujaje. Eti “such as to …” “our”, “maintain”. Mambo mengine yanaaibisha. Na ukute huyo ni linguist kabisa na hizo sio typos!


Sasa mkuu, hebu rephrase hiyo note yote ya mama ili tuone ilipaswa iweje.
 
Kitu gani huyu mama anasema ambacho hakijulikani au ambacho hakijawahi kusisitizwa kabla yake? Kama anataka tofauti basi atufungie vyumbani na afunge mashule, tushamchoka sasa!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Lini mtaanza kututajia na takwimu?
 
Sasa mkuu, hebu rephrase hiyo note yote ya mama ili tuone ilipaswa iweje.
I urge my Fellow Tanzanians to continue to take precautionary measures against Corona (Covid-19) as directed by our Healthcare Professionals such as to regularly wash our hands with running water and soap, wearing masks at all times and always maintain social distancing

I urge my fellow Tanzanians to continue taking precautionary measures against Corona (Covid-19) as directed by our healthcare professionals by regularly washing hands with running water and soap, wearing masks at all times and always maintaining social distancing.

Pamoja na yote hayo, no one should wear a mask "at all times" (hili haliwezekani mkuu) - mask wearing iko regulated. Kwanini basi asiseme "indoors" au "outdoors"??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…